Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia na Teknolojia ya Habari Nape Moses Nnauye amewatoa wasiwasi wakazi wa Bukoba na wanachama wa CCM kuwa Mbunge wao Stephen Byabato atashinda uchaguzi ujao na hakuna mwingine.
"Matokeo ya kura siyo lazima yawe yale ya kwenye box, inategemea nani anahesabu na nani anatangaza. Unajua kuna mbinu nyingi za uchaguzi, Kuna halali, nusu halali na haramu na zote zinaweza kutumika ilimradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe" alisema Nape.
Aliyesema hayo katika Soko la Kashai jana Julai 15 usiku alipoalikwa na Mbunge Byabato kushuhudia ramani na michoro ya Soko jipya la Kashai linalotarajiwa kujengwa.
Kauli ya Chama ~
CCM yakataa maneno aliyosema Nape kuhusu ushindi wa kura unategemea na anayehesabu kura
Pia, utetezi wake:
Kuelekea 2025 - Nape Nnauye: Kauli ya "Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza" ilikuwa ni ya utani
Hata, hivyo, kuna kosa gani alilofanya katika serikali hii!? 🤔...
Mimi binafsi, kutoka katika sakafu ya moyo wangu, sioni ajabu, sishangai na wala sikasirishwi na alichokisema Mh. Nape (tena natumia neno Mh. nikimaanisha anastahili kuitwa Mh.)...
Jamani, si tunataka kiongozi mkweli, ambaye si mnafiki?
Sasa Mh. Nape amekosea kitu gani kuweka wazi kile ambacho wasimamizi wa uchaguzi (inayoitwa tume huru ya uchaguzi) wamekuwa wakikifanya kwa miaka yote?
Kosa lake ni lipi jamani? Kusema ukweli? Mnataka kusema kwamba mlikuwa hamjui kwamba anachokisema Nape ndo huwa kinafanyika siku zote? Uchaguzi wa 2019 (serikali za mitaa) na 2020 (madiwani, wabunge na Rais) anachosema Nape si ndo kilifanyika?
Wote mnajua na mmeshuhudia kile alicho kisema Nape!
Kwa maoni yangu, tunawahitaji viongozi wengi aina ya Nape Mnauye. Pengine umma utawaelewa...na hatimaye labda ufanye uamzi stahiki wa kuchukua hatua.
Nionavyo mimi,Nape ni kama Yuda Iskariotu, mpango wa Mungu usingekamilika bila Yuda Iskarioti kufanya alicho fanya!
Wenye kunielewa wameelewa, ambao hamjanielewa, KAZI IENDELEE