Napendekeza kazi za kuhesabu idadi ya watu (Sensa 2022) ifanywe na wajumbe wa nyumba 10 , pesa zitakazookolewa zikajenge flyover TAZARA

Kwa nini fedha hizo zisijenge barabara ya makete yadi mbeya kupitia tukuyu
 
Wajumbe wa nyumba 10 wana elimu gani??
Maana hii kazi inahitaji elimu kidogo.

Mwisho kabisa acha ubinafsi.
 

1. Sensa hufanywa kwa muda wa siku moja au mbili tu na si zaidi

2. Sensa ya 2022 ni ya kidigitali

3. Sensa haifanyiki kiholela

4. Sensa hufanyika tofauti na 'population registers - prs'

5. Mchakato mzima wa sensa ni lazima ufuate misingi ya fani ya takwimu

6. Zoezi la sensa linatakiwa kufanywa na watu wenye maarifa na wanaojua kutumia vishkwambi na simu janja kuepusha makosa ya data 'taarifa ghafi'

7. Kadri zoezi la sensa linavyochukua siku nyingi ndivyo uwezekano wa kukusanya data mbovu unavyoongezeka

8. Una maoni mazuri, pole kwa changamoto
 
Hata kama wameishia la saba, ili mradi wanajua kusoma na kuandika, sioni tatizo
Wewe una ubinafsi tu.
Hakuna tatizo juu ya kuajiri vijana wa kitz, halafu hao wajumbe wa nyumba 10 ni wangapi nchi hii, huoni utatumia pesa nyingi zaidi kuliko ambavyo ungetumia ukiwapa hao vijana.

Halafu utatumia muda mrefu kama sio mda mrefu basi hizo data 70% zitakua sio sahihi kwasababu ya ufinyu wa muda.
 
1.) Sensa ikifanywa kwa zaidi ya siku 2 kuna utofauti wa matokea ya idadi ya watu? Ukizingatia ni jambo linalofanywa mara moja kwa miaka 10?

2.) Kwani wajumbe wakikusanya data na afisa mtendaji akazi-digitize na kuzituma zinakuwa sio za kidijitali?

3.) Kwani tumesema wajumbe wafanye kiholela?

4.) Kwani nani kasema haifanyiki tofauti na ‘population registers’?

5.) Kwani vigezo vya kuhesabu watu zinataka fani gani? Mjumbe anaejua kusoma na kuandika hawezi kujaza fomu husika?

6.) ‘Tablet’ ni computer kama computer zingine, afisa mtendaji atatumia computer yake kulisha data za wajumbe na kuzituma kwa wahusika.

7.) Data zinakusanywa kwa muda ule ule, kinachokua muda ni digitization ya data itakayofanywa na ofisi ya afisa mtendaji, hivyo haziwezi kuharibika

8.) Maoni ni mazuri hutekelezwa
 
Kila mjumbe anazijua nyumba zake na watu wanaoishi ndani ya nyumba hizo, anaweza akakusanya hizo data chap chap very smoothly, tena kwa posho kidogo sana.
 
Kila mjumbe anazijua nyumba zake na watu wanaoishi ndani ya nyumba hizo, anaweza akakusanya hizo data chap chap very smoothly, tena kwa posho kidogo sana.
Aisee una ubishi ndgu.

Wenye akili washaamua na haitokuja kkubadilika.
Acha tuishie hapa mkuu.
 
Aisee una ubishi ndgu.

Wenye akili washaamua na haitokuja kkubadilika.
Acha tuishie hapa mkuu.
Kama wale wenye akili waliokuwa wanapangisha watu foleni kulipia kodi za majengo ilihali kuna luku? Hopeless..; pia kipo kitakachobadilika, i assure you, kama si leo, basi kesho

 
1. Kufanya sensa kwa zaidi ya siku 2 ni kukiuka misingi ya fani ya takwimu. Na kufanyika kwa siku zaidi hupelekea data kuwa na makosa makubwa kiasi cha kuvuka error tolerance na kukosa reliability. Hilo litapelekea kupata data "matokeo" tofauti na zenye dosari "irrelevant observation, structural error, duplicate, missing value"

2. Zitakuwa ni digital, fahamu: sensa ya 2022 mambo yote yatafanyika kwenye mfumo "system - data collections tools/forms", hivyo basi ukusanyaji = uingizaji wa taarifa electronically, data organization & cleansing (editing - imputing - removal unwanted errors eg: extreme value 'outliers') na data processing 'kuchakata' na mazoezi yatakayohitaji kufanyika na wataalamu wa fani ya Tehama, kwa maono yako hao Maafisa Watendaji wa Mitaa/Kata wataweza? Nafanya kazi kwa karibu sana na wajumbe, madiwani na watendaji, nafahamu competency degree yao, wengi ni wenzangu na mimi - hawajiwezi

3. Kitendo cha kutaka kufanya kitu pasina kufuata taratibu elekezi ni kufanya kitu kiholela. Kama sheria, kanuni, taratibu na miongozo itafuatwa basi hawatakuwa wamefanya kiholela

4. Kuhitajia sensa ifanyike kwa mtindo na muundo huo uliowasilisha kunajitofautishaje na population registers?

5. Rejea "qualities/sifa za mkusanya taarifa", na hii ni moja ya nukta muhimu sana kwenye fani ya takwimu ndiyo maana Chuo cha Takwimu Kilichopo Mashariki mwa Africa (EASTC) kinatoa kozi maalumu ya muda mfupi ya ukusanyaji taarifa, unaweza ukapata picha ya wasifu wa mtu aliyefuzu kwa vigezo vya kitakwimu, kigezo kikuu cha kielimu: awe na astashahada au stashahada ya fani ya takwimu, kozi hizo zote 3 zinaratibiwa na EASTC kwa ushirikiano na NBS na Wizara ya Fedha. Vigezo ni vingi na vyote sitavitaja, ila ni zaidi ya kujua kusoma na kuandika, kwani si kila anayejua hivyo pia anajua kusoma "statistical map" - GIS? na mbona hujauliza swali kwa kuwagusia wajumbe wasiojua kusoma na kuandika? Ni wazi unafahamu baadhi ya sifa basic zinazohitajika. Katika statistical investigation hamna sehemu ambapo utmost care inatakiwa izingatiwe kama kwenye data collection - huu ndo msingi mkuu wa takwimu, hivyo makosa mengi yakifanyika kwenye kukusanya data unakuwa umeshaharibu kila kitu: yaani procedures zote zinazofuata zinakuwa void na matokeo/hitimisho litakalotolewa litapotosha "mislead"

6. Anayetakiwa kukusanya na kuingiza taarifa electronically "tarakilishi/kishkwambi/simu janja" ni karani ambaye kwa mujibu wa mfano wako ni mjumbe, ni wajumbe wangapi wanajua kutumia hivyo vifaa? "User experience", achilia mbali wajumbe, je, watendaji wangapi wanaojua kutumia vishkwambi/tarakilishi/simu janja? Tupo kwenye karne ya 21 zama za mapinduzi ya teknolojia, lakini watanzania wanaojua kutumia hivyo vifaa japo "basic au intermediate" roughly hata 1/3 hawafiki kati ya watu milioni 60 approximately, wajumbe ni wanasiasa - wengi wao wasifu wao unafahamika, hata watendaji wa Mtaa/Kijiji/Shehia pia, walau watendaji wa ngazi ya Kata wanajiweza kidogo. Ifahamike pia kwamba fomu huwa ni nyingi na zina maswali mengi, kama hawatatuliza akili kutoa maboko ni Maguire tu

7. Kama litafanyika kwa muda elekezi itapunguza kuondoa discrepancies 'errancy & fallibility", data za sensa hazitakiwi kuwa accurate bali realible. Sensa siyo zoezi la kuchukulia poa, kutenga kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya zoezi hili tu pekee kunatafakarisha mambo mengi. Hivi unajua hadi zoezi rasmi la sensa linafanyika ni mazoezi mangapi makubwa yametangulia? Halafu hivi zoezi kama Dermacation ambalo ni "ugawaji maeneo tu ya kuhesabia watu - EA" kwa nini Serikali (NBS/OCGS) hawakuwatumia wajumbe/watendaji moja kwa moja? Wao ndo wakazi/wenyeji wa Shehia/Mitaa/Vijiji/Kata/Tarafa/Wilaya/Mkoa - wanaijua mipaka vizuri, hukujiuliza kwa nini NBS/OCGS waliamua kuajiri wataalamu maalumu wa muda kwa ajili ya hiyo activity tu? Kwa nini wasingewapa tu wajumbe/watendaji mambo yaende na tupunguze gharama. Hebu fikiri timu ya wataalamu imezunguka nchi nzima, kulikuwa na haja gani wakati wajumbe/watendaji wapo kila mahali na wametapakaa nchi nzima? Kulikuwa na haja gani ya kuajiri hao wataalamu kwa muda kama siyo matumizi mabaya ya rasilimali fedha na mipango duni? Kwenye dermacation wajumbe/watendaji walitumika ndiyo lakini kama guider na siyo kama wataalamu wakuu, kuna mambo ya kujifunza kidogo kwenye hayo maswali. Wangepewa kazi zote za aina hiyo wakapanganyika ndani ya rekodi na kusimamia pamoja [emoji23]. Takwimu ni fani kubwa mno na ina mambo kibao, inastahili heshima yake kama fani nyingine

8. Sawa bana [emoji4]

9. Naheshimu maoni yako
 
1.) Ukusanyaji wa data unaweza ukafanyika kwa siku mbili, kitachochukua muda ni digitization toka kwenye karatasi kwenda kwenye tarakilishi, hivyo hapatakuwa na tatizo. Hata hivyo, hiyo Misingi unayodai itakiukwa (kama kweli ndio hiyo) , itasababisha vipi data zinazochukuliwa zisiwe za kweli? Kufanya kwa zaidi ya siku 2, kunafanya vipi data zisiwe za kweli?

2.) kama form4 leaver anaweza kutumia tehama, afisa mtendaji ambae nae ni mwajiriwa wa serikali anashindwaje kutumia tehema?

3.) Huo uelekezi ni upi sasa? Kama tunaamua kuwatumia wajumbe wa nyumba 10 si tutaunda maelekezo mapya amabayo yatafuatwa?

4.) Kwani Kufanya kwa muundo tofauti na ambao nauoendekeza kunakutofautisheje na ‘pipulation registers’, labda ungedadavua hilo

5.) Hizo qualities ulizotaja kwamba awe amehitimu chuo cha statustics, hao form 4 leavers mnaowaajiri kuhesabu watu, wamehitimu lini hiko chuo?

6.) Wewe unasema anatakiwa karani mdio aingize, na mimi nakuambia naoendekeza afisa mtendaji ndio aingize, hawawezi kushindwa kutumia kishkwambi.

7.) Hata tukitumia wajumbe wa nyumba 10, tutaweka muda elekezi na tutaufuta.

8.) Sawa
 
We ukisikia dodoso unaona kitu kimoja cha ajaaaabu, mjumbe hashindwi kujaza fomu. Kama kuna training wapewe, hawashindwi!
Probably wengi hawataweza.
Mkuu nalijua dodoso na Nimewahi kufanya hiyo kazi sensa iliyopita.
 

1. Sensa ya 2022 itafanyika kwa njia za kieletroniki 'digital' na siyo kwenye makaratasi rafiki yangu mbona hunielewi aisee? Zoezi la sensa kufanyika kwa siku nyingi kunapelekeaje data ziwe na dosari? Nimedokeza kwenye posti iliyopita pointi namba 1 nilipotaja aina ya makosa ya data ikiwemo duplicate. Hebu tufahamishe kwa muda wa siku 10 utawezaje kudhibiti "dosari/makosa/mabadiliko" ya data yatakayotokana na hali zifuatazo:

  • Idadi ya watoto watakaozaliwa
  • Idadi ya watu watakaopoteza maisha "Watakaofariki"
  • Idadi ya watu watakaohama nje ya EA
  • Idadi ya watu watakaohamia ndani ya EA
  • Matukio yasiyotarajiwa kama majanga "mafuriko nakadhalika" yatakayopelekea watu kuhama/kuhamia
  • Idadi ya watu watakaokuwa safarini

Watakwimu waliangazia hayo na mengineyo ndo maana walithubutu kudhibiti muda maalumu wa kuhesabu watu, kwa muda wa siku moja au mbili hizo hali kitakwimu zinavumilika "error tolerance", lakini masiku yakizidi ni kipengele "mkanganyiko". Kitakwimu haswa huwa sensa inatakiwa ifanyike siku moja tu tena majira ya "asubuhi/alfajiri" au "jioni/usiku" kwa kuwa ni nyakati ambazo watu wengi hupatikana kwenye makazi yao, ama kama zoezi halitakamilika "incomplete coverage" ndani ya siku hiyo moja huongezwa siku nyingine "siku pili" ili kufukia mashino

2. Inalazimu tu kufanya hivyo kwa sababu uhitaji wa nguvu kazi ni mkubwa na zoezi linafanyika ndani ya muda mfupi mno Tanzania nzima, isingekuwa hivyo wangefanya kama walivyofanya kwenye dermacation, wangeajiri wataalamu wachache maalumu

Kwani hamna watu ambao ni illiteracy na wanajua kutumia hivyo vifaa vya tehama? Mbona hukujenga hoja kama hiyo? Elimu ya kidato cha 4 ni kigezo cha chini tu cha kitaaluma ambacho wameangazia na wakaona huenda mtu akiwa nacho anaweza akafit kuvaa jukumu husika, lakini pia wameweka hicho kigezo kwa lengo la kupata muitikio mkubwa wa maombi "kumbuka wanahitaji watu wengi sana", pia naamini wameweka hivyo kwa sababu wahitimu wengi wa madaraja ya juu ya elimu hawaishi vijijini, pia naamini watakuwa wameamua kutoa tu fursa kwa watu wa daraja hilo la kielimu "ni kundi kubwa la watu na wengi hawana kazi rasmi"

Kujua kutumia vifaa vya tehama hakuhusishi elimu peke yake tu, wala hakuhusishi kuajiriwa na serikali wala cheo cha mlengwa, achana na watendaji, mimi nawafahamu hadi wakuu wa Idara na Vitengo wa Taasisi mbalimbali za Serikali "hususani jinsia KE" wasiojua kutumia hivyo vifaa na baadhi yao wanaratibu mazoezi nyeti, au wanajua kutumia kidogo "beginner - basic" kiasi cha kuwafanya washindwe hata kuyaendea majukumu yao kwa weledi, mara nyingi majukumu yao yanayohusisha matumizi ya hivyo vifaa hufanywa na subordinate. Si wao tu, wapo watumishi wengi tu wasiojua kutumia hivyo vitu kwa uzuri "intermediate user", kumbuka tumeanza kutumia hivi vifaa miaka ya hivi karibuni tu maofisini. Kigezo hicho cha kielimu kimewekwa tu kama get pass "kiingilio" lakini haswa kinachokusudiwa ni kule kuweza kumudu yale majukumu. Elon Mask ana msemo wake "Siamini katika vyeti "makaratasi", ninaajiri kwa kuzingatia ujuzi hata kama mhusika hajasoma"

Fani ya Udhibiti wa Rasilimali Watu inazingatia na kuthamini sana madaraja ya kielimu, katika tasnia hii wanaamini katika kuleta ufanisi wa kazi ni vema au lazima kuajiri mtu aliyefuzu kwa daraja la kielimu nafasi husika "mbobezi/mtaalamu". Na ndo maana kwenye post iliyopita nilikutajia vigezo vya kielimu vya kitakwimu (fani husika) kwenye hizi fursa. Naamini kungekuwa na idadi kubwa ya hao wahitimu hapa nchini basi wangetumika kwenye hili zoezi na huenda hata kusingekuwa na mafunzo/semina ya masiku mengi (wale ni wabobezi na wengi wao wana uzoefu wa mazoezi ya aina hii/yanayohusisha matumizi ya vifaa hivyo). Na hata hivyo hicho siyo kigezo pekee kilichowekwa na kitakachozingatiwa kwenye kuchagua watu, vigezo ni vingi tu ikiwemo uzoefu nakadhalika. Na ukizingatia hata njia za kieletroniki za kukusanya taarifa/mapato/kodi ni changa hapa kwetu, hazijazoeleka

Fahamu: nafasi ya Maafisa Tehama iliyowekwa kwenye Tangazo hawatachukua yeyote isipokuwa wahitimu wenye vyeti husika vya Tehama tu. Na inaaminiwa watachukua watumishi wa Kitengo cha Tehama & Habari ngazi ya Halmashauri na kujazia wengine. Nafasi nyingine zilizosalia za ukarani na usimamizi ndo wenzangu na mimi tunaweza ambulia kwani majukumu haya mawili hatuhitaji tuwe tunajua sana kutumia vifaa vya tehama bali basic user tu

Jambo jingine, hizo kazi haziishii kwenye kujua kutumia vifaa vya tehama tu, kuna kujua kusoma ramani za kitakwimu na vikorombwezi vingine kidogo

Katika miko ya takwimu pia nafasi ya "ukusanyaji taarifa" huwa hazitakiwi zifanywe na watu wenye madaraja makubwa ya elimu (Shahada, Shahada ya Uzamili, Shahada ya Uzamivu nakadhalika) isipokuwa tu kama utafiti unaofanyika utakuwa complex sana na unaohitajia maarifa makubwa

3. Sijakuelewa. Ila kama ulikusudia miongozi ipo

4. Hmmm, siwezi kuelezea aisee, nimejitahidi kuandika maelezo mengi sana. Si rahisi ukanielewa kama hujachimba fani husika

5. Rejea pointi namba 2 juu nimejibu

6. Rejea pointi namba 2 juu nimejibu

Wewe ndo unasema hawawezi kushindwa, uhalisia tunaujua sisi tunaofanya nao kazi 24/7

7. Ushauri: Tafuta Mtakwimu akupitishepitishe kwenye vipengele muhimu, fani yao hii

8. Amani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…