Napendekeza kazi za kuhesabu idadi ya watu (Sensa 2022) ifanywe na wajumbe wa nyumba 10 , pesa zitakazookolewa zikajenge flyover TAZARA

Napendekeza kazi za kuhesabu idadi ya watu (Sensa 2022) ifanywe na wajumbe wa nyumba 10 , pesa zitakazookolewa zikajenge flyover TAZARA

1. Sensa ya 2022 haifanyiki kwenye makaratasi rafiki yangu, mbona hunielewi aisee? Zoezi la sensa kufanyika kwa siku nyingi kunapelekeaje data ziwe na dosari? Nimedokeza kwenye posti iliyopita pointi namba 1 nilipotaja aina ya makosa ya data ikiwemo duplicate. Hebu tufahamishe kwa muda wa siku 10 utawezaje kudhibiti mabadiliko ya data yatakayotokana na hali zifuatazo:

  • Idadi ya watoto watakaozaliwa
  • Idadi ya watu watakaopoteza maisha "Watakaofariki"
  • Idadi ya watu watakaohama nje ya EA
  • Idadi ya watu watakaohamia ndani ya EA
  • Matukio yasiyotarajiwa kama majanga "mafuriko nakadhalika"
  • Idadi ya watu watakaokuwa safarini

Watakwimu waliliona hilo ndo maana walithubutu kudhibiti muda maalumu wa kuhesabu watu, kwa muda wa siku moja au mbili hizo hali kitakwimu zinavumilika "error tolerance", lakini masiku yakizidi ni kipengele "mkanganyiko". Kitakwimu haswa huwa sensa inatakiwa ifanyike siku moja tu tena majira ya "asubuhi/alfajiri" au "jioni/usiku" kwa kuwa ni nyakati ambazo watu wengi hupatikana kwenye makazi yao, ama kama zoezi halitakamilika "incomplete coverage" ndani ya siku hiyo moja huongezwa siku nyingine "siku pili" ili kufukia mashino

2. Inalazimu tu kufanya hivyo kwa sababu uhitaji wa nguvu kazi ni mkubwa na zoezi linafanyika ndani ya muda mfupi mno Tanzania nzima, isingekuwa hivyo wangefanya kama walivyofanya kwenye dermacation, wangeajiri wataalamu wachache maalumu

Kwani hamna watu ambao ni illiteracy na wanajua kutumia hivyo vifaa vya tehama? Mbona hukujenga hoja kama hiyo? Elimu ya kidato cha 4 ni kigezo cha chini tu cha kitaaluma ambacho wameangazia na wakaona huenda mtu akiwa nacho anaweza akafit kuvaa jukumu husika, lakini pia wameweka hicho kigezo kwa lengo la kupata muitikio mkubwa wa maombi "kumbuka wanahitaji watu wengi sana", pia naamini wameweka hivyo kwa sababu wahitimu wengi wa madaraja ya juu ya elimu hawaishi vijijini, pia naamini watakuwa wameamua kutoa tu fursa kwa watu wa daraja hilo la kielimu "ni kundi kubwa la watu na wengi hawana kazi rasmi"

Kujua kutumia vifaa vya tehama hakuhusishi elimu peke yake tu, wala hakuhusishi kuajiriwa na serikali wala cheo cha mlengwa, achana na watendaji, mimi nawafahamu hadi wakuu wa Idara na Vitengo wa Taasisi mbalimbali za Serikali "hususani jinsia KE" wasiojua kutumia hivyo vifaa na baadhi yao wanaratibu mazoezi nyeti, au wanajua kutumia kidogo "beginner - basic" kiasi cha kuwafanya washindwe hata kuyaendea majukumu yao kwa weledi, mara nyingi majukumu yao yanayohusisha matumizi ya hivyo vifaa hufanywa na subordinate. Si wao tu, wapo watumishi wengi tu wasiojua kutumia hivyo vitu kwa uzuri "intermediate user", kumbuka tumeanza kutumia hivi vifaa miaka ya hivi karibuni tu maofisini. Kigezo hicho cha kielimu kimewekwa tu kama get pass "kiingilio" lakini haswa kinachokusudiwa ni kule kuweza kumudu yale majukumu. Elon Mask ana msemo wake "Siamini katika vyeti "makaratasi", ninaajiri kwa kuzingatia ujuzi hata kama mhusika hajasoma"

Fani ya Udhibiti wa Rasilimali Watu inathamini sana madaraja ya kielimu, katika tasnia hii wanaamini katika kuleta ufanisi wa kazi ni vema au lazima kuajiri mtu aliyefuzu kwa daraja la kielimu nafasi husika "mbobezi/mtaalamu". Na ndo maana kwenye post iliyopita nilikutajia vigezo vya kielimu vya kitakwimu (fani husika) kwenye hizi fursa. Naamini kungekuwa na idadi kubwa ya hao wahitimu hapa nchini basi wangetumika kwenye hili zoezi na huenda hata kusingekuwa na mafunzo/semina ya masiku mengi (wale ni wabobezi na wengi wao wana uzoefu wa mazoezi ya aina hii/yanayohusisha matumizi ya vifaa hivyo). Na hata hivyo hicho siyo kigezo pekee kilichowekwa na kitakachozingatiwa kwenye kuchagua watu, vigezo ni vingi tu ikiwemo uzoefu nakadhalika. Na ukizingatia hata njia za kieletroniki za kukusanya taarifa/mapato/kodi ni changa hapa kwetu, hazijazoeleka

Fahamu: nafasi ya Maafisa Tehama iliyowekwa kwenye Tangazo hawatachukua yeyote isipokuwa wahitimu wenye vyeti husika vya Tehama tu. Na inaaminiwa watachukua watumishi wa Kitengo cha Tehama & Habari ngazi ya Halmashauri na kujazia wengine. Nafasi nyingine zilizosalia za ukarani na usimamizi ndo wenzangu na mimi tunaweza ambulia kwani majukumu haya mawili hatuhitaji tuwe tunajua sana kutumia vifaa vya tehama bali basic user tu

Jambo jingine, hizo kazi haziishii kwenye kujua kutumia vifaa vya tehama tu, kuna kujua kusoma ramani za kitakwimu na vikorombwezi vingine kidogo

Katika miko ya takwimu pia nafasi ya "ukusanyaji taarifa" huwa hazitakiwi zifanywe na watu wenye madaraja makubwa ya elimu (Shahada, Shahada ya Uzamili, Shahada ya Uzamivu nakadhalika) isipokuwa tu kama utafiti unaofanyika utakuwa complex sana na unaohitajia maarifa makubwa

3. Sijakuelewa. Ila kama ulikusudia miongozi ipo

4. Hmmm, siwezi kuelezea aisee, nimejitahidi kuandika maelezo mengi sana. Si rahisi ukanielewa kama hujachimba fani husika

5. Rejea pointi namba 2 juu nimejibu

6. Rejea pointi namba 2 juu nimejibu

Wewe ndo unasema hawawezi kushindwa, uhalisia tunaujua sisi tunaofanya nao kazi 24/7

7. Ushauri: Tafuta Mtakwimu akupitishepitishe kwenye vipengele muhimu, fani yao hii

8. Amani
Hivi we jamaa unaniandikia mimi risala ndefu namna hii maana yake nini sasa, kwani huwezi ku-summarize hoja zako ukaeleweka, unaleta ngonjera hapa. Anyway, ngoja na mimi nakuandalia essay, tulia hapo hapo, now niko busy.
 
Mtu asiyejua kusoma wala kuandika hawezi kupewa ujumbe, hii kali sasa. Kama hii ni kweli, afisa mtendaji na mwenyekiti watawajibika kumjazia fomu zake, maana wao ndio walifanya uhuni wa kumpa ujumbe.
Unashangaa hilo la kutojua kusoma na kuandika kwa mjumbe wa nyumba kumi!!!
Bungeni wanatakiwa wawe na sifa ya kujua kusoma na kuandika tu,yaani K 2,lakini wapo wabunge wasio na hizo K 2.
 
Unashangaa hilo la kutojua kusoma na kuandika kwa mjumbe wa nyumba kumi!!!
Bungeni wanatakiwa wawe na sifa ya kujua kusoma na kuandika tu,yaani K 2,lakini wapo wabunge wasio na hizo K 2.
Mbunge asiejua K2? Mtaje mmoja
 
Kwa kupitia serikali za mitaa / vijiji (local government) , wajumbe wa nyumba 10 wapewe fomu za sensa na wapite kwenye nyumba zilizochini yao, wapewe wiki moja tu wawe wameshazitembelea nyumba zote zilizochini yao na kuzijaza fomu zote kwa kila nyumba, wakazikabidhi fomu hizo kwenye ofisi za serikali ya mtaa/kijiji, ofcourse wapewe na posho kidogo.

Afisa mtendaji akusanye zote na kuziwasilisha ofisi ya wilaya/mkoa ya sensa kwa ajili ya majumuisho na uchakataji wa taarifa.

Pesa zitakazookolewa ziende zikajenge flyover pale TAZARA, foleni ya malorry pale imesababisha hali kuwa mbaya sana.

=================================
By @ Maulaga59

Najaribu kuangalia changamoto wanazopata maafisa wa sensa wanaotumwa na serikali katika kukusanya taarifa muhimu za idadi ya watanzania.

Ukweli ni kwamba kwa sababu ya mazingira ya Tanzania yalivyo kijiografia ni vigumu sana hawa maafisa kuweza kupata takwimu sahihi za kusudio lao. Kuna sehemu ambazo huwa siyo rahisi kufika kwa gai au kwa mguu kwa sababu mbalimbali kama vile mapori, mabonde, milima, wanyama wakali na kadhalika.

Wenyeji wa maeneo hayo wao wanao uzoefu hata wa kufika makao makuu ya wilaya lakini si kwa wageni na muda mfupi wanaokuwa wamepewa kufanikisha zoezi.

Balozi wa nyumba kumi wangepewa semina za kufanya zoezi hilo wangeweza kuja na takwimu sahihi zaidi kuliko zile za maafisa waliotumwa.

Kila balozi angeweza kupeleka takwimu za watu wake kwenye ofisi ya kata na ofisi ya kata ingeratibu zoezi hilo katika eneo lake, kisha kupeleka ngazi za juu hadi ngazi ya taifa.

Zoezi hili siyo tu lingeleta takwimu sahihi zaidi bali pia lingepunguza gharama kubwa ambazo serikali hutumia katika kufanikisha zoezi zima.

Kwa huu utaratibu unaotumika kila baada ya miaka 10 watu wengi huwa wanaachwa bila kuhesabiwa hasa kwenye maeneo magumu kijiografia.

Nadhani miaka ijayo kazi hii ifanywe na mabalozi wa nyumba kumi.

Nawasilisha.
==================================
Nakupinga vikali mno mana nakumbuka kuna mjumbe fulani kule kitaa alikuwa ajui kusoma wala kuandika ulikuwa ukienda kupata huduma ya uthibitisho wa mtaa anakwambia chukua karatasi na kalamu andika aya maneno hapo ukimaliza unamtoa chochote kitu, embu nambie sasa kwa staili hii hawa wajumbe wa nyumba 10 wanaweza kukidhi maitaji kweli kwenye kuesabu watu
 
Nakupinga vikali mno mana nakumbuka kuna mjumbe fulani kule kitaa alikuwa ajui kusoma wala kuandika ulikuwa ukienda kupata huduma ya uthibitisho wa mtaa anakwambia chukua karatasi na kalamu andika aya maneno hapo ukimaliza unamtoa chochote kitu, embu nambie sasa kwa staili hii hawa wajumbe wa nyumba 10 wanaweza kukidhi maitaji kweli kwenye kuesabu watu
Wewe unaleta story za kufikirika, unajitungia tu...
 
Kwa kupitia serikali za mitaa / vijiji (local government) , wajumbe wa nyumba 10 wapewe fomu za sensa na wapite kwenye nyumba zilizochini yao, wapewe wiki moja tu wawe wameshazitembelea nyumba zote zilizochini yao na kuzijaza fomu zote kwa kila nyumba, wakazikabidhi fomu hizo kwenye ofisi za serikali ya mtaa/kijiji, ofcourse wapewe na posho kidogo.

Afisa mtendaji akusanye zote na kuziwasilisha ofisi ya wilaya/mkoa ya sensa kwa ajili ya majumuisho na uchakataji wa taarifa.

Pesa zitakazookolewa ziende zikajenge flyover pale TAZARA, foleni ya malorry pale imesababisha hali kuwa mbaya sana.

=================================
By @ Maulaga59

Najaribu kuangalia changamoto wanazopata maafisa wa sensa wanaotumwa na serikali katika kukusanya taarifa muhimu za idadi ya watanzania.

Ukweli ni kwamba kwa sababu ya mazingira ya Tanzania yalivyo kijiografia ni vigumu sana hawa maafisa kuweza kupata takwimu sahihi za kusudio lao. Kuna sehemu ambazo huwa siyo rahisi kufika kwa gai au kwa mguu kwa sababu mbalimbali kama vile mapori, mabonde, milima, wanyama wakali na kadhalika.

Wenyeji wa maeneo hayo wao wanao uzoefu hata wa kufika makao makuu ya wilaya lakini si kwa wageni na muda mfupi wanaokuwa wamepewa kufanikisha zoezi.

Balozi wa nyumba kumi wangepewa semina za kufanya zoezi hilo wangeweza kuja na takwimu sahihi zaidi kuliko zile za maafisa waliotumwa.

Kila balozi angeweza kupeleka takwimu za watu wake kwenye ofisi ya kata na ofisi ya kata ingeratibu zoezi hilo katika eneo lake, kisha kupeleka ngazi za juu hadi ngazi ya taifa.

Zoezi hili siyo tu lingeleta takwimu sahihi zaidi bali pia lingepunguza gharama kubwa ambazo serikali hutumia katika kufanikisha zoezi zima.

Kwa huu utaratibu unaotumika kila baada ya miaka 10 watu wengi huwa wanaachwa bila kuhesabiwa hasa kwenye maeneo magumu kijiografia.

Nadhani miaka ijayo kazi hii ifanywe na mabalozi wa nyumba kumi.

Nawasilisha.
==================================
umeanza kuleta roho mbaya ya kimagufuli acha watu wakapige pesa.
 
Hivi we jamaa unaniandikia mimi risala ndefu namna hii maana yake nini sasa, kwani huwezi ku-summarize hoja zako ukaeleweka, unaleta ngonjera hapa. Anyway, ngoja na mimi nakuandalia essay, tulia hapo hapo, now niko busy.
[emoji23]
 
Hivi we jamaa unaniandikia mimi risala ndefu namna hii maana yake nini sasa, kwani huwezi ku-summarize hoja zako ukaeleweka, unaleta ngonjera hapa. Anyway, ngoja na mimi nakuandalia essay, tulia hapo hapo, now niko busy.
Kabla ya yote, kwani mimi napata faida gani kuandika maelezo mengi? Au nikipuuza nikaacha kujibu maswali yako nitapungukiwa nini?
 
Gharama yake ikitajwa hapa si mtakimbiana ....maana wa Tz tunapenda kulalamika ila hatupendi kujitoa kafara kwa ajili ya maendeleo yetu.....

Itoshe kusema awali hatukuwa na maono ya mbali, tuliamini ile mfugale ndio siluhu ya foleni,

Wakati inajengwa ile tulipaswa tujitafakari, binafsi naona tuli puyanga


Interchange ya Ubungo iligharimu 200 B roughly, Exclude VAT
Siasa ilipoingia kwenye taaluma iliaminisha watu kwamba ikijengwa flyover ya upande mmoja airport kuelekea city center eti foleni zingepungua,wamefanikiwa kupunguza za huko inakoelekea tu,lakini barabara inayotoka ubungo kuepekea bandarini ni kama foleni zimezidi kuliko ilivyokuwa awali.
 
Hivi we jamaa unaniandikia mimi risala ndefu namna hii maana yake nini sasa, kwani huwezi ku-summarize hoja zako ukaeleweka, unaleta ngonjera hapa. Anyway, ngoja na mimi nakuandalia essay, tulia hapo hapo, now niko busy.
Kwani awali nilipokuwa naandika kwa muhtasari kilichokuwa kinakufanya ushindwe kunielewa ni nini? Maswali yako yalijengeka katika misingi eidha ya kutonielewa au kutokujua mambo machache muhimu yahusuyo tasnia ya statistics/demography/population. Baada ya kuona hivyo ilinilazimu kuongeza maelezo ili kujaribu kukujengea uelewa mwepesi kwa kuvigusia vipengele vyote vya muhimu kwenye maswali yako. Hiyo ndo maana iliyo nyuma ya huo uandishi ambayo wewe umeuita risala na ngonjera
 
Hivi we jamaa unaniandikia mimi risala ndefu namna hii maana yake nini sasa, kwani huwezi ku-summarize hoja zako ukaeleweka, unaleta ngonjera hapa. Anyway, ngoja na mimi nakuandalia essay, tulia hapo hapo, now niko busy.
Sawa Mjumbe, nasubiri hiyo imla, ZINGATIA: Ni vema hoja zako zitajikita kwenye fani husika na siyo siasa na maoni hewa yasiyo na msingi egemezi

Kwenye fani ya takwimu kuna kauli mbiu mashuhuri isemayo pasina takwimu/data huna haki ya kuzungumza, kunielewa nilichomaanisha hapo kunalazimu ujue maana ya Statistics "singular/plural"

Fani: Population, Demography, Statistics, Economics, Planning, Tehama
 
Pamoja na nia yako nzuri ya kuokoa fedha tatizo ninaloliona kwa hawa mabalozi ni kwamba kwanza kuna jamii ambazo hawapendi kuhesabiwa hivyo wako tayari wahonge ili iandikwe watoto 2 badala ya 7. Pia kuna issues za wahamiaji haramu mipakani wataingizwa kirahisi na mabalozi kuvuta mpunga.
 
Hivi we jamaa unaniandikia mimi risala ndefu namna hii maana yake nini sasa, kwani huwezi ku-summarize hoja zako ukaeleweka, unaleta ngonjera hapa. Anyway, ngoja na mimi nakuandalia essay, tulia hapo hapo, now niko busy.
Wajibu wako ni kujenga hoja kielimu na si kulazimisha watu wafuate maoni yako hata kama yatakuwa yana tija au hayana. Ni busara kuheshimu maoni ya watu hata kama yatakuwa yanakinzana na yako
 
Sensa naifahamu vizuri, sikatai kwamba ni nyeti, ila wajumbe wa nyumba 10 wanazifahamu zaidi nyumba zao kuliko mtu mwingine yeyote, wanawafahamu vizuri hata watu wanaoishi, na pengine anazo namba za simu za watu wote walio chini ya nyumba zake 10. Ni rahisi zaidi yeye akakaribishwa hata sebuleni, akajaza fomu huku wakicheka na kunywa chai na wenyeji, huku wakipeana story za ugomvi wa khadija na Jesca jana yake, zoezi hili litaenda vizuri sana kwa kutumia wajumbe. We tulia hivyo hivyo, majibu yake mtayapata jumatatu ijayo.

Ingekuwa mimi ndiye nina mamlaka, hizo pesa ningezipiga by 20% ,kisha naenda kuziweka kwanza mahali, halafu 20% nawapa wajumbe wa nyumba 10 , 60% inayobaki ningezipeleke kwenye ujenzi wa ma-flyover jiji kote la Dar.
Ficha ujinga wako.
 
Back
Top Bottom