FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 38,920
- 44,970
- Thread starter
-
- #121
Ni kweli, pale Jangwani Fusi namba ‘A’ ndio zinaongoza kwa kupiga mzigo, gari inasukwa kama imetoka kiwandani, ila kwakuwa ni gari ya kazi, hakuna anaejali kuhusu namba. Shida ipo kwenye hizi za kutembelea, namba ‘A’ ni kama tusi hiviMalori ikifungwa vizuri tandamu namba A wa namba D akasome wajanja kwa sasa hawaagizi magari nje sana.
Kwa hio unalalamikia serikali kushindwa kuuza cresta no A ..ulinunua uuze? Serikali haijakataza choma Moto nunua jingneBadala ya mfumo wa sasa wa ‘TxxxAyy> TxxxByy > TxxxCyy > TxxxDyy , na sasa karibia tunaingia namba ‘E’ , ambapo mtu anakuwa anajua kabisa kwamba gari hii imesajili ya zamani au ni mpya.
Napendekeza namba zinazofuata baada ya kuisha kwa namba ‘D’ ziwe katika mfumo wa ku-‘Randomize’ ambapo panakuwa hakuna mtitiririko maalum katika usajili wa namba za magari, hii itasaidia mtu kuuza gari lake kulingana na hali iliyonayo, na sio kuangalia namba, unakuta gari zuri lina hali nzuri ila linakosa soko kisa ni namba A.
=================================
Watu wengi hununua gari toka Japan ili tu aweze kupata usajili mpya kwenye gari lake, na hivyo tunatumia pesa nyingi mno za kigeni kuagiza magari kama taifa, wakati huo huo kuna gari nyingi nchini zina hali nzuri kuliko hata hizo za kutoka japan (imefungwa engine mpya, gearbox mpya, matairi mapya, body halina accident damage, low mileage); ila linakosa soko kisa ni namba C, au B au A, ila kuna watu wanaagiza mikangafu toka Japan kisa tu itapata usajili mpya.
Hii itatoa fursa ya kuanzishwa kwa ‘Car restoration facilities’ ambazo zinalorudisha gari katika hali ya upya kama ilivyokuwa kiwandani, hata hao Japan ndivyo wanavofanya kiasi wakituuzia mkangafu sisi tunaona kama jipya, hii itatengeneza ajira nyingi sana!!!!
Pia itaokoa fedha nyingi tunazotumia kuagiza magari toka Japan, maana mtu ataona anunue hapa hapa nchini restored car ambayo haitamwaibisha barabarani kwa kuwa na plate number ya zamani...
Yote ni ili uuze mkangafu wako ,, pambanaGood idea, ila pia namba ziwe ‘randomized’ , zisionyeshe mtiririko wa kujua ipi imesajiliwa zamani na ipi imesajiliwa recently.
Shida ni kwa hawa wasio na pesa wanataka wauze ist no C milion 7.5 wakati Kuna DQG 8.3m 😁😁 me nasema wapambane tuKwani lengo halisi za hizo namba ni nini hadi mfikie hatua ya kutaka zisiende kimtiririko?
Soma hoja uielewe ndugu. Japan anatajirika kwa kutuuzia mikangafu, kwanini unajua? Kwa sababu wao magari yao wakiyafanyia restoration (rangi, engine nk.) na kuwa kama moya, hapa nchini zikija zinapewa namba mpya kabisa, zile za zamani za Japan zinabaki hukohuko. Ila ukifanya restoration hapa bongo na kuifanya iwe kama mpya, unalazimika kutumia namba zile zile za zamani, sasa hapo ndipo mtihani ulipo, maana mtu atashindwa kurudishanpesa aliyotumia kwenye restoration kwa sababu namba ya zamani inasababisha kupata bei ndogo kwenye soko, hata kama gari ni mpya na ipo katika hali nzuri sawa na ya kiwandani.Kwa hio unalalamikia serikali kushindwa kuuza cresta no A ..ulinunua uuze? Serikali haijakataza choma Moto nunua jingne
Wewe sasa umenielewa, yaani tuna export ajira kwenda Japan kwa sababu ya kijinga kabisa, hiyo gari yako namba A unaweza ukashindwa kuiza kwa bei nzuri, lakini hiko gari lingekuwa Japan halafu likapigwa rangi na kuservive engine nk, likija hapa bongo likapewa na ‘E’ ya sasa, unauza bei hata mara 10, sasa niambie, sisi ni mataahira au ni wendawazimu, just tell me!Nipo na namba A yangu iliingia 0km miaka hiyo maisha yanaendelea. Sijui nitaiuza lini? Ila nimependa idea ya car restoration. Nadhani mtumba wa Japan uliotumika TZ ukibadilishwa kwa kuwekewa engine mpya, gearbox mpya na ukawa pimped utatengeneza ajira iwapo utakuwa na soko. Na kama unavyosema, soko lipo affected na namba sababu wateja wengi wananunua magari si kwa usafiri tu bali na pride au showoff.
Nimekuelewa boss ila tatizo ukifungua madirisha wanapita hadi nyoka, huu mfumo una loophole nyingi sana za wezi na matapeli but still upo sahihi sababu hatutakiwi kubaki nyuma sababu ya kuwaogopa wezi, bora kubadili fikra.Wewe sasa umenielewa, yaani tuna export ajira kwenda Japan kwa sababu ya kijinga kabisa, hiyo gari yako namba A unaweza ukashindwa kuiza kwa bei nzuri, lakini hiko gari lingekuwa Japan halafu likapigwa rangi na kuservive engine nk, likija hapa bongo likapewa na ‘E’ ya sasa, unauza bei hata mara 10, sasa niambie, sisi ni mataahira au ni wendawazimu, just tell me!
🤣🤣🙌Plate number ni number inayoandikwa kwenye plate, na number plate ni plate inayoandikwa number. Sasa chagua wewe ipi ni sahihi
kwahiyo kila mkoa upewe mamlaka ya kufanya hivyo... tuunde vyombo kama mamlaka zamaji?
Thamani ya jumla ya magari nchini itapanda sana, pia itaondoa unyonge barabarani kwa wale wanaokuwa na namba za zamani, ila gari kafunga engine mpya, gearbox mpya, body halina accident kabisa, tairi mpya, ila mtu unashindwa kuuza kwa bei nzuri, kisa namba ‘C’