Napendekeza mfumo wa ‘Randomizer’ kwenye usajili wa ‘plate number’ za magari nchini

Napendekeza mfumo wa ‘Randomizer’ kwenye usajili wa ‘plate number’ za magari nchini

Mfumo unaoupendekeza una faida kwako wewe unayetaka kuuza gari lako ambalo pengine na wewe ulilinunua kutoka hukohuko Japan.

Baada ya kulitumia kwa muda kadhaa sasa unaona wenzio wanaoagiza magari kutoka Japan wasiagize wanunue lakwako. Ili kufanikisha hilo unatamani hata utaratibu wa plate number ubadilishwe ili ukunufaishe wewe.

Hapa Chief unaonesha kujipendelea wewe zaidi kuliko manufaa ya nchi.

Nadhani serikali inapata mapato makubwa zaidi ya kodi kwa magari yanayoagizwa kutoka nje kuliko kodi za kubadili umiliki kwa kuuziana ndani ya nchi.

Utaratibu huu wa plate number uendelee tu, unasaidia angalau kujua chombo cha moto kina muda gani tangu kisajiliwe nchini bila kijali umekifanyia matengenezo.
Nadhani yote haya nimeshayafafanua kwenye uzi.
 
Mi nina C imekaza na wala sifikirii kuiuza kwa sasa na hata nikitaka uza nitauza bei nayotaka mimi.

Wananchi wengi wananunua gari kwa kuangalia number plate ila mtindo huo hau guarantee mtu kupata gari zuri hata kidogo.
Well said... Nimenunua namba C five yrs ago bado iko bomba sana kuliko wenye namba D walioagiza..
 
Badala ya mfumo wa sasa wa ‘TxxxAyy> TxxxByy > TxxxCyy > TxxxDyy , na sasa karibia tunaingia namba ‘E’ , ambapo mtu anakuwa anajua kabisa kwamba gari hii imesajili ya zamani au ni mpya.

Napendekeza namba zinazofuata baada ya kuisha kwa namba ‘D’ ziwe katika mfumo wa ku-‘Randomize’ ambapo panakuwa hakuna mtitiririko maalum katika usajili wa namba za magari, hii itasaidia mtu kuuza gari lake kulingana na hali iliyonayo, na sio kuangalia namba, unakuta gari zuri lina hali nzuri ila linakosa soko kisa ni namba A.

=================================

Watu wengi hununua gari toka Japan ili tu aweze kupata usajili mpya kwenye gari lake, na hivyo tunatumia pesa nyingi mno za kigeni kuagiza magari kama taifa, wakati huo huo kuna gari nyingi nchini zina hali nzuri kuliko hata hizo za kutoka japan (imefungwa engine mpya, gearbox mpya, matairi mapya, body halina accident damage, low mileage); ila linakosa soko kisa ni namba C, au B au A, ila kuna watu wanaagiza mikangafu toka Japan kisa tu itapata usajili mpya.

Hii itatoa fursa ya kuanzishwa kwa ‘Car restoration facilities’ ambazo zinalorudisha gari katika hali ya upya kama ilivyokuwa kiwandani, hata hao Japan ndivyo wanavofanya kiasi wakituuzia mkangafu sisi tunaona kama jipya, hii itatengeneza ajira nyingi sana!!!!

Pia itaokoa fedha nyingi tunazotumia kuagiza magari toka Japan, maana mtu ataona anunue hapa hapa nchini restored car ambayo haitamwaibisha barabarani kwa kuwa na plate number ya zamani...
Kuna magari TxxxAAA mazima na mwonekano mpya kuliko hayo D jambo kubwa ni service na utunzaji
 
Ndiyo maana sasa hivi hutakiwi kuagiza gari lililokua zaidi ya miaka kumi...
 
Sina uhakika na wanachofanya mataifa mengine yanayofanana na sisi, lakini ninachoona mimi wazo lako litawaongezea matapeli uwanja mpana zaidi wa kupiga pesa za wanunuaji wasiokuwa makini.
Hata Japan, Huwa wanaweka Grade Points, Kama ni Repaired, Normal Used, Accident and etc, wanawekaga kwa mtindo wa 4.5,5.0,3.0,2.0 etc
 
Watu wengi hununua gari toka Japan ili tu aweze kupata usajili mpya kwenye gari lake, na hivyo tunatumia pesa nyingi mno za kigeni kuagiza magari kama taifa, wakati huo huo kuna gari nyingi nchini zina hali nzuri kuliko hata hizo za kutoka japan (imefungwa engine mpya, gearbox mpya, matairi mapya, body halina accident damage, low mileage); ila linakosa soko kisa ni namba C, au B au A, ila kuna watu wanaagiza mikangafu toka Japan kisa tu itapata usajili mpya.

Hii itatoa fursa ya kuanzishwa kwa ‘Car restoration facilities’ ambazo zinalorudisha gari katika hali ya upya kama ilivyokuwa kiwandani, hata hao Japan ndivyo wanavofanya kiasi wakituuzia mkangafu sisi tunaona kama jipya, hii itatengeneza ajira nyingi sana!!!!

Pia itaokoa fedha nyingi tunazotumia kuagiza magari toka Japan, maana mtu ataona anunue hapa hapa nchini restored car ambayo haitamwaibisha barabarani kwa kuwa na plate number ya zamani...
Ile sehemu ya kwanza hapana, acha tu ukweli utawale kama gari ya zamani acha ijulikane kuwa imesajiliwa zamani

Hiyo sehemu ya car restoration hiyo ndo real deal, hapo umepatia sana. Huyo mtengenezaji azitengeneze na azibrandi hivyo kama refurbished car watu watanunua tu.

Sema shida moja inayotukwamisha ni trust, tukiweza kuaminiana na kuweka pembeni utimilizaji wa matakwa binafsi kwa gharama kwa wengine ndio tutatoboa.
 
filii sipichi iko kazini
Ni upumbavu tu mkuu ndio unasumbua baadhi ya watu! Eti gari zuri kuliko hata hilo la kutoka Japan, tunatengeneza gari sisi? Si hata hilo nalo limetoka Japan? Bure kazi hili jamaa!
 
Ni upumbavu tu mkuu ndio unasumbua baadhi ya watu! Eti gari zuri kuliko hata hilo la kutoka Japan, tunatengeneza gari sisi? Si hata hilo nalo limetoka Japan? Bure kazi hili jamaa!
Kwani gari si zinafanyiwa restoration na kuzirudisha kwenye upya karibia sawa na wa kiwandani, kwanini isiwe nzuri kuliko used ya Japana ambayo haijafanyiwa restoration? Legeza ubongo
 
Labda ungetoa ushauri ushuru wa magari upunguzwe gari sio anasa, ant dumping principal ishapitwa na wakati, gari ikichoka inakatwa screpa
 
Plate number ni number inayoandikwa kwenye plate, na number plate ni plate inayoandikwa number. Sasa chagua wewe ipi ni sahihi
Siku zote nasikia "a car with registration number T XYZ 123" hiyo nyingine sijawahi kuisikia kwa kweli.
 
Back
Top Bottom