Napendekeza mfumo wa ‘Randomizer’ kwenye usajili wa ‘plate number’ za magari nchini

Napendekeza mfumo wa ‘Randomizer’ kwenye usajili wa ‘plate number’ za magari nchini

Binafsi napenda sana mfumo huu unaonesha gar n la lini.
Swala la kuuza mie naona hali ya gari ndio ifanya kiuzwe kwa bei gan na si namba japo namba nayo inamchango wake

Mfumo hauoneshi gari ni la lini bali limeingia nchini na kupewa usajili wa wakati fulani...
 
FRANCIS DA DON wazo lako ni zuri lakini inaondoa dhana ya mfumo wa biashara huria...

Ni bidhaa chache ambazo zimewekewa udhibiti wa mamlaka fulani, na bidhaa hizo ni zile zenye maslahi kwa serikali...

Lakini bidhaa kama uuzwaji wa magari, ni sawa tu na mtu anayeuza papai zake toka Maneromango au maembe yake toka Bagamoyo, kila mtu anajipangia bei yake...
 
Sina uhakika na wanachofanya mataifa mengine yanayofanana na sisi, lakini ninachoona mimi wazo lako litawaongezea matapeli uwanja mpana zaidi wa kupiga pesa za wanunuaji wasiokuwa makini.

Tanzania tayari siyo mahali pa kuaminika sana kwa ununuzi wa vitu kama magari sababu ya utapeli unaowezeshwa na misrepresentation of facts. Mfano wanaofanya restoration kwa lengo la kuuza, huipamba gari kwa nje huku wakificha madhaifu ya ndani ili kupata bei nzuri.

Tukiongeza mwanya wa kuficha umri wa gari tutazidi kuongeza matatizo kwenye hii biashara. Ni afadhali mtu awe na taarifa sahihi za anachotaka kununua, zikiwepo zile zinazoonekana wazi pamoja na zile zinazomtaka akasome kwenye documents.
Ngoja nimalizie bia kwanza, au basi, nitakujibu asubuhi
 
Is there any known Car Restoration Facility? Ukiacha hawa Makanjanja wa Makumbusho.
 
Mfumo unaoupendekeza OP, hauna tija kabisa zaidi ya kuwanufaisha Madalali wa Magari.

Nowadays kuna TBS. Ukitamka tu TBS mbele ya Dalali wa Magari utaona uso wake utakavyoChange ghafla.

Tunaelekea mbele na sio nyuma. Think Big. [emoji594]
 
Is there any known Car Restoration Facility? Ukiacha hawa Makanjanja wa Makumbusho.
Nani aanzishe facility kama hiyo ale hasara? , labda waanzishe randomized plate numbers
 
Nani aanzishe facility kama hiyo ale hasara? , labda waanzishe randomized plate numbers
Yaani Jombi wewe na hii inshu ya 'Randomised Number Plates' umeivalia Kibwebwe utadhania ni Katiba Mpya!?

Deep down inside of you, know that nothing good will come out of this.

Wishing you best of luck.
 
Badala ya mfumo wa sasa wa ‘TxxxAyy> TxxxByy > TxxxCyy > TxxxDyy , na sasa karibia tunaingia namba ‘E’ , ambapo mtu anakuwa anajua kabisa kwamba gari hii imesajili ya zamani au ni mpya.

Napendekeza namba zinazofuata baada ya kuisha kwa namba ‘D’ ziwe katika mfumo wa ku-‘Randomize’ ambapo panakuwa hakuna mtitiririko maalum katika usajili wa namba za magari, hii itasaidia mtu kuuza gari lake kulingana na hali iliyonayo, na sio kuangalia namba, unakuta gari zuri lina hali nzuri ila linakosa soko kisa ni namba A.

=================================

Watu wengi hununua gari toka Japan ili tu aweze kupata usajili mpya kwenye gari lake, na hivyo tunatumia pesa nyingi mno za kigeni kuagiza magari kama taifa, wakati huo huo kuna gari nyingi nchini zina hali nzuri kuliko hata hizo za kutoka japan (imefungwa engine mpya, gearbox mpya, matairi mapya, body halina accident damage, low mileage); ila linakosa soko kisa ni namba C, au B au A, ila kuna watu wanaagiza mikangafu toka Japan kisa tu itapata usajili mpya.

Hii itatoa fursa ya kuanzishwa kwa ‘Car restoration facilities’ ambazo zinalorudisha gari katika hali ya upya kama ilivyokuwa kiwandani, hata hao Japan ndivyo wanavofanya kiasi wakituuzia mkangafu sisi tunaona kama jipya, hii itatengeneza ajira nyingi sana!!!!

Pia itaokoa fedha nyingi tunazotumia kuagiza magari toka Japan, maana mtu ataona anunue hapa hapa nchini restored car ambayo haitamwaibisha barabarani kwa kuwa na plate number ya zamani...
Maelezo yamejitosheleza kazi kwa wizara ya fedha kushughulikia hili
 
Binafsi napenda sana mfumo huu unaonesha gar n la lini.
Swala la kuuza mie naona hali ya gari ndio ifanya kiuzwe kwa bei gan na si namba japo namba nayo inamchango wake
Namba E mbona ilishafika mamia. Ilishaanza muda.
 
Mfumo unaoupendekeza una faida kwako wewe unayetaka kuuza gari lako ambalo pengine na wewe ulilinunua kutoka hukohuko Japan.

Baada ya kulitumia kwa muda kadhaa sasa unaona wenzio wanaoagiza magari kutoka Japan wasiagize wanunue lakwako. Ili kufanikisha hilo unatamani hata utaratibu wa plate number ubadilishwe ili ukunufaishe wewe.

Hapa Chief unaonesha kujipendelea wewe zaidi kuliko manufaa ya nchi.

Nadhani serikali inapata mapato makubwa zaidi ya kodi kwa magari yanayoagizwa kutoka nje kuliko kodi za kubadili umiliki kwa kuuziana ndani ya nchi.

Utaratibu huu wa plate number uendelee tu, unasaidia angalau kujua chombo cha moto kina muda gani tangu kisajiliwe nchini bila kijali umekifanyia matengenezo.
 
Back
Top Bottom