Napendekeza serikali iweke kipengele cha cheti cha JKT kwenye matangazo yote ya kazi katika Taasisi za kiserikali na utumishi

Napendekeza serikali iweke kipengele cha cheti cha JKT kwenye matangazo yote ya kazi katika Taasisi za kiserikali na utumishi

JKT ya kulazimishana ilikuwa na mashiko miaka hiyo. Ukishaona mpaka Mbowe anafikiria kuajiri Komandaoo kutoka mitaani wakizagaa kuna haja gani ya kulazimishia JKT kama kigezo cha ajira. Ukitangaza leo wanaotaka kujitokeza kujiunga na JKT si dhani kama serikali inaweza kuwachukua wote ni wengi wa kumwaga. Watu wenye Masters ni nachinga na madereva wa Bajaji nna Ubber kama ulifikiri cheti cha JKT kitaku favour upate ajira serikalini nikujidanganya mnyewe. Utaweza kushindana na wamzinga wa babu? Maana nacho ni kigezo chengine hicho.
 
Napendekeza serikali iweke kipengele cha cheti cha JKT kwenye matangazo yote ya kazi katika Taasisi za kiserikali na utumishi.

Hii italeta maana ya vijana wetu kupitia, mafunzo haya ya JKT. Na italeta hamasa kwa wale ambao hawapendi kwenda kulitumikia Taifa huko JKT.

..JKT ilitakiwa ifutwe kwa vijana wa form 6.

..badala yake waende wachache wanaotaka kujifunza mambo ya ufundi na kilimo.

..nilipomaliza form 6 nilipita JKT na sikufaidika na chochote kile.
 
Kuna jamaa kashauri, anasema ukiwa na mtoto/kijana akimaliza form four mpeleke akasome certificate yoyote alafu umpeleke JKT akapate gamba baada ya hapo asubiri ajira.Alafu akamalizia kusema, eti nyie wa degree tulieni kwanza. Hii nchi ngumu sana. {JOKES}.
 
nimeamini unaweza kuwa mkubwa ila akili huna
 
Napendekeza serikali iweke kipengele cha cheti cha JKT kwenye matangazo yote ya kazi katika Taasisi za kiserikali na utumishi.

Hii italeta maana ya vijana wetu kupitia, mafunzo haya ya JKT. Na italeta hamasa kwa wale ambao hawapendi kwenda kulitumikia Taifa huko JKT.
Hivi unafahamu serikali inachukua F6 wachache Sana kwenda JKT? Kifupi wanaoachwa ni wengi kuliko wanaochaguliwa kwenda JKT. Hivyo suala lako halitakuwa kigezo.
Labda tu kama itachukua F6 wote. Na haitawezekana maana budget ya serikali haitoshi.
 
Naunga mkono hoja!

Waliopitia jkt wapewe kipaumbele kwa sababu,

Mosi, wamefundishwa UVUMILIVU na USTAHIMILIVU wa kuishi maisha ya aina yoyote katika mazingira yoyote. Kwahiyo hata kule vijijini ambako watumishi wanapakimbia wakipelekwa wao kwa mafunzo waliyopata tuna expect watafanya kazi bila shida yoyote!

PILI, itaongeza hamasa kwa vijana kwenda kushiriki mafunzo ya jkt bila kukosa kwa watakaokuwa wamechaguliwa

TATU, itasaidia kumotivate vijana kuwa wazalendo na wenye kulipenda Taifa leo

NNE, vyeti vya jkt wanavyopewa havina matumizi kwahiyo kama kigezo cha mafunzo ya jkt kitazingatiwa basi na vyeti navyo vitakuwa vimepata matumizi kwa Njia hiyo!
 
JKT ifutwe tu maana sioni umuhimu wake. Kuna jipya gani mnafundishwa huko JKT?
Mkitoka huko mnaishia kuwa walinzi tu na kulialia
Kabisaaa yaan, hasa ile kwa mujibu wa sheria (f6) ifutwe tyuuh. Haina maana yeyote lol.
 
Wakitoka huko JKT wanaandamana wanataka waajiriwe.
Ukiuliza wanasema vijana wanatengenezwa wawe wakakamavu, ukiuliza ikoje hiyo
Unaamka asubuhi unatembea kilometa 30 halafu mnarudi, kingine kulima, kingine.....
Ni ujinga umejaa pale hakuna lolote. Dunia ya sasa watu wanataka waishi maisha km ya peponi na siyo kuchoshana kwa kutembea wakati gari zipo.
Kabisaaa yaan, hasa ile kwa mujibu wa sheria (f6) ifutwe tyuuh. Haina maana yeyote lol.
 
Hiyo JKT yenu inawafundisha nini zaidi ya kuwa na roho mbaya?
Mngekuwa mnatoka huko mnafika mnajiajiri hapo ningeona JKT ina maana.
Wanauvumilivu na ustahimilivu? Mtu ambaye hajaenda JKT hawezi kuwa na uvumilivu na ustahimilivu?
Nyie ndiyo mnatusumbua huku mtaani mnakuwa vibaka na wezi.
Huko JKT hakuna mlichofundishwa zaidi ya uvumilivu na ustahimilivu?
JKT inatakiwa ifutwe na isiwepo. Sioni faida ya JKT
Naunga mkono hoja!

Waliopitia jkt wapewe kipaumbele kwa sababu,

Mosi, wamefundishwa UVUMILIVU na USTAHIMILIVU wa kuishi maisha ya aina yoyote katika mazingira yoyote. Kwahiyo hata kule vijijini ambako watumishi wanapakimbia wakipelekwa wao kwa mafunzo waliyopata tuna expect watafanya kazi bila shida yoyote!

PILI, itaongeza hamasa kwa vijana kwenda kushiriki mafunzo ya jkt bila kukosa kwa watakaokuwa wamechaguliwa

TATU, itasaidia kumotivate vijana kuwa wazalendo na wenye kulipenda Taifa leo

NNE, vyeti vya jkt wanavyopewa havina matumizi kwahiyo kama kigezo cha mafunzo ya jkt kitazingatiwa basi na vyeti navyo vitakuwa vimepata matumizi kwa Njia hiyo!
 
Hao mafisadi wote waliofilisi viwanda vya umma,walikuwa ni wahitimu wa JKT,hebu nipe faida ya kuwa na hicho cheti cha JKT,mimi naona kama umekurupuka toka usingizini ukaanza kuandika huo uzi.
 
Kwa vile wewe unacho au sio?
Basi na mimi nasema serikali iajiri tuliopitia shule za seminari maana tumefundishwa maadili sana.
Vipi hapo?
 
Back
Top Bottom