Napendekeza taasisi binafsi ziruhusiwe kufanya uchunguzi katika Cyber Crimes

Napendekeza taasisi binafsi ziruhusiwe kufanya uchunguzi katika Cyber Crimes

Konseli Mkuu Andrew

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2013
Posts
749
Reaction score
875
Serikali kupitia wizara husika inapasa kufanya mabadiliko kidogo katika sheria ya uhalifu wa kimtandao ya mwaka 2015 yaani Cyber Crimes Act , 2015 kwani tangu ilipoanzishwa na kupitishwa na Bunge tarehe 22 .05.2015 polisi ndio wamepewa mamlaka ya kufuatilia uhalifu na uchunguzi juu ya masuala ya kimtandao, hali inayopelekea kuwepo na ulasimu sana hasa linapokuja suala la upelelezi.

Napendekeza pawepo na usajili wa taasisi binafsi zitakazo saidia kufanya uchunguzi kwa baadhi ya mambo ambayo yanaigusa jamaa kila siku, mfano sualla la uwizi wa simu jeshi la polisi limekuwa likichukua muda sana hadi kunamwezesha mwizi wa simu ku-bypass simu husika au kuchange imei box na kupelekea kutoonekana tena hiyo simu.
Unaweza hata peleka taarifa ya simu yako unayotumia ukawaambia imepotea na bila kuchezesha unaweza ambiwa bado mwizi hajaiwasha hivyo uwe na subira itapatikana ili hali unayo mkononi.

Mwisho japo sio kwa umuhimu, kuruhusu taasisi binafsi kufanya uchunguzi au upelelezi kutasaidia kuwaishwa kwa kufanyika maamuzi juu ya kesi zinahusiana na uhalifu wa kimtandao.
 
kinachopelekea polisi kuhusika ni dalili za uhalifu katika tukio la upotevu wa simu.

unaweza track mwenyewe,na ukapambana kuifatilia TCRA mwenyewe,ila kumkamata mtu lazima wahusike polisi,kitu kinachofanya zoezi lote la awali kukosa maana kufanywa nawewe.

TCRA inatoa onyo kwa fundi yeyote anayebadilisha imei no,kifungo na fine milion 15 vinaweza kumhusu,ajabu bado watu wanabadili imei sijajua tatizo ni polisi au TCRA au mafundi??
 
kinachopelekea polisi kuhusika ni dalili za uhalifu katika tukio la upotevu wa simu.

unaweza track mwenyewe,na ukapambana kuifatilia TCRA mwenyewe,ila kumkamata mtu lazima wahusike polisi,kitu kinachofanya zoezi lote la awali kukosa maana kufanywa nawewe.

TCRA inatoa onyo kwa fundi yeyote anayebadilisha imei no,kifungo na fine milion 15 vinaweza kumhusu,ajabu bado watu wanabadili imei sijajua tatizo ni polisi au TCRA au mafundi??
sio kama hawafahamiki hao watu la hasha wanajulikana ila nani atawazuia kufanya huo uhalifu wa kubadilisha imei? uhuni huo unafanyika mchana kweupe huko mijini na kwenye majiji kwa mwamvuli wa ufundi simu
 
kumhusu,ajabu bado watu wanabadili imei sijajua tatizo ni polisi au TCRA au mafundi??
Nchi iko mikononi mwa wahuni hii. Huoni tumesajili laini lkn bado matapeli yanapiga simu za utapeli?

Kaylinda kasajiliwa kuuza vifaa vya kielektroniki lkn kachezesha upatu watu kwa kujitangaza kwenye media mpk kaondoka mwenyewe. Vyombo na mamlaka zote zipo tu.
 
Serikali kupitia wizara husika inapasa kufanya mabadiliko kidogo katika sheria ya uhalifu wa kimtandao ya mwaka 2015 yaani Cyber Crimes Act , 2015 kwani tangu ilipoanzishwa na kupitishwa na Bunge tarehe 22 .05.2015 polisi ndio wamepewa mamlaka ya kufuatilia uhalifu na uchunguzi juu ya masuala ya kimtandao, hali inayopelekea kuwepo na ulasimu sana hasa linapokuja suala la upelelezi.

Napendekeza pawepo na usajili wa taasisi binafsi zitakazo saidia kufanya uchunguzi kwa baadhi ya mambo ambayo yanaigusa jamaa kila siku, mfano sualla la uwizi wa simu jeshi la polisi limekuwa likichukua muda sana hadi kunamwezesha mwizi wa simu ku-bypass simu husika au kuchange imei box na kupelekea kutoonekana tena hiyo simu.
Unaweza hata peleka taarifa ya simu yako unayotumia ukawaambia imepotea na bila kuchezesha unaweza ambiwa bado mwizi hajaiwasha hivyo uwe na subira itapatikana ili hali unayo mkononi.

Mwisho japo sio kwa umuhimu, kuruhusu taasisi binafsi kufanya uchunguzi au upelelezi kutasaidia kuwaishwa kwa kufanyika maamuzi juu ya kesi zinahusiana na uhalifu wa kimtandao.
Huewzii kuruhusu bila uwepo wa sheria inayokutambua na kukupa 'avenue' hiyo. Uchunguzi binafsi una mipaka kwa maslahi ya taifa
 
Huewzii kuruhusu bila uwepo wa sheria inayokutambua na kukupa 'avenue' hiyo. Uchunguzi binafsi una mipaka kwa maslahi ya taifa

Hapo ndio tatizo lilipo. Inafahamika mambo mengi yanafanywa na serikali kwa ufanisi duni, ndio maana mambo mengi ya serikali ni ya mlolongo kuliko ufanisi. Ni mambo machache sana yanayofanywa na serikal kwa ufanisi, kitu ambacho serikali inafanya kwa ufanisi ni kukomoa.

Mambo mengi ya sekta binafsi yanafanyika kwa ufanisi na kwa wakati. Mifano mirahisi, upande wa mawasiliano, kampuni za binafsi kama Voda com, Tigo nk zina ufanisi na kwa wakati tena nchi nzima kuliko TTCL. Upande wa elimu, elimu ya binafsi inatolewa kwa ubora na mazingira mazuri kuliko kwenye elimu inayotolewa na serikali. Upande wa afya hali kadhalika.

Hebu tazama hilo suala la vitambulisho vya taifa, ingekuwa ni kampuni binafsi kila anayepaswa kupata kitambulisho angeshapata. Njoo kwenye upande wa umeme. TANESCO haina mshindani lakini huduma mbovu. Ila utashangaa huduma ya ugavi wa umeme yakipewa makampuni binafsi yatafanya vizuri, na TANESCO itabaki hoi kama ilivyo TTCL.
 
Mimi katika mapendekezo yangu niliwahi kupendekeza kuwa polisi wapewe muda maalum wa kufanya uchunguzi miezi mitatu mpaka sita. Ikitokea uchunguzi haujakamilika zipewe kampuni binafsi za uchaguzi, na kampuni hizo binafsi zikifanikisha uchunguzi, fedha watakazodai zikatwe toka kwenye mshahara wa jeshi la polisi. Kwa vyovyote polisi wakishaona mishahara yao inaanza kupungua watafanya kazi kwa weledi.
 
Back
Top Bottom