Napinga hoja ya RC Makalla ya kulazimisha Mabasi yote ya Mikoani kupakia na kushusha abiria Stendi ya Magufuli pekee

Napinga hoja ya RC Makalla ya kulazimisha Mabasi yote ya Mikoani kupakia na kushusha abiria Stendi ya Magufuli pekee

Mimi kinachonisikitisha ni kukosa viongozi wanaoweza kuja na plan za miaka angalau 50 mbele... mbona kina Mwalimu Nyerere waliweza kuweka mipango inayoishi hadi leo? Ukiangalia kituo cha Ubungo hakina miaka mingi tayari kimebomolewa. Hata hiyo ya Magufuli usishangae baada ya miaka mitano ikabomolewa na kuhamishwa tena. Kuhusu aliyoamrisha Makala ni upuuzi kama upuuzi mwingine. Sio lazima mabasi yarundikwe sehemu moja. Labda wangejenga stendi angalau nne jijini Dsm ili kwenda sawa na uhitaji. Hao mama ntilie wangetafutiwa utaratibu mzuri wa kuongeza thamani za biashara zao ingevutia hata wasafiri wasiopenda kula njiani kununua vyakula vyao. Huwezi kunilazimisha kula kwa mama ntilie ambaye uchafu ni mojawapo ya sifa ya yeye kuwa mama ntilie.
Kama kuna fani inadharauliwa ni ya mipango miji. Wao wanaonekana kuwa kazi yao kubwa ni kugawa viwanja tu. Walitakiwa saa hizi wawe wanatayarisha mazingira ya mji utakavyokuwa miaka 50 ijayo. Mipango hiyo inatakiwa iwasilishwe kwa wananchi ili wachangie mawazo na mawazo yao yatiliwe maanani. Mipango inayotarishwa sasa hivi ni academic na baada ya kupokelewa inatupwa kabatini na wana siasa wanafanya wanavyotaka. Mfano ni Dodoma. Mpango Mji wa awali umesahaulika bila wananchi kupewa sababu za kuuacha.

Amandla...
 
Hata stendi ya mabasi ya Mwanza kipindi inatolewa city center kupelekwa Nyegezi kulikuwepo hoja hizi hizi.

Leo hii Nyegezi siyo nje ya mji tena na uanzishwaji wa utitiri wa routes za daladala zimeifanya stand iwe kama IPO city center tu.

Miji "hupanuliwa" wa staili hiyo.

Labda hoja Ingekuwa uwepo wa miundombinu ya ku-accomodate watu wote watakaotumia be stendi hiyo
 
Jiwe alikuwa anaamini zaidi katika ku consolidate mambo kuliko kawaida.
Tatizo ni kudharau fani za wengine na wenye fani hizo kukubali kuburuzwa tu. Hauwezi kuzungumzia stendi ya mabasi nje ya mipango miji. Stendi za mabasi ili ziwe viable zinahitaji kuwa pia kivutio cha biashara za kawaida na ziwe rahisi kufikiwa na usafiri wa kawaida. Ndio maana, tofauti na sisi tunavyofikiri, Intercity Bus Terminals nyingi ziko katikati ya miji ( Port Authority New York, Stockholm,Centraal Amsterdam ZOB Berlin n.k.) na kama iko pembezoni basi inafikika kirahisi sana na usafiri wa mjini kutoka sehemu nyingine za mji ( underground, treni, mabasi ya mjini n.k.). Aidha, hamna dhambi kuwa na intercity bus terminals zaidi yamoja ili mradi nazo pia zinafikika kirahisi kwa usafiri wa kawaida wa mjini ( dala dala, uber, boda boda n.k.).

Badala ya kukimbilia ku consolidate shughuli zote kwenye kituo hicho, angezungumzia namna gani mwendo kasi ingeweza kuunganisha kituo hiki na vituo vya Shekilago na Tandika. Aidha, vituo hivi viunganishwe na vituo vya treni, bandari na airport. Uamuzi wa kujenga intercity bus terminal unahitaji umakini mkubwa na sio wa kuangaliwa in isolation. Tunarudia makosa yale yale tunayoyafanya katika ujenzi wa masoko mjini.

Amandla...
 
Hata stendi ya mabasi ya Mwanza kipindi inatolewa city center kupelekwa Nyegezi kulikuwepo hoja hizi hizi.

Leo hii Nyegezi siyo nje ya mji tena na uanzishwaji wa utitiri wa routes za daladala zimeifanya stand iwe kama IPO city center tu.

Miji "hupanuliwa" wa staili hiyo.

Labda hoja Ingekuwa uwepo wa miundombinu ya ku-accomodate watu wote watakaotumia be stendi hiyo
Huu ni mfano mzuri. Shida ni kuwa watu walisumbuka sana kabla ya mji kupanuka kufika Nyegezi. hapakuwa na haja hiyo. Wangetenga eneo la kutosha kwanza, kufanya kituo cha kupitia (transit) na pale mji unapofika ndio inageuzwa kuwa terminal yenye nafasi ya kutosha tu. Sitashangaa kusikia kuwa tayari kituo kipya kimeisha elemewa wakati vingekuwa viwili shida isingekuwa kubwa kiasi hicho.

Amandla...
 
Naunga mkono hoja. Baadhi ta wenye mabasi wenye stendi zao pale Sinza Shekilango kama Kilimanjaro, Dar Lux, Marangu Coach na mengine, wenye mabasi zaidi ya moja kwa route ya Moshi Arusha, njia rahisi kwao ni route ya Bagamoyo Msata, na sio njia ya Chalinze, kuwalazimisha lazima waanzie Stendi mpya ni kuwatesa tuu bure abiria, after all, wengi wa abiria wa mabasi hayo, haswa wale abiria wa 1st Class, sio wa type ya kununua vitu kwa machinga au kula kwa Mama Ntilie!. Hivyo kama nia ni kuwasaidia Machinga na mama ntilie, then, hizo ni sababu alizotoa Mkuu wa Mkoa ni sababu za kijinga sana!.

Hatuwezi kuendelea kuendesha nchi kijinga jinga hivi halafu utegemee tutapata mafanikio. Il tuendelee , la kupata maendeleo ya kweli de must stop such nonsense!.

p
Aisee! Mkuu P, naona umerejea kwenye u bora wako sasa.
 
Hii kero pia iende kwa mikoa mingine mfano Iringa na Dodoma. Pale iringa stend kuu iko karibu kilometer 20 kutoka iringa mjini na mabasi yanalazimishwa kushusha abiria wote stend kisha yanaenda mjini yakiwa tupu na abiria wanalazimika kupanda dala dala kwenda mjini huko huko ambako mabasi yanaenda.
 
Ni rahisi sana. Jiografia ya kuingia Dar es Salaam imegawanyika katika sehemu kuu tatu.

Moja ni njia inayotoka Kusini ambayo sehemu kubwa inaisha Mtwara.

Pili ni Njia inayotokea Moro ambayo hapo Moro inagawanyika kuelekea Nyanda za juu kusini katika mikoa ya Mbeya,Ruvuma, nchi za Zambia, Malawi n.k na nyingine kuelekea Dodoma.

Tatu ni kutokea Kaskazini ambayo sasa Barabara ya Bagamoyo inatumika kwa kiasi kikubwa.

Kituo cha mabasi cha Magufuli kinawafaa zaidi watu wa njia ya pili kutokea Moro na kidogo wa njia ya tatu kutokea Kaskazini ila hakina tija kubwa kwa watu wanaotokea Kusini

Watu wanaotokea kusini walipaswa wawe na Stendi yao kubwa Mbagala, watu wa kutokea Kaskazini walipaswa wawe na stendi yao kubwa Bunju na magari yao yaishie huko.

Magari yanayotokea Kusini yanashusha robo tatu ya abiria wake Mbagala/Temeke, Magari yanayotokea Moro yanashusha robo tatu ya abiria stendi ya Magufuli magari yanayotokea Kaskazini yanashusha robo tatu ya abiria wake Kuanzia Kibaha/Kimara/Bunju/Tegeta.
Ukiwa na vituo vitatu vikubwa unaondoa hizi kelele za sasa hivi na unapunguza foleni za mrundikano wa mabasi makubwa katikati ya mji.
Kongole mkuu [emoji122][emoji122]
 
Suluhisho lilipaswa kwa serikali, wamiliki wa mabasi, wawakilishi wa abiria na wadau wengine kukaa chini kuzungumza kiuhalisia na kuafikiana, kisha wataalamu wakae chini ili kuja na mapendekezo mahususi kwa mamlaka husika.
 
Hii kero pia iende kwa mikoa mingine mfano Iringa na Dodoma. Pale iringa stend kuu iko karibu kilometer 20 kutoka iringa mjini na mabasi yanalazimishwa kushusha abiria wote stend kisha yanaenda mjini yakiwa tupu na abiria wanalazimika kupanda dala dala kwenda mjini huko huko ambako mabasi yanaenda.
Sasa hii ni akili au tope yaani bus inakwenda mjini tupu wakati huo huo Kuna abiria wanakwenda mjini pia[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kinachotakiwa ni kampuni za usafirishaji kuanzisha shuttle bus kwaajili ya kukusanya abiria wake maeneo husika kama vile shekilango lakini mabasi yanatakiwa kuanzia na kumalizia safari kwenye stendi kuu “Terminal” hivi ndivyo hata majiji yaliyoendelea yalivyopangwa.
Hata Malaori kuingia mpaka ndani ya mji au bandarini ni udhaifu wa watu wa mipango miji.Reli ilitakiwa itumike kutoa mizigo bandarini mpaka kwenye ICD zilizopo nje ya mji.
 
Suluhisho lilipaswa kwa serikali, wamiliki wa mabasi, wawakilishi wa abiria na wadau wengine kukaa chini kuzungumza kiuhalisia na kuafikiana, kisha wataalamu wakae chini ili kuja na mapendekezo mahususi kwa mamlaka husika.
Tatizo la Tanzania ni hili , Mtu anapokuwa kiongozi ghafla anabadilika na kuwa mwenye akili kuliko yeyote yule
 
Kinachotakiwa ni kampuni za usafirishaji kuanzisha shuttle bus kwaajili ya kukusanya abiria wake maeneo husika kama vile shekilango lakini mabasi yanatakiwa kuanzia na kumalizia safari kwenye stendi kuu “Terminal” hivi ndivyo hata majiji yaliyoendelea yalivyopangwa.
Hata Malaori kuingia mpaka ndani ya mji au bandarini ni udhaifu wa watu wa mipango miji.Reli ilitakiwa itumike kutoa mizigo bandarini mpaka kwenye ICD zilizopo nje ya mji.

Hii itafungua hata biashara za motels na lodges .
 
Jiwe alikuwa anaamini zaidi katika ku consolidate mambo kuliko kawaida.

Nadhani zaidi alikuwa haamini katika Planning. Aliona ni kupoteza muda na ni njia ya kuiba pesa. K.m. mradi wa bwawa la Nyerere unafanyika bila tafiti za kutosha za awali kuhusua challenges zilizoainishwa katika taarifa za kimazingira n.k. za awali ambazo zilifanya wenzie kusita kuendelea nao. Hakuwa sahihi katika hili.

Amandla...
 
Jiwe alikuwa anaamini serikali inajua na inaweza kila kitu
Suluhisho lilipaswa kwa serikali, wamiliki wa mabasi, wawakilishi wa abiria na wadau wengine kukaa chini kuzungumza kiuhalisia na kuafikiana, kisha wataalamu wakae chini ili kuja na mapendekezo mahususi kwa mamlaka husika.
 
Naunga mkono hoja. Baadhi ta wenye mabasi wenye stendi zao pale Sinza Shekilango kama Kilimanjaro, Dar Lux, Marangu Coach na mengine, wenye mabasi zaidi ya moja kwa route ya Moshi Arusha, njia rahisi kwao ni route ya Bagamoyo Msata, na sio njia ya Chalinze, kuwalazimisha lazima waanzie Stendi mpya ni kuwatesa tuu bure abiria, after all, wengi wa abiria wa mabasi hayo, haswa wale abiria wa 1st Class, sio wa type ya kununua vitu kwa machinga au kula kwa Mama Ntilie!. Hivyo kama nia ni kuwasaidia Machinga na mama ntilie, then, hizo ni sababu alizotoa Mkuu wa Mkoa ni sababu za kijinga sana!.

Hatuwezi kuendelea kuendesha nchi kijinga jinga hivi halafu utegemee tutapata mafanikio. Il tuendelee , la kupata maendeleo ya kweli de must stop such nonsense!.

p
Pamoja Sana mkuu
 
Naunga mkono hoja. Baadhi ta wenye mabasi wenye stendi zao pale Sinza Shekilango kama Kilimanjaro, Dar Lux, Marangu Coach na mengine, wenye mabasi zaidi ya moja kwa route ya Moshi Arusha, njia rahisi kwao ni route ya Bagamoyo Msata, na sio njia ya Chalinze, kuwalazimisha lazima waanzie Stendi mpya ni kuwatesa tuu bure abiria, after all, wengi wa abiria wa mabasi hayo, haswa wale abiria wa 1st Class, sio wa type ya kununua vitu kwa machinga au kula kwa Mama Ntilie!. Hivyo kama nia ni kuwasaidia Machinga na mama ntilie, then, hizo ni sababu alizotoa Mkuu wa Mkoa ni sababu za kijinga sana!.

Hatuwezi kuendelea kuendesha nchi kijinga jinga hivi halafu utegemee tutapata mafanikio. Il tuendelee , la kupata maendeleo ya kweli de must stop such nonsense!.

p
Duh!! Ni wewe kweli? Mbona lugha kali sana umetumia kama mwandishi mwandamizi?

Ni kweli kauli ya mkuu wa mkoa haikubaliki kisiasa, kijamii, kiusalama, kiafya na kiuchumi, lakini michang ya maoni na ushauri iwe ni ya kistaarabu kwa nia ya kujenga. Mkuu huyo wa mkoa walimleta hapo Dar kwa kuwa kuna 'elites' walimtaka kwa kuwa anaweza kunyumbulika watakavyo kwa manufaa yao, lakini ukweli hauwezi mkoa huo kwa vyovyote na matokeo mtaanza kuyashuhudia kadri siku zinavyosogea.

The only solution is to agree in common that Magufuli Bus Terminal is retained where it is and to prevail its intended purposes as an iconic central surface land transportation hub to both upcountry and across the borders (Ugana, Congo, Zambia, Kenya, Malawi, Zimbabwe, Rwanda, Msumbiji, South Sudan and Burundi).

However, the infrastructure feeding the bus terminal is not convenient and friendly.. therefore as the construction continues at Mbezi Louis, the transporters have to be permitted to do what is beneficial to the passengers, bus owners, and government on the other hand on revenue collection through a well-streamlined plan.

Meanwhile, the government of the United of Tanzania is solemnly requested to process for the new backup bus terminals built at Tegeta/Boko or Bunju and Mbagala to consistently provide quality services to the passengers as diversified significant stakeholders for the economic generation by the investors in the transport sectors and common citizens with small business operations.
 
Stand ya kimataifa wakati wateja wako na utaratibu siyo wakimataifa.
Tuna safari ndefu.
Hilo Jjji lilitakiwa liwe na stand kuu 3 kwa jiografia yake.
1.Mbagala
2.Mbezi
3.Tegeta/kawe
Basi likipita stand kuu mojawapo ndipo lielekee kwenye ofisi yake

Hungesikia matamko ya ajabu yasiyomsaidia msafiri
 
Ni sawa na uwanja wa ndege, ambako ukitaka kusafiri, kama unatokea Kawe, ni lazima utafute usafiri wa kukufikisha JKNIA,
Usifananishe usafiri wa anga na ardhini ni vitu viwili tofauti, utaratibu huu wa Makalla utakua ni usumbufu kwa baadhi ya abiria wanaotokea ktkt ya mji kesi za kuchelewa usafiri zitakua nyingi kutokana na foleni
 
Amos Makalla ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mfadhili wa zamani wa bendi ya FM ACADEMIA ya Kinondoni , bila kufanya utafiti wowote ule leo ametoa amri ya kulazimisha mabasi yote ya mikoani kuanzia safari zao kwenye kituo kikuu cha mabasi ya mikoani cha Mbezi Luis , kinachoitwa kituo cha mabasi cha Magufuli na kushushia abiria wake hapohapo .

Lengo kuu la kauli yake hii ni kujaribu kukusanya watu ili kuneemesha wafanyabiashara waliojazana kwenye stendi hiyo bila mpangilio wowote , Makalla anaamini kwamba abiria wote wakishushwa ama kuanzia safari zao hapo basi watanunua bidhaa za wamachinga waliojazana hapo , hivi ndivyo akili yake ilivyomtuma , kwamba abiria wakomeshwe ili kufurahisha wafanyabiashara , Amesahau kwamba abiria ni bora kuliko wamachinga kwenye mustakabhali wa Safari , hata hivyo sikubaliani naye .

Mbezi Luis eneo ilikojengwa Stendi ya Mabasi ya Mikoani ni nje kabisa ya jiji la DSM , kulazimisha Mabasi yaliyokuwa yanaanzia safari zake Mbagala , Tandika au Kigamboni kuacha kazi hiyo na kulazimisha sasa lazima yote yaanzie Nje ya jiji ni sawa na unyama , kwamba sasa aliyekuwa anapandia basi Mbagala akodi teksi kwa zaidi ya gharama ya tsh elfu 30 ili kulifuata basi Mbezi Luis , kwa vile tu Amos Makalla kajisikia hivyo haikubaliki na ni lazima ipingwe kwa nguvu zote .

Alichotakiwa kufanya Mh RC ni kuhakikisha kwamba basi lolote kutoka kwenye yard yoyote ile binafsi linakoanzia safari lisiondoke DSM bila ya kupita Stendi kuu ama lishushe litakako ila ni lazima lije stendi kuu , Vinginevyo Mh Makalla atamke hadharami Maslahi yake binafsi atakayopata kwa kuwatesa abiria wa Kigamboni , Vikindu , Chamanzi , Mbagala , Tandika na kwingineko waliokuwa wanapata ahueni ya kuanzia safari kwenye maeneo yao ya karibu .

Naomba kuwasilisha .
Kiukweli hata mimi nimemshangaa sana huyu jamaa lakini ikiwa amaeshindwa kuwapanga vizuri watu wanaofanya biashara kiholela nje ya ofisi yake mweneyewe hawezi kua na mpango mzuri kwa mkoa mzima.

Kwanza anachoshindwa kuelewa makala ni kua ile stendi haitoshi kwa mabasi yote kuingia mle tofauti na iliyvyokua ubungo,Pili logistic za Mbezi ni tofauti na Ubungo kabisa hivyo kwa abiria kulazimishwa kushuka mbezi wakati basi linakuja mjini ni kulazimisha watu kuteseka bila sababu na kama kiongozi wa umma alipaswa kuwatazama abiria sio kama kipato cha mamantilie au machinga walijazana pale.

Sijui kwanini viongozi wetu wa sasa kila maamuzi wanayofanya yanawaumiza wananchi.Tumsihi mkuu wa mkoa kuupanga kwanza mji vizuri mbezi yenyewe haina hata accomodation za kutosha kwa abiria wanaoingia usiku sana.
 
Lazima niseme, hii ni ngumu mkuu Erythro.

Pamoja na pendekezo lako la mabasi hayo lazima yapitie Stendi kuu, bado naona Makalla yumo ndani ya mstari, hata kama yeye atakuwa na msukumo wa maslahi tofauti na matakwa ya mabasi hayo kuanzia na kuishia stendi kuu.

Stendi kuwa mbali na mjini siyo hoja, kwa sababu stendi kuu ni lazima ihudumiwe na usafiri toka sehemu zote za mji, kwa hiyo hiyo ni fursa kwa wenye biashara zao za usafirishaji mjini.

Ni sawa na uwanja wa ndege, ambako ukitaka kusafiri, kama unatokea Kawe, ni lazima utafute usafiri wa kukufikisha JKNIA, na hivyo hivyo, kama unaingia, utapata usafiri toka hapo kukupeleka Kawe.

Mimi naona la msingi zaidi ni Makala kuhakikisha sehemu zote za mji wake zipo huduma za kuwafikisha wananchi Stendi kuu ya mabasi, Mbezi Luis.

Lakini pia inabidi niulize swali hapa: kuna ubaya wowote kwa mfano kuwepo kwa vituo kadhaa vya mabasi mjini Dar, kwa mfano kituo cha mabasi yanayoelekea kusini mwa nchi kikawepo Mbagala; kituo cha mabasi yaendayo Nyanda za juu yakaanzia, tuseme Gongo La Mboto, n'k.?

Vipi, mbona hujachangamkia fursa ya Hotel/Guest maeneo hayo mkuu Erythrocyte!
kwa hiyo sasa yale mabasi ya abiria wa mikoa ya Lindi na mtwara sasa waje kushukia mbezi ili kutoa fursa kwa daladala.
 
Back
Top Bottom