Napinga kabisa dhana ya "Mume ni Provider" katika ndoa

Napinga kabisa dhana ya "Mume ni Provider" katika ndoa

Naona kila dalili kuwa ndoa yetu yataishia katika migogoro mizito,

Kwani umeshaanza vijineno vya kashfa!

Naona neno kushirikiana limekukwaza Evelyn Salt

Acha niendelee kutafuta anayeelewa umuhimu wake wa kushiriki kikamilifu katika kujenga familia ya pamoja



Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Haunitaki tena? Mbona nkua nshaanza kukupenda
 
Wanandoa punguzeni uchoyo, ubinafsi na uvivu muone kama hamjaishi kwa amani, ama lah mjiunge na Ney wa mitego.... kupanga ni kuchagua.

Hiki ulichoandika ndio maudhui ya andiko langu

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwa nini ukamtwae nyumbani mwa wazazi wake, kama huwezi ama hutaki kumtunza?

Kwao alikuwa anakula na kuvishwa vizuri hadi siku ulivyomtia maneno maneno yako ya ushawishi hadi akakubali kuishi na wewe.

Mwanaume anayekwepa majukumu yake, hana sifa za kuitwa mwanaume. Shame on you!
Ahudumiwe yeye ni mlemavu wa mwili au akili!! Kwa wazazi wake mwanamke alikuwa akilima, akichunga mbuzi, akienda mtoni kuteka maji, kuuza mazao yanayozalishwa,
 
Hii dhana inatumiwa kama kigezo cha kujustify ukahaba (prostitution) kwa waliolewa, utasikia "mume hanipi hela ndiyo maana najiuza" wenyewe wanaita kudanga au kula vichwa. Wakati tangu enzi za babu zetu wanawake walikuwa wakifanya kazi nyingi za kuzalisha na kukuza uchumi wa familia. Hii dhana ya wanawake kuhudumiwa kama watoto wachanga au walemavu wa akili au malkia wa mchwa, nia yake ni kuwafanya wanaume mabwege na kujistify prostitution tu. Kahaba ni kahaba tu hata umhudumie vipi, kuna wanawake waume matajiri wanawapa hela na huduma zote ila wanatumia hela hizo hizo kuhonga bodaboda na ving'asti (gigillos/Male prostitutes) wazini nao.
 
Hii dhana inatumiwa kama kigezo cha kujustify ukahaba (prostitution) kwa waliolewa, utasikia "mume hanipi hela ndiyo maana najiuza" wenyewe wanaita kudanga au kula vichwa. Wakati tangu enzi za babu zetu wanawake walikuwa wakifanya kazi nyingi za kuzalisha na kukuza uchumi wa familia. Hii dhana ya wanawake kuhudumiwa kama watoto wachanga au walemavu wa akili au malkia wa mchwa, nia yake ni kuwafanya wanaume mabwege na kujistify prostitution tu. Kahaba ni kahaba tu hata umhudumie vipi, kuna wanawake waume matajiri wanawapa hela na huduma zote ila wanatumia hela hizo hizo kuhonga bodaboda na ving'asti (gigillos/Male prostitutes) wazini nao.
Yes, haya madini!
Na wazee zamani waliwachagulia vijana wa kiume mabinti wa kuwaoa!
Sifa kuu za binti Bora wa ndoa zamani zile ni heshima na bidii ya kazi,

Binti mvivu hakupata soko la kuolewa!

Wazazi wenye mabinti walijitahidi kuwafundisha heshima na bidii ya kazi ili binti auzike

Mwanamke ni mwajibikaji wa moja kwa moja wa familia yake

Hapa tutofautishe na mahusiano na kahaba ambapo Mwanaume anawajibika kugharamia kila kitu
Bahati mbaya mentality ya Mahusiano ya kikahaba yanaletwa kwenye ndoa!

Mwanamke awajibike vile alivyo

Kama Ni mama wa nyumbani atawajibika kwa kazi za msingi za ndani

Kama mfanya kazi au biashara, basi kipato chake kinapaswa kuja kuongeza nguvu ya familia
Siku hizi, waume wengi wanapambana kuwafungulia miradi wake zao. Yes, hio ni namna ya kumfanya mke awajibike katika kujenga familia.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Ahudumiwe yeye ni mlemavu wa mwili au akili!! Kwa wazazi wake mwanamke alikuwa akilima, akichunga mbuzi, akienda mtoni kuteka maji, kuuza mazao yanayozalishwa,
Kama hujui mantiki ya mume kumhudumia mkewe au mke kuitunza familia yake (akiwemo mumewe), kila mmoja akitekeleza wajibu wake, sidhani kama hata maana ya familia unaijua wewe.

Hakika bado tuna safari ndefu kama taifa, iwapo watu sampuli yako wangalipo.
 
Kuna 50/50 ya aina mbili.

Traditional 50/50

Mama anafanya kazi (akipenda, na hela ni ya matumizi anayotaka) na mara nyingi si kazi nzito, akili yake inakuwa kwenye kutunza mume na watoto watakaojaliwa huku mwanaume akihudumia familia kila kitu.

50/50 modern imbalanced (napenda kuiita 70/30)

Hii wote mnafanya kazi na kuleta hela nyumbani.
Ila mwanamke bado anafanya kazi ya kubeba mimba, kuzaa kwa uchungu, kulea, kupika na kulipia watoto Ada, kodi n.k (70%)

Mwanaume akichangia mbegu na pesa kwa jinsi awezavyo pekee (30%)

Wewe unataka 50/50 ipi?

Kwa mwanamke kubeba mimba na kuzaa, kisha kulea , tayari anaanza na 50% ya mchango wake kwa familia, hivyo ungependa aongeze ngapi kusaidia zaidi?
 
Babu yako ulimtoa kwenye kundi?
Baba yako ulimtoa kwenye kundi?
Hao wote si walisaidiana na wenza wao kujenga familia?

Mbona unakomment Kama Jambo nililoongea ni jipya machoni mwako?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
1. Babu yangu was a real man, alikuwa na watoto 12 na alibeba majukumu ya kumtunza bibi na baba zangu na mashangazi. ndio maana na babangu kawa real man.

2. Babangu alikuwa real man, alikuwa na watoto 8, wote alitutunza na alibeba majukumu yote kama provider kwa mama na kwetu na akanisomesha pia.

3. Mimi ni real man, nina watoto 6, mke wangu namtunza na nafurahia ninavyokuwa provider, watoto pia. in reality, mke wangu akiwa na hela huwa sihesabu sana kama yetu, mimi ndiye provider hiyo ya kwake, najiona kidume zaidi anapotumia pesa zangu na mimi natafuta kwa bidii kwaajili yake na watoto.


4. wewe inawezekana sio real man, ndio maana unakwepa majukumu, unataka kulelewa na wanawake. Mwanaume halisi hayupo hivyo. badilika.
 
Ndio, napinga!,

Ni dhana ya uongo na inakiuka kabisa asili ya maisha ya ndoa!

Ndoa ni muunganiko wa mtu mume na mtu mke na kuzaa watoto kisha kuwatunza. Jumuia hii ya familia inahitaji mahitaji mbalimbali ya maisha kwa maendeleo yake.

Kuna watu wachache wanaibuka hapa bila hata chembe ya aibu na kutaka kuuaminisha umma kuwa mtu mume yampasa kutafuta mahitaji ya familia but mtu mke pamoja na watoto hawawajibiki.

Wanaume wanapolalamika kwamba wanawake kwenye ndoa wanapenda kuhudumiwa zaidi kuliko kuhudumia, wanaibuka watu hawa na vicomment vyao eti ni jukumu la mume kuprovide, na hiari ya mke kuprovide! Salaleee!

Najaribu kujiuliza hii dhana wanaitoa wapi? Ni taasisi gani imefundisha hivi? Au ni ubunifu katika fikra zao?

Katika Ukristo haipo sijui kule kwa wenzetu!

Kwa Wakristo ipo wazi;

"Zaeni mkaongezeke, mkaijaze dunia na kuimiliki"

Kauli ya Mungu kwa mume na mke ikiashiria ushirikiano wa pamoja katika kuijenga familia na dunia kwa ujumla.

"Si vema mwanaume awe pekeyake, nitamfanyia msaidizi wake"

Kauli ya Mungu ikiashiria matakwa yake ya mke kuwa msaidizi kwa mume. Then why mume awe provider bila kusaidiwa?

"Mume na mke watawaacha wazazi na kuungana na kuwa mwili mmoja"

Kauli ya Mwana wa Mungu ikiashiria ndoa ni mshikamano kwa raha na shida hadi kifo kiwatenganishe.

Then mshikamano gani huo wa mmoja kuprovide?

"Mwanamke amtii mumewe na mwanaume ampende mkewe"

Kauli ya mtume wa Mwana wa Mungu ikiashiria kuwa mwanamke awe tayari kutumika kwa hali na mali mbele ya mumewe.

Maisha halisi ya mwanadamu tangu kale yapo wazi. Mwanaume na mwanamke wamefanya kazi pamoja kwa ajili ya maisha yao.

Tangia enzi za Adam na Eva, enzi za manabii, enzi za Yesu Kristo, nyakati za mitume, nyakati za mwanzo za kanisa Katoliki, nyakati za mtume Mohammed hadi leo, mume na mke wameshirikiana katika kazi.

Wamelima pamoja, wamefuga pamoja.

Mume alivua samaki na mke aliwapika wakala,

Mume alitengeneza visu na mke alitengeneza vyungu na makapu wakauza na kupata riziki ya maisha yao.

Hayo yote yalifanyika kwa maelfu ya miaka iliyopita!

Vipi wewe leo kisa una kijikampuni chako unapata fedha, eti unaanza kuleta propaganda kuwa mahitaji ya familia ni jukumu la mume!

Ikumbukwe dunia imebadilika.

Kwa sasa uchumi hauna mwenyewe tena.

Mwanaume au mwanamke aweza kuhodhi uchumi mkubwa.

Leo hii mke aweza kuwa waziri au raisi na akapata mamilioni ya fedha.

Je, hayo mamilioni ya fedha apeleke wapi iwapo hapaswi kuprovide na kujenga familia yake?

Leo una mshahara mnono au kampuni inakupa fedha nyingi halafu unahisi unaweza kuhudumia familia kwa 100%, then unaanza kuwatukana waume wenzako kuwa hawatakiwi kushirikiana na mke katika kuhudumia familia.

What if mtu kama JPM anakufukuza kazi au anaifilisi kampuni yako, yule mke wako afisa maendeleo ya jamii pale Halmashauri asihudumie familia yenu?

Unajua wakati mwingine watu wakiwa na pesa, pesa zinawalevya na wanaongea vyovyote!

Hii dhana ya wanawake kupenda kuhudumiwa tu bila kuwajibika hata kama uwezo wanao ni dhana mpya! Na imejengwa na waume wenye fedha pale wanapowarubuni kwa kuwaambia, "We mtoto mzuri hautakiwi kupata shida, wakati mwanaume nipo kwa ajili yako, nitakuhudumia chochote utakacho!"

Kauli hizi zimewaharibu wanawake wengi sana.

Mabibi na mabibi zao tangu kale hawakujua huu ujinga. Wao walijua kuolewa ni kazi! Kuamka, kufanya usafi, kwenda kushirikiana na mume shambani, au malisho ya ng'ombe! Leo mwanamke anamshahara wake hataki utumike nyumbani!

Kwani kuna tofauti gani na bibi yetu aliyesuka kapu akauza na pesa ikatumika nyumbani?

Hivi nyie wanaume muliyewapotosha wanawake kwa dhana potofu ya mume ni provider, mumetumia msingi gani wa elimu?

Hapana, mume na mke wawajibike pamoja kuijenga familia. Mume ukiamua kuwa provider, na iwe kwa maamuzi yako, na usishinikize kuwa principle ya ndoa. Kwani maisha hayo si asili ya mwanadamu tangu kale. Labda kama unakusudia kuleta mapinduzi ya mfumo wa uwajibikaji katika ndoa!

Kuna sehemu nilisoma andiko la mwanamke akiwahoji wanaume kwanini awajibike kumtii mume wakati anasaidia kuprovide mahitaji ya ndani?

Swali hili ni sawa na kumhoji mkurugenzi kwanini umtii wakati unachangia maendeleo ya taasisi? Swali hili alitakiwa aliulize Eva kwa Mungu wake.

Bahati mbaya cheo hiki alishapewa mwanamume tayari. Ukimtii Mungu utatii na neno lake. Familia ni taasisi ambayo lazima awepo kiongozi wakuweka direction za maisha. Hata hivyo haulazimiki kutii chochote. Unapaswa kumtii mume kwa yote yaliyomema. Mungu alishafanya uteuzi, labda tusubiri utenguzi na ateuliwe mwanamke siku za usoni!

Mke wajibika kuprovide kwa familia yako pale inapowezekana. Usikwepe wajibu ilihali mukiachana unadai mgao hamsini kwa hamsini.

Mume akifa unadai urithi wa mali zote!

Hata hivyo, hapa, nikiri kwamba asilimia kubwa ya wanawake wanajitoa na kuprovide kwa familia zao. Asanteni sana!

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Wajinga ndio wanakomaa,Mimi mwanamke hawezi kuwa na pesa asitumie kwenye familia namtimua Bora nikae peke yangu
 
Wajinga ndio wanakomaa,Mimi mwanamke hawezi kuwa na pesa asitumie kwenye familia namtimua Bora nikae peke yangu
Wanakomaa wakati huo huo wanaona familia zote mtaani kwake zinavyopambana kwa umoja wa baba na mama!
Wanajisahaulisha jinsi neno golikipa lilivyotrend katika kuwadiscourage wanawake wasiojishughulisha katika kujenga familia

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom