Napingana na Tundu Lissu kuwa ugumu wa maisha umesababishwa na Katiba

Napingana na Tundu Lissu kuwa ugumu wa maisha umesababishwa na Katiba

Waseme wengine. Lile lipumbavu limeangukia pua. Soon utaliskia vyuma vimetatuka linatakiwa lirudi kutibiwa ndo imetoka. Kaja kudai hela zake mbona kasema
Tatizo ulikosea shabaha siku ya tukio Dodoma. Tungekuwa tumeshamsahau Lisu.
 
Magazeti ya leo yamemnukuu Tundu Lissu akisema ugumu wa maisha hautokani na uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan bali ni unatokana na Katiba.

1. Lissu nakuuliza Kwani Katiba ndio imefungua mipaka ya nchi yetu na kuruhusu Wakenya,Wanyarwanda,Wakongomani na Warundi kumiminika hadi mashambani huko vijijini kulangua mazao? hali ilikuwaje miaka ya Magufuli?

2. Katiba ndio imeweka Tozo za miamala ya kibenki na mitandao ya simu? hali ilikuwaje miaka mitano ya Magufuli?

3. Je! Katiba ndio imesababisha wakulima kukosa mbolea na kusababisha kushuka kwa uzalishaji wa mazao?

4. Katiba ndio imesababisha umeme ukatike mara kwa mara na kusababisha uzalishaji viwandani kushuka na kupandisha bei za bidhaa?

Katiba mpya ni hitaji muhimu lakini kuna matatizo hayasababishwi na Katiba na wewe umekwepa kusema waliotufikisha hapa kwa sababu unazozijua wewe na kusingizia Katiba.

Miaka 5 ya Magufuli tulikuwa tunatumia Katiba gani wakati mchele ukiuzwa 900 hadi 1,200 na sasa tunatumia Katiba gani mchele ukiuzwa 4,000
Labda inawezekana anamaanisha katiba iliyopo hawawajibishi viongozi wanaposhindwa kudhibiti majanga
 
Jione ulivyo mpuuzi. So mrema wa 1995 TLP na wa 2015 alikua yule yule? We ni punguani nakwambia
FnUYDz5XEAETQnu.jpeg

Hahahaha embu Lia basi.... au Bado niongeze zingine?
 
Magazeti ya leo yamemnukuu Tundu Lissu akisema ugumu wa maisha hautokani na uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan bali ni unatokana na Katiba.

1. Lissu nakuuliza Kwani Katiba ndio imefungua mipaka ya nchi yetu na kuruhusu Wakenya,Wanyarwanda,Wakongomani na Warundi kumiminika hadi mashambani huko vijijini kulangua mazao? hali ilikuwaje miaka ya Magufuli?

2. Katiba ndio imeweka Tozo za miamala ya kibenki na mitandao ya simu? hali ilikuwaje miaka mitano ya Magufuli?

3. Je! Katiba ndio imesababisha wakulima kukosa mbolea na kusababisha kushuka kwa uzalishaji wa mazao?

4. Katiba ndio imesababisha umeme ukatike mara kwa mara na kusababisha uzalishaji viwandani kushuka na kupandisha bei za bidhaa?

Katiba mpya ni hitaji muhimu lakini kuna matatizo hayasababishwi na Katiba na wewe umekwepa kusema waliotufikisha hapa kwa sababu unazozijua wewe na kusingizia Katiba.

Miaka 5 ya Magufuli tulikuwa tunatumia Katiba gani wakati mchele ukiuzwa 900 hadi 1,200 na sasa tunatumia Katiba gani mchele ukiuzwa 4,000
Soma katiba ibara ya 99-(1) utaelewa maana ya maneno ya lisu. Katiba inamruhusu Rais asababishe ugumu was maisha kwani imemruhusu kutoza chochote bila kuingiliwa na bunge.
 
Huo mchele wa 900 ushawahi kuula au unabwabwaja kama vipi tushawaambia kamfufueni mje muendelee kula michele ya 900 kama huwezi piga kimya ya kale yamepita na sasa ni mambo mapyaaaaaaa tunateleza tu ww unaelalamikia hadi chakula una maisha duni sana
 
Hii ni roho ya mtu ...naweza kusema wewe ndiye mwenye lengo baya na Taifa letu kuliko ata huyo unaemfikiria hivyo. Kwanza kauli zako zinaonyesha wewe sio mtu mwema kabisa. Ungekua mtu mwema tusingeona kauli kama hizi hapa. Kwanza MH.Lissu ni moja ya watanzania ambao wamejaribu kulifanyia Taifa ili kuliko ata wewe usie ata julikana.
Ujio wa Lissu umelivuruga mno lile kundi la yule dikteta, ndio maana nyuzi kuhusu Lissu zinafunguliwa kila muda..
 
Ishu sio katiba mpya tu, ishu ni usimamizi wa hio katiba. Mambo yakiendelea kama yalivyo hata zikija version mpya za katiba kila mwaka hatufiki popote.

Katiba iwe inasimamiwa na vyombo vya dola atakaekiuka anakula umeme chap.
umeeleza safi kwani tusipokua makini katiba itawanufaidha wanasiasa tu kama ilivyo kenya wakati wa chaguzi tu ndo katiba itaonekana imefanya kazi
 
Acha uongo wee mkolomije, mchele gan unapata mjin kwa sh 900 mpaka 1200? Kwann usitoe na reference kipind cha awamu ya tano kuhusu bei ya sukar? Pia issue ya katiba mpya ime contain mambo mengi ya kiuchumi, siasa, na mustakabali mzm wa Taifa letu. Hivyo nyie wakolomije ni ngumu sana kuelewa umuhim wa katiba mpya.
We mpumbavu hakuna familia inayotenga sukari mezani kama mlo ,sukari ni kiungo kama ilivyo chumvi.
 
Jambo zuri ni kwamba Watanzania wengi Leo siyo wajinga kama baadhi ya wanasiasa wnavyofikiri. Huwezi kumwambia mtu athari za COVID-19 zilizovuruga chumi za nchi nyingi Duniani zilisababishwa na kukosekana kwa katiba mpya Tanzania kakuelewa. Ni vigumu kumwambia Mtanzania kuwa mabadiliko tabia nchi na uhaba wa mvua maeneo mengi jambo lililosababisha uhaba wa vyakula na kupelekea bei ya vyakula kuongezeka yamesabishwa n CCM.

Tanbihi: hata sana mbovu kuna wakati inakuwa sahihi
 
Unajua hata maana ya katiba kweli,?
Katiba mpya inaletanga mvua?, Au inalima?,,,
Bei zitakaposhuka mwezi june, kipindi cha mavuno hiyo itakua katiba gani?,
Serikali haipangi bei ya bidhaa, hata mtoto wa chekechea anajua bei ya vitu huamliwa na Supply and demand, na siyo katiba mpya au kuukuu🤷🏻‍♂️
 
Katiba nzuri ni pale serikali itafungua maghala yake na kutoa akiba ya pesa kuwezesha wananchi wapate mahitaji kwa bei rahisi wanayomudu.
 
- kuhusu tozo chanzo chake ni Katiba kwa sababu tozo ni Kodi na Katiba imesema kuwa Hakuna Kodi itakayotozwa hadi iwepo sheria ya kusimamia hiyo Kodi, na pia Katiba imesema bunge halitajadili muswada wowote wa kutoza Kodi hadi Rais aamue hivyo kupitia waziri wa fedha, hivyo basi tozo zote zimetokana na Katiba hii ya 1977, (tozo za haki na zisizo za haki)
-kuhusu ruzuku na kushuka kwa uzalishaji ni Kwa sababu muundo WA serikali ni mbovu, maeneo yenye uzalishaji yalitakiwa yajengewe miundombinu ya kufikika, na pia hayo maeneo/ mikoa ilitakiwa ipewe mamlaka ya kujipangia na kujiamulia yenyewe kitu ambacho hakiwezekani kwa Katiba hii.
  • kuhusu kukatika umeme pia Katiba imechangia, kwa sababu Viongozi wamekuwa sio wawajibikaji, but wanawajibika kwa Rais tu na sio kwa Wananchi
  • kuhusu kufungua mipaka na wageni kuingia, pia Katiba inachangia kwa sababu Viongozi hawawajibiki Kwa Wananchi, wanajua kwa udhaifu wa Katiba wataiba kura na wataendelea kuongoza hata kama kilo Moja ya Michele iwe 7000/-,
Akili kubwa imetumika hapa. Ningekuwa karibu nawe, ningekununulia makange ya Ngamia
 
Nakula mahindi milipuko hapa.

Huwa nafurahi kukuta mada za Kupinga/Bila kupinga

Nitawapongeza nyote mlio kazini kwa kuendesha Propaganda.
Kwani Katiba ndio imefungua mipaka ya nchi yetu na kuruhusu Waomani,Wazungu,,Wasomali na Wahindi kumiminika hadi mashambani huko vijijini kulangua mazao? hali ilikuwaje miaka ya Magufuli? au Jakaya, au Mwinyi?


Niulize tu, Mbona nyie CHADEMA hamna jeuri ya kusema ni matunda(matatizo)ya CCM tunayolishwa badala ya Kukimbilia Magufuli, Wanyarwanda, Waburundi mbona hamuwataji Wagagaigikioko?

Wapuuzi sana CHADEMA na nyote wanaowatumia. Iwe ni Mabeberu wa CCM, Mabeberu wa Siasa, Mabeberu Uchwara Mabeberu wa Ulaya, Mabeberu wa Omani, Mabeberu wa Ubeligiji yaani kila aina ya Ubeberu....

Pamoja na hadaa kubwa inayoendeshwa na CCM, Ni afadhali Wananchi wawachague wao, kwani kuna uwezekano Mkubwa Magufuli(ii) atatokea mumo. Lakini kwa Ulaghai na Uhadaa unaoendeshwa na CHADEMA hapana. HAPANA muwe wakweli.

Aluta Continua.

Kitaeleweka.
 
Back
Top Bottom