Napingana na Tundu Lissu kuwa ugumu wa maisha umesababishwa na Katiba

Kwani nani kasema kesi itafunguliwa kwa katiba ya sasa? Kutakua na mahakama huru kama Kenya hivyo Rais hatoi mshahara Wala kuteua majaji so obvious kajamba nani anaweza kushinda kesi kama Ile ya BBI
 
Reactions: Ame
Mimi nilimwelewa Lissu kuwa katiba imerundika madaraka makubwa ya ki-Mungu mtu kwa Rais, anaamua lolote juu yenu, lakini kungekuwa na mfumo wa katiba mzuri unaoweza kudhibiti mamlaka ya Rais, hali isingekuwa hivi. Kwa Sasa maisha magumu au mazuri hutegemea Rais aliyepo anaendeshaje nchi. Mfumo wa katiba nzuri, Rais ndiye atakayefuata katiba inasemaje, sivyo ilivyo katiba hii ambayo Rais ni Mungu mtu anaamua tu mtaishije.
 
Haya Ni mambo Magumu, weka CV yako tuone tunabishana na level gani, maana ulivyoanza, ingawa sikusoma yote unatia mashaka
Japo simkubali Lisu kama individual lakini nakubali argument yake...Nimeona huruma watanzania wanashindwa kwenye kutambua mambo ya msingi na mambo ya propaganda
 
Kwakuwa yeye ni mwanadamu mkamilifu au sio. Ndo maana akafika nchi za nje na kuanza kumchamba marehemu. Sawa
Marehemu mwenyewe alitaka kumwua Lissu baada ya kushindwa kumwua akamnyima matibabu na akamvua Ubunge,kama ni wewe ungeendelea kusifia hilo jambo?
 
Wa kurudi kwao ni huyo
Lissu asije kutuchafulia amani ya nchi yetu hapa. Yani mtu anahangaika na wazungu kutwa, wanae kawaacha nje kaja kuwasomba wapumbavu hapa. Na nyie mnaingia kingi.

Kwa hiyo we unaamini lissu anauchungu na hili taifa? Pathetic
Na VISA yake bado anayo, haijaisha.......
 
Vijana wa ccm kuelewa jambo niwagumu Sana

Alisema Ili jambo lolote lijadiliwe na bunge kwadharula nilazima president awe ameruhusu ,mwenendo huu upandaji chakula na uozo mwingine ,means rais hajataka mambo yajadiliwe pengine ...
 
Marehemu mwenyewe alitaka kumwua Lissu baada ya kushindwa kumwua akamnyima matibabu na akamvua Ubunge,kama ni wewe ungeendelea kusifia hilo jambo?
Magufuli ndo alimvua ubunge? Ukiambiwa ulete ushahidi wa kwamba alitaka kumuua utauleta?
 
Wewe unauliza maswali?!!!
 
Katiba ndo system au mfumo wa Kila jambo kwenye nchi na Lisu kusema katiba ndo inaleta kila kitu hata chakula mezani yupo sawa, katiba inafanishwa na maziwa ya mama kwa mtoto mchanga na ndo maana inaitwa mother land yaani bila ardhi huwezi kusimama Bali kulala tu yaani ukiwa umedondoka imagine pale tetemeko la ardhi linapotokea kama unaweza kusimama bila kuanguka Sasa bila katiba iliyobora hakuna kitu kizuri kinachoweza kufanyika zaidi ya tetemeko kwa Kila mtu kasoro aliyesehemu isiyo na tetemeko yeye atasikia malalamiko ya tetemeko bila kumuathiri.

Sasa kwa vile system au mfumo ndo kitu Mungu alituelekeza tuwe tunaanza nacho Ili mambo mengine yawe sawa basi hatuna budi kuhitaji Kwanza hiyo katiba Bora na Ili uamini zaidi kwanini hao waliounda serikali mwanzo waliweka katiba iliyofaa kwa wakati huo? Ni Ili wapate mfumo Bora na dhabiti wa kuwaongoza na sasa unatakiwa uwe update Ili uendane na wakati tuliopo, Mungu alisema katika ngazi ya familia cha Kwanza baba anatakiwa awe na kazi Ili aweze kutoa mahitaji ya familia Sasa angalia vijana ambao ni baba wa kesho hawana kazi sasa hicho chakula na mahitaji ya familia vitatoka wapi? Iwapo katiba bora inayoendana na wakati uliopo itatengenezwa basi wananchi watataka serikali ndogo watayoimudu kuihudumia na vyeo vingi vitaondolewa kwenye system ya kutumikiwa na wananchi Bali vikawa vyeo vya kufanya kazi zinazoonekana na hao wengi waliokuwa mzigo kwa wananchi watasimama kwenye msingi wa kudai mazingira ya uwepo wa kazi Ili nawao waingize kipato, imagine Leo watu wanalia chakula bei ghali wakati Kuna mikoa mvua mwaka mzima au Kuna sehemu za kuchimba visima vya umwagiliaji lakini wakuu wa mikoa na wilaya wapo hawajitikisi kusaidia hivyo visima kwa vile ya kupewa vyeo vya kupokea mishahara, Kuna mikoa inaishi kwa soko moja tu yaani watu kupata mahitaji mpaka waende mjini wapoteze muda hakuna mipango ya kusogeza masoko makubwa Kila sehemu Ili kuleta ajira nyingi zitazoleta chakula mezani, Barabara mpya za kusogeza huduma karibu inakuwa wimbo hakuna maamuzi ya kufikiri kwa wakati tuliopo, mambo mengi kama maji, elimu, umeme, hospital pamoja na teknolojia vyote ni vyanzo vya ajira na huduma vinafanyika kwa njia ya propaganda kwa kizazi cha Leo yaani bosheni kwamba mfano mnaahidiwa hospital kubwa cha ajabu inajengwa zahanati, Sasa haya yote ya bosheni na propaganda Ili yazimwe tunaona katiba mpya ni muhimu maana italeta msingi wa kuwajibika na kazi na hata hiyo slogan ya kazi iendelee maana yake bila kuwafanya watu wafanyekazi au kuweka mifumo ya Kila mtu kufanya kazi basi hakuna atayeweza kula na kupata mahitaji yake.
 
Wewe unawaza marinda kama mwenzako huyu!
 
Mkuu! Ukushakuwa na Rais ambae hayaoni matatizo na kuyachukulia hatua stahiki!

Hata ukiwa na katiba ya Umeme ni kazi bure kabisaaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…