Hapana, napingana nawe kwasababu zifuatazo;
- Unapodai kuhusu tozo chanzo chake ni katiba, unakuwa umeandika statement iliyojifunga, kwasababu, katiba ni maandishi tu, yaliyopo kwenye makaratasi, hivyo ili hayo maandishi yawe na impact [positive au negative] lazima yapelekwe kwenye vitendo..
Sasa swali la kujiuliza, ni nani anayepeleka hayo mambo kwenye vitendo?
Jibu ni Rais, yeye ndie hupeleka hayo yote kwenye vitendo, kwasababu kama tujuavyo, ili sheria yoyote iliyopitishwa na bunge ianze kufanya kazi, sharti itiwe sahihi na Rais ili ianze kutumika, hivyo kama sheria hiyo itakuja kuwa na maumivu kwa mtanzania, wakulaumiwa ni Rais kwasababu yeye ndie aliyeruhusu itumike.
- Kuhusu ruzuku na kushuka kwa uzalishaji unadai chanzo ni muundo mbovu wa serikali, sasa kwani kiongozi wa hiyo serikali ni nani? jibu ni Rais, huyu ndie anayepanga serikali yake iwe vipi, kama ikiwa na muundo mbovu, basi yeye ndie chanzo cha kushindwa kuipanga serikali yake lazima alaumiwe.
- Kuhusu kukatika kwa umeme nako unailaumu Katiba, huu wako sasa ni usanii, unadai viongozi sio wawajibikaji, nikuulize nani mwenye jukumu la kuwateua hao viongozi? jibu ni Rais, hivyo kama ameamua kuwakumbatia viongozi wasio wajibika, lawama lazima ziende kwake, fair and square!.
- Kufungua mipaka na wageni kuingia nako unalaumu Katiba kwasababu viongozi hawawajibiki, swali kwako tena, kwanini nani mwenye jukumu la kuwateua na kuwatengua viongozi wasiowajibika? jibu ni Rais.