Nashangaa waliofurahi Dkt. Dorothy Gwajima kuondolewa Wizara ya Afya

wataalamu wenyewe walikuwa hawamkubali, utawaongozaje watu wasiokuelewa?
 
Uyo mama hana lolote la maana alilofanya kweny iyo sector ya afya zaid maigizo tu ikwa lipo nitajie ata 1 tu afadhal ya uyo ummi mara [emoji817]
Kwa hiyo miezi 12 aliyofanya kwa nafasi ya waziri kwa yale aliyofanya wewe ingekuchukua miaka 50. Kifupi mbegu aliyopanda kwenye clinical audit kubaini makosa ya uzembe wa wazi wa kitabibu unaopeleka watu kuzimu kabla ya wakati, audit ya fedha za uchangiaji huduma kuwa nyingi zinaishia mfukoni, medicine audit kuwa dawa nyingi zinaishia kusikojulikana: kazi hii ilikuwa inaenda kuleta mabadiliko makubwa ya kihistoria. Ila kwa kuwa waanzisha kazi huwa hawamalizi, basi endeleeni mliopo acheni kelele. Jiungeni na SMAUJATA huko nako kuna audit ya matukio ya ukatili yanayokandamizwa.
 
Siwezi kuongea kwa niaba ya kila waziri wa afya toka uhuru. Naweza zungumzia wataalamu wa muda wangu na uelewa wangu given the bunch.

Na Dr Gwajima hana mpinzani provided unaelewa medical management.
Safari za nje zimepungua nini ?Naona ulivyomuona juzi Ummy akiwa New York City,Ulitamani angekuwa mkeo na wewe. Pole Gwajima D anafaa hapo kwenye gender. Kwanza masters yake si alisoma maendeleo ya jamii ?
 
Vita ya korona na misimamo yake ilikuwa vita ya serikali nzima acha kujifanya waziri ana uwezo wa kupanga na kupangua hoja za kitaifa. Sasa kama dunia na hiyo WHO nao kila asubuhi walikuwa na majibu yao ulitaka kwa nini Dorothy Gwajima ashikilie jambo hilo hilo ambalo hata dunia bado haina uhakika na Tanzania na vyombo vyake imesema twende hivi. Acha porojo jiunge na SMAUJATA.
 
Sijaelewa ulichoandika mkuu
 
Kwamba Waziri wa kilimo awe mtaalamu wa kilimo,ulinzi awe mwanajeshi na rais awe na political science degree
 
Kwa katiba yetu tunayoitumia sasa, waziri siyo lazima awe mtaalam wa wizara husika. Waziri ni mwanasiasa, kwa sababu ili uwe waziri lazima uwe mbunge (mwanasiasa). Kazi ya waziri ni kuhakikisha anasimamia ilani ya chama chake kimesema kitafanya nini kuhusu wizara husika.
Huko ndani ya wizara wamo wataalam wa wizara husika, hao hushughulika na mambo ya kitaalam ya uendeshaji wa wizara.
Wizara ya afya imewahi kuwa na mawaziri wenye taaluma ya afya, mfano kina Dr. Aaron Chiduo, Prof. Sarungi, Prof.Mwakyusa, Dr. Hussein Mwinyi na wengine, wote hao pamoja na taaluma zao walikuwa wanasiasa. Wakati mwingine hutokea hao unaowaita mawaziri wataalam huboronga sana kwa kujidai wanajua kuliko wote kwenye wizara kisa cheo.
Angalia wizara ya ulinzi ilivyotulia, sidhani kama huyo mama waziri ni mwanajeshi, hata hivyo jeshi linaboreka kiutendaji kupita wataalam wa kijeshi waliopo. Ummy ni mwasheria bila shaka, chini yake kuna wataalam wa kutosha ukianzia na katibu mkuu wake. Kama wizara haifanyi ni issue ya leardeship tu na wala siyo professionalism. Hukutenga fedha za kutosha kwenye afya unategemea nini!!
Mwanasiasa huangalia upepo unakoelekea basi. Kama Kuna korona na Rais kaibuka na hoja ya nyungu, haijalishi waziri ni taaluma gani, ndiye atakayeongoza japo anajua kiafya siyo, tulimuona Gwajima enzi hizo.
Aliyejaribu kusimama kwenye taaluma nadhani naibu wake Dr. Ndungulile alijaribu kupinga aliishia kuondolewa.
Tubadili katiba tuondoe kipengele cha waziri lazima awe mwanasiasa (mbunge) labda watateuliwa kwa kuzingatia professionalism. Asante.
 
Kuwa Daktari haina maana unaweza kuwa kiongozi mzuri hata uwekwe kwenye taasisi ya fani yako...
Ni kweli na ndio maana watu experienced katika fani ile ndio watu wanaofaa katika taasisi yeyote ile !! Ndio maana kwenye sekta binafsi maombi ya kazi yanaambatana na uzoefu wa kazi sio madigirii pekee !!
 
You nailed it !! 👍
 
Wasema kweli hapa Nchini huwa wanapata suluba nyingi sijui ni kwanini !!!
 
Hivi mnajua kama kuna kitengo cha tiba asili cha wizara chenye mkurugenzi msaidizi eneo husika na baraza la tiba asili na sheria ya bunge? Na wanalipwa mshahara kabisa wa Kodi za wananchi? Na kama kujifukiza huyo Dorothy Gwajima alijifukiza dawa za kujifukiza za taaluma ya tiba asili iliyop kisheria. Na hyo ndiyo ulikuwa msimamo wa serikali kutumia dawa za tiba asili ambazo zipo kisheria. Sasa shida ya Waziri hapo nini kama siyo shida yenu wenye sheria na taaluma na baraza? Yeye alitoa mfano tu jinsi gani mfanye.
 
Ndugu zangu, tuache propaganda za mitandaoni kuchafua watu na kujadili watu, tuungane pamoja kupambana na hali ya ukatili nchini kupitia jukwaa huru la smaujata uwe shujaa wa jamii halisi kupambana na uvunjifu wa haki za binadamu, ubakaji, ulawiti na unyanyasaji wa watoto ambao unaharibu sura ya taifa letu,


Jiunge na watanzania wengi walioungana katika kampeni huru ya kupinga na kutokomeza ukatili nchini, jamii ina matatizo mengi sana ambayo tunaweza kufanyia kazi na kuonesha nguvu ya mitandao katika kumaliza shida za watu kuliko kujadili mapungufu ya watu na kutengeneza ligi za kisiasa mitandaoni.

Hata kama waziri ummy kuna pahala anaonekana kutofanya vizuri, nani kamshauri cha kuboresha akakataliwa?


Lakini pia tunaona namna waziri gwajima anavyojituma katika wizara mpya ya maendeleo ya jamii, hii wizara anaitendea haki sana na kuna muda watanzania wanyonge wanaona kama alichelewa maana anaibua mambo yanayoigusa jamii moja kwa moja.


Chini ya mwenyekiti wake

~ sospter mosewe bulugu

Kataa ukatili, wewe ni shujaa [emoji1491]*

*(shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii tanzania (smaujata)

https://forms.Gle/dtgthrutlhxjp2cua
 

Attachments

  • IMG_20220922_232514_405.jpg
    122.9 KB · Views: 1
Mkuu umeongea mengi lakini hukusema chocjote.
 
Tatizo ni kwamba kila mmoja anajifanyaa mjuaji sana na kutaka kuipoteza jamii hasa kwa propaganda za mtandaoni. Mpaka sasa dhamira ya alie post sijaielewa kabisa . Watu mnashindwa kutafakari jamii inakumbwa na wimbi kubwa la ukatili.

Katikaa muda mfupi tu wa wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia wanawake na makundi maalum mama Dorothy amefanya na anafanya vitu vinavyo igusa jamii ki ustawi.

Lakin watu wachache wanakaaa na kuipotosha jamiii. Wote mnaosoma na ku comment Mada hii isio na ustaarabu achaneni na mitazamo hasi na unganeni na kampeni huru ya kupinga ukatilii nchi SMAUJATA
 
Tumia Busara na usomi wako kujieleza!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…