Nashauri safari za mabasi kutembea saa 24 zisitishwe, vifo vitamaliza watu

Nashauri safari za mabasi kutembea saa 24 zisitishwe, vifo vitamaliza watu

Kwema wakuu?

Kwa Hali ilivyo usalama barabarani nyakati za usiku ni mdogo madereva hawazingatii Sheria barabarani wakati wa usiku maana hamna Oolisi. Malori nayo ndio mida yao ya kukimbia so ajali ni nyingi mno. Madereva pia usiku wanasinzia barabarani sababu ya uchovu.

Kuna siku nimesafiri na basi la Frester kwenda Dar es Salaam, kufika Morogoro usiku kama saa nane, dereva anataka kugonga semi za mafuta sababu ana overtake pia hamna Polisi barabarani.

Hivyo hivyo gari la Abood juzi tumetoka Dar dereva anaendesha kwa kasi pia tulilipanda pale Mbezi saa kumi na moja alfajiri gari halikufanyiwa service maana ilikuwa inatoka mkoani na watu wanashuka pale Mbezi na sisi tunapanda sababu hawana muda wa service.

Chonde chonde Serikali sitisheni hizi safari.

NB: Hata ajali mchana zinatokea lakini chanzo hasa ni madereva kuendesha magari usiku so wanachoka wanakosa focus ya kuendesha mchana na kupelekea kupata ajali
Si kweli. Hizi zako ni fikra hafifu sana, zilizojaa woga..

Watu ni lazima wafanye kazi 24hrs...

Badala ya kutoa ushauri bagazi kama huu, badala yake ungeshauri serikali kuimarisha taratibu za kiusalama muda wote si kwa ajili ya biashara ya usafirishaji tu bali kwa biashara zote mijini na vijijini..

Kwa sekta ya usafirishaji, ni kuhakikisha tu kuwa tunakuwa na drivers professionals na wanaozingatia ethics za usalama barabarani. Vivyo kwa upande wa mamlaka za usimamizi wa sekta hii, hawapaswi kulala. Wafanye kazi 24hrs ..

DUNIA INAENDA KASI SANA KTK NYANJA ZA KIJAMII NA KIUCHUMI. SISI HATUPASWI KUBAKI NYUMA. TUNATAKIWA KWENDA MBELE. KAZI ZOTE NI LAZIMA ZIFANYIKE MASAA 24..

Ushauri wako ni wa kurudisha nyuma jitihada hizi...
 
Hoja ya mtoa post ni ya kweli. Kwa dharau za madereva wetu., mchana tu makosa mengi je usiku?
Si kweli. Ni fikra na maoni yake tu na tunauheshimu..

Lakini kosa la dereva mmoja au wawili haiwezi kuwa ni jumla ya madereva wote...

KAZI ZOTE NI LAZIMA ZIFANYIKE KWA MASAA 24. MUHIMU NI KUIMARISHA TARATIBU ZA KIUSALAMA TU...
 
Hizi akill hizi! Mleta mada namfananisha na wale watu ambao ikitokea ajali sehemu wanashauri yawekwe matuta
 
Back
Top Bottom