Nashauri safari za mabasi kutembea saa 24 zisitishwe, vifo vitamaliza watu

Nashauri safari za mabasi kutembea saa 24 zisitishwe, vifo vitamaliza watu

Habar za kishamba unaleta izo aisee,ajal mda wwote tu ule acha watz wafurarah maisha na safar za usiku hasa wafanya biashara imesaidia sana pia imetoa ajira nying sana kampun zimeongeza mabus drivers wamepata shavu conductors pia wakisitisha watu wataenda wap maana safar zitapungua kutokana na mda wa kukaa barabara hmna so acha ushamba huo na kimbelembele ahadi ikifika imefika halafu ajar haina muda mzee so acha ushamba
 
Sometimes we need to risk.
Maisha kama yapo,yapo tu.
Kikubwa ni kuwa na Imani ya safari kuwa nzuri,vinginevyo tutarudi nyuma.
Nafikiri itafutwe namna ya kuboresha.
Ushauri: Kila baada ya Km 50 pawepo na ukaguzi,lakini pia ifungwe mifumo ya ufuatiliaji wa Magari na mwisho Magari yote ya safari za usiku yafanyiwe maalumu.
 
Mmeanza kuomba pooo?

Si tulisema humu lakini haikueleweka?!

Learning by mistakes is very cost ful
 
Kuruhusu basi zitembee masaa 24 kiukweli ni hatari sana hasa majira ya usiku.

Oya we wahuni wa mabasi usiku wanamwaga moto siyo poa wale jamaa niliwahi kuzishuhudia gari za mwanza Dar hasa zikiwa zinaenda mwanza majira ya usiku bus inapita kasi hata jina la ubavuni huwezi kulisoma, kweye kuovertake anaweza kukaa kulia na akazikata hata gari 10 bila tahadhari, alafu huwa hawarudi kushoto wanatembea na mstari wa kati
Ndio maana tunasema safari za usiku sio tatizo bali madereva wa kuendesha kwa kuchukua tahadhari ndio shida kuwapata katika Nchi hii !!
Na baadhi ya matajiri wa mabasi hayo wanafurahia mabasi yao yanapofika mapema sana huko yaendapo hivyo huwa hawawakatazi madereva wao kwenda mwendo wa kasi !!

Vinatakiwa vidhibiti mwendo kwenye mabasi !
Basi lisiwe na uwezo wa kukimbia zaidi ya 80 kph !
Na iwekwe sheria ya kifungo kwa atakaye kiharibu kidhibiti mwendo kwenye Basi !
 
Hata hivyo ni enforcement kuimarishwa na elimu ya usalama barabani kwa wote abiria na madereva.

Maana hata mchana ajali zinatokea nyingi tu .
 
Usiku safari ziendelee lakini enforcement , ukaguzi wa magari , elimu itolewe mara kwa mara.

Na maeneo ya mijini kufungwe CCTV Cameras
Tutakuwa Taifa la watu wa ajabu wa kushikiwa akili kiasi hicho kwamba dereva asiweze kujitambua kuendesha gari kwa usalama bila shuruti?!
 
Kwema wakuu?

Kwa Hali ilivyo usalama barabarani nyakati za usiku ni mdogo madereva hawazingatii sheria barabarani wakati wa usiku maana hamna polisi. Malori nayo ndio mida Yao ya kukimbia so ajali ni nyingi mno. Madereva pia usiku wanasinzia barabarani sababu ya uchovu.

Kuna siku nimesafiri na basi la Frester kwenda Dar es Salaam, kufika Morogoro usiku kama saa nane, dereva anataka kugonga semi za mafuta sababu anaovetake pia hamna polisi barabarani.

Hivyo hivyo gari la Abood juzi tumetoka Dar dereva anaendesha kwa kasi pia tulilipanda pale mbezi saa kumi na moja alfajiri gari haikufanyiwa service maana ilikuwa inatoka mkoani na watu wanashuka pale Mbezi na sisi tunapanda sababu hawana muda wa service.

Chonde chonde serikali sitisheni hizi safari.
NB: Hata ajali mchana zinatokea lakini chanzo hasa ni madereva kuendesha magari usiku so wanachoka wanakosa focus ya kuendesha mchana na kupelekea kupata ajali
Je zile ajali kibao za mchana kweupee una maoni gani
 
Gari lingekua lako ungefanya service ukifika dar na ukifika moro unafanya ungeweza. Mbona unaongea vitu vya ajabu sana.

Gari hizo zina ratba yake ya service sio kila siku. Unadhani service ni kuweka mafuta. Unajua ifike mahali wana jf kama hujui uliza.. Gari hujawahi miliki unaanza leta stry za service every return day. Daah
Ni kweli service huwa ina ratiba(schedule)

Niliwahi kuona service tag kwenye gari fulani iliandikwa service imefanyika (mf 234300KM halafu itafanyika tena 235300KM)

Ukiangalia hapo ni baada ya mileage fulani ndio service itafanyika.

Pia service inaweza kufanyika kwa dharura ikitokea.
 
Mkui wewe ulijuaje kama gari halina service?
Ulikagua nini na nin?
 
Kwema wakuu?

Kwa Hali ilivyo usalama barabarani nyakati za usiku ni mdogo madereva hawazingatii Sheria barabarani wakati wa usiku maana hamna Oolisi. Malori nayo ndio mida yao ya kukimbia so ajali ni nyingi mno. Madereva pia usiku wanasinzia barabarani sababu ya uchovu.

Kuna siku nimesafiri na basi la Frester kwenda Dar es Salaam, kufika Morogoro usiku kama saa nane, dereva anataka kugonga semi za mafuta sababu ana overtake pia hamna Polisi barabarani.

Hivyo hivyo gari la Abood juzi tumetoka Dar dereva anaendesha kwa kasi pia tulilipanda pale Mbezi saa kumi na moja alfajiri gari halikufanyiwa service maana ilikuwa inatoka mkoani na watu wanashuka pale Mbezi na sisi tunapanda sababu hawana muda wa service.

Chonde chonde Serikali sitisheni hizi safari.

NB: Hata ajali mchana zinatokea lakini chanzo hasa ni madereva kuendesha magari usiku so wanachoka wanakosa focus ya kuendesha mchana na kupelekea kupata ajali
Uko Sahihi 💯 kuendesha gari usiku kunaitaji uzoefu mkubwa na umakini Kwa Sababu usiku sio mchana sababu zilizopelekea kuruhusu safari hizi ni za kibiashara Zaidi sio kiusalama wewe fuatilia maeneo mengi kama utaona trafick usiku au tochi usiku ni uhuru wa manyani TU.
 
Bado kuna uzembe katika usimamiaji,inaweza kuwa ni kweli kuna udhaifu kwa madereva lakini pia inaweza kuwa kuna uzembe kwenye mamlaka za usimamizi....
Kwahiyo Mkuu gari imetembea Kilometres 1,000 ikifika hamna kuikagua ngoma isambe, ndio hiki unachojaribu kutuambia wewe unayemiliki gari?
 
Sheria zetu kwenye adhabu ya uzembe wa kupelekea upotevu wa maisha au ulemavu wa kudumu ni butu.

Imebaki kuwatishia kuwafutia leseni tu basi.

Sasa kufutia leseni kuna noma gani kwa mfano?

Maisha mbona huendelea shega tu !
 
Si mlitaka ruti za usiku
Haya hizo hapo
Mnalialia nini tena,wabongo tatiZo
Hamjuwi mnataka nini!

Ova
 
Karibia nchi zote usafiri ni masaa 24. TUAMKE
Natamani pamoja na hoja yako hi usleze kidogo kuhusu mambo yafuatayo;
1. Miundombinu inaruhusu?
2. Mamlaka zinakuwepo barabarani usiku?
3. Watanzania wanaweledi na wanautumia?
 
Back
Top Bottom