Nashauri wasomi wa Chuo Kikuu kujiingiza kwenye kazi ya kutafsiri movie

Mtoa mada anachitaka kufanya ni kuwasilisha Business Proposal ya kuuza PIZZA na Burger buza au Mbagala Bishara ita feli vibaya sana.
Hapana mkuu haiwezi kudoda hata kidogo.

Kuna tamthilia flani zinarushwa tbc, azam, startime na startv nao walianza majuzi kati hapo kuonyesha zilizo_tafasiriwa na siyo kuelezea movie na kuna watu hawaachi/kukosa kuangalia daily huko buza, mbagara, manzese, uswahili, kijenge, ikipinda, isewe nk.
 
Sasa hoja naona ni Movie sio kutafsiriwa Movie ya yesu kivyovyote lazima i takeover sikwajiri imetafsiriwa kwaajiri ni ya yesu nikianza kukulistia movie zote zilizotake over za ma DJ si itafika usiku hapa.
Namna ilivyotafsiriwa ndiyo imechangia kuvutia watu. Ingetafsiriwa kwa miluzi na makelele wala isingebamba hata kama ni ya Yesu. Na hawa watu wa kitaa wanaoangalia movie za kutafsiriwa siyo wajinga kwamba hawajui kitu kizuri wakikiona. Wanawaangalia wakina mark na Rufufu si kwamba wanawapenda ni kwasababu tu hawana mbadala.

Kama kweli wanapenda miluzi na kelele watakuwa ni peke yao dunia nzima kitu ambacho ni kigumu.
 
Huyo kwanza aangalie behind the scenes za Animation movies za Hollywood ndio atatambua sio kila mtu anayeweza kazi hiyo, na pia sana sana wanapendelea kutumia wasanii wa movies waliobobea tayari kwa nyanja ya uigizaji.
Unafikiri mtu aliyemaliza chuo atakuwa na uwezo wa kuajiri voice talents kila anapotaka kutafsiri movie? Si pesa itaishia huko!!
 
Watengenezaji wa filamu wakiwa na mawazo kama yako sidhani kama wangeandaa movie kwa garama kubwa (Sci-Fi, action n.k) labda comed.

Asilimia kubwa ya filamu ni uongo na kadiri teknolojia inavyosogea wanaendelea kukusogezea behind the scene tena zile sehemu nyeti ambazo mtu kama wewe huwezi sema "hapo ni uongo"

Kumbuka kuelezea sana movie na matukio kunaondoka uzuri/attention kwa mtazamaji, maana utakuwa umejua nini kinafuata badala ya kuisumbua akili kujua nini kinafuata.
 
Nishakaa sana Video Library.

Soko la ma DJ nowadays sio single movie kwasasa ni Series.

Marindhiano yanaweza kuwa hivi:
Biashara ya movie ipo hivi MA DJ Soko lao kubwa sasahivi ni Series/Season na kila kipindi kunakuwa na Season zinazouza sana na kila Week wanatoa muendelezo WA vipande vya Season....Unachosema uwenda kikawa na mantiki pale itapotokea Season hizi wakatokea wafasiri wa mtindo wa unaouzungumzia na huku kuna ma DJ then ndio tungeona majority wangeamia upande gani...Hiki kijawai tokea kikitokea kitakuwa kipimo.
 
Ni wazo zuri ila sio kwa wasomi wetu wa vyuo vikuu.Labda watoto wa form 4 au A level ndo wafanye hivo.
 
Wale walioitafsiri ile Sultan nimewakubali kwa kazi waliyoifanya, jamaa sauti inaendana sambamba na mdomo wa muigizaji kiasi kwamba unaweza kuamini muigizaji anazungumza kiswahili
Sasa wafanye kazi kama zile. Wajikusanye waliopita shule kama wale waliosomea maigizo na wafanye kazi kama hiyo. Kazi yao kubwa iwe kupata studio na vifaa vyake.
 
Mkuu hivi umenielewa nilichoandika au una reply tu!
 
Uwe makini na muvi za nje kwani wenyewe wakikukuta utakiona cha moto, hakikisha unapata ruhusa toka kwao.
 
Hivi mtu ukiamua kuvitafsiri vitabu vya kiingereza na kuvichapisha kwa kiswahili, haiwezi kuwa ni fursa nzuri kibiashara?
Fursa nzuri ndio, lakini ka ni vitabu itabidi upate ruhusa (copyright) kutoka kwa mwenye kitabu na editor wake. Usipofanya hivyo kuna chances ya kuchukuliwa hatua za kisheria na wenyewe.
 
Uwe makini na muvi za nje kwani wenyewe wakikukuta utakiona cha moto, hakikisha unapata ruhusa toka kwao.
Inategemea nje wapi, za Ulaya hakuna wa kukufuata, labda hapa Afrika sanasana ukanda huu wetu wa Eastern Afrika
 
Siku mzungu akiamua kupeleka watu mahakamani kwa kutafsiri kazi zao bila ruhusa ndio mtaona joto ya jiwe
 
Nimewauliza wanachuo flani hapa chato et wanadai Ni kazi cheap Sana!

Eti sio hadhi yao.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…