Nashauri wasomi wa Chuo Kikuu kujiingiza kwenye kazi ya kutafsiri movie

Mkama nzinza.
 
Ukitaka kujua mambo ya kihistoria na kigeography tazama movie za ommy dj haswa season daah wewe tu jamaa anajua sana [emoji110][emoji4]
 
Ommy dj kutoka arusha ni mmoja wapo wa hawa wasomi wa chuo yuko vizuri yeye anapiga series za kizungu shida yake ya tangia utotoni ni matusi hapo mvumiliane tulijaribu kumrekebisha tukashindwa
Utasikia, na jinsi anavyowapa makavu jamaa zake wanyaturu.
 
Wakati unaweka pozi kuielezea ak47 tanesco wanakuangalia tu
 
Ngoja wakutaje movie zijazo alafu wanamalizia

"tunapiga bao, wewe mtoto wa kwa mama nani unasema tunatafsiri uongo njo na wew mamaae..."

Hawa jamaa ni vipaji tu vya kupiga zogo vya tokea shuleni za msingi mkuu.
 
Sheria hizo zinasimamiwa hapahapa nchini na mamlaka husika chini ya sheria ya copyright.
Hata huku kwetu ziko lakini hakuna kesi au lawama kutoka nje nimeiskia, hizi zetu tu ndio balaa kuifanyia marekebisho bila kibali kutoka kwa wenye filamu na bodi kuu
 
Utakuwa unwaonea sana DJ's (Dj MACK , DJ AFRO , DJ MURPHY n.k )
kwa kutaka kutoa translation ya kila kilicho semwa kwa sababu hizi

Kazi za DJ ni utangazaji - ahakikishe muangaliaji anaielewa Movie kiundani na sio kuwa translator wakutoa maneno kutoka katika kingereza na kuleta katika kiswahili , Kwa hiyo kuna muda atatoka nje ya mada au kuna mda atatumia sentensi nyingine ila maana itabaki pale pale.

Ni kweli kabisa kuna time DJ wanakosea na nikutokana na kuchoka, pia kupoteza focus ( focus kwa DJ ni dakika 15 tu - kuendelea mdomo unakua mzito na story zile zakunogesha zinapungua )

NAITUPIA LAWAMA KWA BODI YA FILAMU NA VIONGOZI WANAOHUSIANA NA AJIRA Kwanini?
Kuna fursa ya Dubbing na Movies Subtitle
Dubbing ni utoaji wa sauti ya kingeraza katika movie na kuiweka kwa lugha ya kiswahili huku sauti ikilandana na matendo(mfano mzuri Kulfi inayo rushwa Azam )
Subtitle ni kuziwekea movies tafsiri ya kiswahili kwa kuandika maneno juu ya video
Viongozi hawa ndo wana jukumu la kuangalia vijana wanao kaa nyumbani kwa miaka 10 bila kupata kazi. Wange anzaisha kama Hub ambazo vijana wakua wanafanya yao then kinachopatikana kinatumika
Hizi hub hazitakua chini ya serikali bali zitajitegemea zenyewe kutokana na ishu ya copyright

Soko la movies kwa Tanzania ni kubwa sana, Ila Hakuna wa kulicheki hili soko .
 
Ommy Dj anajitahid sana kuelezea movie kwa undan na anajua mambo mengi sana ya kihistoria,kisayansi na kijografia #Bravoo ommy d
 
Wabongo wengi wanapenda zaid mbwembwe za mtafsiri na sio usahihi wa kinachotafsiriwa. Yaan unakuta jamaa anatafsiri ktu tofauti kabisa na subtitle lakn anatia mbwembwe na vimaneno vya uongo uongo unajikuta unaenjoy kumsikiliza
 
Nikiambiwa nichague kuuwawa au kuangalia muvi zilizotafsiriwa ninachagua kuuwawa.
Watu wanapenda zile mbwembwe na madoido za dj wala sio kwamba hawawez kuangalia kwa kusoma subtitle
 
N kama zile movie za wahnd, znazorushwa azam tv kama sikosei,,, wanaongea kihindi but sauti unaskia maneno ya kiswahili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…