Nashindwa kabisa kumuelewa Tundu Lissu, moja kati ya wanasiasa niliokuwa nawakubali sana

Ninazoziona kwa Lissu ni frustrations za aina ya Siasa zinazoendeshwa na Mbowe.

Siasa za kujikombakomba kwa Watawala na kulamba makalio huku wao wakiwaua Vijana na Wazee wa CHADEMA.

Mardhiano gani wakati hakuna kilichobadilika mauwaji yako palepale ndio maana Lissu kakubali kulipiwa Fomu na mhanga wa jaribio la mauwaji 'Sativa' huu ni ujumbe mkubwa sana kwa Watawala.
 
Yaani ndani ya Ubongo wako Mkuu akili yako inamuwaza Lissu kila baada dakika kadhaa maana unamuanzishia nyuzi kama vile jamaa ni mtu hatari sana.
 
Watu wengi nilikuwa naona ni waumini wa Lisu tena wako tayari kufa nae leo hii wamemgeuka?
.
Napata wasiwasi hata waliompiga Lisu risasi huenda wapo ndani ya chadema.
Wakamsingizia Magufuli
 
Yaani ndani ya Ubongo wako Mkuu akili yako inamuwaza Lissu kila baada dakika kadhaa maana unamuanzishia nyuzi kama vile jamaa ni mtu hatari sana.
Yes anaharibu Chama ninachokipenda, atakigawa na kukiua milele kama vyama vile 19. That is my concern. Nilimpenda sana Lisu na chadema! Naamini katika democracy, uhuru wa mawazo, katiba mpya, uchaguzi huru and the like!
 
Lissu ana hoja zake zijibiwe tafadhali.

Alisema kwenye chama kuna fedha haramu za Abdul ,mimi nikawa siamini ila majuzi alipokazia na hadi kumtaja sasa aliyempeleka Abdul nyumbani kwake, mhusika ndio akajitokeza.

Kutaka kumzima Lissu asiongee mengi zaidi ni dalili ya kuficha uchafu mwingi ulio kwenye chama.

Chama kama kimejitanabaisha ni cha kidemokrasia basi kifuate kinachohubiri kila siku kwa chama cha majizi.

Utasemaje unafuata demokrasia wakati huna ukomo wa madaraka?

Utasemaje unafuata demokrasia kama wajumbe wananunuliwa kwa pesa kama bidhaa?
 
Leo ndio hafai?

Mbona mlimpa jukwaa la kupambana na JPM kuwania Urais? Au kwa kuwa anaongea msioyapenda?
Kwa recent behavior, recent matamshi yake yasiyokuwa na kaba ya ulimi! KUROPOKA...kumbe alikuwaAMEFICHA MAKUCHA. SHORT OF THIS LISU WAS SMART, VERY SMART.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…