Mgonga Like
JF-Expert Member
- Mar 30, 2015
- 1,255
- 1,659
Achanane tu huyo anafurahisha mdomo wake, hapo hata kulima tu nusu eka ukute ajawaiWe unaeandika utumbo huu ni mkulima au umejiskia tuu uandike!!?
Unajua shida tunayoipata sisi mipaka ikifungwa mbeha wewe!!?
Alafu nmekumind kishenzi yaan.
Wewe ni mkulima ama unaongea tu? Unafahamu shuruba na gharama za kilimo? Unajua bei za pembejeo na vibarua?? Hilo ni tatizo kwa mkulima hakuna mfano jamaa wakibana wakulima msimu ujao wa mavuno twafa!Wakulima Walime, Watanzania tule kwani Kenya tu ndo wanamatumbo peke Yao?.. Viongozi wetu sio wajinga na sisi Watanzania tupunguze uoga, changamoto kidogo tu mshaanza kupost Mabandiko, Kama hawanunui wao tutauza kwingine watakapo hitaji, ikishindikana tuuziane humuhumu Maisha yaendelee mi hua hainingii akilini kununua debe la Mahindi 20,000 wakati mengine yanapelekwa Kenya huko.. hii Ni Vita ya kiuchumi na Kenya wameshaona Kuna uwezekano wakageuka koloni la Tanzania.. Punguzeni Uoga Vijana, maendeleo hayaji bila changamoto.. Sengwile Makamanda!!
Bwana kwa sababu ukitoka kucheza pool table na kubet unakuta chakula kwenye hotport una haki ya kuongea haya. Lakini kwa wale tunaoshinda maporini uko tukilima tunajua madhara yaliyoko mbele yetu. Hoja kwamba tutauza nchi zingine nayo ni kujipa matumaini tu. Sijui kama una kumbukumbu vizuri mwa 2017 tulihangaika kutafuta soko la mahindi hadi yakaharibikia ndani. Kwa kipindi hicho tumbo lako ulimwazima nani? Unakumbuka kilichowakuta wakulima wa Mbaazi ? Bei imeporomoka kutoka 3,000/= hadi TZS 200/= kwa kilo. Korosho mnakumbuka pia kilichotokea? Kwahiyo tusijipe matumaini. Hali itakua mbaya. Ni kilio kwa wakulima wa mahindi.Wakulima Walime, Watanzania tule kwani Kenya tu ndo wanamatumbo peke Yao?.. Viongozi wetu sio wajinga na sisi Watanzania tupunguze uoga, changamoto kidogo tu mshaanza kupost Mabandiko, Kama hawanunui wao tutauza kwingine watakapo hitaji, ikishindikana tuuziane humuhumu Maisha yaendelee mi hua hainingii akilini kununua debe la Mahindi 20,000 wakati mengine yanapelekwa Kenya huko.. hii Ni Vita ya kiuchumi na Kenya wameshaona Kuna uwezekano wakageuka koloni la Tanzania.. Punguzeni Uoga Vijana, maendeleo hayaji bila changamoto.. Sengwile Makamanda!!
Nani kakuambia chief, mzigo upo chini kwa chini mzee, hakuna wa kuzuia hii kitu.Hizo GMO ilikuwa enzi za serikali dhaifu. Sasa hivi zimepigwa ban.
Awamu hii kila mjinga anaishauri Serikali cha kufanya na bahati mbaya sana ushauri huo unasikilizwa na kukubalika zaidi kuliko wa Watalaamu. Waganga wa kienyeji wanashauri dawa bora za mitishamba, huyu nae anashauri mbegu zilizitumiwa na Mtwa Mkwawa ndo zitumike badala ya zile zinazoboreshwa mara kwa mara. Mbegu hizo za mahindi za kuvuna magunia matatu kwa eka bado zipo na Wakulima wengi bado wanazitumia siyo kwa sababu anazotoa huyu mjinga bali ni kukosekana kwa uelewa. Mabeberu hawatumii mahindi kwa chakula wala hawalimi sana mahindi ingawa wanatumia sana kama chakula cha mifugo kwa hiyo hawawezi kutumia raslimali zao na wakati kuboresha mmea ambao ni mgeni katika mazingira yao. Watalaamu wetu wanajitahidi sana na wanafanikiwa kuboresha hizo mbegu asili ili mkulima avune magunia 40 kwa eka ili apate chakula cha kutosha familia na ziada wauziwe wengine pamoja na mabeberu wakalishe mifugo yao. Magonjwa ya mimea, wanyama hata ya Binadamu yapo tu na mapya yanaendelea kujitokeza kama Changamoto ya kupumua na vita ya kuyaangamiza ni endelevu kwa juhudi za Watalaamu wetu na mabeberu.Nilitamani kuanzisha uzi kuhusu hili suala lakini nashukuru kwa bandiko hili maana limelenga kile nilichotaka kusema.
Binafsi nimekuwa mdau wa kilimo kwa muda mrefu sana, kuanzia kulima mpaka kushiriki makongamano mbalimbali yanayohusiana na sekta ya kilimo na kuna hoja kadhaa ambazo wakulima wamekuwa wakizitoa kwa Serikali lakini kutofanyiwa kazi na hii sasa ndio majibu yake, japo inabidi kutafiti zaidi kama kweli Kenya wanasema ukweli au ndio VITA YA KIUCHUMI.
Hoja kubwa ambayo imekuwa ikitoka mara kadhaa ni kuhusu suala la mbegu, wadau wameshauri mara nyingi turudi kwenye mbegu zetu za asili maana hizi tunazoambiwa za kisasa zina changamoto nyingi sana, mojawapo ni hii ya kushambuliwa na wadudu hali inayopelekea wakulima kutumia madawa mengi sana ili kuweza kulinda mazao yao, na hili nimelishuhudia kwa macho yangu, sasa kwa hali hii tutajiteteaje kwamba mahindi yetu hayana sumu?
Wakulima watanielewa vizuri kwenye hili,
Na hapo nimeongelea madawa kwenye mahindi pekee, rudi kwenye nyanya, matikiti nk, huko ndio usiseme, dawa inayomwaga huko huwezi amini kwamba inaingia tumboni kwa binadamu.
Mimi nashauri wadau wa kilimo wasikilizwe, ianzishwe bank ya mbegu zetu za asili kuliko kutegemea hizi za kisasa tunazoletewa maana wakati mweingine kuzitunza ni ngumu sana kwasababu ya kushambuliwa na wadudu.
Halafu kama hatuwaamini Mabeberu ( Bill Gates) kwenye chanzo za COVID kwa nini tunahamasisha wakulima wetu watumie mbegu zao, Rejea matumizi ya mbegu zilizofanyiwa GMO huku nako kuna madhara mengi zaidi.
Huu ulikuwa unyama wa kiwango cha kutisha sana ! Kenya wasingekuwa waungwana hili jambo lingeleta vita vya makombora .Ccm inakurupuka kwa misifa ambayo haina maana, jaribuni kutafuta mzizi wa fitna View attachment 1718502
Pamoja na kutopinga kila uliloandika, lakini nakuomba ujielimishe kwanza ili ujue tatizo kwa kina zaidi ya hivyo unavyodhani.Kati ya majirani zetu ambao wanapaswa wawe soko letu kubwa la bidhaa za kilimo na biashara nyingine ni Wakenya.
Ila Kati ya watu ambao tumekuwa tukiishi nao Kama maadui kwa miaka sita Sasa ni Kenya.
Nchi inayotaka kuinua wakulima na wafanyabiashara uwekeza kwenye diplomasia ya eneo lilipo soko. Sisi sijui Wataalamu wa mahusiano wanaona Nini huko ofisini Hadi kila siku waibue migogoro na Kenya.
Sasa hivi wenzetu wanaona ni vyema waagize chakula kutoka Brazil na Mataifa mengine ya mbali kuliko kutegemea Tanzania, matamko yamekuwa mengi na yasiyo na tija kwa ustawi wa wakulima wetu.
Na hii imepelekea hata uhusiano wetu na nchi nyingine za Afrika Mashariki uwe na mashaka.... protocol ya free movement of goods and services imebaki kuwa kwenye makaratasi tu. Tubadilike, tukitaka kukua kiuchumi tuwekeze kwenye mahusiano na waliotutangulia kiuchumi, tujifunze kwa china na Marekani.
Kwa Kweli kuwaunguza wale Vifaranga haikua sawa wangerudishwa huko ingekua sahihi zaidiCcm inakurupuka kwa misifa ambayo haina maana, jaribuni kutafuta mzizi wa fitna View attachment 1718502
Kwenye hili diplomasia yetu imefeli wapi?Jifunze diplomasia na elimu ya biashara ndipo utoe challenge,la sivyo,kaa kimya!
Wewe fanyia tathmini hayo masaburi unayotumia kufikiri. Ni mjinga wa mwishoFala wewe, kichwani sijui umejaza nini hebu kifanyie tathmini kwanza kichwa chako.
Sasa kwanini usilaumu ujinga wa viongozi wa Kenya?kwa hivyo wewe unaona ni sawa wananchi wa pande zote waumie kwa sababu ya UJINGA wa viongozi wao?!.
kumbuka hao maviongozi mshahara na posho zao ziko palepale!.
Kosa la Magufuli kwenye hili ni nini?Kwanini ya Rais wa TLS anaendelea kutrend toka jana? Naweka nukuu yake "Kuna mtu anataka nchii yote mtu mmoja awe ndiye anafikiria kwaajili yetu tu". Ndo hali ilivyo kwa vijana wa CCM. Jamaa akisema hata leo wang'olewe meno mawili mawili ili wapunguze kula nyama watasema "Rais ni mzalendo kwelikweli hataki tunenepe hovyo."
Sasa hapa unamlaumu nani? Waliofunga si wakemya kwamba hayo mahindi yenu yana sumu? Selikali ya tz kosa lake liko wapi?ww fala kilimo cha tz wateja wetu wakubwa ni kenya
mipaka ikifunguliwa gunia la mahindi linauzwa hadil 120k na sometimes wanalifata hap hapa
tangu wafunge gunia linacheza 30-50k
Acha ujinga maana hata tuta la viazi huna. Leo Rukwa na Katavi mahindi gunia 30000 na mengine yanakomaa shambani. Tunapigwa pin ya soko unasema viongozi wako siyo wajinga!? Viongozi gani unaoongelea? Hawa wanaojali posho za vikao kuliko ustawi wa wakulima!?!Wakulima Walime, Watanzania tule kwani Kenya tu ndo wanamatumbo peke Yao?.. Viongozi wetu sio wajinga na sisi Watanzania tupunguze uoga, changamoto kidogo tu mshaanza kupost Mabandiko, Kama hawanunui wao tutauza kwingine watakapo hitaji, ikishindikana tuuziane humuhumu Maisha yaendelee mi hua hainingii akilini kununua debe la Mahindi 20,000 wakati mengine yanapelekwa Kenya huko.. hii Ni Vita ya kiuchumi na Kenya wameshaona Kuna uwezekano wakageuka koloni la Tanzania.. Punguzeni Uoga Vijana, maendeleo hayaji bila changamoto.. Sengwile Makamanda!!
Usishangae huyo ndo Hussein Bashe.Hii nchi ina viatu sana