Nasikitishwa na uhusiano wetu na Kenya, unaumiza wakulima na wafanyabiashara

Nasikitishwa na uhusiano wetu na Kenya, unaumiza wakulima na wafanyabiashara

We unaeandika utumbo huu ni mkulima au umejiskia tuu uandike!!?
Unajua shida tunayoipata sisi mipaka ikifungwa mbeha wewe!!?

Alafu nmekumind kishenzi yaan.
Achanane tu huyo anafurahisha mdomo wake, hapo hata kulima tu nusu eka ukute ajawai
 
Wakulima Walime, Watanzania tule kwani Kenya tu ndo wanamatumbo peke Yao?.. Viongozi wetu sio wajinga na sisi Watanzania tupunguze uoga, changamoto kidogo tu mshaanza kupost Mabandiko, Kama hawanunui wao tutauza kwingine watakapo hitaji, ikishindikana tuuziane humuhumu Maisha yaendelee mi hua hainingii akilini kununua debe la Mahindi 20,000 wakati mengine yanapelekwa Kenya huko.. hii Ni Vita ya kiuchumi na Kenya wameshaona Kuna uwezekano wakageuka koloni la Tanzania.. Punguzeni Uoga Vijana, maendeleo hayaji bila changamoto.. Sengwile Makamanda!!
Wewe ni mkulima ama unaongea tu? Unafahamu shuruba na gharama za kilimo? Unajua bei za pembejeo na vibarua?? Hilo ni tatizo kwa mkulima hakuna mfano jamaa wakibana wakulima msimu ujao wa mavuno twafa!
 
Ni kweli, serikali ilitazame suala hili kwa mapana yake. Kwa kuongzea tu ndugu mleta mada, suala hili halijawaathiri tuu wafanyabiashara Bali hata sisi wakulima.
Hivi Sasa gunia la mahindi Katavi linauzwa kwa Elf 35000 badala ya 80000 Kama zamani. Mwaka Jana wakulima waliitikia vizuri wito wa Mh Rais kuchapa kazi. Basi serikali itusaidie kwa kuweka mazingira mazuri/ kututafutia solo la mazao hayo.
 
Wakulima Walime, Watanzania tule kwani Kenya tu ndo wanamatumbo peke Yao?.. Viongozi wetu sio wajinga na sisi Watanzania tupunguze uoga, changamoto kidogo tu mshaanza kupost Mabandiko, Kama hawanunui wao tutauza kwingine watakapo hitaji, ikishindikana tuuziane humuhumu Maisha yaendelee mi hua hainingii akilini kununua debe la Mahindi 20,000 wakati mengine yanapelekwa Kenya huko.. hii Ni Vita ya kiuchumi na Kenya wameshaona Kuna uwezekano wakageuka koloni la Tanzania.. Punguzeni Uoga Vijana, maendeleo hayaji bila changamoto.. Sengwile Makamanda!!
Bwana kwa sababu ukitoka kucheza pool table na kubet unakuta chakula kwenye hotport una haki ya kuongea haya. Lakini kwa wale tunaoshinda maporini uko tukilima tunajua madhara yaliyoko mbele yetu. Hoja kwamba tutauza nchi zingine nayo ni kujipa matumaini tu. Sijui kama una kumbukumbu vizuri mwa 2017 tulihangaika kutafuta soko la mahindi hadi yakaharibikia ndani. Kwa kipindi hicho tumbo lako ulimwazima nani? Unakumbuka kilichowakuta wakulima wa Mbaazi ? Bei imeporomoka kutoka 3,000/= hadi TZS 200/= kwa kilo. Korosho mnakumbuka pia kilichotokea? Kwahiyo tusijipe matumaini. Hali itakua mbaya. Ni kilio kwa wakulima wa mahindi.
Musimu huu soon tutauza gunia la kilo 100 kwa elfu 20, imagine umelima ekari moja kwa sh laki moja na ishirini, umepanda mbegu kilo kumi kwa ekari, una walipa watu wa kuhudumia shamba, na wastani wa ekari moja ni gunia 15. ACHENI USHABIKI KUNA WATU WATAUMIA.
 
Fuatilia hotuba ya JK akilihutubia bunge la kenya wakati akitoa salamu zake za kuwaaga majirani zetu kenya, yule aliyetabiliwa na JK kwamba anaweza kuja na akaharibu mahusiano Kati yetu tayari yupo ikulu ya TZ"
 
Nilitamani kuanzisha uzi kuhusu hili suala lakini nashukuru kwa bandiko hili maana limelenga kile nilichotaka kusema.

Binafsi nimekuwa mdau wa kilimo kwa muda mrefu sana, kuanzia kulima mpaka kushiriki makongamano mbalimbali yanayohusiana na sekta ya kilimo na kuna hoja kadhaa ambazo wakulima wamekuwa wakizitoa kwa Serikali lakini kutofanyiwa kazi na hii sasa ndio majibu yake, japo inabidi kutafiti zaidi kama kweli Kenya wanasema ukweli au ndio VITA YA KIUCHUMI.

Hoja kubwa ambayo imekuwa ikitoka mara kadhaa ni kuhusu suala la mbegu, wadau wameshauri mara nyingi turudi kwenye mbegu zetu za asili maana hizi tunazoambiwa za kisasa zina changamoto nyingi sana, mojawapo ni hii ya kushambuliwa na wadudu hali inayopelekea wakulima kutumia madawa mengi sana ili kuweza kulinda mazao yao, na hili nimelishuhudia kwa macho yangu, sasa kwa hali hii tutajiteteaje kwamba mahindi yetu hayana sumu?

Wakulima watanielewa vizuri kwenye hili,

Na hapo nimeongelea madawa kwenye mahindi pekee, rudi kwenye nyanya, matikiti nk, huko ndio usiseme, dawa inayomwaga huko huwezi amini kwamba inaingia tumboni kwa binadamu.

Mimi nashauri wadau wa kilimo wasikilizwe, ianzishwe bank ya mbegu zetu za asili kuliko kutegemea hizi za kisasa tunazoletewa maana wakati mweingine kuzitunza ni ngumu sana kwasababu ya kushambuliwa na wadudu.

Halafu kama hatuwaamini Mabeberu ( Bill Gates) kwenye chanzo za COVID kwa nini tunahamasisha wakulima wetu watumie mbegu zao, Rejea matumizi ya mbegu zilizofanyiwa GMO huku nako kuna madhara mengi zaidi.
Awamu hii kila mjinga anaishauri Serikali cha kufanya na bahati mbaya sana ushauri huo unasikilizwa na kukubalika zaidi kuliko wa Watalaamu. Waganga wa kienyeji wanashauri dawa bora za mitishamba, huyu nae anashauri mbegu zilizitumiwa na Mtwa Mkwawa ndo zitumike badala ya zile zinazoboreshwa mara kwa mara. Mbegu hizo za mahindi za kuvuna magunia matatu kwa eka bado zipo na Wakulima wengi bado wanazitumia siyo kwa sababu anazotoa huyu mjinga bali ni kukosekana kwa uelewa. Mabeberu hawatumii mahindi kwa chakula wala hawalimi sana mahindi ingawa wanatumia sana kama chakula cha mifugo kwa hiyo hawawezi kutumia raslimali zao na wakati kuboresha mmea ambao ni mgeni katika mazingira yao. Watalaamu wetu wanajitahidi sana na wanafanikiwa kuboresha hizo mbegu asili ili mkulima avune magunia 40 kwa eka ili apate chakula cha kutosha familia na ziada wauziwe wengine pamoja na mabeberu wakalishe mifugo yao. Magonjwa ya mimea, wanyama hata ya Binadamu yapo tu na mapya yanaendelea kujitokeza kama Changamoto ya kupumua na vita ya kuyaangamiza ni endelevu kwa juhudi za Watalaamu wetu na mabeberu.
 
Kati ya majirani zetu ambao wanapaswa wawe soko letu kubwa la bidhaa za kilimo na biashara nyingine ni Wakenya.

Ila Kati ya watu ambao tumekuwa tukiishi nao Kama maadui kwa miaka sita Sasa ni Kenya.

Nchi inayotaka kuinua wakulima na wafanyabiashara uwekeza kwenye diplomasia ya eneo lilipo soko. Sisi sijui Wataalamu wa mahusiano wanaona Nini huko ofisini Hadi kila siku waibue migogoro na Kenya.

Sasa hivi wenzetu wanaona ni vyema waagize chakula kutoka Brazil na Mataifa mengine ya mbali kuliko kutegemea Tanzania, matamko yamekuwa mengi na yasiyo na tija kwa ustawi wa wakulima wetu.

Na hii imepelekea hata uhusiano wetu na nchi nyingine za Afrika Mashariki uwe na mashaka.... protocol ya free movement of goods and services imebaki kuwa kwenye makaratasi tu. Tubadilike, tukitaka kukua kiuchumi tuwekeze kwenye mahusiano na waliotutangulia kiuchumi, tujifunze kwa china na Marekani.
Pamoja na kutopinga kila uliloandika, lakini nakuomba ujielimishe kwanza ili ujue tatizo kwa kina zaidi ya hivyo unavyodhani.

Hapa unaona upande mmoja tu wa Tanzania, umejaribu kutazama na huko kwingine mchango wake katika tatizo ukoje?

Kwa sasa nakupa hiyo 'homework' fupi kwa kuanzia.

Ukitaka tutalijadili hili kwa kina chake.

Na ifahamike, sijatetea makosa ya serikali hii kama yapo, naitetea Tanzania tu.
 
Mi natamani mpaka wetu na kenya ufungwe kabisa,tusihusiane kabisa yan..hawa wakenya si wenzetu kama si tunavyowachukulia..anyway,jamaa wanaumia sana na lile bomba la hoima,
 
kwa hivyo wewe unaona ni sawa wananchi wa pande zote waumie kwa sababu ya UJINGA wa viongozi wao?!.

kumbuka hao maviongozi mshahara na posho zao ziko palepale!.
Sasa kwanini usilaumu ujinga wa viongozi wa Kenya?
 
Kwanini ya Rais wa TLS anaendelea kutrend toka jana? Naweka nukuu yake "Kuna mtu anataka nchii yote mtu mmoja awe ndiye anafikiria kwaajili yetu tu". Ndo hali ilivyo kwa vijana wa CCM. Jamaa akisema hata leo wang'olewe meno mawili mawili ili wapunguze kula nyama watasema "Rais ni mzalendo kwelikweli hataki tunenepe hovyo."
Kosa la Magufuli kwenye hili ni nini?

Kwamba uhusiano na Kenya siyo mzuri?
 
ww fala kilimo cha tz wateja wetu wakubwa ni kenya
mipaka ikifunguliwa gunia la mahindi linauzwa hadil 120k na sometimes wanalifata hap hapa
tangu wafunge gunia linacheza 30-50k
Sasa hapa unamlaumu nani? Waliofunga si wakemya kwamba hayo mahindi yenu yana sumu? Selikali ya tz kosa lake liko wapi?
 
Wakulima Walime, Watanzania tule kwani Kenya tu ndo wanamatumbo peke Yao?.. Viongozi wetu sio wajinga na sisi Watanzania tupunguze uoga, changamoto kidogo tu mshaanza kupost Mabandiko, Kama hawanunui wao tutauza kwingine watakapo hitaji, ikishindikana tuuziane humuhumu Maisha yaendelee mi hua hainingii akilini kununua debe la Mahindi 20,000 wakati mengine yanapelekwa Kenya huko.. hii Ni Vita ya kiuchumi na Kenya wameshaona Kuna uwezekano wakageuka koloni la Tanzania.. Punguzeni Uoga Vijana, maendeleo hayaji bila changamoto.. Sengwile Makamanda!!
Acha ujinga maana hata tuta la viazi huna. Leo Rukwa na Katavi mahindi gunia 30000 na mengine yanakomaa shambani. Tunapigwa pin ya soko unasema viongozi wako siyo wajinga!? Viongozi gani unaoongelea? Hawa wanaojali posho za vikao kuliko ustawi wa wakulima!?!
 
Back
Top Bottom