Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

TumainiEl

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
6,782
Reaction score
12,716
Natabiri ya kuwa jaribio lolote la kubadili katiba na kurefusha ukomo wa Rais litazua Moto wa kisiasa ambao haukuwahi kutokea tangu kuwepo kwa Taifa hili.

Yani hamtoamini wala kudhania. Itakuwa ni siku mbaya na nzito kwa Taifa ndipo sote tutaamini kweli kuna deep state in side state.

Nasali Jambo hili lisitokee wala kusemwa tu. Madhara yake yatatutesa sana kama Taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwanza kabisa, niseme mimi si mtetezi wa Magufuli wala CCM. Ni mtetezi wa haki na mchambuzi wa siasa na mantiki.

Magufuli nishamsema sana, hivyo, ninachoandika hapa si kwa sababu ya kumtetea Magufuli.

Twende kwenye hoja baada ya dibaji hiyo.

Magufuli ameshasema mara kadhaa hataki kuongeza muhula wa urais.

Kwa nini mnafanya hili suala kuwa hoja?

Hususan kama kuna makosa mengi sana ambayo Magufuli ameshayafanya ambayo yanaweza kujadiliwa kama hoja halali, factually, na si speculation?

Mimi naona wapinzani wa Magufuli kuongelea hili kunaonesha yafuatayo.

1. Hawana focus. Wanakuwa kama mtu tajiri mwenye hela nyingi sana (wana hoja nyingi sana halali za kumsema Magufuli) lakini ambaye bado anaenda kukopa hela benki kwa riba kubwa sana (licha ya kuwa na hoja nyingi halali za kumsema Magufuli, wanaenda kukopa hoja ambayo haina uhalali ya kuhusu makosa ambayo hayajafanyika,kiasi cha kufanya watu wahoji umakini wao).

2. Hawajadili mambo kwa facts. Bali kwa speculations.

3. Wanahukumu kosa ambalo wanafikiri litatetendeka, badala ya kuhukumu kosa lililotendeka. Hili ni jambo hatari. Kwa msingi huu, Magufuli anaweza kuamka siku moja akasema ameota waponzani wanataka kumpindua. Akawafunga wote.

4. Wanapoteza muda na nguvu kujadili speculations wakati kuna mambo muhimu ya kubana sasa hivi kama wizi wa kura katika uchaguzi, tume huru ya uchaguzi, katiba mpya etc.

5. Wanaonesha paranoia. Kitu ambacho hakifai katika uongozi.
 
Mkuu,
Kwa hali ilivyo mtaani jambo lolote ambalo halihusu namna ya kuwapunguzia wananchi ugumu wa maisha litakutana na ukingazi mkubwa sana maana hali halisi tuliyo nayo sasa ni "we have nothing to loos by fighting against the tyranny" watujaribu waone!
 
Sorry ina maana hata nyakati kusoma hujuwi? Basi poa asante
Unakubali mtu kuhukumiwa kwa kosa ambalo hajalifanya?

Yani nikwambie wewe unaonekana utaiba kesho.

Halafu wewe useme sitaiba.

Halafu tukupige mawe kwa madai kwamba utaiba kesho.

Unakubali?

Kwa nini mnamhukumu mtu kwa makosa ambayo mnafikiri atafanya 2025, wakati tayari ana.makosa aliyoyafanya ambayo mnaweza kumhukumu bila kubashiri mambo yatakayotokea mwaka 2025?

Mnafanya ionekane kama vile Magufuli ana uhaba wa makosa aliyoyafanya, na hivyo, mnalazimika kumtungia makosa atakayoyafanya mwaka 2025 na kumhukumu.kwa hayo.

Magufuli ana uhaba wa makosa aliyoyafanya tayari?
 
Natabiri yakuwa jaribio lolote la kubadili katiba nakurefusha ukomo wa Rais litazuwa Moto wa kisiasa ambao haukuwahi kutokea tangu kuwepo kwa Taifa hili.

Yani hamtoamini wala kudhania. Itakuwa ni siku mbaya na nzito kwa Taifa ndipo sote tutaamini kweli kuna deep state in side state.

Nasali Jambo hili lisitokee wala kusemwa tu. Madhara yake yatatutesa sana kama Taifa.

Mungu ibariki Tanzania.

Katiba itabadilishwa na kutakua shwari Kama ilivyokua ktk uchaguzi huu. Siku Magu anaapishwa nchi nzima ilikua busy na mapokezi ya bi Zari na Diamond.

Kwa aina ya raia wa nchi hii Magu atatawala hadi mola wake atakapomtwaa.
 
Back
Top Bottom