Natafuta Audio Clip ya zaidi ya Dk 5 ambayo Rais Samia anazungumza Kiingereza

Natafuta Audio Clip ya zaidi ya Dk 5 ambayo Rais Samia anazungumza Kiingereza

We mjinga, tega sikiontukuelimoshe. Huwezi kutenganisha uelewa wa mtu na kujua kiingereza kwa hapa Tanzania. Asiyejua kiingereza maana yake hajaelimika. Kwasabb elimu yetu inatolewa kwa lugha ya kiingereza. Sasa mtu ataipataje elimu kama lugha inayotumika kuipata hiyo huijui??

Nchi unazoona zomeendelea lkn watu wake hawajui kiingereza ni kwamba wanatumia lugha zao kufundishia. Hawatumii Kiingereza.

Umenielewa we mfuasi wa jiwe?? Halafu hata wewe hujui kiingereza ndiyo maana inakuuma sana tukiwakosoa wasiojuq kiingereza. Pole sana
Yaan huna hata uwezo wa kujenga hoja.Kama uwezo wako wa kujenga hoja ni mdogo kiasi hiki,ni heri ukae kimya. Elewa hoja zangu kama ifuatavyo:. 1.Tafiti zinaonyesha ,nchi nyingi zilizoendelea zimetumia lugha zao shuleni .Mfano China,Urusi,Japan,Uingereza ,nk. 2.Ili tuendelee tunahitaji kutumia lugha yetu.Wizara ya elimu ibadilishe sylabus zote kutoka kiingereza ziwe kiswahili.Maneno ya technology yabadilishwe yawe ya kiswahili.Tutapata taabu kwa muda mfupi Lakin watu watasoma na kuelewa vizuri.Kwa Sasa wengi wanakariri tu.Hawaelewi vizuri,kwa kuwa wanajifunza kwa kukariri tu kiingereza.Wangejifinza kwa kiswshili wangeelewa vizuri Sana.China,Japan,Korea,India,wameendelea kwa kutumia lugha za kwao.Sisi tumekamatwa na ukoloni ,hata akili zetu hazifanyi kazi kwa ajili ya ujinga na upumbafu mwingi.Yaan unasifia mtu kuongea kiingereza?Na Utaona ,mpaka ujinga ulikolea tukapewa mpaka majina ya wakoloni.Peter,Samuel,John,Patrick.Ikinga mtupu.Hatutaki vya kwetu.Masatu,Ngunagwa.Ni ngumu Sana kuendelea kwa ajili ya kupenda vya watu.
 
.Maneno ya technology yabadilishwe yawe ya kiswahili.
Sasa tulinza munkari wako nami nitulize wangu tuelimishane.

Unashauri tuibadilishe maneno ya teknolojia yawe kwa kiswahili. Teknolojia ya nani? Huoni kwamba tutaendelea kukariri zaidi?

Hao wanaotumia lugha zao wamepiga hatua kiteknolojia na hivyo Wana teknolojia zao. Wanatengeneza vyao, wanaviita majina ya kwao na wanawafundisha watoto kwa lugha yao.
 
Ondoa upumbavu kichwani mwako, lugha ni zaidi ya utamaduni. Lugha ni nyenzo ya mawasiliano, ndio maana unaona Umoja wa Ulaya wanatumia Kingereza japo wote sio waingereza na Uingereza haipo EU.
Umesema kweli tupu,na umemaliza mjadala.Ni ujinga kupenda lugha isio yako.Lugha ndio utamaduni wako,utapendaje utamaduni usio wako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sahihi
Ni kwamba elimu yetu tunafundishiwa kwa kutumia english na hivyo english imekuwa ni kipimo cha moja kwa moja cha kiwango cha elimu ya mtu kwa maana kama kawa huwezi kuzungumza vizuri kiingereza tafsiri yake hukuwa unaelewa masomo darasani.
 
Mambo hayaishii hapo tu Mkuu, sheria zetu ziko kwa lugha ya kigeni zaidi. Na sidhani kwamba ni kosa Lisu kumsema mwanasheria mwenzake kushindwa kuongea kiingereza, maana mengi kwenye kozi zao yanafundishwa kwa kiingereza. Sasa utashangaa alipitia tundu lipi akaukwaa uanasheria. Na si hivyo tuu, msomi ni vizuri akaupinda mgongo afahamu angalau lugha kuu mbili ikiwepo moja ya kigeni. Kwani kiingereza nani alikudanganya ni lugha ya kutisha? Watu waache uvivu. Zipo nchi ukifika unakuta watu wengi wanaongea lugha nne. Niliwahi kufika duka moja uswiss nilipokuwa naulizia bei ya kitu kwa kiingereza, mara akaingia mteja, muuzaji akaanza kuongea naye kifarannsa, mara akaingia mwingine akaanza kuongea naye Kitaliano, mara akaingi mwingine wakaanza kijerumani. Nilipouliza inawezekanaje kirahisi namna hiyo nilijibiwa kuwa nchini mwao hiyo ni kawaida watu huongea lugha nne hadi tano.
Sasa kinachotushinda kujifunza mbili tu (ukiacha ya kabila lako) ni nini?.
Tuache kujilegeza tuhimizane tusonge mbele.
Lugha yeyote ile maana yake ni mawasiliano baina ya wanadamu, kama mnaelewana kwenye hiyo lugha mnayoongea inatosha hivyo hivyo !! Lugha ya kiingereza sio maana yake kusoma sana, wapo wengi tu wanaongea kiingereza kizuri lakini hawana elimu yeyote kubwa,
 
Hivi ni Mungu alitupa akili hii watanzania au tumejitafutia wenyewe ya kufuatilia raisi kama anaongea kiingereza kizuri au la.
Inasikitisha sana.
 
Hata waafrika wa nchi zingine za Afrika hatuoni wakifanya ujinga kama huu, ni ajabu sana kuhukumu uelewa na elimu ya mtu kwa kuangalia uwezo wao wa kuongea kiingereza.

Ni aibu sana.
 
Ila mimi sioni kama ni sahihi kwa sababu unaweza ukashindwa kuongea na kuandika vizuri ila ukaweza kusoma na kusikia kiingereza na hivyo ukaweza kupata maarifa yeyote yaliyo kwenye lugha ya kiingereza.
 
"Nitafurahi sana nikipata audio Clip ambayo itazidi dk 5 Rais wetu Mpendwa akichana mistari kwa kiingereza"👇👇

Screenshot_20220221-105600.png
 
Hapo shida iko wapi? Toa makosa uliyoyaona then nikusaidie.
Is it grammatically correct to say ;

Thanks for the chance = hapo katafsiri kiswahili kwenda kingereza moja kwa moja.

Alipaswa kusema Thank you for this opportunity.

Vile vile hakupaswa kusema ;

Iam really aprreciate being here.

Alitakiwa kusema = i am thankful being here.
 
Is it grammatically correct to say ;

Thanks for the chance = hapo katafsiri kiswahili kwenda kingereza moja kwa moja.

Alipaswa kusema Thank you for this opportunity.

Vile vile hakupaswa kusema ;

Iam really aprreciate being here.

Alitakiwa kusema = i am thankful being here.
Wewe ndio upo zama za mawe, yupo sahihi sana.
 
Back
Top Bottom