Natafuta mganga wa kienyeji konki

rozali, mawe na udongo kwa ajiri ya nn kama sio uchawi sasa huo
 
Duh ndugu yani nimesoma nimeumia sana, naomba uniruhusu nikufate pm ndugu yangu kama hautojali
 
Acheni akili mgando hayo masharti yako pande zote,kwa Mungu Nako Kuna Masharti tena makubwa tu! Muhimu ni Yale masharti ambayo yanakupa matokeo chanya kw upande wako.
Babu zetu hawakujua Kuna Yesu na Allah walikuwa na Miungu Yao na walifuata masharti na kufanikiwa!
Pia kama hayajakukuta ya Dunia utapuuza waganga ila kwangu nawaita WATAALAMU WA JADI, kiukweli naamini harakati zao na tangia nimekuanao karibu mambo yangu yanasonga sana tu.

Kwa ufupi ukiwa na Elimu nzuri ya darasani na kufika Elimu ya Juu alafu ukapata MTAALAMU sahihi na mzuri utafurahia matunda ya Elimu Yako na hutozulula na bashasha KAMWE riziki utazipata nyingi sana.
Nasisitiza kupata MTAALAMU SAHIHI.
 
Zamani nilikuwa naona Mfanyabiashara akifirisika labda aliendekeza Starehe au kakosea masharti ya Mganga ila yalivonikuta toka hapo Namuheshimu sana Mjasiriamali alienizidi na ambae anapitia changamoto naamini kabisa kuna mambo mengi hapaswi kulaumiwa au kusemwa vibaya
 
Usiite mawazo ya mtu akili mgando, hili ni jukwaa huru sio kila unacho amini wewe ni lazima na mimi nikiamini, we mshauri kila unacho amini ni sawa na mimi nimshauri kile kwangu naona ni sawa.

MWISHO YEYE ATACHAGUA NI LIPI LITAMFAA.
 
Haya mambo yasikie tu,unaweza kutupiwa kitu yani likitoka tatizo moja linaingia lingine kila unachofanya hakiendi,kila kitu kinafeli hadi watu wanakukimbia,kumbe unakuta kuna mtu kafanya yake anacheki movie inavyoendelea.Haya maisha usipopambana binadamu watakufanya kitu kibaya sana!Utasikia ooh alikuwa tajiri akafilisika,mzuri lakini haolewi,ana akili lakini hafanikiwi nk hapo unakuta watu walishafanya yao muda tu
 
Ukisoma kisa cha huyu bwana utakubalina na Mimi kwamba hata huko kwa Yesu na Allah Kuna MASHARTI yakufuata ili ufanikiwe. Kwa ufupi tu Mafanikio yeyote lazima yaambatane na MASHARTI OVER.
Muache kubeza MASHARTI ya waganga etii oohhh kwa Waganga Kuna MASHARTI acheni kabisa huo ni upotoshaji.
 
Inauma sanaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…