Natafuta mganga wa kienyeji konki

Natafuta mganga wa kienyeji konki

Utatoa shukrani gani ili nikuunganishe na mganga konki! Yuko Kwa Msisi Tanga! Yaani hata ukitaka kumgeuza mtu kuwa nyoka, anageuka! Ukitaka kumuweka kwenye chupa, ni dakika 0 tu.

Sharti ni kutakiwa tu kutoa hiyo shukrani isiyo na hiyana, kabla ya kuunganishwa.
Mkuu! Na wewe hauko mbali kwenye connection za namna hii??
 
Sasa mtoa mada awa waganga wote ulio pewa utaanza na yupi?
Lkn ukiwez tumia akili/fikra kudeal na binadamu for future inakuwa poa..
Ukiaanza kwend kwa waganga utawaumiz watoto wako/kizazi chako kitaaribik maana ukiende kwa mganga umashaingia kweny agano lingin so ata watoto wako watafuatw so be careful
 
Kuna Mwanangu mmoja,alidhulumiwa na rafiki ake baada ya kudhulumiwa huyo rafiki ake akamfanyia mbaya nyingine ya maisha,jamaa akapambana akatatua matatizo yote aliyosababishiwa na huyo rafiki ake aliemdhulumu.

akaja akaniambia CONTROLA nataka kwenda kwa mganga kumtoa uhai flani,nikamuuliza uko serious? akasema YES nipo serious,nikamshauri usimuue tumfanyie tu uhuni wa mjini ili abaki na uhai wake ila awe na adabu kila akikuona.

akasema hapana Boss nataka kumpoteza sitaki kumuona kabisa, nikamwambia Poa baba ngoja nikutaftie namba za mtu ila andaa nauli yako kabisa,akasema haina shida.

Nikampa namba kweli wakaongea akaambiwa apande gari aende yeye kama yeye akashtaki kwa mwalimu mkuu (mganga) kweli kesho yake mwanangu akaniaga akaniambia CONTROLA mi nasepa kwa mzee kufanya yangu.

Safari ikaanza jamaa akaenda,kufika akashtaki bibi (mganga) akamuuliza mara kumi kumi,kijana uko tayari kufanya unachotaka,jamaa akasema ndio bibi nimeamua kweli.

Bibi (mganga) akamwambia kama kweli uko tayari naomba kaniletee PAKA mweusi, asiwe na doa popote pale mlete,Nataka ukimleta ndio tumtumie kufanya unachotaka.

Mwanangu akasema sawa bibi,akamuachia bibi sadaka pale akamuaga akaondoka akarudi town, weekend tuko zetu nyama choma tunachangamsha meno ndio jamaa ananisimulia safari yake ilivyokua na anahitajika kufanya nini.

nikamuuliza sasa mwanangu paka mweusi unamtoa wapi? akaniambia tulia wewe controla mimi mwenyewe paka mweusi nawajua paka weusi walipo,basi tukataniana pale mwisho tukaachana.

Nikaendelea na mishe zangu,jamaa na yeye na mishe zake huku akitafuta paka mweusi, tafuta tafuta na wewe hajapata, Akapata mfugaji mmoja wa Paka yupo bagamoyo (huyu n mfanyabiashara wa paka) ana paka kila aina wana majina ki ukweli ukifika pale unaweza hisi sijui wale n sungura,kumbe ni paka.

kufika pale jamaa paka mweusi anae mmoja tu ila huyu paka ana kidoti cheupe kidogo sana mkiani,jamaa angu akasema nipe huyo huyo namtaka.

nikamvuta pembeni nikamwambia,(oya bibi kakwambia anataka paka mweusi tiiii huyu si ana kidoti?) akaniambia tulia weweee najua ntavyofanya.

Akatoa pesa akahesabu noti kadhaa,akampa muuza paka tukaekewa paka wetu kwenye boksi tukaenda mtia kwenye gari haoo tukageuka kurudi town.

Kufika town,jamaa ana furaha isiyo kifani ila mimi moyoni kengele ya Alarm ilishalia,tukaenda kwake nikamuacha na paka wake mimi nikaenda zangu home.

Huku nyuma mwana akaenda nunua SUPER BLACK akamchovya paka mkia kwenye kile kidoti,akatulia ikakauka akampga blower nyoya likawa jeusiiii paka akawa mweusi tiiiiiiiiii,hana tone la weusi hata mahali hata upewe umkague mwezi mzima huwezi jua kitu.

Akaniambia BOSS naenda fanya kazi yangu rasmi,akaniaga akaenda kwa bibi jamani jamani jamani duniani kuna waganga feki na kuna waganga ORIGINAL

Bibi aligundua yule paka ana doti mkiani na rafiki angu mimi akafukuzwa kwa hasira na akapewa adhabu juu (siwezi zisema).

Lengo la hii simulizi fupi ni nini Maya? kuwa makini sana na waganga wana masharti magumu (hasa wale waganga OG) na fanya ufanyavyo ukishafanya kazi na mganga lazima kuna sharti utabaki nalo maishani mwako,hasa hili la kutoa uhai wa mtu (sijasema unataka kutoa mtu uhai)

waganga hawaui bali wanachukua wale watu wote mnaotaka wauliwe,kisha unapewa huyo mtu umfanye unachotaka. Huku nyuma ndugu watajua mtu kafa ila ukweli n kwamba waganga hawaui ukitaka ku ua utamuua mwenyewe kwa mikono yako. Kuwa makini na waganga maya.

Kama kuna aliekukera unataka tumshikishe adabu ni simple sana, nina team ya adhabu uje na pesa tu nzuri useme unachotaka halafu utaona atachofanywa huyo aliechokonoa furaha ya moyo wako,ila waganga ni kujitafutia stress tu.

Nitafute nikupe team ya WASIOJULIKANA kwa bei rahisi sana.

Ila kama ni mganga wa ukweli na umedhamiria,haya ila sikushauri narudia tena sikushauri.
Kwahiyo mwanangu wewe una gang la uhalifu na unajisifia kabisa lipo kikazi ipo siku yenu, kuna jamaa mmoja yule jamaa ni mzambia ni ana sura ya kikatili alikamatwa mwanza polisi walimhisi wakamkamata aliambiwa afungue simu yake alipoifungua polisi walikuta jamaa kafanya mauaji mengi sana maiti 20 na kutuma feedback kwa waliomtuma, siku ya mwizi 40 ipo pale pale
 
Back
Top Bottom