Natafuta mtu mwenye asili ya Kihindi kumuajiri au kufanya naye biashara

Natafuta mtu mwenye asili ya Kihindi kumuajiri au kufanya naye biashara

Mkuu wazoefu wa biashara wanasema ni heri ufanye kazi na watu unao weza kuwabadilisha muda wowote ila sio kutoa hisa
Kumiliki biashara moja watu wawili au zaidi ni kuhatarisha biashara yako/yenu
Ubia huu nina amani kufanya na muhindi anaejielewa ambao wengi wapo committed na utafutaji sisi hela ndogo tu ukipata na ukichaa unaanza hapo hapo
 
Asante kwa kunielewa
Nia yangu kubwa ni hivi biashara ya vifaa vya pikipiki ni ya kuuza vitu vidogo vidogo so nikishiriki na mtu ambae hana akili ya kuelewa kuwa pale ndo ofisini kwetu pa kupatia ugali lazima nitajutia tu maana kinachoniuma ni hii style niliyoitumia kukusanya hizi pesa nimesave bila kutoa kwenye account ya UTT AMIS miaka 6 so nahisi gawio linalotoka halifanani na ukubwa wa hela yangu nimeanza kuwaza hata nikikosa huyo muhindi itabidi nitafute binti mwenye elimu ila asie na mambo mengi awe anakaa ndani ya duka coz siwezi hesabu kila siku bidhaa itakuwa biashara mateso kwangu.

Unakosea mkuu,, kusema biashara mateso kama wewe mwenye biashara hutaki kuteseka nani sasa ateseke kwa ajiri yako??? Kama unapenda bata nenda tu katumie hizo hela kwenye hiyo bata unayotaka taka
 
Msichana wa kichanga umesema unawazia kumuajiri? Ila hivi kweli kwa biashara ya 70 mil umuajiri mhindi? Faida yote utamlipa mshahara, yaani usijitetee wala nini, hadi hapo naona huwezi biashara kabisa wewe, maana huwezi management ya biashara, na kama huwezi usimamizi jua hakuna biashara itakuwa, usimamizi ndio kigezo kikubwa sana kwa biashara kukua, kumtegemea mtu asimamie, tayari ni dalili 99% ya kufeli, capital sio issue, watu hawajui tu kwanini biashara zinakufa, capital ziko sana tu, tatizo unasimamia vipi hadi biashara yako ikue, kuna ushindani, kodi, kudhibiti uwizi, kudhibiti matumizi yasio ya lazima kwenye biashara yako na kuijua vema biashara yako..
Kila la kheri
 
Utatimua wangapi huku wanakuibia wewe hujui

Kumpata mtu mwaminifu ni bahati tu,, kwahiyo huwezi ukampata mtu mwaminifu bila kumpa nafasi ya kufanya kazi kama vipi tutafute watu kama sisi tuliopigika kimaisha lakini pia uendeshaji wa biashara na wafanyakazi unatakiwa utumie saikolojia vizuri kumtawala huyo mfanyakazi, sio yeye ndio akutawale kisaikolojia hata ukipata huyo muhindi akijua kucheza na akili yako atakupiga tu
 
Mkuu kuhusu ubia h
Ubia huu nina amani kufanya na muhindi anaejielewa ambao wengi wapo committed na utafutaji sisi hela ndogo tu ukipata na ukichaa unaanza hapo hapo
Mkuu kuhusu ubia hili sio wazo zuri.. mimi sio mfanya biashara lakini elimu ya biashara naijua kiasi, ubia sio mzuri kwa maisha yako hata kwa familia yako hapo baadae siku ambazo wewe utakuwa haupo, ubia una changamoto nyingi, migogoro mingi sana ikiwemo changamoto kwenye suala la utoaji maamuzi, kutofautia kimawazo, visasi vya ajabu ajabu, kukomeshana, ubishi, kutokuwa na uaminifu kwa baadhi ya wamiliki, kuzungukana kwenye biashara, kutengenezeana hasara feki kwenye biashara, kulogana, kila mtu kutaka ubosi, kila mtu anataka awe yeye ndo yeye kwenye biashara e.g CEO pamoja na hayo yote huwezi kumkaripia mmiliki mwenzio, huwezi kumfukuza, huwezi kumshitaki kienyeji huwezi kumhoji hoji hovyo n.k

Haya yote yateleta mkanganyiko kwenye biashara hatimae biashara kufa, suala la ubia lina hitaji umakini sana kuliko kutafuta mfanyakazi unayeweza kumtimua muda wowote lkn pia mfanyakazi atafanya kazi kwa kuogopa kutimuliwa,, Fanya biashara wewe mwenyewe mkuu
 
Unakosea mkuu,, kusema biashara mateso kama wewe mwenye biashara hutaki kuteseka nani sasa ateseke kwa ajiri yako??? Kama unapenda bata nenda tu katumie hizo hela kwenye hiyo bata unayotaka taka
Nitateseka kwenye vitu vyenye tija vya kufanikisha biashara yangu sio niteseke kwa ajili ya kumlinda mjinga
 
Mkuu kuhusu ubia h

Mkuu kuhusu ubia hili sio wazo zuri.. mimi sio mfanya biashara lakini elimu ya biashara naijua kiasi, ubia sio mzuri kwa maisha yako hata kwa familia yako hapo baadae siku ambazo wewe utakuwa haupo, ubia una changamoto nyingi, migogoro mingi sana ikiwemo changamoto kwenye suala la utoaji maamuzi, kutofautia kimawazo, visasi vya ajabu ajabu, kukomeshana, ubishi, kutokuwa na uaminifu kwa baadhi ya wamiliki, kuzungukana kwenye biashara, kutengenezeana hasara feki kwenye biashara, kulogana, kila mtu kutaka ubosi, kila mtu anataka awe yeye ndo yeye kwenye biashara e.g CEO pamoja na hayo yote huwezi kumkaripia mmiliki mwenzio, huwezi kumfukuza, huwezi kumshitaki kienyeji huwezi kumhoji hoji hovyo n.k

Haya yote yateleta mkanganyiko kwenye biashara hatimae biashara kufa, suala la ubia lina hitaji umakini sana kuliko kutafuta mfanyakazi unayeweza kumtimua muda wowote lkn pia mfanyakazi atafanya kazi kwa kuogopa kutimuliwa,, Fanya biashara wewe mwenyewe mkuu
Vyote vinawekwa kisheria
 
Nitateseka kwenye vitu vyenye tija vya kufanikisha biashara yangu sio niteseke kwa ajili ya kumlinda mjinga

Unahitajika umakini mkubwa sana kwenye kulitumia hili neno "mjinga"

Kama unataka kuendesha biashara kiboss zaidi tafuta chawa wa kuaminika, mtu aliyetokea kukuelewa sana kipindi cha nyuma au hata mkiwa shule lakini bado hajatoboa, mchukue huyo kaa nae karibu akusaidie kwa kazi zako

Wakumbuke masela zako wa enzi hizo wasaidie hao nao watakusaidia kwa moyo wao wote
 
Jaman mimi ni muajiriwa nafasi fulani ya juu kidogo hapa nchini. Nimeweza kupata mil 70 ambayo ni matokeo ya SAVING ya muda mrefu na hela zangu fulani nilikuwa nazidai kulipwa.

Mpango nilionao ni kuanzisha biashara ya spears za pikipiki na tri cycles (guta au Toyo). Changamoto niliyonayo ni kuwa mimi muda mkubwa wa usimamizi sina, nimewaza kumuweka wife naye kasema hawezi acha ajira yake aingie kwenye biashara ambayo hata haijui (in short wife sio mtu wa biashara).

Nikawaza nipate hata msichana mmoja wa Kichaga mwenye uwezo wa kutumia computer kwa sababu nimepanga niweke CCTV CAMERA na MFUMO WA MAUZO WA KIDIGITAL ila bado imani na hawa watu weusi sina kabisa. Nilishafungua ka biashara cha hizi simu ndogo maarufu kama viswaswadu nikaweka mtoto wa Aunt alichonifanya sina hamu hata ya kuhadithia.

Nirudi kwenye mada iliyonifanya nifungue uzi huu sasa. Nimewaza nipate Muhindi ili nimuajiri au tufanye kama partnership, i mean yeye awekeze kwenye Management mimi CAPITAL kwa sababu target yangu mimi ni kuua biashara za wenye viduka vidogo vidogo vya spear hapa wilayani ili nitawale soko kwa mikakati ifuatayo:

1. Kuteka mafundi wazuri wa injini, umeme na mechanics wazuri wenye jina kwa kuwalipa kukaa mbele ya duka langu ambalo lipo hapa city center.

2. Nimepata eneo ambalo lipo kando kando ya barabara hapa mjini ambalo kwa mbele lina uwazi mkubwa kiasi cha kuweza ku accomodate mafundi wengi mbele.

3. Kazi yangu nadeal sana na watu wa nje i mean wazungu,wachina Waindi n.k hivyo nina rafiki zangu wachina huwa wanaagiza na kufuata containers za spears huko china na wana duka la jumla KKOO hivyo wameniambia kwenye order zao wata include na yangu ili nipate kwa bei nzuri.

4. Kuuza kwa bei ya vunjabei kwa sababu mimi nitapata kwa bei ya chini sana hivyo ni rahisi kunifikia mzigo kwa bei ndogo sana.

5. Kuwa na offer kila jumamos kila ataekuja pale dukani kufanya services na maintenance atajaziwa mafuta nusu lita kama offer kila mmoja.

Anyway nimewaza ili mipango yangu iende sawa nahitaji mtu wa kusimamia alie serious ila wabongo siwataki kwa sababu za tabia zetu za WIZI, UMALAYA, UVIVU, EXCUSES NA UJINGA UJINGA AMBAO BILA KUPATA WA KUVICONTROL HULETA HASARA KWENYE KAMPUNI.

NB: Mwenye jamaa m INDIA 🇮🇳 anaejielewa aje inbox please usiniletee WAPEMBA nataka Muhindi nitamlipia PERMIT ili tufanye kazi ili tunyanyuke wote.

Ukikosa Muhindi tafuta kijana wa Kiislam anayesali lakini pia awe amekwenda shule kiasi na pengine awe na pass ya hesabu. Utanishukuru baadae!!!
 
Back
Top Bottom