Nataka kuachana na Mwanamke niliyemtolea mahari

Nataka kuachana na Mwanamke niliyemtolea mahari

Jaribu kuchunguza,kiburi cha huyo binti kinasababishwa na nini? Kingine hii kesi tumeisikia upande mmoja tu,pengine huyo binti nae anayo ya kusimulia kuhusu wewe,

Miaka 20 ni binti mdogo,hajajua bado ndoa ni nini,jaribu kutumia wazee ili wamuweke sawa au aeleze tatizo lake ni nini au anataka nini?

Maisha ya ndoa sio rahisi kama unavyofikiria,maisha ya ndoa ni mtihani mgumu sana,utaacha wangapi na kuoa wangapi?

Kitendo cha huyo Baba kutokutaka kupokea mahari kinasababishwa na ugomvi na chuki aliyojijengea dhidi ya huyo mkewe aliyeachana nae,mzee anaonekana ana nongwa sana na amejenga kama uadui na mtalaka wake na akawaingiza na wanae pia kwenye hiyo chuki,

Usikurupuke kuchukua maamuzi,jaribu kwanza kutafuta solution,maisha ya ndoa yana mengi sana,wengi wapo kwenye ndoa zao coz ya uvumulivu tu.
Nakubaliana na yote uliosema ila kipengele cha umri wa miaka 20 kuwa ni mdogo hilo nakataa.
 
Mkuu zungumza na mama yake mzazi mwambie amuache mtoto wake aishi maisha yake ya ndoa aache kbs kumchunguzachunguza na kumshauri, awambie ndugu zake waache kumfuatilia mkeo ili aishi maisha yake bila majungu ya kijijini.
Mwambie mkeo haya ni maisha kati yako wewe na yeye asiyasimulie kwa mtu yoyote wala kutaka ushauri kwa mtu yoyote kwa mambo madogomadogo ya ndani ya nyumba, mweleweshe kuachana kwenu ndani ya kipindi kifupi kutamchafulia jina yeye zaidi kuliko wewe na anaweza asiolewe tena.
Mzee wake kukataa mahari pengine alikuwa anamjua bint yake kitabia au wazazi wengine hukataa mahari ili usiende kumnyanyasa mtoto wao kwa ng'ombe wa laki tatu kwa jina la mahari.
Wakati mwingine usiharakie jambo kwa kasi hiyo, ulitakiwa kuwapa muda ndugu zako wakutafutie mke walau kwa uchache mwaka mmoja hata vijiji vya jirani, hata gari huwezi nunua kwa haraka namna hiyo lazima upate washauri.
 
Back
Top Bottom