Nataka kuachana na mwanamke

Nataka kuachana na mwanamke

Ni muda mwingine tena.

Anaomba ushauri huyu rafiki yangu mwanzoni alinishauri sana nioe tufanane ila nikamwambia mimi sina kazi na siwezi mtunza mke, leo yamemkuta....

"Ni miaka minne sasa tangu ampate shemeji/wifi yenu ila kiukweli, mambo aliyofanya alipokuwa single ni makubwa na mengi kuliko hivi sasa (ata mimi ni shahidi), kwann hebu msikilize...

"Ndani ya miaka kumi niliyoishi kama single nimeweza kujenga nyumba , kuanzisha biashara ya duka na yote nilikuwa pekee yangu tena nikiwa jobless nikipambana na ujasiriamali pekee.

Nikasema kwa kupata hivyo vichache hebu nivute jiko la mkeka ukizingatia serikali nayo ilinivuta karibu nikawa mtumishi official,

Aisee ikawa kosa kubwa maana hadi leo tuna mtoto mmoja mwanamke ni mama wa nyumbani, mshahara above 900,000, biashara za duka zimelala mtoto bado ana miaka 2.

Naona ninapoelekea nitapakaa rangi upepo yaani baada ya kuoa nimeona kama vile kuna mzigo umeniangukia yaani sifurukuti rafiki yangu".😳😳

"Je kuna uwezekano nikarudi single maana miaka inasonga sioni moja wala mbili mbele, mshahara hautoshi kabisa kulea familia yaani unaisha kwa matumizi ya nyumbani tu

msaada tutani maana nilivyokuwa single nili-enjoy ila huku ngoja tuwaachie wazoefu (sauti ya upole), ....😪😪😪"

Kwa mawazo yangu mafupi nawaza huwenda kuna pahala alikosea ila isiwe taabu siyo vibaya tukamshauri sipendi kuficha changamoto na mimi kujifanya mwl...

Karibuni
Tatizo sio mkeo, tatizo ni wewe.
 
Ni muda mwingine tena.

Anaomba ushauri huyu rafiki yangu mwanzoni alinishauri sana nioe tufanane ila nikamwambia mimi sina kazi na siwezi mtunza mke, leo yamemkuta....

"Ni miaka minne sasa tangu ampate shemeji/wifi yenu ila kiukweli, mambo aliyofanya alipokuwa single ni makubwa na mengi kuliko hivi sasa (ata mimi ni shahidi), kwann hebu msikilize...

"Ndani ya miaka kumi niliyoishi kama single nimeweza kujenga nyumba , kuanzisha biashara ya duka na yote nilikuwa pekee yangu tena nikiwa jobless nikipambana na ujasiriamali pekee.

Nikasema kwa kupata hivyo vichache hebu nivute jiko la mkeka ukizingatia serikali nayo ilinivuta karibu nikawa mtumishi official,

Aisee ikawa kosa kubwa maana hadi leo tuna mtoto mmoja mwanamke ni mama wa nyumbani, mshahara above 900,000, biashara za duka zimelala mtoto bado ana miaka 2.

Naona ninapoelekea nitapakaa rangi upepo yaani baada ya kuoa nimeona kama vile kuna mzigo umeniangukia yaani sifurukuti rafiki yangu".😳😳

"Je kuna uwezekano nikarudi single maana miaka inasonga sioni moja wala mbili mbele, mshahara hautoshi kabisa kulea familia yaani unaisha kwa matumizi ya nyumbani tu

msaada tutani maana nilivyokuwa single nili-enjoy ila huku ngoja tuwaachie wazoefu (sauti ya upole), ....😪😪😪"

Kwa mawazo yangu mafupi nawaza huwenda kuna pahala alikosea ila isiwe taabu siyo vibaya tukamshauri sipendi kuficha changamoto na mimi kujifanya mwl...

Karibuni

Ukileta mke unapungua kila kitu half and if not strong hata zaidi, vunavyopungua:

1. Juhudi ya kutafuta hela.
2. Ku take risky.
3. Kama ana nuksi na ushetani.
 
Nyie wanawake mnachosha mno mimi nimesema sioi hadi uzeeni bora nikalelewa na house girl kwa kutumia pesa zangu kuliko kuishi na tegemezi.
Kukimbia tatizo sio kusolve tatizo....wakae chini wajadiliane namna gani wataongeza kipato...Ila wanawake sie sometimes ujuaji mwingi, hicho kikao cha kujadili kuongeza kipato kinaweza kuishia kwenye ugomvi.
 
Sana tu yaani vitu vya nyumbani kama vyakula vinakomba pesa yote.

Anabaki kusubiria mwisho wa mwezi tena,😳 huu si ni utumwa?
Kwani hana bajeti? Je kwa mwezi unatumia kiasi gani?

Binafsi nakushauri kuwa, hayo ni mapito tu, ups and down kwenye ndoa zipo!

Naamini unapokuwa na familia nidhamu ya matumizi inakuwa juu kuliko kuwa single.

Kitu cha msingi ni kuwa na bajeti ya mwezi lakini pia kumuelimisha mwenza wako kuepuka matumizi yasiyo na tija.

Naamini utafika unapo kusudia.
 
Ukileta mke unapungua kila kitu half and if not strong hata zaidi, vunavyopungua:

1. Juhudi ya kutafuta hela.
2. Ku take risky.
3. Kama ana nuksi na ushetani.
hapa kama vile kuna ukweli ndani yake vile, sasa ni vipi ajitoe humu?
F3P_IgKWgAArkKy (1).jpeg
 
Kwani hana bajeti? Je kwa mwezi unatumia kiasi gani?

Binafsi nakushauri kuwa, hayo ni mapito tu, ups and down kwenye ndoa zipo!

Naamini unapokuwa na familia nidhamu ya matumizi inakuwa juu kuliko kuwa single.

Kitu cha msingi ni kuwa na bajeti ya mwezi lakini pia kumuelimisha mwenza wako kuepuka matumizi yasiyo na tija.

Naamini utafika unapo kusudia.
Bajeti anapanga mke, maana akianza kumpangia gharama za chakula, kuhudumia mtoto na yeye mwenyewe, jamaa anabakia na pesa ya kuangalia mechi za epl tu vibanda umiza ni shabiki wa arsenal 😳😳😳
 
Nilimshauri awali hakuamini eti laki tisa ni kubwa aiseee 😅😅😅😅...ngoja ncheke kama mazuri.. hebu mnisaidie nimshauri vipi? 😳😳
1. Atambue kwamba "ukitaka kwenda haraka nenda peke yako ila ukitaka kufika mbali nendeni wengi"

2. Akumbuke kwamba Mwanamke sio ndugu yake, hivo akishindwa kabisa kuhudumia basi huyo mwanamke ataondoka na atamuacha na madeni

3. Mwisho, Hatujui alikotoka na hatujui life style yake na kwao, aende kwa wazazi wake aweke wazi kila kitu wao watamshauri kutokana na
i/ Walivomlea
ii/ wanavomfahamu mke wake
iii/ watamfunua kama kuna changamoto za kiroho

🙏
 
Back
Top Bottom