Nataka kujilipua na Volvo XC 90. Ushauri wenu wadau

Nataka kujilipua na Volvo XC 90. Ushauri wenu wadau

Itoshe kusema kwamba, Waswedish wanatengeneza vyombo vyenye uhakika katika mabasi na Malori kuna SCANIA NA VOLVO hawana mpinzani. kwenye SUV tunajua Japs na Germans wanachuana vikali lakini tunamuunderestimate huyu mnyama VOLVO XC 90

watakuja watu wa Subaru na Toyota, nataka muangalie hii video nayoiweka hapa chini mpaka Range kakaa, na hiyo TLC kakalishwa sasa inakuwaje kwa ndogo?

Team Volvo mnipe uzoefu wa hii gari? Reliability, Comfortability yake Safety na Upatikanaji wa spares zake

Angalia hiyo video [emoji117][emoji117][emoji117][emoji117][emoji117]

View attachment 2480369View attachment 2480392View attachment 2480393View attachment 2480394
Brother, huo wimbo wimbo kwenye hiyo video unaitwaje? Wimbo mzuri mno!.
 
Shida ya Volvo XC90 ya 2005 na 2014 unaweza usione major exterior differences.
Ni rahisi kujua; kwani kuna tofauti sana kwenye designs za tail lights, front grill Volvo logo, Volvo emblem (large lettering ya rear logo) ya nyuma na parking sensors etc.
Shida ya Volvo XC90 ya 2005 na 2014 unaweza usione major exterior differences.
2005 model
1688554094397.png

1688554112433.png


2014 model
1688554230760.png

1688554248140.png
 

Attachments

  • 1688553910428.png
    1688553910428.png
    217.3 KB · Views: 28
  • 1688553955486.png
    1688553955486.png
    264.8 KB · Views: 25
Chukua boss. Five years of owning one.

Ila nunua angalau la kuanzia 2011; ukiweza 2014. Hiyo 2nd generation kama pesa ipo chukua ya kuanzia 2016.

XC90 ni bonge la gari. Chukua diesel D5. Hii ni turbocharger na inaweza kufanyiwa stage 1 tuning.

Shida ni moja kubwa. Za kuanzia 2011 zote zinakuwa ni Euro 5 kwenye suala la exhaust emission regulations. Hivyo, kwa diesel zinakuwa na vitu vinaitwa diesel particulate filter (dpf) na exhaust gas recirculation (egr). Hii ni mifumo ya kuzuia uchafu wa mazingira kwenye magari ya diesel. Tatizo linakuja kuwa kama wewe siyo mtu wa kusafiri safiri sana (yaani mtu wa safari za home-work-home za mjini), D5 itakuletea shida. Kwani dpf na egr zitajaa na kuziba zile carbon soot/deposits. Dpf ni chujio la hizo gas mbaya na egr urudisha hizo gas mbaya ndani ya injini ili zisitoke kuchafua mazingira. Dpf na egr zikijaa carbon, hapo a spiral of problems ufuata. Una machaguo matatu manne ya kutibu. Moja ambalo ndiyo bora, uwe unafanya safari za mbali angalau mara kadhaa kwa miezi ili uruhusu exhaust kupata joto la kuchomq vizuri hizo carbon soots. Safari fupi fupi, exhaust haichemki vya kutosha kuchoma carbon. Mbili, kuna additives za kununua na kuweka kwenye mafuta, ambazo ufanya kazi ya kusafisha dpf na egr. Hii ni suluhisho lisilo la kudumu na la gharama, na kwa uzoefu wangu siyo la uhakika sana. Tatu, tumia hizi obd2 diagnostic machines kufanya forced regeneration ya dpf. Pata machine yenye function ya kuruhusu kuipa moto exhaust gari ikiwa imesimama, mpaka carbon soot utoka kwenye dpf. Hii nayo siyo ya kudumu, kwani gari nyingi zinaruhusu forced regeneration mara tatu tu. Nne, fanya dpf na egr deletes. Hizi ni reprogramming ya ecu (control box) ili kuifundisha gari kwamba dpf na egr hazipo tena. Hii inaenda pamoja na physical removal ya dpf. Mara nyingi egr inabaki lakini. Changamoto ya hii ni kupata mtaalamu wa uhakika wa kufanya remapping ya hizi ecu za European makes. Maana remapping yake inahitaji umakini mkubwa mno, makosa kidogo tu, upelekee a spiral of problems. Kwa mazingira yetu ya kibongo hii ndiyo suluhisho la kudumu endapo remapping itafanyika kwa usahihi. Kama pesa si shida unaweza kupelekea ecu Afrika ya Kusini au hata Ulaya. Maana remapping inaweza kufanyika hata kama gari halipo hapo.

Ukiona diesel pasua kichwa chukua petrol. Ila chukua T5 ya kuanzia 2011 au ukiweza T6 ya kuanzia 2016.

Utafurahia sana gari. Ila kuwa makini na mafuta. Jitahidi siku zote uweke kwenye vituo vya Total, Puma, Oryx na Engen tu. Maana European makes na mafuta machafu ni kujitafutia shida. Ingawa unaweza kufanya pia remapping ya kuruhusu gari iweze kuvumilia mafuta ya kiwango duni. Au utumie fuel treatment angalau mara 1-2 kwa mwezi.

Mafundi pia kuwa makini. Wengi wanaweza kusema wanaweza, kumbe ni makanjanja. Hapa ni muhimu kulijua gari lako vizuri haswa. Tembelea fora mbalimbali za Volvo. Cheki mafundi na watalaamu wa Volvo Youtube. Pia kuwa na obd2 yako ndogo ya kuangalia afya ya gari lako mara kwa mara.

Na daima lazima ufanye preventive maintenance. Mfano, ujue kama kuna part ambayo gari likifika umbali fulani, ni lazima ukibadilishe n.k.
MKUU MAELEZO YAKO YANAONESHA HIZI GARI UNAZIJUA VEMA SANA......ILA PIA UMEKIRI UNAMILIKI VOLVO KWA MIAKA 5 SASA...NAOMBA UNISAIDIE GARAGE UNAYO
TENEGENEZEAGA-NITASHUKURU UKINIPATIA NAMBA ZAO. ASANTE
 
MKUU MAELEZO YAKO YANAONESHA HIZI GARI UNAZIJUA VEMA SANA......ILA PIA UMEKIRI UNAMILIKI VOLVO KWA MIAKA 5 SASA...NAOMBA UNISAIDIE GARAGE UNAYO
TENEGENEZEAGA-NITASHUKURU UKINIPATIA NAMBA ZAO. ASANTE
Sijui upo wapi.
Kwa Dar, cheki Modo garage, Kigamboni. Pia kuna garage moja ipo kule Mbezi kwa Zena (Mwai Kibaki Rd) maeneo karibu na bar ya Amsterdam. Jina limenitoka, ila ukiulizia tu utafika.
Kwa Arusha na Dodoma, cheki Denso garage.
Kwa Dodoma, cheki pia Kyando garage, Kizota.
 
HII REMAPING INAFANYIKA HAPA HAPA BONGO MKUU?TUPE LOCATION BASI KAMA NI HAPA BONGO
Bongo ukimaanisha Darisalama? Kama ndiyo, cheki Outmax wapo Mwananyamala au pia Automax wapo Mikocheni karibu na Sekondari ya Alpha.
 
Sijui upo wapi.
Kwa Dar, cheki Modo garage, Kigamboni. Pia kuna garage moja ipo kule Mbezi kwa Zena (Mwai Kibaki Rd) maeneo karibu na bar ya Amsterdam. Jina limenitoka, ila ukiulizia tu utafika.
Kwa Arusha na Dodoma, cheki Denso garage.
Kwa Dodoma, cheki pia Kyando garage, Kizota.
Nashukuru mkuu...nilipata nyingine pia ipo opposite na mataa ya ITV.....Kama uanatokea bamaga ni upande wa kushoto,wanapaita kwa BIG....au kwa engneer.
 
Yupo sahihi ndiyo na wala sipindi. Na ndivyo wanavyofanya watu wengi wenye uwezo mdogo. Na hiyo hasa ndiyo point yangu. Kujaribu kufanya hili kundi kubadilika kifikra. Kununua vitu kulingana na uwezo wao na siyo kuonyesha ufahari.
Wewe ndo uwezo mdogo , swala la mtu kutaka kununua kitu na kuuliza sio baya anataka kupata uzoefu ilikufanya maamuzi sahihi , kama ulikuwa huna cha kuchangia ungekaa kimya ...

Hao matajiri unaowasema hawakurupuki kununua gari sababu tu wanapesa wanafanya research pia kulingana na interest zao...

Kingine sio kila mtu anunua gari kama chombo cha usafiri ingekuwa hivyo kila mtu angenunua IST , kuna watu magari wananunua kama hobby au starehe .... Acha negative thinking....
 
Wewe ndo uwezo mdogo , swala la mtu kutaka kununua kitu na kuuliza sio baya anataka kupata uzoefu ilikufanya maamuzi sahihi , kama ulikuwa huna cha kuchangia ungekaa kimya ...

Hao matajiri unaowasema hawakurupuki kununua gari sababu tu wanapesa wanafanya research pia kulingana na interest zao...

Kingine sio kila mtu anunua gari kama chombo cha usafiri ingekuwa hivyo kila mtu angenunua IST , kuna watu magari wananunua kama hobby au starehe .... Acha negative thinking....
Ndugu akili kisoda mbona unadandia vitu vilivyokuzidi uwezo? Kuna kuuliza kwa aina nyingi na unapouliza mambo ya gari huku ukiwa na hofu juu ya gharama basi wewe ni mjinga kwa sababu unataka kubena mzigo unaokuzidi uwezo. Sikushangai sana kwa sababu hata magari ya mtumba yalipoanza kuingia kwa wingi, kuna wengi walikimbilia kununua ma-Ranger Rover lakini walipaki baada ya miezi michache kwa kushindwa gharama. Hayo ndiyo manyumbu wanaowaza kununua magari ''kwa hobby'' kama wewe.
 
Ningekushauri ujisomee gazeti la What Car hao wako vizuri sana kwa kupambanua magari ya kila aina kuanzia ubora mpaka mapungufu yake

Kwa kweli Volvo aina zote nimeendesha zikiwa mpya kabisa na ni ngumu kuelezea sana ila 60 niliipenda ilikuwa imetulia sana
 
Hii kauli ya dunia Ni Kijiji hua Ni rahisi sana kuisema,ila kwny utekelezaji hua inaponza sana.
Shipping inatutofautisha kati ya wao na sisi.... u buy a spare lkn when its comes kwenye shipping unajikuta u paid 150% zaidi!.....
 
Ndugu akili kisoda mbona unadandia vitu vilivyokuzidi uwezo? Kuna kuuliza kwa aina nyingi na unapouliza mambo ya gari huku ukiwa na hofu juu ya gharama basi wewe ni mjinga kwa sababu unataka kubena mzigo unaokuzidi uwezo. Sikushangai sana kwa sababu hata magari ya mtumba yalipoanza kuingia kwa wingi, kuna wengi walikimbilia kununua ma-Ranger Rover lakini walipaki baada ya miezi michache kwa kushindwa gharama. Hayo ndiyo manyumbu wanaowaza kununua magari ''kwa hobby'' kama wewe.
Ndugu akili kisoda mbona unadandia vitu vilivyokuzidi uwezo? Kuna kuuliza kwa aina nyingi na unapouliza mambo ya gari huku ukiwa na hofu juu ya gharama basi wewe ni mjinga kwa sababu unataka kubena mzigo unaokuzidi uwezo. Sikushangai sana kwa sababu hata magari ya mtumba yalipoanza kuingia kwa wingi, kuna wengi walikimbilia kununua ma-Ranger Rover lakini walipaki baada ya miezi michache kwa kushindwa gharama. Hayo ndiyo manyumbu wanaowaza kununua magari ''kwa hobby'' kama wewe.
Unabidi uelewe kitu kimoja unaweza kuwa na pesa ya kununua gari lolote lile na kuhudumia lakini sababu huna elimu ya hilo gari , connection ya mafundi na info nyingine ikafanya gari usidumu nalo ..

Inawezekana hata kumiliki gari ujawahi na unaandika huo upuuzi ukiwa umekaa kwenye kochi la baba ako unasubili Mama apike Ugari ule... Ila kama ulifika hata chekechea wahenga walisema " kuuliza sio ujinga" ...

Kutokana na swali la mdau unaona watu walivyotoa madini na uzoefu wao , hata wewe chizi umejifunza kitu hata ikitokea umeokota gari utajua garage ya kwenda kufanya service......
 
Kwenye malori na mabus hakuna wa kumfikia mswiden

Gari dogo sina experience nalo, kabla hujalinunua uliza kwanza spea zake and services

Ushauri wangu NUNUA MJAPAN, hapa ni mwisho wa maneno🙌
 
kwa wengi wasichokijua tu ni kuwa Volvo ana branch yake kabisa Tanzania. wapo along Nyerere road kama unaedna Airport. acheni kudanganyana eti spare hamna! we huna uelewa
 
kwa wengi wasichokijua tu ni kuwa Volvo ana branch yake kabisa Tanzania. wapo along Nyerere road kama unaedna Airport. acheni kudanganyana eti spare hamna! we huna uelewa
Niliwahi kwenda pale 2019 kwa ajili ya service, wakasema wanajishughulisha na trucks tu.
 
Volvo kodi yake sio kubwa pia TRA wanaangalia gari zilizo kwenye soko ndio wanaongeza kodi Volvo unaweza kupata ya miaka ya karibuni tu na ukalipa kodi nafuu tofauti na kampuni zingine kama Toyota...
Ni gari nzuri zina Confort,speed ipo na balance..
 
Back
Top Bottom