Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,345
- 10,885
Volvo Xc90 vs Bmw x5 vs Audi q7.
What will you take?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Volvo Xc90 vs Bmw x5 vs Audi q7.
What will you take?
Kwingineko kupi huko? Performance? Reliability? Prestige? Sustainability? Emissions?Ukiachana na safety kwingineko sio nzuri sana na interior mara nyingi zinakuwa za kawaida
Yeah. 2016 na kuendelea.Napata shida kati ya xc90 na x5. I hope unazungumzia 2017 na kuendelea.
Gusia matumizi ya kila siku
Xc90 kuanzia 2016 inavutia sana. Halafu hai-shoutYeah. 2016 na kuendelea.
Volvo ni gari nzuri kwa usalama wako, mojawapo ya gari zenye rekodi nzuri kwenye ajari. Ndio wagunduzi wa seat belt na hawakuweka patent kila kampuni itumie.
Ukiachana na safety kwingineko sio nzuri sana na interior mara nyingi zinakuwa za kawaida
Sijawahi tumia X5 na Q7. Hivyo nitakuwa bias. Ila, nitatumia XC90 jana, leo na kesho kwa town na road tripsGusia matumizi ya kila siku
Hamna gari hapo utalia kaka magari ya kimarekani hayo speak zake utajuuutaaItoshe kusema kwamba, Waswedish wanatengeneza vyombo vyenye uhakika katika mabasi na Malori kuna SCANIA NA VOLVO hawana mpinzani. kwenye SUV tunajua Japs na Germans wanachuana vikali lakini tunamuunderestimate huyu mnyama VOLVO XC 90
watakuja watu wa Subaru na Toyota, nataka muangalie hii video nayoiweka hapa chini mpaka Range kakaa, na hiyo TLC kakalishwa sasa inakuwaje kwa ndogo?
Team Volvo mnipe uzoefu wa hii gari? Reliability, Comfortability yake Safety na Upatikanaji wa spares zake
Angalia hiyo video 👉👉👉👉👉
View attachment 2480369View attachment 2480392View attachment 2480393View attachment 2480394
Reliability sio kubwa sana na repairs & spare parts zina bei juu kidogo. Ratings zake ukiachana na safety haina the best performance. Ni brand nzuri lakiniKwingineko kupi huko? Performance? Reliability? Prestige? Sustainability? Emissions?
Ukilinganisha gari zipi? Maana kama ni likes za Mercs, BMW na Audi, Volvo is way more reliable and maintenance cheaper. Performance, yes imezidiwa na hao.Reliability sio kubwa sana na repairs & spare parts zina bei juu kidogo. Ratings zake ukiachana na safety haina the best performance. Ni brand nzuri lakini
Hiyo sio gari ya Kimarekani.Hamna gari hapo utalia kaka magari ya kimarekani hayo speak zake utajuuutaa
Hamna gari hapo utalia kaka magari ya kimarekani hayo speak zake utajuuutaa
Bro. Naomba fungua PM au start convo nikureply. Nitashukuru sana.Chukua boss. Five years of owning one.
Ila nunua angalau la kuanzia 2011; ukiweza 2014. Hiyo 2nd generation kama pesa ipo chukua ya kuanzia 2016.
XC90 ni bonge la gari. Chukua diesel D5. Hii ni turbocharger na inaweza kufanyiwa stage 1 tuning.
Shida ni moja kubwa. Za kuanzia 2011 zote zinakuwa ni Euro 5 kwenye suala la exhaust emission regulations. Hivyo, kwa diesel zinakuwa na vitu vinaitwa diesel particulate filter (dpf) na exhaust gas recirculation (egr). Hii ni mifumo ya kuzuia uchafu wa mazingira kwenye magari ya diesel. Tatizo linakuja kuwa kama wewe siyo mtu wa kusafiri safiri sana (yaani mtu wa safari za home-work-home za mjini), D5 itakuletea shida. Kwani dpf na egr zitajaa na kuziba zile carbon soot/deposits. Dpf ni chujio la hizo gas mbaya na egr urudisha hizo gas mbaya ndani ya injini ili zisitoke kuchafua mazingira. Dpf na egr zikijaa carbon, hapo a spiral of problems ufuata. Una machaguo matatu manne ya kutibu. Moja ambalo ndiyo bora, uwe unafanya safari za mbali angalau mara kadhaa kwa miezi ili uruhusu exhaust kupata joto la kuchomq vizuri hizo carbon soots. Safari fupi fupi, exhaust haichemki vya kutosha kuchoma carbon. Mbili, kuna additives za kununua na kuweka kwenye mafuta, ambazo ufanya kazi ya kusafisha dpf na egr. Hii ni suluhisho lisilo la kudumu na la gharama, na kwa uzoefu wangu siyo la uhakika sana. Tatu, tumia hizi obd2 diagnostic machines kufanya forced regeneration ya dpf. Pata machine yenye function ya kuruhusu kuipa moto exhaust gari ikiwa imesimama, mpaka carbon soot utoka kwenye dpf. Hii nayo siyo ya kudumu, kwani gari nyingi zinaruhusu forced regeneration mara tatu tu. Nne, fanya dpf na egr deletes. Hizi ni reprogramming ya ecu (control box) ili kuifundisha gari kwamba dpf na egr hazipo tena. Hii inaenda pamoja na physical removal ya dpf. Mara nyingi egr inabaki lakini. Changamoto ya hii ni kupata mtaalamu wa uhakika wa kufanya remapping ya hizi ecu za European makes. Maana remapping yake inahitaji umakini mkubwa mno, makosa kidogo tu, upelekee a spiral of problems. Kwa mazingira yetu ya kibongo hii ndiyo suluhisho la kudumu endapo remapping itafanyika kwa usahihi. Kama pesa si shida unaweza kupelekea ecu Afrika ya Kusini au hata Ulaya. Maana remapping inaweza kufanyika hata kama gari halipo hapo.
Ukiona diesel pasua kichwa chukua petrol. Ila chukua T5 ya kuanzia 2011 au ukiweza T6 ya kuanzia 2016.
Utafurahia sana gari. Ila kuwa makini na mafuta. Jitahidi siku zote uweke kwenye vituo vya Total, Puma, Oryx na Engen tu. Maana European makes na mafuta machafu ni kujitafutia shida. Ingawa unaweza kufanya pia remapping ya kuruhusu gari iweze kuvumilia mafuta ya kiwango duni. Au utumie fuel treatment angalau mara 1-2 kwa mwezi.
Mafundi pia kuwa makini. Wengi wanaweza kusema wanaweza, kumbe ni makanjanja. Hapa ni muhimu kulijua gari lako vizuri haswa. Tembelea fora mbalimbali za Volvo. Cheki mafundi na watalaamu wa Volvo Youtube. Pia kuwa na obd2 yako ndogo ya kuangalia afya ya gari lako mara kwa mara.
Na daima lazima ufanye preventive maintenance. Mfano, ujue kama kuna part ambayo gari likifika umbali fulani, ni lazima ukibadilishe n.k.
Kodi ya XC90 2016 ni 17m tuu, kama unahitaji jipange CIF tuu
Shida ya Volvo XC90 ya 2005 na 2014 unaweza usione major exterior differences.Gari modern ni nzuri lakini ukipata za kuanzia 2011 - 2014 bado utakuwa vizuri na pengine maintenance costs zitakuwa nafuu kidogo.
Kutaka kujua kitu sio ufahari wala uwezo mdogo pana watu vitu wanavijua kweli mimi napoulizia hicho kitu inanirahisishia kuelewa hapo sioni tatizo na gari sio Big ishu saana kama tunavyoaminishwa toeni madini ili watu waendeshe au waishi maisha rahisi kupitia kwa wanaojua...Yupo sahihi ndiyo na wala sipindi. Na ndivyo wanavyofanya watu wengi wenye uwezo mdogo. Na hiyo hasa ndiyo point yangu. Kujaribu kufanya hili kundi kubadilika kifikra. Kununua vitu kulingana na uwezo wao na siyo kuonyesha ufahari.