Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Gari ambazo nina uzoefu nazo ni Howo na Shacman.

Ngoja nianze na Howo .
Howo ni miongoni mwa Gari za Kichina nzuri sana hasa kwenye utumiaji wa mafuta .Ukitaka kununu gari kama hii ni vema ukanunua Brand new .Maana bei ya mpya inashabiana na Bei za Scania used.Faida ya Howo mpya ni kuwa ina utumiaji mzuri wa mafuta hasi kulingana Horse Power (HP) yake ni 371. Katika biashara ya magari kitengo cha mafuta ni chagamoto so unapoata gari inayokula mafuta vizuri inapungiza gharama za uendeshaji. Pili Howo ikiwa mpya na ukapata dereva mzuri na mzoefu itakuchukua muda mrefu sana kupata hitilafu za mara kwa mara.Kwa kifupoi haina breakown za mara kwa mara na itakuchukua miaka Mitano mpaka 8 kuanza kusumbua.Kwa hiyo miaka kama utakuwa umeitumia vizuri utakuwa umeshrushisha hela yako na umeshanunua nyingine tena .
Upatikanaji wa spare ni rahisi kwa Tanzania ka sasa kuna mawakala wengi wa SINOTRUCK hapa Bongo so spare si tatizo.Pia spare zake bei affordable

Hasara za Howo.
Life span ya hizi gari ni fupi ukiliganisha na gari kama Scania .So ni vizuri kuitunza vizuri ili na yenyewe ikutunze pia.Service za mara kwa mara ni muhimu .
Ni muhimu ni kuwa mafundi wazuri na wanajua gari si bora fundi. Ikupendeza mara moja moja uwaite wenyewe wachina waicheki.
Gari za Shacam.
Ni gari ngumu na zenye nguvu sana, Nguvu kubwa inatoka kuwa na Horse Power kubwa kuna za 420HP na 440 HP .HP kubwa inasababisha ulaji mkubwa wa mafuta .
Fiada za Shacman ni pamoja na kuwa na nguvu kubwa gari kama hiii ni ngumu kukwama sehemu za rough Roads.Hii inaweza kupita sehemu ngumu kwa mfani mvua inanyesha huko migodini ni ngumu sana kukwama.
Inawe uwezo wa kubeba mzigo mikubwa kwa mfano inaweza kuungwa na trailer ya Lowbed na ikabeba mzigo heavy sana.

Hasara ya Shacman
Utumiaji mkubwa wa mafuta huchangia gharama za kiu edeshaji kuwa kubwa.
Life span yake pia si ndefu kama ilivuo gari nyingi za kichina.
vipi kuhusu hizi MAN naziona zimekuwa nyingi nyingi barabarani
 
Nimepata kama mil 100 baada ya kuvuna vanila huko Bukoba. Sasa nahitaji nijiingize kwenye biashara ya usafirishaji na wazo langu ni kununua scania kama kwenye picha

Nimepanga kuanza na moja kutokana na kiasi nilicho nacho

Naomba wenye uzoefu, kama biashara ikienda vizuri, kwa mwezi naweza ingiza kiasi gani?
View attachment 1484199


Swali la nyongeza 24 June 2020
Vipi biashara ya kusafirisha
Mafuta vs Mizigo

Kwa swali lako, jitahidi kujifunza basics za biashara; kabla ya kuamua unawekeza wapi lazima ufanya utafiti binafsi na ujihakikishie binafsi unafanikiwa!

Biashara sio how much money I make only, hayo yanaathiriwa na:

  • Uwezo binafsi na busara ya kufanya biashara.
  • Mahusiano na wateja, dereva na jamii nzima.
  • Upatikanaji wa Biashara husika, namaanisha wateja.
  • Mamlaka husika na Sheria za uendeshaji wa hiyo biashara!

Haya ni ya muhimu kabla ya kusema naingiza ziku ngapi kwa siku! Huwezi ingiza kitu kama una gari jipya la Japan kama:

  • Hauna skills za biashara na namna ya kushughulika na dereva etc.
  • Hauna namna nzuri ya kutafuta na kushughulika na wateja.
  • Haujatafiti vibali na vitu gani unaitaji ili ufanya biashara kihalali.....
 
Mimi ninaipenda hii biashara ya usafirishaji ila kuna mdau alinishauri kwanza nianze na fuso ya kawaida ama tandam.
Ni kweli ila kwa kuwa bado ni mshamba kidogo na vyombo vya moto...nakushauri ungeanza na mkokoteni wa mizigo pale Kariakoo ama Temeke sokoni. Mdogo mdogo utafika tu,
 
Japo sipo kwenye mood ya kuandika, lakini nikipita kimya nitakua sijakutendea vema wala kuitendea vyema nafsi yangu.
Nina uzoefu niseme wa kutosha kuweza kutoa 'expart opinions' kwa mtu anyetaka kuanza biashara ya usafirishaji kwa kumiliki malori.
Nawapongeza wachangiaji wenzangu kwenye uzi huu, ila kuna mawili matatu nimegundua toka kwa hao wenzangu japo kuu hasa ni hili.
-Wengi hawana taarifa kamili na sahihi juu ya bei na uhalisia wa aina anuai za magari pia uhalisia katika sekta nzima ya usafirishaji hapa nchini.
Wengi wameshauri na umeonesha kuridhika na ushauri juu ya kuanza na Fusi-tandam. Mimi kwa uzoefu wangu sikushauri kuanza na tandam kwa sababu zifuatazo;
+ Gharama. Ununuaji na ubireshaji wa tandam huweza kufika 80-100mil hii ni gharama kubwa sana kwa gari ya tandam ukilinganisha na performance yake barabarani.
+Matunzo. Tandam ina gharama kubwa sana katika matunzo hasa hasa engine. Ukumbuke ile ni engine yenye HP kama 200 hivi lakini inabebeshwa tani 18 hivyo injini huchoka haraka na kuhitaji kubadilishwa. Ni kawaida kwa life span ya injini kwenye tandam kuwa miaka minne japo mara nyingine huweza kujikongoja hadi 8 kutokana na nidhamu yako ya kuibebesha mzigo
+Mifumo ya uendeshaji. Tandam nyingi hasa hasa nikiwa ni mzigo hata tani 12 tu ujue haina uwezo wa breaking za ghafla so katika kipengere hiki tegemea neema ya Mungu na kuthibitisha hili fuatilia ajali za tandam kugonga gari nyingine kwa nyuma utaambiwa sababu.

Kama utaamua kuanza na gari toka ukoo wa mzee Mitsubishi basi achana na tandam ila chukua fuso kipisi beba tani zako 7au 8 baas. We mwenyewe jiulize tu gari ulikua designed kubeba tani 5 ila Bongo Pasua Kichwa Engineering wanaifanya ibebe tani 18.
USHAURI WANGU SASA.
Kwa mtaji wa milion 100, anza na gari ambayo gharama ya manunuzi yake hadi kuingia road yaani horse na trailer yake isizidi 80ml.
Hapa utaona kipi rahisi kwako either kuagiza used ulaya au used ya kibongo bongo, ambapo kwangu naona ni sawa tu japo hakikisha kama ni used ya kibongo bongo usichukue iliyoingia nchini zaidi ya miaka miwili nyuma.
Hapo ukitaka kuagiza ni vema ukaanza na gari ambazo ni rafiki kwa mafundi na vipuri vyake mara ipatapo faida. Nashauri Scania series 4 yoyote kati ya 114 au 124 horsepower yoyote hamna shida najua hiyo hadi inakaa road itakugharimu kwenye 60ml hivi na trela lake ni 20ml tu.
Anza na safari za local na kwa kuwa wewe ni mgeni basi kichwa chako ni halali ya Dalali na atakupiga sana katika miezi mitatu ya kwanza hadi kichwa kikukae sawa utengeneze wateja wako. Route zinatofautiana na msimu kwani kuna wakati nyanda za juu kubalipa na kuna wakati kanda ya ziwa kunalipa.

Oya nimechoka kutype, ntaendelea kesho
bei za madalali zinajulikana sio rahisi kupigwa.vipi kuhusu 113?
 
bei za madalali zinajulikana sio rahisi kupigwa.vipi kuhusu 113?
Siishauri sana japo ni chombo ya kazi haswa, hii ikizingua unagonga nyundo mbili tatu chombo inakaa sawa.
Ila hizi gari z R series jamani kama ndio unaanza hii biashara USIGUSE narudia USIGUSElabda uwe mzoefu kwenye sekta hii. Chukua 124L auu 114 L utanishukuru baadae na hiyo 124 HAKIKISHA ISIWE RED DOT iwe 124 420 plain maana red dot itakubidi ukafumue mfumo wote wa upoozaji ili ikae kikazi
 
Ni kweli ila kwa kuwa bado ni mshamba kidogo na vyombo vya moto...nakushauri ungeanza na mkokoteni wa mizigo pale Kariakoo ama Temeke sokoni. Mdogo mdogo utafika tu,
Mnafungua id mpya,alafu mnaleta porojo.
Nishatoka kwenye ayo maisha ya mkokoteni miaka ya 2000,kwa sasa naweza kukulisha wewe na ukoo wako wote mpaka kijiji chenu.
Kama unabisha sema nianze kuwalisha.
 
Siishauri sana japo ni chombo ya kazi haswa, hii ikizingua unagonga nyundo mbili tatu chombo inakaa sawa.
Ila hizi gari z R series jamani kama ndio unaanza hii biashara USIGUSE narudia USIGUSElabda uwe mzoefu kwenye sekta hii. Chukua 124L auu 114 L utanishukuru baadae na hiyo 124 HAKIKISHA ISIWE RED DOT iwe 124 420 plain maana red dot itakubidi ukafumue mfumo wote wa upoozaji ili ikae kikazi
wanasema changamoto ya 113 ni ulaji wa mafuta
 
wanasema changamoto ya 113 ni ulaji wa mafuta
Hivi umewahi kukutana na R iliyochanganyikiwa au 124 red dot iliyovurugwa??😁😁😁😁 siishauri 113 kwa sababu moja tu nayo ni kuwa imekua gari ya kizamani sana kiasi kwamba haina comforty kwa driver pia vipuli vyake ni mwendo wa used. Kuhusu mafuta ni kweli japo sio sana ukilinganisha na 124
 
Tanzania yapo magari mangapi?? yote yametumbukia ? biashara zote zina risk mkuu, na zote zina risk za kuhatarisha na kuua mtaji wote , ndio maisha yalivyo, tuna options mbili tu either tufanye au tusifanye
Kwamba ukizaa mtoto akifa unaacha kuzaa au basi na watu wengine pia wataacha kuzaa.
 
Sikiliza mkuu mimi sina dharau ila huwa naangalia mtu amenijibu vipi na mimi ndio namjibu kulingana na majibu yake.
Ukija vizuri nitakujibu vizuri na ukija vibaya nitakujibu vibaya accordingly yaani ni mtu napanda na kushuka.
Ila wewe ukitaka nikunyenyekee hapo kweli utaniona mimi nina dharau au jeuri.
Wewe dogo nakuonaga kama una dharau na kejeli nyingi sana, kwa muda mfupi niliokua humu jf nimeona comment zako hua kama kwanza unakurupuka , halafu unawaona watu wote mafara wewe ndio una akili, wewe nimekuona ni mtu ambaye huyajui maisha, hivyo"Vihela" unavyoviita ni vyake na jasho lake, ana haki ya kutumia atakavyo, kejeli katika maisha havitakusaidia lolote, kwa behaviour hio hutofika popote utabaki kusugua benchi tu hapo ulipo. Usiipangie pesa ya mtu kazi, ipangie pesa yako, usione watu mafara. Chunga sana dogo.
 
Kifo hicho mkuu kwa nini usikope tractor la NewHolland au zile gari za tata.
 
Usimpangie mwenzako mkuu anajua anachokifanya hadi kuamua kununua gari la mizigo
 
Mayai yote (Hiyo mil 100)ukiweka kwenye kikapu kimoja (biashara moja)inaenda kula kwako!Hiyo hela igawe kiasi kwamba ufanye biashara zaidi ya mbili.
 
Huyo hajui systems za breki chief.
Siku nikipata muda, nitakuja nitowe somo la jinsi upepo unavyo fanya kazi kwenye systems za magari hasa Scania
Mkuu nakukumbusha ukipata muda toa somo tuweze kunufaika. Asante
 
Back
Top Bottom