Natamani kupenda tena

Natamani kupenda tena

Kila heri mamy, Mungu ni mwema utapata hitaji la moyo wako.
Ila nakushauri usiangalie sana mwonekano wa mtu maana 'sura sio roho' anaweza kuwa na mwonekano uupendao lakini akawa na tabia usizopenda!
 
Nakushauri mtafute mwanaume Wa maisha yako na awe mumeo pia mzae watoto wazuri mkatekeleze amri ya mungu sawasawa na mapenzi yake ...umheshimu nawe akuheshimu ...lakini haya yote hayatakamilika kwa mwanadamu Dada ila ni kwa kumtanguliza mungu mbele ...ili akatete na mwanaume utakaekutana nae awe na hofu ya kumjua mungu ...naamini

Mwezi mwaka na siku kama ya Leo ..next year utakuwa unaishi na mumeo unaemtafuta na ataishi na mwanao kama mwanae na atampenda kwa dhati ...mungu akupe hekima na busara

By Living kereth
 
Between the line nahisi anahitaji sana mwanaume wa kumuoa. Sema hajagundua kuwa hao anaowapenda yeye siyo waoaji bali wanafuata chura sijui muonekano wake. Ushauri wangu asisikilize sana moyo wake. Akubali 'kujifunza kumpenda mwanaume' huko huko mbele kwa mbele. Akifanya hivi ataolewa mapema given qualities anazojipambanua kuwa nazo.

Halafu pia hajaelewa kuwa mtoto ni kikwazo kwa wanaume wengi when it comes to marriage. So she has to choose smartly kama kweli anahitaji kuolewa. Hao hao anaowavalia uso wa mbuzi sijui kuwa serious ndo angepata muoaji humo then ajifunze kumpenda taratibu huku maisha yanasonga.

Akiendelea na style yake ya kupenda anaowapenda tu ilihali ana mtoto na age ndo hiyo inazidi kupaa, akyamama wanaume watamchezea sana. Hapo najua wanafuata hiyo chura but when it comes to marriage wanalala mbele.

Yangu ni hayo, usiku mwema
Nashukuru ila mie kwangu ndoa nii majaliwa, siwezi kuiwaza ndoa wakati hata ambae nitamaliza nae maisha yangu sina, ikitokea ndoa kheri ila nataka nianze na stage ya chini sitaki kukurupuka. Bora tuishie kwenye urafiki au uchumba lakini si kuingia kwenye ndoa sababu tu nampenda mtu. Niko tayari hata kuolewa ba miaka 40 ila nimpate nitakaempenda. Sijakata tamaa ya maisha bado kuwa na mwanaume ili tu niolewe. Asante kwa maneno yako lakini
 
Hongera sana mrembo!
Mmebaki wachache sana mabikira duniani
Usije ukamuuzi Mungu kwenye amri yake ya sita.kila la kheri!
Bikra??? hahahahahaa... sinayo mkuu. Nilimaanisha sijatumika muda mrefu
 
Kila heri mamy, Mungu ni mwema utapata hitaji la moyo wako.
Ila nakushauri usiangalie sana mwonekano wa mtu maana 'sura sio roho' anaweza kuwa na mwonekano uupendao lakini akawa na tabia usizopenda!
Asante dear.. nimekumiss lakini.
 
Nakushauri mtafute mwanaume Wa maisha yako na awe mumeo pia mzae watoto wazuri mkatekeleze amri ya mungu sawasawa na mapenzi yake ...umheshimu nawe akuheshimu ...lakini haya yote hayatakamilika kwa mwanadamu Dada ila ni kwa kumtanguliza mungu mbele ...ili akatete na mwanaume utakaekutana nae awe na hofu ya kumjua mungu ...naamini

Mwezi mwaka na siku kama ya Leo ..next year utakuwa unaishi na mumeo unaemtafuta na ataishi na mwanao kama mwanae na atampenda kwa dhati ...mungu akupe hekima na busara

By Living kereth
Amen kaka angu....
 
Moyo wangu uko tayari kupenda tena ila kinachonipa mawazo ni wapi nitampata mwanaume nitakaempenda kwa dhati, nina tatizo na kuwaamini wanaume wa Dar ila pia sitaki mapenzi ya mbali sababu yalinipotezea mwanaume niliyempenda kuliko mwanaume mwingine chini ya jua.
Na shida yangu sasa huwa nampenda mtu siku ya kwanza nimemuona ila katika pitapita zangu sijaona mtu wa kumpenda mpaka leo yan wanaonifuata hamna hata mmoja anaenivutia.
Njoo na mikoani labda utampata
 
Sifa ya nini? Chura ipo sema hii ni tatizo sababu hata kama mtu hana mpango na mimi unakuta anakuja kumbe kafuata chura tu. Sitak mwanaume aje kwangu sababu ya chura au uzuri, nataka anipende nilivyo
Be patient 2 mpenz wak wa maixha anakuja soon 2
 
Back
Top Bottom