Natamani sana Ndoa za dini ya Kiislamu " Its the best marriage Ever"

Natamani sana Ndoa za dini ya Kiislamu " Its the best marriage Ever"

Nyenyere,
Nawaza UJINGA ikiwa Kiungo cha mwili wako kinaweza kukatwa kuepusha kuharibu viungo vyengine na kulinda Afya yako Ije iwe ndoa ndo kiwe kitu cha milele na mtu mlie juana ukubwani tu na kila mtu na fikra zake .hapo ndo mmoja anawe kupanga kumuua mwenziwe ili awe huru Kwenye uislamu ndoa Si utumwa ni Maslahi na maelewano kama hamna ruhsa kuepukana nayo ili kila mtu awe huru
 
Nawaza UJINGA ikiwa Kiungo cha mwili wako kinaweza kukatwa kuepusha kuharibu viungo vyengine na kulinda Afya yako Ije iwe ndoa ndo kiwe kitu cha milele na mtu mlie juana ukubwani tu na kila mtu na fikra zake .hapo ndo mmoja anawe kupanga kumuua mwenziwe ili awe huru Kwenye uislamu ndoa Si utumwa ni Maslahi na maelewano kama hamna ruhsa kuepukana nayo ili kila mtu awe huru
Umesema kweli, KWENYE UISLAM. Lakini ndoa haina maana hiyo uliyoitoa, ndio maana huko ndoa imepoteza maana yake. Hoja ya msingi hapa tujiulize, kwa nini leo hii divvorce rates imekuwa kubwa kuliko zamani? Nini kimebadilika?

Ukipata jibu la hilo swali utajua mzizi wa tatizo. Mimi ni mkristo, namshukuru Mungu kwa sababu ya ndoa yangu. Napitia changamoto za kawaida tu ambazo hazijalishi kama ni mwislamu ama mkristo, kwa kiasi kikubwa Mungu ameniepusha na majaribu yanayoshinda uwezo wa mwanadamu kuvumilia.

Sasa nikikuambia, habari ya talaka ni mfumo wa mwanamume kumuumiza mwanamke na pia ni roho ya ubinafsi. Ni ngumu kunielewa hapa hata kwa wanawake kwa sababu ya fikra tulizopandikizwa, lakini ni ukweli mweupe kabisa kiwa thamani ya mwanamke hupanda mbele ya jamii pale anapoolewa na hushuka maradufu pale anapoachika.

Mwanamke akiachwa hutazamwa kama bidhaa isiyo na thamani na huongelewa negatively na wanaume walio wengi. Wako wanawake ambao baada ya kuachia walipata ndoa nyingine stable, lakini wengi wao waliishia kuwa wadangaji ama washirika wa waganga wa jadi. Sababu kubwa ni kuwa mwanamke hakuumbwa kuolewa na kuachwa hovyo, kwani thamani yake inaambatana na yule mtu wake wa kwanza, aliyeutoa usichana wake na kumwingiza kwenye daraja ya mwanamke.

Ukitaka kuhibitisha hili jiulize ni wanaume wangapi waliofanikiwa kimaisha watakwenda kuoa mwanamke mwenye ndoa 3, ama ni vijana wangapi ambao wana malengo kimaisha (wasiopumbazwa na maumbo ya kisasa) wataacha kujitwalia mabinti wabichi wakaoe watalaka.

Ndoa za wake wengi ni namna ya KUJIBU TAMAA YA KINGONO YA MWANAMUME kwa kigezo za kumsaidia mwanamke. Watu wamehalalisha uzinzi kwa kujipachika jukumu la kuwasaidia wanawake ingawa mpaka leo hakuna ndoa yenye furaha kwa sababu tu mume ana wake wengi. Huku ni kudanganyana na sio ukweli halisi.

Furaha ya kweli ni ipi? Je,
1. Ni kuoa wanawake wengi?
2. Kuwa na uwezo wa kutoa talaka wakati wowote?

Nasubiri majibu

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
adolay,
Ni kweli kabisa kila ndoa inachangamoto zake ila mfumo ndo unaopelekea kuonekana hiki bora kukiko chengine mfano itokezee Binti yako umemlea katika mazingira mazuri ya kiimani ya dini yake akaja mume akaigiza kua ni mtu mwema sana mkampa baada ya hapo Rangi halisi ya mume ikajitokeza mlevi mpigaji Muasharati .Je unamuokoaje Binti yako katika mateso hayo au ndo mpaka afe mmoja wao
 
Nyenyere,
Nikianza na ongezeko la talaka hii inatokana na wanandoa wenyewe kutokufata taratibu halisi za ndoa ama kukwepa misingi halisi ya ndoa kitu chochote kisipokua na msingi madhubuti hakiwezi kudumu.

Mimi ni Muislam na Nina wake wawili na sijawahi kuacha hata Mara moja na naona tofauti kubwa nilipokua na mke mmoja na baada ya kua na wawili IPi furaha ya kweli.

1 ni kua katika ndoa ya maelewanoa na makubaliano kwa hiari yenu wote sio kulazimishana Maana yake Ukiona ndoa ya Kiislamu ipo maana yake hakuna alielazimishwa hapo migogoro ni kawaida kutokea na kutatuliwa kwa taratibu maalum zilizowekwa hatua kwa hatua Kwa upande wa imani yako ndoa nini ?

Ukisema kua mwili mmoja rudia Nilipowaza ujinga inafika kipindi inabidi kiungo kikatwe kuepusha madhara zaidi
 
ALI V. MUSSA,

Umejibu vema mkuu, ongezeko la talaka inatokana na wanandoa wenyewe kutokufuata taratibu halisi za ndoa ama kukwepa misingi halisi ya ndoa. Huu ni ukweli kabisa, nakupa tano kwa hilo.

1. Ndoa za siku hizi hazifuati misingi ya ndoa hivyo kupelekea watu kutalikiana hovyo.

2. Ndoa za siku hizi zimejengwa kwenye tamaa ya kukidhi kiu ya ngono kuliko kujenga familia stable. Wanandoa wanaoana ili tu kujaribu kukata kiu ya ngono, hawana mtazamo mwingine kuhusu ndoa, ndio maana UJINGA WA KISASA ni habari za vibamia, mashimo makubwa n.k. Katika hayo yote hakuna msingi wa ndoa.

3. Sijakuelewa unaposema ndoa za kulazimishana kwa sababu ninachoelewa ni kwamba mwanamke na mwanamume wanakuw na consent kisha wanaamua kuwa wanataka kuoana. Hakuna anayemshikia bunduki mwenzake, ni hiari ya moyo. Sasa wawili hawa wakikubaliana wanaamua kuita watu na kuweka ushahidi mbele yao na mnele ya Mungu kwamba wameamua kuungana hivyo mwingine asijaribu kuwaingilia.

Inapotokea wamepishana ama kukorofishana iweje mtu mwingine ahusike hapo? Kwa nini kumnyooshea kidole mtu wa tatu kuwa amewalazimisha kuungana wakati hata hakushiriki kuwapa mashauri waoane?

Ndoa ya kikristo imepaswa ijengwe katika msingi wa kumwamini Mungu. Kwamba umwamini atakupa mke ama mume bora, lakini swali linalowatesa wengi na kuwafanya wabaki kuzini hovyo ni hili:

Je, umemwamini Mungu kiasi cha kufuata maagizo yake na kusubiri akuonyeshe mke au mume wa maisha yako?

Ni wangapi leo wanaweza kusimama na kusema waliingia kwenye ndoa kwa kufuata vigezo vya Mungu? Wengi weru tunaingia kwenye ndoa kwa kufuata vigezo vilivyowekwa na dunia, tunajitwalia wake na waume wa upofu wetu. Mambo yawapo magumu tunatamani tuwaache tutafute wengine, kwa sababu hawa hawakuwahi kuwa wenza wetu hata hivyo. We pre empt God.

Kwa sababu tunaona katika mazingira ya umalaya halafu tunategemea tuishi kwa utakatifu, basi tunajikuta tukitapatapa tu, tuna elimu ya umalaya na ukahaba imeijaza mioyo yetu, halafu tukiingia kwenye ndoa tunataka tuishi kwa elimu ya Mungu ambayo hatuna. Tutajiita wana wa Mungu huku tukimtumikia shetani, kwani kiujazacho moyo wa mtu ndicho kiutokacho.

Suluhu ya hili sio kuoa wake wengi, kwani katika hao pia kama hujafuata misingi ya ndoa bado talaka zitaendelea tu. Misingi ya ndoa ndio jibu kama ulivyobainisha hapo juu. Huwezi kutumikia mabwana wawili, kwa maana utampenda zaidi huyu kuliko mwingine, hata mtume alimpenda zaidi Bi Aisha kuliko wakwze wengine, ni maumbile tu hayo.

Jifunze misingi ya ndoa kabla ya kuingia kwenye ndoa, uli unapooa uoe kwa motive sahihi nawe utampata aliyesahihi kwako. Hivi ndivyo ilivyokuwa tangu kale, watu walioa kwa malengo sahihi kwa kuzingatia misingi ya ndoa, ndipo ndoa nyingi zilidumu.

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
Ni kweli kabisa kila ndoa inachangamoto zake ila mfumo ndo unaopelekea kuonekana hiki bora kukiko chengine mfano itokezee Binti yako umemlea katika mazingira mazuri ya kiimani ya dini yake akaja mume akaigiza kua ni mtu mwema sana mkampa baada ya hapo Rangi halisi ya mume ikajitokeza mlevi mpigaji Muasharati .Je unamuokoaje Binti yako katika mateso hayo au ndo mpaka afe mmoja wao

1. Utaratibu wa uchumba umeenda wapo

2. Taratibu za kusomana tabia zimeenda wapi

3. Kwanini historia ya kijana na wazazi isijulikane

A. Ndoa za chapchap kama chapati za maji ndio matokeo yake hayo ...... unaoa asbh jion talaka.....unaoa Jumatatu.....Jumamosi talaka. Mzigo wake abebe mwenyewe mpaka kwa aliemfugisha hilo doa lisilofutika.

B. Mimi sishughuliki na matatizo ya binti, dada au ndugu yangu ambaye kwa utashi, akili na maono yake kajichagulia Mume/Mke
Sababu ndoa nijukumu lake na huyo mwenza wake. Ashughulike na majanga yake.
 
Mwisho wa siku upendo wa ndoa ukiwa upo hizi sheria za ndoa hata hazi apply chochote tatizo sio sheria za kidini kuhusu ndoa tatizo ni kumpata aliye sahihi kwako au munae endana tu
 
Naungana na wewe kabisa mkuu kwa 100%, yaani umeongea kitu ambacho siku zote huwa nnakisema kwa watu.

Tena umeniwahi tu mimi mwenyewe nilikuwa najiandaa kuleta uzi kama huu wako.

Ndoa za kiislamu ni ndoa bora kabisa na wanawake wa kiislamu ni wanawake bora kabisa kwa ndoa.

Btw, i am Christian by religion.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwisho wa siku upendo wa ndoa ukiwa upo hizi sheria za ndoa hata hazi apply chochote tatizo sio sheria za kidini kuhusu ndoa tatizo ni kumpata aliye sahihi kwako au munae endana tu
Umenena vema kabisa, tofauti ya ndoa za kisasa za kikristo na zile za kiislamu ni moja tu;

Waislamu wanaruhusu trial and error, wakristo wao hawana hicho kitu. Ukichagua umemaliza, lakini zote zinakwepa msingi wa tatizo, kumpata mtu sahihi.

Ndoa zaa kiislamu kwa kiasi kikubwa zinajibu tamaa ya mwili sio kwa kuleta suluhisho la kudumu, bali kutoa uhuru wa kuoa na kuacha kadri mtu anavyowaka tamaa. Mimi kimsingi huwa sizichukulii kama ndoa bali huwa naziona kama makubaliano maalum kukaa kwa muda kadri mtakavyoona inafaa. Hakuna ndoa ya kweli hapo, nikimtamani mwanamke namwoa namtumia, nikimchoka namtafutia sababu namwacha ama natafuta mwingine tena naongezea. Mwisho wa siku nakuwa na zizi la wanawake ambao nitakiwa naacha na kuoa wengine kadri navyotamani. Ni shida tupu

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
Back
Top Bottom