Nategemea kwenda Shinyanga kwa pikipiki aina ya Boxer, CC 125

Nategemea kwenda Shinyanga kwa pikipiki aina ya Boxer, CC 125

HAOJUE TR 150
1695553097887.jpeg

ni kama hii mkuu
 
Tabu yote hiyo ya nini mkuu?

Hiyo pesa ya kupambana na mafuta ningeshauri upandie basi kwa usalama wako, Dar <> Shinyanga ni umbali mrefu sana...

Kila la kheri...

Ndugu wanajamvi nategemea kwenda Shinyanga nikitokea Dar es salaam kwa Piki piki boxer cc125 mwenye uzoefu itakuwa vyema ukanisaidia.

Nataka kujua mafuta naweza kutumia kiasi gani. Je, nijiandae kwa changamoto gani barabarani pikipiki hii ninayotaka kuitumia ni mpya. na nina tegea kwenda na kurudi....

View attachment 2760635.
 
Hii inaruhusu sana mkuu. Unaendesha huku umerelax sana
ila asikwambie Mtu mkuu safari ya pikipiki inachosha make sure hata kama wanasema si salama kiafya Piga ENERGY DRINK.

Asee pikipiki unaweza fika kati kati ukasimamisha lori ukawambia wakubebe na pkpk yako.

Safari inachosha, nilifata pikipiki Tanga ilikua inauzwa Laki 5 nikaipga service ili itembee tu kisha nikawa nakuja nayo dar Nilijuta na ile safari ilibaki kidogo nishushe chozi. Saivi pikipiki kama sio Mpya Siendeshi wala siigusi narekebisha nauza.

Maxmum time yamimi kukaa na pk pk yangu ni 2yrs kisha nauza sizidishi,kama mteja hajapatikana naiweka pembeni nanunua nyingine ile naitaftia mteja taratbu.

Hamna chombo hatari na rahisi kukutoa maisha kama pikipiki chakavu.
 
Mkuu unafika vizuri pikipiki inafika popote tu. Sina uzoefu ila kuna jamaa huwa anaenda korogwe kwao na kurudi usiku wake kwa kutumia boxer 125cc
 
Ndugu wanajamvi nategemea kwenda Shinyanga nikitokea Dar es salaam kwa Piki piki boxer cc125 mwenye uzoefu itakuwa vyema ukanisaidia.

Nataka kujua mafuta naweza kutumia kiasi gani. Je, nijiandae kwa changamoto gani barabarani pikipiki hii ninayotaka kuitumia ni mpya. na nina tegea kwenda na kurudi....

View attachment 2760635.
Ushauri wangu: Kabla hujaondoka huko uliko kwenda Shinyanga andika na wasia wako
 
Kuna wale madogo waliamua kwenda Karatu kwa pikipiki aina ya SanLG kutokea Morogoro, hata Dumila hawakuiona wakakata moto! Kuna mwalimu aliamua kusafiri kwa pikipiki kwenda kumzika mamake huko Simiyu akitokea Dodoma Msalato sec. Hata Manyoni hakuiona akakata moto! Tutofautishe pikipiki za masafa marefu wanazotumia Wazungu na hizi bodaboda! Kwa bahati unaweza kufika salama lakini iwe "at your own risk!"

Walikata moto kwa ajali ama nini??
 
Ndugu wanajamvi nategemea kwenda Shinyanga nikitokea Dar es salaam kwa Piki piki boxer cc125 mwenye uzoefu itakuwa vyema ukanisaidia.

Nataka kujua mafuta naweza kutumia kiasi gani. Je, nijiandae kwa changamoto gani barabarani pikipiki hii ninayotaka kuitumia ni mpya. na nina tegea kwenda na kurudi....

View attachment 2760635.
Kama unatoka dar kwenda shinyanga basi, ukirudi pitiliza mojakwamoja muhimbili mwaisela tutakuja kukuaga huko na tumatunda na juice
 
Ndugu wanajamvi nategemea kwenda Shinyanga nikitokea Dar es salaam kwa Piki piki boxer cc125
Unaenda kuonyesha huko kijijini kama unamiliki pikipiki? Umeamua kuangalia na kufurahia mazingira? Au unajiandaa kuwa komando?

Dah, kama abiria upo ndani ya VVIP bus za Dar-Mwanza na Shinyanga bado unaona kero na mateso, sipati picha mwendesha pikipiki halafu boxer!

Kupanga ni kuchagua!
 
Mkuu mi Nina boxer cc150 Huwa napiga sana hizo safari mpaka Kuna nyakati nishawahi sinzia nikiwa road kutokana na uchovu, nakumbuka Kuna siku nilisinzia mpaka pkpk ikasimama yenyewe ndipo nikashtuka nlikuwa natumia Honda Manji(cc125).

Kwa safari yako Dar to Shy
Hakikisha pkpk ipo fresh Kwa maana umeifanyia service ya kutosha na hakikisha nat zimekazwa vzr(zinakawaida ya kulegea, ni hatari sana), tairi weka oko(ziwe tubeless), honi iwe poa,sight mirror, breaks zote ziwe vzr, indicators zote ziwe poa, Oil tumia zenye kumudu umbali mrefu km vile Oryx, Mogas, Advanced etc. Pia beba baadhi ya spana muhimu kama vile size 10, 19,20 etc Kwa ajili ya kutatulia matatizo madogo madogo. Funga walau tofali moja la block ili kupata utulivu na kupunguza kuyumbayumba ukipigwa na upepo mkalli.

Kwa upande wako, Vaa jacket nzito sana, kofia ngumu,viatu vya kupanda mpaka kwenye ugoko, miwani, gloves ngumu za mikono ili kujikinga na baridi nyakati za usiku, begi ambalo utaweka vinywaji hasa energy na maji.

Kuhusu wese, Lita moja inatoboa km 35 mpaka 45, hivyo ni kupiga tu hesabu zako(tumia minimum km 35 Kwa Lita).

Ukiwa safarini, Vaa earfone zako weka nyimbo au simulizi ufurahie safari na pia ikate usingizi. Pia, ukihisi uchovu simama pumzika, nawa maji usoni au km Kuna huduma ya kuoga is best option, sight mirror iwe unajiupdate muda wote, jitahd kubana upite kushoto Kwa mstari wa road kuepuka kujisahau alafu ukashtuliwa na honi ya GSM au HOOD. Kuwa makini muda wote Kwa kuchukua taadhari zote za kiusalama, kumbuka gari kubwa zikiwa main road huwa hawajali waendesha pikipiki wanawachukulia watu wabishi hivyo hawajali kama nawe unategemewa na familia.

Kumbuka:
Kuomba Dua muda wote, beba vitambulisho Incase ili iwe rahisi, pia toa updates Kwa mtu wako wa karibu ili kama utarest iwe rahisi kufuatilia, kama una familia andika wosia.

Nikutakie safari njema, enjoy the View mkuu.
 
Back
Top Bottom