National crisis: Vijijini hakuna watu kabisa, wamebaki wazee wachache na vijana walevi wa visungura

Nadhani tittle lilipaswa kusomeka
Crisis in Kilimanjaro! Vijijini hakuna watu wamebaki wazee wachache na vijana hopeless walevi kupindukia!
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… True kwa kilimanjaro
Mna uhakika na hili ?
Tuna uhakika buashee kule migombani nguvu kazi ni wapare, wachagga waliopo ni wachache na wanasaidiwa.
 
Kwanini? Serikali isiwaruhusu taasisi binafsi kufanya sensa ya watu na makazi kunaweza kuwa hatua muhimu katika kuhakikisha uwazi na uhalisia wa takwimu za idadi ya watu. Hapa kuna baadhi ya sababu za kwanini hatua hii inaweza kuwa na manufaa:

1. Uhakika wa Takwimu
Taasisi binafsi zinaweza kuleta mbinu tofauti za ukusanyaji wa data, na kwa hivyo zinaweza kutoa picha halisi zaidi ya idadi ya watu. Hii inaweza kusaidia kubaini ukweli kuhusu idadi ya watu na kuwepo kwa makazi.

2. Kujenga Uaminifu
Wakati wananchi wanapohisi kuwa takwimu za serikali haziko sahihi, kuhusisha taasisi zisizo za kiserikali kutasaidia kujenga uaminifu. Wananchi wataweza kujiridhisha na taarifa wanazopewa, na hivyo kuimarisha imani yao katika mchakato wa sensa.

3. Kujibu Maswali ya Kijamii
Kuwepo kwa sensa huru kutawasaidia wananchi kuhoji na kuelewa kwa undani masuala yanayohusiana na idadi ya watu, kama vile mtindo wa uhamiaji na mabadiliko ya makazi. Hii itasaidia katika kupanga sera bora za maendeleo.
4. Kuwezesha Mipango Bora ya Maendeleo
Takwimu sahihi zinahitajika ili kuandaa mipango ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Ikiwa idadi ya watu inajulikana kwa uhalisia, serikali na wadau wengine wataweza kupanga na kutekeleza miradi inayokidhi mahitaji halisi ya wananchi.

5. Kujenga Ushirikiano
Kuhusisha taasisi binafsi katika sensa kutajenga ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi, kuwezesha ufikivu wa rasilimali na utaalamu mbalimbali. Ushirikiano huu unaweza kuleta mabadiliko chanya katika ukusanyaji wa data.

Hitimisho
Hatimaye, kuruhusu taasisi binafsi kufanya sensa ya watu ni hatua muhimu ambayo inaweza kusaidia kulinda haki za wananchi na kuleta uwazi katika mchakato wa kukusanya taarifa. Serikali inahitaji kuzingatia mawazo haya ili kuweza kuboresha hali ya maisha ya watu na kuwa na takwimu zinazoweza kuaminika. Hii si tu itasaidia katika kubaini idadi halisi ya watu, bali pia itachangia katika maendeleo endelevu ya nchi.
 
Ukitaka kujua nchi ina vijana wangapi tangaza ajira kila mkoa tarehe ya interview iwe moja. Vigezo usiweke vigumu na mshahara ahidi mzuri kwa level zote kuanzia drs la 7 hadi degree.
 
Ungeenda direct tu kwenye point unataka watu wazaliane kama sungura,
Usizunguke sana.
 
Dunia ina watu bilioni 8, hata wakipungua nusu na kubaki watu bilioni 4 bado ni watu wengi sana.
Mwaka 1960 dunia ilikuwa ina watu bilioni 3 tu.
 
Ukitaka kujua nchi ina vijana wangapi tangaza ajira kila mkoa tarehe ya interview iwe moja. Vigezo usiweke vigumu na mshahara ahidi mzuri kwa level zote kuanzia drs la 7 hadi degree.
Idadi ya vijana unao wasemea haiwezi kufika 30 million!
Je hao walio Baki 30 millions plus wako wapi?
 
Mkuu ondoa hofu watu vijana kijijini wapo...

Siku nyingine ukienda kijijini tegea siku yenye mechi kali tafuta kibandaumiza utashangaa,

Ila kwenye pombe hapo kwa kweli vijana tumekwisha(kina mulokozi wanatembea na fursa).

Ila pia mtawanyiko wa watu unategemea fursa za eneo, kuna maeneo kwa kijana anajitambua lazima alale mbele.
 
Tatizo sio kwamba watu hawapo!
Hakuna watu 60 millions ❌❌❌❌❌
 

Jua Kali unataka uwaone watu Nje wakikaangwa kama Karanga?

Pesa hakuna unataka watu waende huko Bar kujiuza?
 
Idadi ya vijana unao wasemea haiwezi kufika 30 million!
Je hao walio Baki 30 millions plus wako wapi?
Kwenye bodaboda,
wamachinga,
Makondakta na wapiga debe,
Wauza maji, juice, pipi na biskuti
Makuli,
Panya Road,
Wapaka rangi,
Bar maids
 
Huyo anayesema crisis in kilimanjaro nadhani hajawah kufika huko , hebu ufanye uje kwanza ukianzia na rombo utembee kata zote za rombo then uje utoe mrejesho , otherwise acha kuongea nonsense
 
Mambo mengine yanachekesha Sana

Nyerere wakati anatawala nchi kulikuwa na watu mil 12 nchi nzima.

Leo anaibuka MTU hapa anadai Tanzania Ina watu laki 5 .

Kuna thread ukisoma unajua mtu kaamua kuchangamsha genge .
Atakua kaamkia bar yawezekana ni mlevi wa kupindukia. Akili mbovu kabisa.
 
Tunaomba idadi ya watoto wa kike na WA kiume walio zaliwa siku ya Xmas !
Nenda ofisi ya taifa ya takwimu ama wizara ya afya ama zunguka mahospitali yote tanzania, msisumbue watu, tukiwa pungufu ama zaid inakusaidia nini wewe na familia yako, wewe kama unaona watu pungufu umeruhusiwa kuoa wanawake hata 30, wazalishe wote watoto kumikumi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…