Naufananisha Uwanja wa Ndege wa Chato na Ofisi ya Spika ya Urambo

Sawa mkuu. Sasa hizo ndege zinazotua Chato kwa sasa ni zipi .....!?
 
Unaweza kuniambia kwanini moshi inabarabara nyingi za lami mtaani kuliko wilaya yoyote Tanzania ni kweli kwamba barabara hizo zilipitishwa bungeni.
Dhambi haihalalishwi kwa kufanya dhambi. Hayo ya Moshi kama ni madudu walaumiwe wazazi wetu waliokuwa na uwezo mdogo wa kuhoji mambo.

Hivi Sasa watanzania siyo wajinga. Chato international airport ni tunda la udikteta
 
anataja miradi yooote ila Chato na burigi hazitaji.
kwenye mabango amepiga kashika mikono anatia huruma kama sio yeye?? ngoja alazimishe kushinda hahahahaaa na anajua ndio msimu wa mwisho hana cha kupoteza this time tutalimia meno kwelikweli
 
Wat

Watu dizaini yako ni wale mnaoamini katika ukanda ukijengwa hai sawa bila chato hapana,hai ni wilaya na chato ni wilaya na ukizingatia ukuaji wa miji ni halali kabisa kwamba kiwanja cha ndege lazima kikae mbali na mji .
Usiunge mkono huu upuuzi kwa kuwa unaishi Chato. Huu ujenzi wa international airport ni tunda la udikteta uliokomaa
 
Mmeshazoea kusambaza Sera zisizo na mashiko almashauri zote zinatakiwa ziwe na viwanja vya ndege kwenye mipango endelevu ya miji,pia hoja ya kufananisha gaboloni ni mfu,kipindi hicho nchi ya Kongo ilikuwa na ndege o1 tu ya rais,alafu huo mji ulikuwa ni mdogo huwezi fananisha na chato ambayo ni mji unaokuwa kwa kasi na ni njia ya kwenda miji mingi na inapakana na ziwa na miji mikibwa kama mwanza na kahama pia uwanja aliujenga kwa manufaa yake binafai ila wa chato upo kwenye ramani ya almashauri,hoja ya kutotumiaka wa gaboloni ni kwamba mpaka sasa Kongo haina shirika LA ndege na haina ndege ,sasa sisi tunazo na zinaongezwa na na lengo tufikie lengo la kufanya usafiri wa ndege uwe wa kawaida katika nchi yetu na kufikia 2025 kila wilaya ipate kiwanja cha ndege cha kiwango cha lami.
 
We kinachokuuma Ni Nini? Ikiwa maendeleo analeta kote.
 
Usiunge mkono huu upuuzi kwa kuwa unaishi Chato. Huu ujenzi wa international airport ni tunda la udikteta uliokomaa
Hivi kinachosababisha uone anasa ni nini hiyo lami au urefu wa uwanja au umeona kuna jengo LA abilia linalofanana na LA songwe,chadema msiturudishe miaka ya 2000 kuona ndege wilayani mpaka mzungu aje afuate madini mimi naunga mkono magufuli kujenga viwanja nchi nzima na kununua ndege naelewa faida ya kupanda ndege na kamwe siungi mkono watanzania kuona ndege kama anasa lazima ndege ziwe kitu cha kawaida ndani ya nchi yetu Mimi,we we,bibi,babu tuzipande pindi tunapoitaji kusafiri ombi language kwa rais ajaribu kuziongeza ili ziwe kama bodboda uzuri Uganda imegundua mafuta ivyo tutapata mafuta ya ndege kwa bei ndogo.
 
Those places were abandoned kwa sababu hakuna mtu alitaka kwenda kuishi huko .... same itakuwa Chato International Airport, wakina mama wa kisukuma watakuwa wanaanikia mpunga hapo na kuna mjengo ambayo yatakuwa abandoned baada ya 2025!!
Kwanza wewe inaonekana hujawahi kupanda ndege,kwa tunaojua umuhimu wa kupanda ndege tunajua faida yake kutokea dar mwanza Massa 16,dar kigima 18,sasa ukuwa na ndege nyingi bei itashuka na kila MTU anaweza kupanda kwenda popote na hizi ndege ni kama gari tu nazo zinaitaji sehemu mzuri za kutua wala si anasa tuungane kumpigia kura magu ili apite aendelee kujenga viwanja kama vilivyojengwa kigoma,mtwara,songea,mbeya,rukwa,kagera,hai, arusha,mwanza,iriga,njombe na sehemu nyingine ndege ni usafiri wa haraka na unapunguza muda wa kukaa njiani tumuunge mkono ili watu wote tupande ndege.
 
Dah!!!!,Jamaa alikula sana maisha.
 
Wewe unasema nini. Nimepanda ndege za ATC ya Mwalimu. Inawezekana hata huyo unayemtetea alikuwa bado hajapanda ndege.

Tunachozungumzia hapa ni justification ya kujenga uwanja Chato .... hiyo bado hamjafanya!!
 
Kwa biashara gani hapo chato kwa uwekezaji wa PESA kwa mabilion?

Mbona JK hakujenga AIRPORT kule MIONO ili Watalii waende Sadani National Park?

TAFAKARI..
Mkuu afadhali Saadani ilikuwepo lakini hata hiyo Burigi-chato imetengenezwa kwa kusafirisha twiga na simba wetu wengi wamefia huko wengine wamehamia kwa Kagame na amewafungia huko. Ukienda burigi utaendelea kushuhudia utalii wa tumbili na nyani (primates) kama tulivyozoea! Hawa ni wabinafsi zaidi ya mashetani. Eti ana mpango wa kuagiza bulldozer kubwa ili 😢😢😢😢😢😢kuhamishia mlima kilimanjaro chato!
 
Ujajibu swali la msingi kwanini ulalamiki flyover inajengwa dar? Why kujenga uwanja chato Ni nongwa? Kwani watu wa chato sio watanzania? Ungejua mantiki ya swali langu using uliza swali
Unajua kazi ya freeway interchange kwa jina lingine ni fly over huwa zinajengwa sehemu zenye msongamano wa magari. Na dsm msongamano upo Sasa kwanini alalamike
 
MaCCM yanatetea uwanja wa Chato kwa kupanic, hii inaonyesha ni kwa namna gani huyu Jesus feki wao anavyo boronga mambo, inawapatia wakati mgumu sana kutetea maujinga yake.

#FutaCCMyaMagufuli
Gharama za kuhudumia Uwanja wa ndege ni kubwa sana na zinalipwa na Ada ya Kutua ndege lakini kama ni ndege moja tu ya Serikali ndo inatua hapo kwa mwaka ikimleta mama wa Rais kusherehekea Krismas Ina maana gharama zote zinalipwa na Serikali. Huyo mama angeweza kupelekwa kwa helicopter mpaka nyumbani kwake na pesa za kujenga uwanja na kuutunza zingetumika kutatua matatizo ya upatikanaji wa maji safi na salama ya Vijiji lukuki hukohuko Kanda ya Ziwa au madarasa ya shule za huko au madawati au vyoo au au au .... Kuhudumia mbuga za wanyama ni gharama kubwa sana zinazotakiwa kulipwa na mapato ya utalii ambao nao unasuasua kwenye mbuga zote na Burigi itachukua miaka zaidi ya 50 kufikia wingi wa wanyama kama Serengeti. Ruaha ndo Mbuga kubwa kuliko zote na wanyama wengi lakini Uwanja wa ndege mkubwa utakaokuwa karibu ni ule wa Msalato, Dodoma utakapokamilika kwa Sasa ukiwa bado kwenye mpango tu. Kiongozi wa nchi anatakiwa aangalie matatizo na fursa za nchi nzimà badala ya eneo moja dogo kwa sababu nyepesi binafsi. Vivutio vyetu vya utalii havijatumika kwa viwango vya juu kama inavyotakiwa ili viweze kugharamia huduma zote za utunzaji wao kwa sababu ujio wa watalii ni mdogo sana kwasababu huduma muhimu kwa watalii zinakosekana. Viongozi wetu hasa wa Awamu hii ni wajinga sana hawajui kuwa kivutio kikubwa zaidi kuliko vyote kwa nchi yoyote ya kitalii ni watu wa nchi husika wanavyoishi na maingiliano yao na watu wengine. Nchi yetu inajulikana dunia nzimà kuwa wananchi wake ndo watu wanaoongoza kuwa hawana furaha, kwa hiyo mtalii mwenye furaha atasita kuja kuwatembelea Wabongo wasio na furaha na kwenda nchi nyingine.
 
Wewe unasema nini. Nimepanda ndege za ATC ya Mwalimu. Inawezekana hata huyo unayemtetea alikuwa bado hajapanda ndege.

Tunachozungumzia hapa ni justification ya kujenga uwanja Chato .... hiyo bado hamjafanya!!
Sasa kwani ujuhi kuwa ni suala la mipango miji kila almashauri lazima kuwe na uwanja wa ndege na lazima sasa viwanja vya ndege vyote viwekewe lami kwa kuwa ndege zipo na zinaongezeka sasa nikuulize je. Ni chato tu ndio kimejengwa kiwanja cha lami.
 
Sasa hivi ameeandia sera za lissu
Bima ya afya na kuwezesha sekta binafsi
 
Ujajibu swali la msingi kwanini ulalamiki flyover inajengwa dar? Why kujenga uwanja chato Ni nongwa? Kwani watu wa chato sio watanzania? Ungejua mantiki ya swali langu using uliza swali

Wewe kijana ni mpumbavu. Yaani economic sense kwa flyover ya Dar huioni?? Economic sense ndio inapaswa kuwa sababu pekee ya kufanya maamuzi yanayohusu uchumi!! Uwanja wa Chato ulipaswa kujengwa Dodoma! Na economic sense ingekuwa “kuwezesha safari za kimataifa kuka mji wa kiserikali/kiutawala”.

Kama hutaelewa economic sense, hutakuja kujua kwanini vijijini hakuna maji ya bomba, na yako mijini!! Hutakuja kujua bidhaa moja ina bei tofauti kati ya Kigoma na Dar es Salaam. Economic sense!!!
 
Ndugai amewahi kuitumia hii ofisi?
 
Najiuliza kama Tanzania bado ina master plan ya viwanja vya ndege. Miaka ya nyuma, miundombinu yote mikuu ilikuwa inaandaliwa master plans zinazotafitiwa na kujadiliwa kikamilifu kisha kuwekewa mipango ya utekelezaji. Hii ni kutokana na gharama kubwa sana za rasilimali hizo na umuhimu wa kuepuka kuishia kuwa na “magofu” yasiyo na faida yoyote (white elephants). Master plans hizo hupitiwa na kuboreshwa baada ya miaka kuongeza, kupunguza na kurekebisha viwango vya miradi kutegemeana na mabadiliko mbalimbali.

Siku hizi inaelekea ujenzi wa miundombinu unategemea zaidi maamuzi na maagizo ya Rais. Pamoja na hivyo, itakuwa vyema basi kama wahusika wakuu wangekuwa wanatolea ufafanuzi mzuri (articulation) kuthibitisha maamuzi ya aina hiyo yana msingi tokea kwenye mipango mikuu ya maendeleo, infrastructure master plans, na mipango ya utekelezaji.

Kiutaratibu, kabla ya utekelezaji, mradi kama wa Chato ungeweza kuingizwa kwenye masterplan na kupewa maelezo ya kitaalamu yanayoeleweka badala ya kufanywa kuwa suala la propaganda za makada wa kisiasa. Muda ulikuwepo. Haipendezi kuwaachia makada wa CCM kuja na utetezi mfu kama: “Chato sio Burundi”; “hata wakazi wa Chato nao wanahitaji maendeleo”; “tunakuza utalii”; nk. Hoja sampuli hiyo ndizo zilizotumika kuhalalisha ujenzi wa kiwanja cha ndege cha kiwango cha kuhudumia Concorde kijijini kwa Mobutu. Zinamfanya Rais aonekane “wa ajabu kweli kweli” mtake, msitake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…