Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Unajua sababu ya Nchi kutokukopesheka??
Kwanza Mwalimu alikataa madini yasichimbwe kama Serikali haitapata asilimia 50 ya mapato yatakayo patikana ! = Waliokuja wajanja baada yake wakaruhusu mikataba ikatiwa saini Serikali ikawa inapewa asilimia 3 % ya mapato yanayo patikana kwenye dhahabu 😱 !

Nchi ilishindwa kukopesheka kwa sababu Nchi ilikuwa na deni la Dollar billion 8 inasemekana !
Mabepari lengo lao ilikuwa wakubaliwe kuchimba madini kwa bei Chee waliyokuwa wanataka wao !
Na pia walilazimisha ili Nchi iweze kukopeshwa na IMF ni lazima Mwalimu akubali thamani ya pesa ya Tanzania ishushwe !

Yote hiyo ilikuwa ni kumkomoa Mwalimu kwa sababu ya kwanza kuzisaidia Nchi nyingi za kusini mwa Africa kudai na kisha kupata Uhuru wao,
Tulikuwa tukibadili dolla ya marekani kwa shs 5 za Tanganyika na baadaye za Tanzania !

Mwalimu alifanyiwa hujuma na Mabeberu kwa sababu ya misimamo yake ya kukataa kunyonywa Rasilmali za Nchi !!
Weka Hiyo Akilini Mkuu 🙏👍
Izo hujuma hata mabeberu wenyewe kwa wenyewe wanafanyiana, na jukumu la kiongozi ni kuzi-outsmart izo hujuma.
 
Naona mfuasi wa Nyerere, mada imekupiga kwenye mshono, sasa kama uko Ethiopia na Kenya walitaabika ndio halali na sisi tutaabike.

Kuna ajenda ya siri nyuma ya kutukuzwa sana kwa Nyerere, lakini ukiangalia hali ilivyokua kipindi chake mfano umasikini nankushughulikiwa kwa walipishana nae mawazo kama Oscar Kambona.

Ukiangalia current consenquencies za maamuzi yake mfano kuto-review katiba licha ya kuona imempa Rais umungu mtu utagundua teacher hakuwa na maajabu kama anavyotukuzwa.
Maajabu yake ni kutembea nchi nzima miaka ile barabara zote ni vumbi tupu akitafuta uhuru wa Tanganyika, maajabu ni kuwa rais wa kwanza sawa na kina Sekou Toure, Jomo Kenyatta na waasisi wengi wa afrika.

Maajabu ni kujenga viwanda katika mikoa yote kwa lengo la kuinua uchumi, changamoto alizokutana nazo akiwa rais ni kubwa kwani miaka yake ilikuwa ni ya kujenga msingi wa kitaifa tofauti na marais waliyokuja baadae na kukuta misingi ipo tayari.
 
Ali- fail parefu, aliendesha nchi kwa kufuata misingi ya usawa wakati ata vitabu vya dini vinatambua matajiri na masikini na mpaka watumwa

Basically, aliendesha nchi kiimani zaidi na siyo kiualisia. Alizuia wapambanaji akawaita mabepari na mabeberu na akawa karibu na mediocre

NCHI ILIMSHINDA, HE WAS NAIVE
 
Maajabu yake ni kutembea nchi nzima miaka ile barabara zote ni vumbi tupu akitafuta uhuru wa Tanganyika, maajabu ni kuwa rais wa kwanza sawa na kina Sekou Toure, Jomo Kenyatta na waasisi wengi wa afrika.

Maajabu ni kujenga viwanda katika mikoa yote kwa lengo la kuinua uchumi, changamoto alizokutana nazo akiwa rais ni kubwa kwani miaka yake ilikuwa ni ya kujenga msingi wa kitaifa tofauti na marais waliyokuja baadae na kukuta misingi ipo tayari.
Uhuru wa nchi teacher alitangulizwa mbele na kanisa katoriki hakuupambania yeye mwenyewe kama jeshi la mtu mmoja.

Hizo changamoto alizokutana nazo ndizo kiongozi anatakiwa kuzitatua, hakuna excuses.

Mazuri alikua nayo mabaya alikua nayo, lakini kiujumla nchi ilimshinda ndio maana akaamua kung'atuka.
 
Ali- fail parefu, aliendesha nchi kwa kufuata misingi ya usawa wakati ata vitabu vya dini vinatambua matajiri na masikini na mpaka watumwa

Basically, aliendesha nchi kiimani zaidi na siyo kiualisia. Alizuia wapambanaji akawaita mabepari na mabeberu na akawa karibu na mediocre

NCHI ILIMSHINDA, HE WAS NAIVE
Alizijua hulka zetu za kuchukiana sisi kwa sisi, vitabu vya dini vinaandika maelezo ya jumla zaidi kuliko uhalisia wa afrika yetu.

Kuna umafia mwingi umefanyika na unaendelea kufanyika mfano pale wizara ya ardhi kuna makundi ya vijana wasomi wenye kutafuta pesa kwa njia za dhuluma za ardhi za watu. Ukiwa huna pesa utahangaishwa milele na hupati hati yako ukitoa milioni 10 mpaka 20 unapewa hati yako.

Ni mitandao ya wizi imeletwa na hulka zetu sisi wenyewe, Mwalimu kuja na sera za ujamaa ni kwa sababu alizijua hizi hulka kabla sisi hatujazaliwa, alifahamu kwamba bila ya elimu hakuna ukombozi kwa mtanzania wa kawaida.

Hivyo ujamaa ulikuwa na lengo la kuleta a level playing field, kuwa uwanja wa haki sawa kwa wote, na alifanikiwa mapema sana kwani bila ya kuwepo ujamaa kwa misingi yetu wenyewe sioni ni kwa namna gani haya yanayotokea Kenya leo hii yasingeweza kutokea hapa Tanzania.

Alihakikisha unyonyaji haustawi kwani unapokuwepo kunakuwa na taifa lenye uonevu unaokuja siku moja kulipuka na vifo vingi vinaweza kutokea.

Tunamlaumu kwa sababu hatukuwa ndani ya akili yake kwa wakati huo wa miaka ya kutafuta uhuru na mwanzo wa nchi iliyo uhuru.
 
Hakuuchukia utajiri kama utajiri aliiona jamii yetu kwa wakati ile ikiwa bado ipo nyuma sana kielimu na katika masuala mengi hivyo ujamaa ulikuwa na lengo la kuepuka uwepo wa matajiri wachache sana miongoni mwa maskini wengi sana.

Mwalimu hakuwa malaika lakini alijaliwa na Mungu maono makubwa, aliziona hizi hulka zilizokuja kuichafua haswa awamu ya nne na kuendelea. Kwamba angeruhusu uwepo wa matajiri miaka ile hao wachache wenye elimu wangewaumiza wengi wasio na watetezi.

Alikwepa misuguano ya kitabaka ambayo ingeweza kuzaliwa kwa kuruhusu wachache wawe na nguvu na wengi wakose mtetezi.

Alisambaza elimu ili iwe silaha ya mtoto wa mkulima kuweza kuitumia katika vita za kimaisha.

Anaweza kulaumiwa pia kwa kuleta ujamaa kwani huwa hauruhusu ubunifu wa mtu mmoja mmoja na unatengeneza wajinga wengi.
Hoja mfu, alichukia watu kuwa matajiri, alitaka wote wafanane vipato, alisema mtu alipelekwa jangwani akae peke yake hawezi kuwa tajiri,ila atakua tajiri kwa kunyonya wengine, yaani mimi na familia yangu tufanye kazi kwa bidii,tukuze kipato,tupate mtaji,tuajiri watu na kuongeza uzalishaji hivyo kipato kiongezeke,uite huo unyonyaji!?.. hakuwa na maono yoyote
 
Uhuru wa nchi teacher alitangulizwa mbele na kanisa katoriki hakuupambania yeye mwenyewe kama jeshi la mtu mmoja.

Hizo changamoto alizokutana nazo ndizo kiongozi anatakiwa kuzitatua, hakuna excuses.

Mazuri alikua nayo mabaya alikua nayo, lakini kiujumla nchi ilimshinda ndio maana akaamua kung'atuka.
Changamoto za Tanzania ya 1964 sio za hii ya 2024, tunamhukumu Mwalimu kwa akili za 2024 bila ya kujua kwa kina zipi haswa ni changamoto za wakati ule.
 
Hoja mfu, alichukia watu kuwa matajiri, alitaka wote wafanane vipato, alisema mtu alipelekwa jangwani akae peke yake hawezi kuwa tajiri,ila atakua tajiri kwa kunyonya wengine, yaani mimi na familia yangu tufanye kazi kwa bidii,tukuze kipato,tupate mtaji,tuajiri watu na kuongeza uzalishaji hivyo kipato kiongezeke,uite huo unyonyaji!?.. hakuwa na maono yoyote
Asingekuwa na maono leo hii tungekuwa sawa na Kenya katika lindi la vita na misuguano ya kijamii isiyokwisha.
 
Wanaomlaumu Nyerere bila ya kujua mengi ya wakati ule wengi ni vijana wadogo ambao wakati wa awamu yake walikuwa aidha hawajazaliwa au watoto chini ya miaka kumi, ambao bado hawajaanza kusikiliza taarifa za habari na kuelewa nini anachokisema mtangazaji..
Na wengine wamelishwa matango pori na wale waliokuwa wamebanwa na Mwalimu wakashindwa kufanya Ufisadi waliokuwa wakiutaka !
A.k.a wanyonyaji ! 😆😀
 
Changamoto za Tanzania ya 1964 sio za hii ya 2024, tunamhukumu Mwalimu kwa akili za 2024 bila ya kujua kwa kina zipi haswa ni changamoto za wakati ule.
Changamoto ni ujinga, umasikini na maradhi,lakini hakujenga shule hata moja,na chuo kikuu kimoja,Ili kudhibiti watu wasisome, wakati huohuo kukata watu mishahara kuchangia harakati za ukombozi kusini mwa africa
 
Izo hujuma hata mabeberu wenyewe kwa wenyewe wanafanyiana, na jukumu la kiongozi ni kuzi-outsmart izo hujuma.
Alifanya mengi sana mazuri na aliacha mengi sana mazuri ila walipokuja wasomi wazuri wakabomoa kila kitu na kuuza kwa bei chee kila kitu kilichokuwepo!
Kuanzia Viwanda mpaka mashirika ya Umma !
Kama huvijui Viwanda na Mashirika ya Umma yaliyokuwepo basi wewe utakuwa ni kijana uliyedanganywa na Wanyonyaji wa Mali za Umma !
 
Nyerere aliacha viwanda kila mkoa tena vile vikubwa.. MWATEX, MUTEX, General Tyre na vingine vingi tu, nani alikuja kuviua?.

Alijenga msingi wa kila mtu kwenda shuleni na kupata elimu tena bure kabisa, tunamlaumu Nyerere kwa kumuonea, kuna mengi ya kijinga yamefanyika baada ya mwaka 1985 akiwa ameshatoka ikulu.
Kabisa kabisa ! 🙏
 
Izo hujuma hata mabeberu wenyewe kwa wenyewe wanafanyiana, na jukumu la kiongozi ni kuzi-outsmart izo hujuma.
You are Right 🙌
Wajanja na wasomi wazuri waliofuata baada ya Mwalimu walifaulu sana juzi-outsmart hujuma za Wazungu kwa kuwaita hao hao Wazungu waje wachimbe Dhahabu kwa kutugawia asilimia 3 ya mapato ya dhahabu itakayouzwa. 🙄

Tukaviuza Viwanda vyote vilivyokuwepo kwa Ushauri na masharti ya IMF kwamba Serikali isifanye Biashara !
Kukaviuza Viwanda vyote kwa Bei ya Bure kabisa. 🙄

Kisha wakaja wajanja na wasomi Zaidi wakawa-outsmart tena Wakubwa kwa kuingia mikataba ya Uchimbaji wa Gesi ambayo Kiongozi mmoja akaja kutuambia kwamba pale tulishapigwa hatuna chetu 😳🙄🤦🏽‍♂️

Kweli tumefanikiwa sana Kuwa-outsmart Wakubwa wa Dunia 🙌🤦🏽‍♂️
 
Iko hivi nazani hata kesho ukiamka huwezi kumkoza mzee wa miaka 70,80 na kuendelea,au tafuta sehemu ya tukio husika lililowahi kutokea halafu waulize wahusika wa pale hasa wazee,utaupata ukweli no utafaidika kuliko kusoma vitabu vilivyoandikwa kwa kupotosha ukweli
Uko sahihi kabisa. Binafsi nawaheshimu mno wazee kwa sababu hiyo. Kuna mzee fulani mitaa ya Ilala alikuwepo siku ya sherehe za uhuru huwa ananisimulia mno mikasa iliyotokea. Tatizo wazee wengi huwa kuna mambo wanaishia kuguna na kuelezea juu juu.
 
Hayo mambo yalikuja baada ya vita ya Kagera (tulifunga mikanda). Kabla ya hapo us dollar ilikuwa shilingi tano. Na ndiyo ilikuwa nauli ya uda (da

Walitaka kupindua nchi live na kusababisha uasi kwa kufadhiliwa na hawa mnaowarudisha leo kuja kuchukua rasilimali alizokuwa amazitaifisha .

Hebu mkae mtafakari kuwa ingekuaje kama kila kitu kingebaki mikononi mwa Wazungu ,waarabu na wahindi?
Tungekua na uhuru gani ?
Yaani mpaka ikulu ilikua ni mali ya wazungu ,majaji wote walikua ni wazungu , Askari wote wenye vyeo walikua ni wazungu. Nyumba zote zinazomilikiwa leo na NHC zilikua za waarabu na Wahindi na wao ndio walikua wanafanya biashara kwenye nyumba zao katikati ya miji yote nchini . Maeneo yote ya Ofisi za wakuu wa Wilaya kama BOMAN ni maeneo ya Wazungu na neno la Waingereza . Mashamba yote ya Korosho,pamba, Mkonge, Korosho, Chai,Tumbaku, Zabibu, Maaple ,Minazi , Machungwa ,Misufi, Maembe , Shahiri, ngano, mahindi na maharage kule Arusha n. k yote yalikua ya wazungu . Waafrika hawakua hata na maeneo ya kujenga zaidi ya kuishi kota za wazungu na kuwa vibarua . Mapori yote yalikua ni mali ya serikali .
Tanganyika haikua na viwanda vingi wakati wa Mkoloni kwa sababu viwanda vingi vilikuwa Kenya na Zimbabwe . Tanganyika ilikua ni sehemu ya kuchota mali ghafi.

Mtume na Nabii Mtakatifu Julius Kambarage Nyerere Nabii wa Afrika na Mzalendo alitaifisha Mali zote na ardhi za Mashetani waliokuja kuwaua waafrika na kutwaa rasilimali zao walizoumbiwa na Mungu kwa ajili ya vizazi vyao wakiwemo Wamasai Waliofukuzwa na Waarabu koko toka Misri kwenye bara la Mtu mweusi . Na leo Waarabu wale wale wamewafata tena kule Loliondo kwa mgongo wa mjukuu wao mwarabu koko.

Nyerere akajenga viwanda vingi sana ili kutumia malighafi zetu wenyewe kuzalidha. Tulizalisha nguo na nyuzi kwa pamba zetu wenyewe . Tulikua na viwanda vya mafuta ya Karanga leo hata ukimwambia Abadili kuwa tulikua na mafuta ya Karanga ,tan band badala ya Blue band ya Kenya hajui ,anachojua ni kuagiza makontena ya mafuta kutoka Indonesia na China basi na kutangaza kuwa watanganyika hawawezi kuzalisha vitu vyao . Kanga za urafiki zilikua ni bora sana zikishindana na kanga za Kenya.

Kwa hali ilivyokuwa Chuki ya wale walionyanganywa mali zao ilikua ni kubwa sana kwa Nyerere. Na Ukumbukwe hakua ni Mwanajeshi bali Raia lakini Mzalendo kama Mwanajeshi ,Hali iliyopelekea kuwa na majaribio mengi ya kumpindua lakini kutokana na uzalendo wa Watanganyika waliokua wanampenda Rais wao majaribio yote yalishindikana. Hujuma za kiuchumi ziliendelea zaidi baada ya Kuanguka kwa Umoja wa Kisovieti. Nyerere akasoma alama za Nyakati za Mfumo wa Vyama vingi na jinsi nguvu ya Mataifa makubwa inavyotumika kutumia pesa kuleta vita na uasi kwenye nchi za Afrika kushinikiza vyama vingi. Nyerere hakutaka kuwa rais wa Nchi ya Kibepari mana yeye na chama chake hakuamini katika unyama wa mabeberu na dhulma za nchi za Kibepari. Akaamua kung'atuka madarakani.

Kilichofuata ni Wale wale waliokua wanatamani maisha ya anasa kuanza kujipanga kupitia Demokrasia ili wakamate na kuifanya mali yao wakiwemo vijana walipoenda siasa za kujilimbikizia mali kwa kukwapua mali za umma. Walijimilikisha mpaka nyumba ambazo hata Wakoloni hawakuzifanya mali binafsi. Waliuza mapaka nyumba za Polisi ,mahakama,TISS n.k. na kuzifanya mali zao na familia zao na marafiki zao.
Wakajiwekea sheria za mafao na mishahara mikubwa na marupurupu makubwa bila kujali hali ya uchumi wa nchi. Wakabadilisha utamaduni wetu wa kuitana Ndugu na kutunga sheria ya kuitwa Mheshimiwa. Wanajiona wao sio ndugu zetu bali waheshimiwa na kuanza kujiona kama wazungu weusi mbaya zaidi wakawa wabaya zaidi ya wakoloni chini ya mifumo kinyama ya Kibepari.

Tujiulize,
Tulikua watu milion 14 maji bure , umeme ni Mita madeni kibao.
Elimu bure vitabu vimejaa librari tunapewa mpaka madaftari na penseli.
Matibabu bure .
Wafanyabiashara wachache .
Simu madeni kibao.
posta madeni kibao.
Benki kubwa mja NBC .
Wafanyakazi kama walimu walikua na maisha mazuri na shule za serikali zilikua za bweni zikiwakutanisha wanafunzi kutoka kila sehemu alimradi awe amefaulu kwa ufaulu wa Juu.
Bado vita ya Uganda ikaibuka, vita za Nchi za kusini ambazo zilikua zinatokana na waafrika wenzetu kudai uhuru hivyo Tanganyika ikawa ndiyo mfadhili na msaada mkubwa kwao kijeshi.
Kama sio uzalendo Mwalimu angewezaje kujenga viwanda na mashirika ya umma zaidi ya 360 kwa mazingira kama hayo ?

Leo hii , Tuko mil.65 tozo kila mahali. Watalii kibao,mabilionea wa ndani kibao, Wafanyabiashara kibao.
Majengo yanayolipa kodi ya majengo na ardhi ni mengi nchi nzima.
Bandari inapitisha mizigo ya ndani na nje mara mia moja zaidi ya kipindi cha Mwalimu.
Wafanyakazi wanadhulumiwa pesa zao za pension kwa sababu tu ya ubinafsi wa Mabepari kuanzisha miradi ya kifisadi na wao kuwa mabilionea huku watumishi wakibaki kuwa fukara. Badala ya kuwapiga kitanzi wezi kwenye mifuko ya jamii ya wafanyakazi kama NSSF wanaopigiwa mabomu na risasi ni wale wanaodai mafao yao ambayo yamegeuzwa kuwa dili la watu kupiga pesa kwa kujenga majengo yasiyo na tija kwa wafanyakazi zaidi ya Watu wachache kupiga dili.
Wakaja watawala walimfuata Nyerere wakaungana na wapiga dili kujilimbikizia mali huku wakiwateua marafiki zao kusimamia mashirika ya umma kwa lengo la kupeana fadhila na sio kuendeleza mashirika . Bodi za mashirika za kumwaga lakini wamewekwa Makada na marafiki ili wachote pesa za kampeni kurudishana madarakani na kuendelea kutafuna nchi.

Wengine sasa wanakuja na marafiki zao wakijifanya ni wawekezaji kumba ni wao na kujimilikisha mpaka bandari na kila sehemu yenye kukusanya pesa tu. Hawataki kujenga viwanda bali kuanzisha makampuni ya kushika tenda za serikali kuchota pesa . Hawajengi kiwanda cha Sukari na Mbolea ,hapana wanataka kutengeneza vikampuni vya kuingiza sukari bila Kodi halafu wanauza kwa bei ya juu wapige pesa .

Hawa kamwe hawatamsifia Mwalimu zaidi ya kuwasifia wale waliowaruhusu na kuwawekea mazingira mazuri ya kuigeuza nchi kuwa shamba la wageni wao.

Wengine waliambiwa huyu Mzee akiendelea kuwa Hai wewe huwezi kuwa Rais kamwe .

Mwalimu akaondoka akiwa mzima kwenda check akarudi akiwa paradiso. Nini kilitokea bado hakijawekwa wazi kabisa kiuchunguzi na hakijachunguzwa.

R.I.P.Mwalimu JKN.
Shujaa wa nchi za Kusini Mwa Afrika na wengine leo wanapata fursa ya kupiga picha kwenye vikao vikubwa duniani kwa mgongo wako .
Shukrani ya Punda ni Mateke
Wewe umeandika stori za kusoma vitabuni ambazo ziliandikwa kwa ajili ya kuwapamba Viongozi,Tofautisha viwanda alivyofitaifisha Nyerere na viwanda alivyovijenga. Ninachojua mimi baada ya Azimio la Arusha selikali ilitaifisha vitu vingi Sana, kumbuka hivi viwanda,makampuni zilikuwa na management zake,baada ya kutaifisha ilibidi waweke manegement za selikali ambazo watu wake hawana uzoefu taratibu zikaanza kupungua ufanisi mpaka kufa kabisa mfano kiwanda cha kusindika Nyama Tanganyika Pekers,kilikuwa kinaajiri zaidi ya wafanyaka 2000 kabla ya kupata uhuru na kilikuwa kinauza nyama iliyosindikwa inje ya inchi na kuiingizia Tanganyika pesa za kigeni,leo hii ni uwanjwa wa maombi,hapo wa kulaumiwa siyo Nyerere

Chukulia mfano mdogo South Afrika ya makaburu ilikuwa bora zaidi kuliko ya sasa,Nelson mandera hakuwa mjinga hakuna alichotaifisha kutoka kwa wazungu,lakini Mugambe alijikuta inaharibu uchumi wa Zimbabwe baada ya kutaifisha mashamba ya walowezi, kiuharisi aliyoyafanya Nyerere hayana tofauti na aliyoyafanya Mugabe
 
Unajua sababu ya Nchi kutokukopesheka??
Kwanza Mwalimu alikataa madini yasichimbwe kama Serikali haitapata asilimia 50 ya mapato yatakayo patikana ! = Waliokuja wajanja baada yake wakaruhusu mikataba ikatiwa saini Serikali ikawa inapewa asilimia 3 % ya mapato yanayo patikana kwenye dhahabu 😱 !

Nchi ilishindwa kukopesheka kwa sababu Nchi ilikuwa na deni la Dollar billion 8 inasemekana !
Mabepari lengo lao ilikuwa wakubaliwe kuchimba madini kwa bei Chee waliyokuwa wanataka wao !
Na pia walilazimisha ili Nchi iweze kukopeshwa na IMF ni lazima Mwalimu akubali thamani ya pesa ya Tanzania ishushwe !

Yote hiyo ilikuwa ni kumkomoa Mwalimu kwa sababu ya kwanza kuzisaidia Nchi nyingi za kusini mwa Africa kudai na kisha kupata Uhuru wao,
Tulikuwa tukibadili dolla ya marekani kwa shs 5 za Tanganyika na baadaye za Tanzania !

Mwalimu alifanyiwa hujuma na Mabeberu kwa sababu ya misimamo yake ya kukataa kunyonywa Rasilmali za Nchi !!
Weka Hiyo Akilini Mkuu 🙏👍
Mkuu kila jambo lina wakati wake,Hadi leo tuna chuma tena kwa wingi lakini hatuna fedha na tekinologia ya kuchimba na kuchakata,vivyo hivyo,Helium gas,Gesi asilia,mkaa wa mawe,nickel,Tin,Dhahabu,almasi,Tanzanite hadi hata phosphate tupo tupo.Hatujielewi kama leo tunajengewa hata vyumba vya madarasa na maliwato jiulize kama ilikuwa sahihi kuomba uhuru 1961.
 
Maajabu yake ni kutembea nchi nzima miaka ile barabara zote ni vumbi tupu akitafuta uhuru wa Tanganyika, maajabu ni kuwa rais wa kwanza sawa na kina Sekou Toure, Jomo Kenyatta na waasisi wengi wa afrika.

Maajabu ni kujenga viwanda katika mikoa yote kwa lengo la kuinua uchumi, changamoto alizokutana nazo akiwa rais ni kubwa kwani miaka yake ilikuwa ni ya kujenga msingi wa kitaifa tofauti na marais waliyokuja baadae na kukuta misingi ipo tayari.
Nitajie viwanda vilivyojengwa na Nyerere
 
Wewe umeandika stori za kusoma vitabuni ambazo ziliandikwa kwa ajili ya kuwapamba Viongozi,Tofautisha viwanda alivyofitaifisha Nyerere na viwanda alivyovijenga. Ninachojua mimi baada ya Azimio la Arusha selikali ilitaifisha vitu vingi Sana, kumbuka hivi viwanda,makampuni zilikuwa na management zake,baada ya kutaifisha ilibidi waweke manegement za selikali ambazo watu wake hawana uzoefu taratibu zikaanza kupungua ufanisi mpaka kufa kabisa mfano kiwanda cha kusindika Nyama Tanganyika Pekers,kilikuwa kinaajiri zaidi ya wafanyaka 2000 kabla ya kupata uhuru na kilikuwa kinauza nyama iliyosindikwa inje ya inchi na kuiingizia Tanganyika pesa za kigeni,leo hii ni uwanjwa wa maombi,hapo wa kulaumiwa siyo Nyerere

Chukulia mfano mdogo South Afrika ya makaburu ilikuwa bora zaidi kuliko ya sasa,Nelson mandera hakuwa mjinga hakuna alichotaifisha kutoka kwa wazungu,lakini Mugambe alijikuta inaharibu uchumi wa Zimbabwe baada ya kutaifisha mashamba ya walowezi, kiuharisi aliyoyafanya Nyerere hayana tofauti na aliyoyafanya Mugabe
Una ujinga mwingi bwana mdogo.
 
Back
Top Bottom