Nauliza swali NEC na Polisi kuhusu utekwaji wa wagombea wa upinzani katika chaguzi

Nyerere aliwahi kusema Kaburu ni kaburu tu hata kama ni mweusi🤣
 
Kama kuna taasisi inayosimamiwa kisheria nchi hii ni Tume ya uchaguzi yani kila hatua ipo inafanyaika kisheria na kwa uwazi hayo ya kutekwa sijawahi ona uthibitisho wenye mashiko zaidi ya siasa nyepesi za waliokosa. ninachofahamu mimi ni kwamba kila baada ya uchaguzi huwa kuna kesi za uchaguzi na hata uchaguzi uliopita nilisikia Nec wakisema juu ya kesi za uchaguzi na kama tukirejea kesi kama hizi huwa tunasikia madiwani na hata wabunge wakati mwingine mahakama zinatengua ubunge au udiwani wao.
 
Wewe ni aidha mnufaika wa ccm au uko nec au nje ya nchi maana mara zote kila uchaguzi WAGOMBEA wa UPINZANI huwa wanatekwa on the way kurudisha fomu wakati mwingine wanashambuliwa au ofisi za nec wilayani halmshauri zinaondoa watumishi pale wanapojua mgombea wa UPINZANI anarudisha fomu lakini je umesahau kifo cha akwilina kilitokeaje?
 
Nadhani hayo mambo yapo kisheria zaidi na kama kuna mtu alitekwa ilipaswa aripotiwe kwenye mamlaka husika ambapo ni polisi ili waweze kutimiza majukumu yao kulingana na mashtaka hayo,kwahiyo hapo sijaona ni kwa namna gani NEC inahusika moja kwa moja na kwa jinsi navyofahamu kuna kesi za uchaguzi zilikuwa zinashughulikiwa baada ya uchaguzi wa 2020 kumalizika na mojawapo ya kesi ni ile ya udiwani ambapo ilipelekea kuenguliwa kwa diwani wa kata ya Kagerankanda iliyopo wilaya ya Kasuru(Kigoma).So kwa maoni yangu hapo sijaona kosa kwa NEC, naomba kuwasirisha kwa mtoa mada[emoji120]
 
Nadhani hapo NEC imetajwa tu kufurahisha genge maana haipiti siku watu wakaacha kuitaja.

Mgombea kama anatekwa akiwa ndani ya Ofisi za NEC wanaweza kujibu lakini kama wagombea au vyama vinafanyiana uhuni huko mtaani na hawatoi taarifa Polisi hilo ni suala lingine.

Ila Wagombea nao wanaendekeza njaa, wapo ambao wanarubuniwa na kupewa hela mwisho wa siku hawarudishi fomu na kudai wametekwa. Maana muda wa kurejesha fomu ukipita tu utawaona ndio wanaonekana.
 
Lumumba fc una shida sana. Nyie ndio mnaodai ccm ilishinda🤣🤣🤣
 

..hoja yako ingekuwa na mashiko kama tungekuwa na jeshi la polisi linalotenda haki sawa kwa vyama vyote.

..tumefika mahali jeshi la polisi limekuwa sehemu ya Ccm hivyo sio mahali sahihi kwa mpinzani kupeleka malalamiko yake.
 
..hoja yako ingekuwa na mashiko kama tungekuwa na jeshi la polisi linalotenda haki sawa kwa vyama vyote.

..tumefika mahali jeshi la polisi limekuwa sehemu ya Ccm hivyo sio mahali sahihi kwa mpinzani kupeleka malalamiko yake.
Hiyo jamaa hamna kitu
 
Kwahiyo wanarubuniwa na kutekws mbele ya polisi?
Nyie ndio Mama Samia anawaita mna akili ndogo
 
Mimi Niko zangu kitaa napambana kivyangu usinihusishe na hayo mambo lakini tunasema ukweli wa mambo yalivyo katika uhalisia wake sio kila Uzi mkiuleta hapa tushadadie bila kufikiria
 
Mimi Niko zangu kitaa napambana kivyangu usinihusishe na hayo mambo lakini tunasema ukweli wa mambo yalivyo katika uhalisia wake sio kila Uzi mkiuleta hapa tushadadie bila kufikiria
Huna ukweli wowote hapo lumumba fc team roho mbaya tu. Watu wanabambikiwa makesi na DPP kasema waachiwe wewe ni nani unapinga? Mkurugenzi Takukuru alisema kuna kesi 247 za wapinzani za kugushi akazifuta kwa maelekezo ya Mama Samia.

Nyie team roho mbaya sijui mkoje.Ndio kusema hamuoni?
 
Mimi Niko zangu kitaa napambana kivyangu usinihusishe na hayo mambo lakini tunasema ukweli wa mambo yalivyo katika uhalisia wake sio kila Uzi mkiuleta hapa tushadadie bila kufikiria

..Tangu mfumo wa vyama vingi urudishwe mwaka 1992 hakuna mgombea wa Ccm aliyeenguliwa na Tume ya Uchaguzi.

..Wapinzani peke yao ndio wamekuwa wakienguliwa, na ktk uchaguzi wa 2020, Tume ilivunja rekodi kwa kuengua wapinzani wengi kuliko wakati wote.
 
Wamejifunza Urusi hayo mambo
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kutekana na Tume wapi na wapi jamani pengine wagombea wenyewe wanahujumiana maana siasa ni mchezo mchafu wanafanya mambo ya hovyo halafu mtu anadhani ni Tume sidhani kama ni sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…