Naumaliza mwaka Kwa machungu ya kuachana na mwanaume wangu niliyempenda sana

Naumaliza mwaka Kwa machungu ya kuachana na mwanaume wangu niliyempenda sana

Kuna kitu kagundua kuhusu wew!!
1. Either kapewa maneno na rafik yako wa karibu kuhusu michepuko yako!!
2. Au kakutana na mwanaume wako wa zamani akawa anasimulia Jinsi unavyokuwa kitandani then unampa mpka sehem jamaa ananyimwaga.
3. Anakupenda sana ila ameamua akae pembeni akuache kidogo labda umekuwa una mwonyesha dharau hadharani kwamba wew una pesa kuzidi yeye au mzuri saaana. Hata alipokuja kujitambulisha kwenu Kuna vitu aliambiwa ama alisikia wazazi wanaongea kuhusu yeye havikumpendeza!!!
Trust me hizo reason inabid uzichunguze!!! inatokea na imeshatutokea pia. Be strong tafuta Tatizo ni Nini? Otherwise ndo bye bye
Mkuu pamoja Na yote sijawahi muonesha dharau
Labda aliona unalazimisha sana ndoa na yeye hayupo tayarii so akaona bora akupotezee kimya kimyaa kuliko kuendelea kuumiza kichwa mtu ambae huelewii na huna subra.
Ndoa alitaka mwenyewe rick
 
Ubalikiwe sana mtumish wa BWANA.

MUNGU ni MWAMINIFU SANA
Nakuombea uushinde hii changamoto iliyoko mbele yako, ningepata namba yako ya cm ingekuwa vizuri lakin nitajaribu kukuelezea hata kwa kuandika tu

Ukisoma kitabu cha kwanza cha nabii samweli sura ya tatu utaona kwamba MWENYEZI MUNGU aliinuka akamwita nabii samweli kuanzia mara moja hadi mara tatu, lakin nyakati zote hizo tatu ambazo MWENYEZI MUNGU alimwita samweli badala ya samweli amwitikie MUNGU na amwendee MUNGU yeye nyakati zote hizo alimwendea kuhani El

Mpaka kuhani El akajiongoze akamwambia samweli sikuiiti mimi bali huenda unaitwa na MWENYEZI MUNGU kalale tena ukiitwa mwitikie MUNGU na mwendee MUNGU

Sasa hapa nataka nizungumze kitu mtumish Kuna kitu kinaitwa macho ya KIROHO au macho ya ROHO au macho ya ROHONI, HAKUNA KITU KIBAYA KAMA KUKOSA MACHO YA ROHO UTATESEKA SANA

tunamuona samweli akiseka hajui amwendee nani kati ya MUNGU na kuhani El, badala ya amwendee MUNGU yeye anamwendea kuhani El mpaka MWENYEZI MUNGU mwenyewe anayahamisha macho ya ROHO kutoka kwa samweli anayapeleka kwa kuhani El, kuhani anagundua kwamba kwa macho ya ROHO huyo kijana samweli anaitwa na MUNGU

Narudia tena MWENYEZI MUNGU anayahamisha macho ya ROHO kutoka kwa samweli anayapeleka kwa kuhani El, kuhani El anagundua kwamba kwa macho ya ROHO kwamba huyo kijana anaitwa na MUNGU

Sasa ndo wewe sasa MWENYEZI MUNGU amekuita katika wito wa ndoa sasa wewe ulichokosea umekosa macho ya ROHO au macho ya ROHONI badala utafute MUME wewe umeenda kutafuta mtu tu ili mradi mwanaume kwa sababu ni mwanaume, kwahiyo MWENYEZI MUNGU alichoamua kukifanya kwako ni kuyahamisha macho ya ROHO au macho ya ROHONI na kuyapeleka kwa huyo mnyakusa

Ndipo huyo mnyakusa akatambua kwamba kumbe wewe maria unahitaji ndoa na yeye hahitaji ndoa kama kuhani El alivyotambua kuwa samweli anaitwa na MUNGU na yeye kuhani El hamuiti samweli ndipo kuhani akamwambia nenda unaitwa na MUNGU wala Mimi sikuiiti

Sasa basi huyo kijana wako mnyakusa baada ya kupata hayo macho ya ROHO kaamua akae kimiya kwa maana yeye huenda siyo muoaji ndo maana kakaa pemben

Sasa wewe badala ushukuru kwa MUNGU unataka kujiua tena why unataka kuzihuzunisha mbingu,

MAISHA YA NDOA NI KITU ENDELEVU SANA USIFE MOYO WALA USIILAUMU MIPANGO YA MUNGU
JIKUBALI MTUMISH USIJE KUHALIBIKIWA

Asante

Kama ungenipm nikapata namba yako tungeongea vizuri binti wa MUNGU

BWANA na amani yake awe pamoja na wewe
Amina ahsante Ila tulikua tunaombea mahusiano Na sadaka tunatoa Na tayar Alianza kuchukua hatua za ndoa Kwa kuwaataarifu wazaz wake ili watume wazee nyumbani Kwa utambulisho
 
Hello wakuu,

Nimeona nishare sababu niko katika hali mbaya. Mawazo mabaya ya kujidhuru yananijia kichwani. Sijawahi kupenda kama nilivyompenda yeye. Kila kitu kilikuwa vizuri, ghafla akakata mawasiliano. Wiki 3 sasa nikimpigia hapokei, sms hajibu.

Nimehangaika, nikaongea na dada na kaka yake lakini bado alinikalia kimya. Mara ya mwisho kuwasiliana naye tulizungumza vizuri tu. Mipango yetu ilikuwa tufunge ndoa na alipanga mwezi huu aje nyumbani kujitambulisha. Lakini ghafla kimya chake kikatokea.

Baada ya kimya kirefu, siku 5 zilizopita nikamtumia sms ya kuachana lakini hakunijibu kitu. Naumia sana. Sijawahi kumkosea chochote ila ameamua kunifanyia ukatili huu. Naumia na najiuliza maswali ambayo sipati majibu.
Yaliyonikuta mimi nitakuja kusimulia maana kila mtu wa karibu niliyemshirikisha ali kiri jambo langu ni kubwa na gumu!!
 
Mungu akawe faraja yako katika kipindi hiki kigumu unachopitia lakini fahamu kuwa yote hayo yatapita ni swala la muda wanasemaga "time is the best healer" pia tafta wimbo unaitwa faraja by abakurikiye yesu naamini utafarijika
Amina ahsante
 
Mmmhh ila bongo mtu hujafunga naye aina yoyote ya ndoa unamuita mume wako!!!
Sasa kaenda kwa mke halisi kaa kwa kutulia utasikia tarehe ya ndoa.
 
Back
Top Bottom