Naungana na Shigongo Mawaziri na Watumishi wote wa serikali watoto wao wasome shule za serikali

Naungana na Shigongo Mawaziri na Watumishi wote wa serikali watoto wao wasome shule za serikali

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo amesema huko tunapoenda tuweke utaratibu kuwa mtu akichaguliwa kuwa waziri, mtoto wake asome shule za serikali. Amesema hii itasaidia kufanya mawaziri wasimame mitaala na kuunda sera zenye maslahi mapana kwa taifa

Amesema hayo akijadili bajeti ya elimu iliyowasilishwa bungeni na waziri wa Elimu, prof Adolf Mkenda, ambapo ameshauri mitaala isisitize elimu kwa vitendo na sio nadharia pekee, pia lugha ya kufundishia isiwe na mkanganyiko ambapo ameshauri kama ni kiswahili kifundishwe kuanzia la kwanza hadi la tatu. Kuanzia la tano mtoto atumie kiingereza ili asipate shida anapoingia sekondari kama ilivyo hivi sasa kwa wanafunzi waliosoma shule za serikali na waliosoma shule binafsi.
 
Pesa inaongea we watu 19 wanalipwa Billion 8 unafikiri mchezo
 
Kwanini lazima iwe hivyo? Kila mtu ampeleke mtoto wake anapoweza/anapotaka. Kufanya kazi serikalini sio kosa la kuchaguliana namna ya kutumia hela zako
 
Kwanini lazima iwe hivyo? Kila mtu ampeleke mtoto wake anapoweza/qnapotaka. Kufanya kazi serikalini sio kosa la kuchaguliana namna ya kutumia hela zako
Lengo ni kuhakikisha shule za serikali zinapata huduma na elimu bora. Kinyume na hapo shule za serikali zitaendelea kuwa sehemu ya kwenda kuvutia uzee.
 
Badala atafute namna ya kuzisaidia hizo shule, yeye anatafuta namna ya kuwashusha wengine ili walingane na kiwango cha chini, sijui ni wivu au ujinga tuu
 
Yeye mbona wake wako english medium 😂😂😂

Aanze yeye
 
Kusoma shule ya serikali ni adhabu?! Nashukuru kwa kujua leo, acha watoto wa masikini waendelee na adhabu.

Itakuwa ni kumlazimisha... Sio sahihi. Kila mtu ana uhuru wa kumsomesha mtoto wake anapotaka yeye.
 
Back
Top Bottom