Nauza bajaj niliyoichukua kwa mkopo, atakayeitaka atatakiwa kurudisha rejesho

Nauza bajaj niliyoichukua kwa mkopo, atakayeitaka atatakiwa kurudisha rejesho

Nimesoma maelezo yako. Ila situation ya jamaa ngumu. Apige kazi ili arejeshe mkopo kila wiki, hapo bado hajaweka fedha ya matumizi (ukute ana familia pia), pia gharama za uendeshaji bila kusahau siku mbaya kibiashara. Hii biashara inaweza kuwa reasonable kama angenunua cash na awe anafanya biashara mwenyewe. Katika vitu vingi vinavyofanya biashara nyingi za Bongo zife ni uaminifu wa wafanyakazi!
Ni kweli.

Kwa sisi tunaofanya mikataba mitaani huwa hesabu inakuja kila siku kumi akiongeza hapo zake mbili ila hizo za kampun huwa wanataka instantly kama wiki wiki siku kumi ni siku kumi hawataki maelezo hapa ndipo mkataba unapomuwia ugumu.

Angepewa fursa ya kusogea siku mbili mbele angeweza akatoboa.
 
Ni hatari sana; hizi hesabu ni ngumu
Rejesho kwa wiki 139,400 kwa muda miezi 24

Kimahesabu: 139,400 X 4 = 557,600/- kwa mwezi

557,600 x 12 = 6,691,200/- kwa mwaka

6,691,200 x 2 = 13,382,400/- kwa miaka miwili

Ili urudishe huu mkopo wa namna hii unahitaji ''discipline'' ya hali ya juu.
Hii si bei ya noah mpya kabisa kwenye karatasi ..!?
 
Nilikopa bajaj TVS KING TUKTUK mpya kwa kampuni flani ila nilitanguliza Tsh 1m kama dhamana, imetembea km 300 tu na ina bima ndogo, ina fire extinguisher, Latra na triangle zake ikiipata ni road tu.

Rejesho ni 139,400 kwa wiki nimesharejesha mwezi kama na kitu. Kwa anaehitaji hii bajaj na deni lake ili akimaliza deni iwe yake aje pm mi nahitaji laki 8 tu kati ya milioni niliyotanguliza,kisha namkabidhi.

Karibuni na picha hizi hapa;

Ukimaliza miaka 2 bajaji itakuwa umeilipia 14,497,600 (milioni kumi na nne laki nne, elfu tisiini na saba na mia sita)

139,400 kwa wiki zidisha wiki 52 kwa mwaka zidisha miaka 2.

Nadhani sasa umeshagundua kuwa jamaa wamekuingiza cha kike kiasi fulani.
 
Ni hatari sana; hizi hesabu ni ngumu
Rejesho kwa wiki 139,400 kwa muda miezi 24

Kimahesabu: 139,400 X 4 = 557,600/- kwa mwezi

557,600 x 12 = 6,691,200/- kwa mwaka

6,691,200 x 2 = 13,382,400/- kwa miaka miwili

Ili urudishe huu mkopo wa namna hii unahitaji ''discipline'' ya hali ya juu.
Mkuu umempunguzia deni, kwa wile analipa kwa wiki, kwenye mwaka mmoja kuna wiki 52x139400x2 = 14,497,600/=
 
Unashangaa dereva Bajaj kuingiza Tsh 30,000/= per day?hiyo hela hata bodaboda wanaofanya kazi yao kwa umakini ni ndogo wao kwa siku wanafunga siyo chini ya 50K kinachowaangusha ni wanawake hakuna cha zaidi.

As for me,huo mkataba ni rahisi tena rahisi sana changamoto anazipata jamaa kutokana na hakukaa akapiga hesabu zake vizuri wapi itafanya kazi au dereva siyo muaminifu etc,Bajaj wanapata hela kwa siku kulaza 60K chuma ikiwa full tank na hesabu ya boss ameshatoa ni ishu ndogo sana,75% rout zangu nazozunguka town natumia usafiri huu so nimekuwa nauliza uliza sana kwa madereva na ndicho wanachoniambia.

Mimi nafanya hii biashara,nimeianza 2020 kipindi kile kwa siku ilikuwa 20,000/= mkataba miaka miwili mwaka jana mwishoni nikapandisha 25,000/= sasa piga hesabu hapo inakuwa bei gani na hela wanaleta,Bajaj hasa hizi TVs ni chombo kimoja imara sana mtu akifanikiwa kumaliza mkataba ana miaka nane mbele hata zaidi kukimiliki kikimuingizia hela na service yake kwa siku 18 haizidi 27K.

Engine yake kwa mtunzaji mzuri kuanza kumsumbua ni kuanzia miaka sita so mara nyingi faida wanaipata zaidi madereva ila wale wanaojitambua.
Muache wizi hiyo kazi naifahamu atakama dereva anafanya kazi za kusomba mizigo ya wamama sokoni hiyo pesa ni ngumu kupata
 
Hizo za benk bahati mbaya unakuta siyo wengi wanaojua ndiyo maana kama hivi mtu anajipiga pin.

Nilipo-bold,umesema kweli hata mimi dereva wa kwanza nilieanza nae alinichanganya kiasi nikaona hii siyo kazi,kwanza simu hapokei akipokea anakwambia yupo garage chombo kimesumbua (ina miezi minne tu Bajaj mpya) niki-check GPRS inaniambia inatembea eneo fulani,nilivunja mkataba na hela yangu 500K akabaki nayo.
Aise pole sana ndio madereva walivyo wengi sio waaminifu wengine wanachinja vifaa wanauza na kama ndio mgeni kwenye biashara ndio wanakuchezea michezo michafu. Wengine wanaweka bond kisa makamari hasa vijana usumbufu unakua ni mwingi.
 
Muache wizi hiyo kazi naifahamu atakama dereva anafanya kazi za kusomba mizigo ya wamama sokoni hiyo pesa ni ngumu kupata
Hahah mkuu mbona umefika mbali kiasi hiki?

Hakuna wizi hiyo kazi ni kazi kama zilivyo kazi nyengine unaajiriwa unamuingizia mwenye kampuni mill 30 kwa mwezi ikifika mwisho wa mwezi anakupa chako 1 mill kama mshahara unabaki unakenua meno na hakuna siku atakurithisha kampuni tofauti na huku unaumia ndani ya muda fulani baada ya hapo unapata maisha,wapo wasomi wameweka vyeti makabatini wanaifanya wanajutia kwanini walikuwa wanajidhalilisha kuzunguka na bahasha za khaki kutafuta kazi za ”ndiyo boss ndiyo boss".

Kila kazi ina principle na codes zake muhimu kuzizingatia hawa Bajaj&bodaboda drives wanapata sana hela tatizo lao sketi haziwapiti mbali.
 
Ni hatari sana; hizi hesabu ni ngumu
Rejesho kwa wiki 139,400 kwa muda miezi 24

Kimahesabu: 139,400 X 4 = 557,600/- kwa mwezi

557,600 x 12 = 6,691,200/- kwa mwaka

6,691,200 x 2 = 13,382,400/- kwa miaka miwili

Ili urudishe huu mkopo wa namna hii unahitaji ''discipline'' ya hali ya juu.
Hapo bado hujaweka 2M (1M aliyoanza nayo Kama cash, 1M nyingine ni ile aliyoifanyia rejesho) Kama nimemuelewa sawa. Jumla ni Kama 14M+ hivi.
Hawa jamaa ni zaidi ya wanyonyaji isee.

Sent from my Nokia 1.4 using JamiiForums mobile app
 
Rejea post ya mtoa uzi Kuna 1m amesha toa tayari je atarejeshewa akishamaliza mkopo?
Pia kumbuka rejesho ni kwa wiki si kwa mwezi. Hivyo miezi 24 ni sawa na majuma 52 x 2.
Kwa hivyo hesabu hesabu sahihi ni:
Tsh 139400 (rejesho la kila juma) x 104 (majuma ktk miezi 24) + TSh1,000,000 (downpayment) = Tsh 15,497,600. Pesa inatosha kununulia IST kabisa.

Waswahili wanaita kausha damu.
 
Ni hatari sana; hizi hesabu ni ngumu
Rejesho kwa wiki 139,400 kwa muda miezi 24

Kimahesabu: 139,400 X 4 = 557,600/- kwa mwezi

557,600 x 12 = 6,691,200/- kwa mwaka

6,691,200 x 2 = 13,382,400/- kwa miaka miwili

Ili urudishe huu mkopo wa namna hii unahitaji ''discipline'' ya hali ya juu.
Umekosea kidogo, mwaka una wiki 52 (365/7) kwa wiki 104 jumla inakuja kama 14.5m hivi, mwezi wa wiki 4 kamili ni february tu. Mingine inazidi wiki 4....
 
Hapo bado hujaweka 2M (1M aliyoanza nayo Kama cash, 1M nyingine ni ile aliyoifanyia rejesho) Kama nimemuelewa sawa. Jumla ni Kama 14M+ hivi.
Hawa jamaa ni zaidi ya wanyonyaji isee.

Sent from my Nokia 1.4 using JamiiForums mobile app
Hatari sana... lakini kuna dereva bajaji hapo katoa experience yake mbona kama mambo ni possible kabisa mkuu sema tu utakuwa umenyonywaa parefu na kesho haitabirikii kabisa.
 
Hatari sana... lakini kuna dereva bajaji hapo katoa experience yake mbona kama mambo ni possible kabisa mkuu sema tu utakuwa umenyonywaa parefu na kesho haitabirikii kabisa.
Ila Bajaj zimekuwa nyingi Sana hasa kwenye miji mikubwa kiasi kwamba wameanza kukataa kutoa usajili. Mfano mzuri ni Mbeya.
Japo anaweza kutoboa Ila ni kwa jasho na damu.

Sent from my Nokia 1.4 using JamiiForums mobile app
 
Ni hatari sana; hizi hesabu ni ngumu
Rejesho kwa wiki 139,400 kwa muda miezi 24

Kimahesabu: 139,400 X 4 = 557,600/- kwa mwezi

557,600 x 12 = 6,691,200/- kwa mwaka

6,691,200 x 2 = 13,382,400/- kwa miaka miwili

Ili urudishe huu mkopo wa namna hii unahitaji ''discipline'' ya hali ya juu.
Mikopo yote ya bajaji Ni hivi..Tena wengine unarudisha Hadi milioni 14
 
Back
Top Bottom