Nawakubali sana Waislamu kwenye kuzika, nawaza niweke kwenye wosia wangu nikifa nizikwe isizidi masaa 24

Nawakubali sana Waislamu kwenye kuzika, nawaza niweke kwenye wosia wangu nikifa nizikwe isizidi masaa 24

Matayarisho ya kuzika ni yepi..!? Ok! Sawa! vipi kama hayo matayrisho yatakamilika ndani ya saa moja ama mbili!? 😊
Mtu akifa hakuna haja ya kumzika harakaharaka bila sababu za msingi ndio maana kuna dawa za kuzuwia maiti kuoza na mochwari zipo ili kusubiri matayarisho ya kuzika yakamilike
 
Nyinyi wakristo mnaamini yesu alikufa na kuzikwa ! Swali ni je , Yesu alivyokufa kulingana na imani yenu
( sisi waislamu hatiamini kuwa Nabii Isa mwana wa Maryamu alikufa bali tunaamini alipaishwa kwenda mbingu bila kuonja mauti na atarudi duniani kabla ya Kiyama na atamuua dajjaali) YESU ALIZIKWA BAADA YA SIKU NGAPI ?!
Nabii Isa atarudi tena duniani?
 
Watu huwa wanazikwa wakiwa hai. Nina ushahidi kule kwetu Kuna mtu alizima masaa zaidi ya 7 ila ilibidi wazike kesho yake lakini jamaa aliamka na Hali Leo mzima. Sasa tungezika haraka si tungekuwa tumeua sisi??

Angalau marehemu akae hata masaa 10+ ndo azikwe Kuna faida yake pia
Umesema alizima...ukimaanisha HAKUFA🙂 hiko kijiji chenu cha ajabu sana kwamba kilitaka kuzika mtu aliezimia, kwa maana hakuna hata mtu mmoja anaejua MTU ALIYEKUFA!? 🤣
 
Nabii Isa atarudi tena duniani?
Naam! Hadithi sahihi zimethibitisha kuwa Nabii Isa atarudi duniani na atashukia maeneo ya Siria.
Kati ya mambo atakayoyafanya baada ya kurudi duniani ataua nguruwe,atavunja misalaba na atamuua kiumbe muongo , muovu na npotoshaji mkubwa atakayekuwepo kipindi hicho anayeitwa Masiyhi Dajjaali.
 
Katika uislamu ni dhambi kubwa kumchoma maiti hata angekuwa maiti huyo siyo mwislamu.
Katika hadithi mtume anasema kuvunja mfupa wa maiti ni sawa na kuvunja mfupa wa mtu ambaye hajafa.
Na kuhusu kuzika Allaah amesema kuhusu ardhi.
"{ ۞مِنۡهَا خَلَقۡنَٰكُمۡ وَفِيهَا نُعِيدُكُمۡ وَمِنۡهَا نُخۡرِجُكُمۡ تَارَةً أُخۡرَىٰ }
[Surah Ṭā-Hā: 55]

Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine
( tutakufufueni siku ya qiyaama)"

Na nasikia wachungaji wakati wa mazishi huwa wanamwambia maiti.
" Ulitoka kwenye mavumbi na sasa unarudi katika mavumbi................."
Imani za kuchoma maiti ni Imani za kipagani japo nasikia kuna askofu huko Afrika kusini aliusia akifa achomwe moto na kweli alivyokufa wakamchoma! Hata hapo Kenya kuna mwanasiasa mkongwe alikuwa ni jaji wakati wa serikali ya mkoloni akausia akifa achomwe na alipokufa alichomwa kama miaka miwili au mmoja na nusu iliyopita.
Japo wahindi mabaniani Bado wanachomana kwa moto wa kuni siku hizi kuna mashine maalumu za kuchoma maiti kwa moto wa umeme na kuacha majivu matupu!.
Mimi siyo mwislamu hivyo haya maelezo na hiki Kiarabu hakinisaidii. Nahitaji maelezo katika Ukristo kama kumchoma maiti ni tatizo. Asante ndugu yangu 🙏🏿
 
Mimi siyo mwislamu hivyo haya maelezo na hiki Kiarabu hakinisaidii. Nahitaji maelezo katika Ukristo kama kumchoma maiti ni tatizo. Asante ndugu yangu 🙏🏿
Hujasikia wachungaji wa kikristo wakisema kuwa mtu aliyetoka kwenye mavumbi atarudi kwenye mavumbi?!
Isitoshe kama upo siriasi kweli unataka kujua kama dini ya kikristo inaruhusu kuchoma maiti badala ya kuzika kwenye udongo unapaswa kumuona kiongozi wako wa kanisa unapofanya ibada umuulize na yeye atakupa majibu rasmi yanayoendana na dini na dhehebu lako , ama hapa jamii forums kila mtu atakupa majibu kulingana na uelewa wake na kulingana na misingi ya dini na dhehebu unalolifuata!
 
Hujasikia wachungaji wa kikristo wakisema kuwa mtu aliyetoka kwenye mavumbi atarudi kwenye mavumbi?!
Isitoshe kama upo siriasi kweli unataka kujua kama dini ya kikristo inaruhusu kuchoma maiti badala ya kuzika kwenye udongo unapaswa kumuona kiongozi wako wa kanisa unapofanya ibada umuulize na yeye atakupa majibu rasmi yanayoendana na dini na dhehebu lako , ama hapa jamii forums kila mtu atakupa majibu kulingana na uelewa wake na kulingana na misingi ya dini na dhehebu unalolifuata!
Mtu anaweza asiende mbinguni kisa tu alichomwa moto badala ya kuzikwa? Hili ndilo swali langu kuu. Nitawaona wanazuoni wanaohusika mkuu. Asante.
 
Mtu anaweza asiende mbinguni kisa tu alichomwa moto badala ya kuzikwa? Hili ndilo swali langu kuu. Nitawaona wanazuoni wanaohusika mkuu. Asante.
Haswaa! Kuwaona wataalamu husika ni jambo la muhimu ili kupata muongozo sahihi kulingana na dini yako.
Japo binafsi kwa umri wa 48 yrs nilioishi duniani na kukaa na jamii zenye Imani tafauti tafauti nahisi siyo rahisi kuambiwa inafaakuchomwa.
Kwa mfano yapasa kujiuliza je askofu,padri, paroko au mchungaji atakuja kufanya maombi ya kiroho kwa ajili ya maiti inayoenda kuchomwa?! Nakumbuka wakati wa msiba wa Edward Lowasa ambaye alikuwa chifu wa wamasai kuna vitu wamasai walishindwa kuvifanya ( ikiwa pamoja na kumzika Lowasa ndani ya ngozi ya ng'ombe) kwa kuheshimu Imani yake ya kikristo.
 
Tatizo kuna watu wanadhani kumzungusha maiti mikoani au kumvundika ndio vyema zaidi
Ila kuna wengine wanasema tunazika haraka labda bado ana uhai
Hivi hata mende akiwa kafa utashindwa kujua kama ana uhai au hana?

Binadamu mbwembwe nyingi na mwisho wa siku unazika tu
Kweli kabisa mzee wangu, asilimia 99 huwa daktari anathibitisha kuwa mtu ameshafariki suala la kuiweka maiti ni kuidhalilisha, maana mtu anaanza kutoa harufu au anabadilika rangi kama alipata ajali au alikuwa na vidonda vinaanza kuwa mtihani, kibaya zaidi wafiwa wanahuzunika sana wakijua ndugu yao amekufa na yupo somewhere.

Yote hayo ya nini? zika mtu akakutane na alichokichuma kwenye umri wake, unamuweka mtu wiki mbili ratiba ndefu bajeti kubwa, msiba ukiisha madeni kibao, ya nini?.
 
Mwendo wa haraka ndo mpango
Na siku hizi wasafirishaji wa maiti wanapata ajali sana, sisi tuko barabarani kila siku tunakutana na mengi unakuta maiti inapiga mzinga tena inarushwa nje ya jeneza na ndugu wawili watatu wanafuata, sasa haijulikani maiti ilikuwa ipi maana wameshatriple.

Mtu amekufa aheshimiwe aogeshwe vizuri, avalishwe sanda atiwe pamba maskioni na matundu yote afukiwe hiyo ni hatua katika maisha yetu hakuna namna.
 
Mtu anaweza asiende mbinguni kisa tu alichomwa moto badala ya kuzikwa? Hili ndilo swali langu kuu. Nitawaona wanazuoni wanaohusika mkuu. Asante.
Hatujawekewa taratibu za kujichoma moto baada ya kufa kwetu, utaratibu uliowekwa ni kurudishwa kwenye udongo ambayo ndio main content yetu, ukijichoma ukifika huko unarudishwa upya hapo utaeleza kwa urefu ilikuwaje.
 
Kweli kabisa mzee wangu, asilimia 99 huwa daktari anathibitisha kuwa mtu ameshafariki suala la kuiweka maiti ni kuidhalilisha, maana mtu anaanza kutoa harufu au anabadilika rangi kama alipata ajali au alikuwa na vidonda vinaanza kuwa mtihani, kibaya zaidi wafiwa wanahuzunika sana wakijua ndugu yao amekufa na yupo somewhere.

Yote hayo ya nini? zika mtu akakutane na alichokichuma kwenye umri wake, unamuweka mtu wiki mbili ratiba ndefu bajeti kubwa, msiba ukiisha madeni kibao, ya nini?.
Mungu atunusuru kwa kweli na atustiri
Hilo la gharama ndio huwa wananiacha hoi
Hivi unakaa siku saba au zaidi na kila asubuhi unataka upewe Chai na mikate

Na mchana na jioni walishwe na sidhani kama wanachangia kitu zaidi ya kuwakomoa wafia
.
Mila zingine wanabadili ziwe dini
 
Mungu atunusuru kwa kweli na atustiri
Hilo la gharama ndio huwa wananiacha hoi
Hivi unakaa siku saba au zaidi na kila asubuhi unataka upewe Chai na mikate

Na mchana na jioni walishwe na sidhani kama wanachangia kitu zaidi ya kuwakomoa wafia
.
Mila zingine wanabadili ziwe dini
Wanakomoa tu, kwenye uislamu watu wakifiwa wao ndo wanapaswa kuandaliwa chakula na kukirimiwa, cha ajabu waislamu wenyewe mtu akifariki wao wafiwa ndo wanaanza kutafuta nyama na michele.
 
Mi wananikera sana mtu kafa leo na leoleo wanazika, tena wanaikimbiza maiti kwenda makaburini. Kule tu kukimbia na maiti kuwahi kuzika naona kama ni imani tu ya kishenzi, unakimbizaje maiti vile?
Kiimani ni kwamba, mtu anapofariki awaishwe katika makazi yake bila kucheleweshwa, kama nu mtu wa khei ataikuta, kama ni mtu wa Shari ataikuta, na apelekwe haraka akakutane na alichovuna. Ila unapochelesha maiti ni uzwazwa sana, haitafifuka, haiongezi kitu, haitendi mema Tena.
 
Wee utazikwa hujafa vizuri.
Mahitaji Ubani ,Sanda mkeka chaaap kwa haraka
 
Wanakomoa tu, kwenye uislamu watu wakifiwa wao ndo wanapaswa kuandaliwa chakula na kukirimiwa, cha ajabu waislamu wenyewe mtu akifariki wao wafiwa ndo wanaanza kutafuta nyama na michele.
Inahuzunisha sana
Huku Ulaya mambo ni tofauti kabisa
Kwanza mnapewa ratiba ya mazishi
Mnaenda Msikitini mnaondoka mpaka maleloni
Mkizika au kumsitiri basi mtaambiwa kuna mlo umeandaliwa Hoteli fulani wote muende huko
Baada ya hapo mnatawanyika kila mmoja anafuata shughuli zake

Sisi mambo ni tofauti kabisa watu hawqna Imani
Wanadhani wanawafariji wafiwa kumbe wanazidi kuwaumiza

Mungu atusamehe
 
Back
Top Bottom