Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Sitaki niwachoshe kwa maneno mengi. Nawaambieni tu kwa kifupi na kwa uhakika. Bakuli la michango analolitembeza mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu si la kubezwa au kumezwa. Yaweza kuwa ni kwa kujua au kutokujua, Lissu anaruka kikwazo kikuu kilichosukwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu: ukata kwa vyama vya upinzani. Ukata tata ungewakata na kuwavuta wapinzani nyuma na kuwafanya washindwe kufanya kampeni.

Mipango kabambe ilishasukwa kitambo kuvifanya vyama vya upinzani mwaka huu kuandamwa na ukata wa kifedha. CCM yetu yenyewe, kwakuwa ina rasilimali za kutosha na kutisha na kwakuwa imejibanza kwenye koti la Serikali, ilijiandaa kujidai itakavyo kwenye kampeni hizi huku wapinzani wakishindwa kufanya kampeni. Mipango ilisukwa vyema. Kampeni zina gharama nyingi: usafiri, malazi,mavazi, chakula, vifaa vya sauti, majukwaa na kadhalika.

Mipango ya kuufanya ukata umee kwenye vyama vya upinzani ilianza miaka kadhaa iliyopita. Karibu kila chama kikubwa cha upinzani hapa nchini vikiwemo CHADEMA, ACT na NCCR-Mageuzi kina chama au vyama rafiki nje ya Tanzania. Marafiki hao wa nje husaidia vyama hivyo kifedha hasa kwenye harakati kama hizi za kiuchaguzi. Na hakukuwa na ubaya kuhusu kusaidiana huko. Lakini, mwaka huu misaada hiyo imepigwa pini. Imezibwa. Hakuna misaada tena. Ukata!

Lissu ajaziwe bakuli lake. Achangiwe. Hata mimi, kama mfuasi ninayejinafasi wa demokrasia ya vyama vingi, nimeshamchangia Lissu. Lazima tuwe na mgombea strong wa upinzani ili kutufanya tuchague vyema. Lazima mwaka huu mchuano mkali uwe kati ya Dkt. Magufuli na Lissu. Lazima tusikie sera za kila mmoja wao na tuamue. Bakuli la Lissu, hata kama litakejeliwa na kudhihakiwa, lina maana kubwa: linaruka mipango ya kidhalimu ya kutengeneza ukata kwa wapinzani.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma, Tanzania)
 
CCM ilitega mitego yake ili vyama vishindwe kufanya kampeni matokeo yake Chadema inawezeshwa na wananchi wenyewe ama kweli kumpiga teke chura ni sawa na kumuongezea mwendo
 
Mkuu VUTA-NKUVUTE unasahau kwamba:

1) Kampeni siyo za Urais tu, kuna Wabunge na Madiwani. Wote hao wanahitaji fedha kumudu kampeni. Je, chama kilijipangaje mapema, maana muda wa Uchaguzi Mkuu hujulikana?

2) Viongozi wa CHADEMA, na kwenye kampeni zinazoendelea, Lissu mgombea Urais amesikika akidai CCM imeharibu uchumi watu wamekuwa masikini kuliko awamu zilizopita. Hao wanaombwa kuchangia CHADEMA wana uwezo gani au ndio mpango wa kuwafanya masikini ili hayo madai yawe kweli?

3) CHADEMA, kama chama kikuu, kilikuwa kinapata mabilioni ya ruzuku. Isitoshe wabunge nao wamechangia kila mwezi na kufikisha mabilioni. Je, hii fedha imetumikaje maana hata ofisi, japo moja ya chama, haijajengwa.

Hiki ndio chama cha kuomba kuchangiwa gharama za kampeni?
 
Mkuu VUTA-NKUVUTE unasahau kwamba:

1) Kampeni siyo za Urais tu, kuna Wabunge na Madiwani. Wote hao wanahitaji fedha kumudu kampeni. Je, chama kilijipangaje mapema, maana muda wa Uchaguzi Mkuu hujulikana?

2) Viongozi wa CHADEMA, na kwenye kampeni zinazoendelea, Lissu mgombea Urais amesikika akidai CCM imeharibu uchumi watu wamekuwa masikini kuliko awamu zilizopita. Hao wanaombwa kuchangia CHADEMA wana uwezo gani au ndio mpango wa kuwafanya masikini ili hayo madai yawe kweli?

3) CHADEMA, kama chama kikuu, kilikuwa kinapata mabilioni ya ruzuku. Isitoshe wabunge nao wamechangia kila mwezi na kufikisha mabilioni. Je, hii fedha imetumikaje maana hata ofisi, japo moja ya chama, haijajengwa.

Hiki ndio chama cha kuomba kuchangiwa gharama za kampeni?
Nimekusoma najaribu kukuelewa na "nondo" zako ila sikuelewi.

1. Matumizi ya ruzuku ya Chadema ni kwaajili ya mambo mengi, kuna kulipa mishahara ya wafanyakazi, na mambo mengine ya uendeshaji chama, zaidi unaambiwa ruzuku imekatwa na serikali ya Magufuli, na hata kama ingekuwepo, Chadema wanapata milioni 200 na kitu kwa mwezi, hizo hazitoshi kugawa kwa matumizi ya chama mikoa yote Tz Bara, nakushangaa sijui kitu gani hiki ulichokiandika.

2. Pointi yako namba mbili ndio inazidi kuonesha ulivyo kilaza, sasa kama Chadema inachangiwa na masikini wewe shida yako ni ipi? umeambiwa wale marafiki wao wa nje wamebanwa wasiwachangie na serikali ya Magufuli, sasa wewe ulitaka wachangiwe na nani? kwanini unawadharau watanzania na hali zao mbaya kiuchumi zilizosababishwa na sera mbovu kuwekeza kwenye vitu badala ya watu? hujui hizo mia mia za hao masikini zikijumlishwa kitapatikana kikubwa!.

3. Pointi yako namba tatu nimeshaijibu kwenye namba moja, rudi juu kaisome tena.
 
Jibu swali langu la kwanza. Mimi namnukuu Lissu anadai wananchi wapo hoi kwa miaka mitano,kwa nini anawachangisha?
Unauliza maswali ya kipuuzi puuzi tu hebu fikirisha huo utopolo wako uliobaki kiduchu'

Wananchi kuwa hoi miaka mitano ni matokeo ya huyo 'mshamba' wako kuendesha nchi kama familia yake kule kijijini.
 
Back
Top Bottom