Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Kwani ile michango waliokuwa wanakatwa wabunge kwa ajili ya uchaguzi iko wapi? Wananchi wana hali mbaya kwa nini muwachangishe?
Kulikuwa na programs mbalimbali za CDM ni msingi zimekuwa zinaendelea wakati wote baada ya mikutano kuzuiwa. Hizo zote ni gharama.

CCM walinunua wabunge wengi toka upinzani ili vyama vya upinzani vikose gawio linalotokana na uwiano wa wabunge.

Hivyo pesa ambayo CCM ilikuwa ikitumika kununulia wabunge, ingerudi CCM kwa njia nyingine kupitia ogisi ya msajili wa vyama.

Mbinu hizi zote ndizo zilizomfanya Magufuli kuamini kuwa hata uchagyzi ukaachwa kuwa huru kabisa, hakuna mgombea wa upinzani ambaye angefurukuta. Yanayotokea sasa, ni mshangao mkubwa kwa Magufuli, Bashiru na Polepole - mabingwa hawa wa siasa za fitina, hila na udanganyifu.
 
Hazitoshi mkuu. Ccm pamoja na kula ruzuku ya m. 850 bado inategemea favour toka GT , Na wafadhili wakubwa akina Aziz unaona amekabidhi vyombo vyake vya habari vyote huko. So usishangae

Mzee Tupa Tupa ana hoja . Changa Tu Mzee ndiyo u Tz
CCM inatumia pesa zake kama ulivyosema ruzuku,vyanzo toka miradi mbalimbali na vitega uchumi.

JPM alikataa hata mkutano mkuu kuwa unadhaminiwa na matajiri ambao walikuwa wanakiharibu chama.

Michango ya wabunge wa chadema ilikuwa takribani bil 8 kwa miaka mitano unasema haitoshi?
 
Yaleyale ya makamanda wasiotumia akili. Ruzuku inatolewa kwa mujibu wa sheria. Ruzuku alikuwa anajilipa mwenyekiti wetu,sema nyie wenzangu mnaogopa kusema ukweli.
Hizo "akili" zako unazojidai nazo za ajabu kweli, bora za kuku, kwani zile pesa za mifuko ya jamii zinazotafunwa hazipo kisheria?! Nani aliekudanganya Magufuli anafuata sheria?

Kuanzia 1.5 t, uwanja wa ndege Chato, ununuzi wa ndege, hayo yote yamefanyika bila kufuata taratibu.
 
Kwani tatizo liko wapi? Wabunge wa Chadema walikuwa wanakatwa pesa kuchangia mfuko wa kuendesha uchaguzi wa mwaka 2020 kwa chama chao. Hizo pesa ziko wapi mpaka mchangishe watu?
Wewe huwa ni popoma mzuri, kwahiyo hao viongozi wa chama kuanzia ngazi za wilaya mpaka Taifa unawalipa wewe??? Wewe kazi yako nikukata viuno TU, Mambo ya msingi huwezi kuwa na uelewa nayo.
 
Zile pesa za mifuko ya jamii zinazotafunwa hazipo kisheria?!
Ndio haya ambayo yanakitia aibu Cdm. Pesa gani za mifuko ya jamii ambazo Ccm imezichota? Tumia akili kwa manufaa ya Cdm

Zamani serikali ilikuwa inakopa na ilikuwa inachelewa kulipa hiyo mifuko ya jamii. Mimi na Dk Slaa tunajua kwa undani.
 
Yes, ccm wa roho mbaya na mbinu za hovyo sana! Kampeni wamefanya miaka mitano peke yao! Vyombo vya habari vinarusha mikutano ya kampeni zao yote peke yao! Pesa wamejichotea wao zote peke yao, kisha wakaminya na kuzuia vyama vingine visipate misaada bali wao peke yao! Wameengu wagombea wa ubunge na udiwa ni karibu kwenye vyama vyote lakini wabunge na madiwani waliopita bila kupingwa ni wao pekea yao! Ndugu zangu tuzidishe support kwa CHADEMA tulikombowe taifa letu! Haiwezekani yaani kila kitu ni CCM peke yao!
 
Ndio haya ambayo yanakitia aibu Cdm. Pesa gani za mifuko ya jamii ambazo Ccm imezichota? Tumia akili kwa manufaa ya Cdm

Zamani serikali ilikuwa inakopa na ilikuwa inachelewa kulipa hiyo mifuko ya jamii. Mimi na Dk Slaa tunajua kwa undani.
Wewe ni andazi, wastaafu hawajalipwa pensheni zao miaka miwili una habari au unaropoka tu na ukamanda wako feki? mpaka wengine wanafariki bila kulipwa!.

Unajua kwanini serikali imeweka fao la kujitoa mpaka miaka 55? hujui kitu kamanda uchwara.
 
Wajinga wengi mko ccm, magufuli alipocuaguliwa alikuwa na hela? Mnaiba Kodi zetu mmajifanya za ccm. F.u
Hata kama yeye JPM akuwanazo lakini zilitumika pesa aijalishi zimetolewa na chama ama mtu.
kama CCM wapo madarakani wanatumia pesa kufanyia kampeni waweze kubaki madarakani, inakuwaje Chedema wanaotaka kuitoa madarakani CCM hawana fedha za kampeni,hivi mnania kweli ya kuchukua nchi ama mnapoteza muda tu?
 
Mbowe hata tukichanga yee anakura ela tu. Ndo maana mimi niriachaga kuchanga
kuandika kwenyewe hujui, hatuhitaji mchango wako na kampeni zinasonga mbele...hakuna cha fiesta na watu wanajaa, jaribuni nyie kufanya mkutano bila wasanii mpate uhalisia wa namna mnavyokubalika!.
 
Wewe ni andazi, wastaafu hawajalipwa pensheni zao miaka miwili una habari au unaropoka tu na ukamanda wako feki? mpaka wengine wanafariki bila kulipwa!.

Unajua kwanini serikali imeweka fao la kujitoa mpaka miaka 55? hujui kitu kamanda uchwara.
Nakushangaa kamanda mwenzagu. Hayo yanfao la kujitoa pale IKulu rais wa JMT aliwaida wadau wote wa vyama vya wafanyakazi,halikurudishwa?

Mbona watu wanastaafu na kulipwa? Au sema fungu linachelewa.
 
Wekeni nguvu kwa wagombea ubunge na madiwani. Wana njaa ya kufa mtu kwenye kampeni zao. Kumtunza lissu pesa ni kupoteza pesa.
 
Sitaki niwachoshe kwa meneno mengi. Nawaambieni tu kwa kifupi na kwa uhakika. Bakuli la michango analolitembeza mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu si la kubezwa au kumezwa. Yaweza kuwa ni kwa kujua au kutokujua, Lissu anaruka kikwazo kikuu kilichosukwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu: ukata kwa vyama vya upinzani. Ukata tata ungewakata na kuwavuta wapinzani nyuma na kuwafanya washindwe kufanya kampeni.

Mipango kabambe ilishasukwa kitambo kuvifanya vyama vya upinzani mwaka huu kuandamwa na ukata wa kifedha. CCM yetu yenyewe, kwakuwa ina rasilimali za kutosha na kutisha na kwakuwa imejibanza kwenye koti la Serikali, ilijiandaa kujidai itakavyo kwenye kampeni hizi huku wapinzani wakishindwa kufanya kampeni. Mipango ilisukwa vyema. Kampeni zina gharama nyingi: usafiri, malazi,mavazi, chakula, vifaa vya sauti, majukwaa na kadhalika.

Mipango ya kuufanya ukata umee kwenye vyama vya upinzani ilianza miaka kadhaa iliyopita. Karibu kila chama kikubwa cha upinzani hapa nchini vikiwemo CHADEMA, ACT na NCCR-Mageuzi kina chama au vyama rafiki nje ya Tanzania. Marafiki hao wa nje husaidia vyama hivyo kifedha hasa kwenye harakati kama hizi za kiuchaguzi. Na hakukuwa na ubaya kuhusu kusaidiana huko. Lakini, mwaka huu misaada hiyo imepigwa pini. Imezibwa. Hakuna misaada tena. Ukata!

Lissu ajaziwe bakuli lake. Achangiwe. Hata mimi, kama mfuasi ninayejinafasi wa demokrasia ya vyama vingi, nimeshamchangia Lissu. Lazima tuwe na mgombea strong wa upinzani ili kutufanya tuchague vyema. Lazima mwaka huu mchuano mkali uwe kati ya Dkt. Magufuli na Lissu. Lazima tusikie sera za kila mmoja wao na tuamue. Bakuli la Lissu, hata kama litakejeliwa na kudhihakiwa, lina maana kubwa: linaruka mipango ya kidhalimu ya kutengeneza ukata kwa wapinzani.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma, Tanzania)
Jana nimechangia mabadiliko kwa shilingi za kitanzania 180000
 
Wewe huwa ni popoma mzuri, kwahiyo hao viongozi wa chama kuanzia ngazi za wilaya mpaka Taifa unawalipa wewe??? Wewe kazi yako nikukata viuno TU, Mambo ya msingi huwezi kuwa na uelewa nayo.
Kwa hiyo unadanganya watu ili iweje? Kama Chadema ingekuwa inapeleka pesa wilaya zote Tanzania kungekuwa na hali kama hii?
Ofisi nyingi katika wilaya zimefungwa, au unajifanya hujui?
Ruzuku ilikuwa mil 360, deni la mbowe mil 100. Mil 50 anajilipa yeye. Sasa hapo za kulipa watu wilayani zingetoka wapi?

Changisheni wapuuzi wenzenu.
 
Back
Top Bottom