Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Sitaki niwachoshe kwa meneno mengi. Nawaambieni tu kwa kifupi na kwa uhakika. Bakuli la michango analolitembeza mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu si la kubezwa au kumezwa. Yaweza kuwa ni kwa kujua au kutokujua, Lissu anaruka kikwazo kikuu kilichosukwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu: ukata kwa vyama vya upinzani. Ukata tata ungewakata na kuwavuta wapinzani nyuma na kuwafanya washindwe kufanya kampeni.

Mipango kabambe ilishasukwa kitambo kuvifanya vyama vya upinzani mwaka huu kuandamwa na ukata wa kifedha. CCM yetu yenyewe, kwakuwa ina rasilimali za kutosha na kutisha na kwakuwa imejibanza kwenye koti la Serikali, ilijiandaa kujidai itakavyo kwenye kampeni hizi huku wapinzani wakishindwa kufanya kampeni. Mipango ilisukwa vyema. Kampeni zina gharama nyingi: usafiri, malazi,mavazi, chakula, vifaa vya sauti, majukwaa na kadhalika.

Mipango ya kuufanya ukata umee kwenye vyama vya upinzani ilianza miaka kadhaa iliyopita. Karibu kila chama kikubwa cha upinzani hapa nchini vikiwemo CHADEMA, ACT na NCCR-Mageuzi kina chama au vyama rafiki nje ya Tanzania. Marafiki hao wa nje husaidia vyama hivyo kifedha hasa kwenye harakati kama hizi za kiuchaguzi. Na hakukuwa na ubaya kuhusu kusaidiana huko. Lakini, mwaka huu misaada hiyo imepigwa pini. Imezibwa. Hakuna misaada tena. Ukata!

Lissu ajaziwe bakuli lake. Achangiwe. Hata mimi, kama mfuasi ninayejinafasi wa demokrasia ya vyama vingi, nimeshamchangia Lissu. Lazima tuwe na mgombea strong wa upinzani ili kutufanya tuchague vyema. Lazima mwaka huu mchuano mkali uwe kati ya Dkt. Magufuli na Lissu. Lazima tusikie sera za kila mmoja wao na tuamue. Bakuli la Lissu, hata kama litakejeliwa na kudhihakiwa, lina maana kubwa: linaruka mipango ya kidhalimu ya kutengeneza ukata kwa wapinzani.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma, Tanzania)
Kwa hiyo CCM ndo iliwambia wale pesa za ruzuku?
Mzee tupa sina uhakika kama una mapenzi kwa CCM, sema wewe ni kamanda, maana mada zako zinaonyesha kitambo sana.
 
Kwani ile michango waliokuwa wanakatwa wabunge kwa ajili ya uchaguzi iko wapi? Wananchi wana hali mbaya kwa nini muwachangishe?
Unateseka?
images.jpg
 
Endelea kuteseka mkuu. Kachemsha CAG, kachemsha Director wa Taa Kuu Kuu Tu, utaweza wewe uliye nyuma ya keyboard ya Itel?
Mimi nateseka nini? Anateseka mgombea wenu,mara aanguke jukwaani,mara achangishe pesa. Kwa nini asitulie maana hata kura laki mbili hapati.
 
Wacha ajilipe na kuchanga tutachanga.Wako wanaotumbua kodi za wananchi miaka zaidi ya 50 ukiwaona wameshiba kweli kweli na nchi iko vile vile mbona hatusemi.
Yaleyale ya makamanda wasiotumia akili. Ruzuku inatolewa kwa mujibu wa sheria. Ruzuku alikuwa anajilipa mwenyekiti wetu,sema nyie wenzangu mnaogopa kusema ukweli.
 
Mnasema hatupo kwenye uchumi wa Kati.

Wananchi ni maskini,

Halafu mnatembeza bakuli kwa maskini.
Mimi siwezi kuwachangia ni hiyari yangu silazimishwi na wanaochangia ni hiyari yao hawalazimishwi!

Wanachanga kwa utashi wao wenyewe!

Unakelwa na nini Mkuu!?
 
Tunaendelea kuchanga mkuu na hatutachoka mpaka tuikomboe nchi kutoka kwa beberu na dukteta ccm
 
Sitaki niwachoshe kwa meneno mengi. Nawaambieni tu kwa kifupi na kwa uhakika. Bakuli la michango analolitembeza mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu si la kubezwa au kumezwa. Yaweza kuwa ni kwa kujua au kutokujua, Lissu anaruka kikwazo kikuu kilichosukwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu: ukata kwa vyama vya upinzani. Ukata tata ungewakata na kuwavuta wapinzani nyuma na kuwafanya washindwe kufanya kampeni.

Mipango kabambe ilishasukwa kitambo kuvifanya vyama vya upinzani mwaka huu kuandamwa na ukata wa kifedha. CCM yetu yenyewe, kwakuwa ina rasilimali za kutosha na kutisha na kwakuwa imejibanza kwenye koti la Serikali, ilijiandaa kujidai itakavyo kwenye kampeni hizi huku wapinzani wakishindwa kufanya kampeni. Mipango ilisukwa vyema. Kampeni zina gharama nyingi: usafiri, malazi,mavazi, chakula, vifaa vya sauti, majukwaa na kadhalika.

Mipango ya kuufanya ukata umee kwenye vyama vya upinzani ilianza miaka kadhaa iliyopita. Karibu kila chama kikubwa cha upinzani hapa nchini vikiwemo CHADEMA, ACT na NCCR-Mageuzi kina chama au vyama rafiki nje ya Tanzania. Marafiki hao wa nje husaidia vyama hivyo kifedha hasa kwenye harakati kama hizi za kiuchaguzi. Na hakukuwa na ubaya kuhusu kusaidiana huko. Lakini, mwaka huu misaada hiyo imepigwa pini. Imezibwa. Hakuna misaada tena. Ukata!

Lissu ajaziwe bakuli lake. Achangiwe. Hata mimi, kama mfuasi ninayejinafasi wa demokrasia ya vyama vingi, nimeshamchangia Lissu. Lazima tuwe na mgombea strong wa upinzani ili kutufanya tuchague vyema. Lazima mwaka huu mchuano mkali uwe kati ya Dkt. Magufuli na Lissu. Lazima tusikie sera za kila mmoja wao na tuamue. Bakuli la Lissu, hata kama litakejeliwa na kudhihakiwa, lina maana kubwa: linaruka mipango ya kidhalimu ya kutengeneza ukata kwa wapinzani.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma, Tanzania)
Nilishachanga Laki moja ngoja nikaongeze na hii elfu kumi niliyotaka kunywa Supu muda huu. Najua kwa siku moja sifi njaa.
 
Kwani ile michango waliokuwa wanakatwa wabunge kwa ajili ya uchaguzi iko wapi? Wananchi wana hali mbaya kwa nini muwachangishe?
Wana wa nchi wametoa wapi hiyo hali mbaya awamu hii ya tano, magufuli ametokomeza umaskini Tanzania, yahani wa tz ni matajiri hakuna mfanowe, acha wachangie demokrasia nchini mwao iweze kunawiri na kistawi, ebo!
 
Sio kila jambo utake liandikwe uku kwenye mitandao.We kaa ukijua mambo ni mengi,sio hadi tuiponze Jamii forum ndo ujue mambo ni mengi.watu wanakaa kimya tu.
Ndio haya ambayo yanakitia aibu Cdm. Pesa gani za mifuko ya jamii ambazo Ccm imezichota? Tumia akili kwa manufaa ya Cdm

Zamani serikali ilikuwa inakopa na ilikuwa inachelewa kulipa hiyo mifuko ya jamii. Mimi na Dk Slaa tunajua kwa undani.
 
Nimekusoma najaribu kukuelewa na "nondo" zako ila sikuelewi.

1. Matumizi ya ruzuku ya Chadema ni kwaajili ya mambo mengi, kuna kulipa mishahara ya wafanyakazi, na mambo mengine ya uendeshaji chama, zaidi unaambiwa ruzuku imekatwa na serikali ya Magufuli, na hata kama ingekuwepo, Chadema wanapata milioni 200 na kitu kwa mwezi, hizo hazitoshi kugawa kwa matumizi ya chama mikoa yote Tz Bara, nakushangaa sijui kitu gani hiki ulichokiandika.

2. Pointi yako namba mbili ndio inazidi kuonesha ulivyo kilaza, sasa kama Chadema inachangiwa na masikini wewe shida yako ni ipi? umeambiwa wale marafiki wao wa nje wamebanwa wasiwachangie na serikali ya Magufuli, sasa wewe ulitaka wachangiwe na nani? kwanini unawadharau watanzania na hali zao mbaya kiuchumi zilizosababishwa na sera mbovu kuwekeza kwenye vitu badala ya watu? hujui hizo mia mia za hao masikini zikijumlishwa kitapatikana kikubwa!.

3. Pointi yako namba tatu nimeshaijibu kwenye namba moja, rudi juu kaisome tena.
Obama wa Marekan 200i alichangisha pesa kwa ajili ya kampeni wanashangaa hawa utopolo wa Tandale
 
Nimekusoma najaribu kukuelewa na "nondo" zako ila sikuelewi.

1. Matumizi ya ruzuku ya Chadema ni kwaajili ya mambo mengi, kuna kulipa mishahara ya wafanyakazi, na mambo mengine ya uendeshaji chama, zaidi unaambiwa ruzuku imekatwa na serikali ya Magufuli, na hata kama ingekuwepo, Chadema wanapata milioni 200 na kitu kwa mwezi, hizo hazitoshi kugawa kwa matumizi ya chama mikoa yote Tz Bara, nakushangaa sijui kitu gani hiki ulichokiandika.

2. Pointi yako namba mbili ndio inazidi kuonesha ulivyo kilaza, sasa kama Chadema inachangiwa na masikini wewe shida yako ni ipi? umeambiwa wale marafiki wao wa nje wamebanwa wasiwachangie na serikali ya Magufuli, sasa wewe ulitaka wachangiwe na nani? kwanini unawadharau watanzania na hali zao mbaya kiuchumi zilizosababishwa na sera mbovu kuwekeza kwenye vitu badala ya watu? hujui hizo mia mia za hao masikini zikijumlishwa kitapatikana kikubwa!.

3. Pointi yako namba tatu nimeshaijibu kwenye namba moja, rudi juu kaisome tena.
Maelezo ya point number mbili yamedhihirisha ulivyo sawa na ulichokiandika.
 
Sitaki niwachoshe kwa meneno mengi. Nawaambieni tu kwa kifupi na kwa uhakika. Bakuli la michango analolitembeza mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu si la kubezwa au kumezwa. Yaweza kuwa ni kwa kujua au kutokujua, Lissu anaruka kikwazo kikuu kilichosukwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu: ukata kwa vyama vya upinzani. Ukata tata ungewakata na kuwavuta wapinzani nyuma na kuwafanya washindwe kufanya kampeni.

Mipango kabambe ilishasukwa kitambo kuvifanya vyama vya upinzani mwaka huu kuandamwa na ukata wa kifedha. CCM yetu yenyewe, kwakuwa ina rasilimali za kutosha na kutisha na kwakuwa imejibanza kwenye koti la Serikali, ilijiandaa kujidai itakavyo kwenye kampeni hizi huku wapinzani wakishindwa kufanya kampeni. Mipango ilisukwa vyema. Kampeni zina gharama nyingi: usafiri, malazi,mavazi, chakula, vifaa vya sauti, majukwaa na kadhalika.

Mipango ya kuufanya ukata umee kwenye vyama vya upinzani ilianza miaka kadhaa iliyopita. Karibu kila chama kikubwa cha upinzani hapa nchini vikiwemo CHADEMA, ACT na NCCR-Mageuzi kina chama au vyama rafiki nje ya Tanzania. Marafiki hao wa nje husaidia vyama hivyo kifedha hasa kwenye harakati kama hizi za kiuchaguzi. Na hakukuwa na ubaya kuhusu kusaidiana huko. Lakini, mwaka huu misaada hiyo imepigwa pini. Imezibwa. Hakuna misaada tena. Ukata!

Lissu ajaziwe bakuli lake. Achangiwe. Hata mimi, kama mfuasi ninayejinafasi wa demokrasia ya vyama vingi, nimeshamchangia Lissu. Lazima tuwe na mgombea strong wa upinzani ili kutufanya tuchague vyema. Lazima mwaka huu mchuano mkali uwe kati ya Dkt. Magufuli na Lissu. Lazima tusikie sera za kila mmoja wao na tuamue. Bakuli la Lissu, hata kama litakejeliwa na kudhihakiwa, lina maana kubwa: linaruka mipango ya kidhalimu ya kutengeneza ukata kwa wapinzani.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma, Tanzania)
Naunga mkono hoja zote
 
Kwani ile michango waliokuwa wanakatwa wabunge kwa ajili ya uchaguzi iko wapi? Wananchi wana hali mbaya kwa nini muwachangishe?
Kumbe hata CCM mnajua kua mmewatia umasikini wananchi?.
Kila mabadiliko yanahitaji gharama, hivyo sio mbaya kwa mwananchi kuchangia kwa aliyenacho, kama hana alazimishwi kuna njia nyingine ya kuchangia kiifikia ahadi ya maendeleo ya kweli
 
Back
Top Bottom