Nawaonea huruma rafiki zangu, usiombe kuzaa na mwanamke asie na akili

maji ya gundu

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
3,070
Reaction score
4,698
Habari za jumapili wana jukwaa, bila shaka najua mnaendea vizuri na matatizo yenu.

Kuna hili jambo haliongelewi sana ila linatesa sana vijana. Iko hivi nna rafiki zangu Kama wanne wamezaa tu na wanawake hawajafanikiwa kuishi pamoja, asee hili jambo usiombe likukute ishia tu kuliona kwa wenzio maana kwa haya nayoona wanayopitia ni hatari kwakweli

Kuna mmoja juzi mzazi mwenzie kamtukana sana afu hana ata sababu ya msingi

Kwani wanawake mkizalishwa bila kuolewa nini huwa kinawatokea kwene bongo zenu maana haya ninayoyashuhudia

Yaani ukitaka kujua tabia halisi ya mtu wako akuzalie, yaani ukishamzalisha ndo utamjua vizuri kila kitu hadi uvumilivu wake unapoishia

Poleni sana mliozaa na wanawake wasio na akili mna nafasi kubwa Sana ya kupoteza watoto wenu

Ni vile tu hamuongei ila mnapitia mengi sana, nimejaribu kuvaa viatu vya marafki zangu nimeshindwa kabisa.

Niwatakie weekend njema
 
sio kweli …… hii story haijakamilika kama upande wa pili hawajasema chochote
 
Ni kweli lazima tuonekane hatuna akili,umenizalisha kunioa umekataa bado unataka mawasiliano nami ya nini sasa.Mi ukishasema hunihitaji futa kumbukumbu zote zinihusuzo.Damn! Tunaishi Mara moja ......ukiniacha naachika kweli!
 
Mwanaume anayemzalisha mdada kisha kumtelekeza mtoto na Mama yake hii haikubaliki,usimpomlea mwanao unategemea nani akulelee?
Mwanaume lazima ukubali majukumu yako na kupambana ili kuyatimiza majukumu hayo na huo ndio Uanaume.
 
1-Akili zako zinakutuma kila mtu ana matatizo kama yako?
2-Kulialia kwa mwanamke mara zote ni kutokuwa na akili tu au hatunzwi ipasavyo?
3-Hayo maneno umeyatoa wapi wakati umeeleza kuwa huwa hawaongei?
4-Acha kuwatungia watu uongo kwamba wana matatizo kumbe ni weye tu umeshiba uji wa ulezi ukaanza kufikiria visivyokuwepo.
 
Waambie rafiki zako watoe pesa za kuwahudumia watoto na mama zao waone kama watatukanwa tena.Ukiwa na pesa mwanamke anaanzaje kukutusi? Huo ujasiri wa kuitukana Benki/ATM anautoa wapi?
 
Wewe unayejikaza kuja kuongea upupu huku hivi unajua kuzaa wewe sema .
Unajua hapo wewe akili yako inakutosha hapo ulipo hujitambui .

Umewahi telekezwa na wazazi, ndugu na mwanaume aliyekupa mimba wewe halafu mtoto ananjaa wewe nawe unanjaa hakuna mtu anayekusemesha uko nakamfuko navinguo vya mtoto na nguo zako unalia huna hata vocha ya kumtaarifu mtu ???
Wewe unatafuta laana fulani ya kizazi chako na channe.
Hujijui bado ..
Muombe Mungu leo akusamehe kabisa na umind your own business .
Kumbe jamii forum kuna watu badoo akili hawana hivi mnajiona sisi ni tunamatumbo yakujazwa jazwa tu eh! Ukitaka umjue mwanamke uzae naye ???

Nasisi wanawake tuwe naakili eti sio kila mtu unafungua mbususu wengine wanaume ni vichaa kweli naapa
 
Mwanaume anayemzalisha mdada kisha kumtelekeza mtoto na Mama yake hii haikubaliki,usimpomlea mwanao unategemea nani akulelee?
Mwanaume lazima ukubali majukumu yako na kupambana ili kuyatimiza majukumu hayo na huo ndio Uanaume.
Acha tu rafiki angu ….. kuna siku nilikua pale Magomeni hospital ofisi ya mganga mkuu sehem ya Ustawi

Dada kaja analia pale baba hahudumii mtoto wao mzuri tu masikini

ila tuishi humo humo 🙏🏽
 
umesema ni rafiki zako wanamajanga hayo tena wanne

wewe tegemezi katafte hela uache kudandia visentisenti vya malezi ya watoto wao na kuwapumbaza hao wanne ili wakae kibachela km wewe.

saa ingine unajiuliza mbona mwanaume huyu atuekewani ila akielekezwa,na marafiki zake anaelekea kumbe ndo nyie mnanyemelea visenti ili asahau wajibu wake.


kazalishe na wewe uwe bize uache kunanga mahusiano ya wenzio.
 
Umesema ni rafiki zako wanamajanga hayo tena wanne

Wewe tegemezi katafte hela uache kudandia visentisenti vya malezi ya watoto wao na kuwapumbaza hao wanne ili wakae kibachela km wewe.

Saa ingine unajiuliza mbona mwanaume huyu atuekewani ila akielekezwa,na marafiki zake anaelekea kumbe ndo nyie mnanyemelea visenti ili asahau wajibu wake.

Kazalishe na wewe uwe bize uache kunanga mahusiano ya wenzio.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…