Nawezaje kupata mkopo wa Tsh. Milion 1 na laki 2 kwa dhamana ya vyeti vyangu?

Nawezaje kupata mkopo wa Tsh. Milion 1 na laki 2 kwa dhamana ya vyeti vyangu?

Ndg nawezaje kupata mkopo wa tsh Milion 1 na laki 2 tu, kwa dhamana ya vyeti vyangu? Cheti cha Diploma-CBE, cheti cha Degree-TIA, ikiwa pamoja na vyeti vingine mf cha form 4, cha kuzaliwa n.k

Ni vyeti original kabisa pia bado navihitaji kwani sijakata tamaa kuhusu Ajira, hivyo sio kwamba navitelekeza hapana. Kiukweli nina shida nahitaji msaada.

Niko tayari kulipa kwa riba na kuandikishana kwa mwanasheria, kwasasa nipo Mkoa wa Pwani ya Kibaha.

Naomba kuwasilisha kwenu wana JF.
Rudisha hivyo vyeti huko ulikosoma wakurejeshee ada yako!
 
Unadhani cheti kinaokotwa,cheti kinagharamiwa yaani mtu analipa ada ili akipate hicho cheti husika,unachokidharau.
Siyo suala la kudharau cheti bali ni kuwa cheti hakina faida yeyote kwa third party , na kama muhusika yeye anaona kina faida basi akigeuze kimpatie hicho kiwango cha pesa anachokihitaji, msitafute sympathy kwenye mambo yaliyo wazi
 
Kama unadhani hivyo vyeti vinathamani kuliko pesa basi nenda Bank ukakope uweke bond hivyo vyeti, na aliekushauri hvo mwambie akusindikize

Ukitoka bank uje na mrejesho
Acha dharau. Umri na maneno yako havina uwiano. Mtu anapozungumza jambo litafakari. Utu, hekima busara viwe mbele. Nadhan una watoto... Kuna beba mawazo ya mtu kw mtazamo chanya usipayuke
 
Sure, japo hakina monetary value kuwa dhamana lakini cheti ni cha thamani sana, tunapitia magumu thats why inafka mahal tunaomba msaada, dunia ya leo mtu kukusaidia n kaz sn. Na kimfaacho mtu chake ndio maana naomba msaada kwa kigezo cha vyeti niktambua kbs hakfai kuwa dhamana, ila kw msamalia atayeguswa anisaidie angalau bas niweke vyet tu ishara kuwa nitalipa deni, bado navhtaj hv vyet sijavikatia tamaa lkn kw sasa napitia uhitaj wa hicho kias cha fedha na sina msaada nikaona niweke mawazo yng JF
Endelea kushirikisha ubongo wazo la cheti ni la hadhi ya chini sana. Omba kwenye ukoo wenu wanaokufahamu, ongea na ndugu wauze mashamba, waweke rehani mifugo, nyumba, na chochote chenye thamani, vyeti, NIDA, Leseni...ukimpa mkopaji ni Zero value hawezi kuvitoa akapata pesa yake[emoji848][emoji848]
 
Acha dharau. Umri na maneno yako havina uwiano. Mtu anapozungumza jambo litafakari. Utu, hekima busara viwe mbele. Nadhan una watoto... Kuna beba mawazo ya mtu kw mtazamo chanya usipayuke
Usilete mtazamo chanya wakati wewe unaleta vitu ambayo haviwezekani

Tatizo la sisi wabongo tunapenda kuambiwa maneno mazuri mazuri

Abadani huwezi pewa mkopo kwa Bond ya vyeti,
Tafta bond inayoeleweka nenda ukakope la sivyo unapoteza muda wako bure

Endelea kukaa hapa ukisubiri kuambiwa maneno mazuri mazuri
 
Unadhani cheti kinaokotwa,cheti kinagharamiwa yaani mtu analipa ada ili akipate hicho cheti husika,unachokidharau.
Cheti kina thamani zaidi ya hio millioni moja lakini kwa mwenye cheti sio mwengine pesa hio million 1 ina thamani kwa watu wote Duniani, elimu ndogo tu Hapo ni makaratasi tu kwa mtu mwengine.
 
Muulize tukimpa achague Kati ya milioni moja na cheti cha certificate
Yeye atachagua nini
Nitachagua cheti mkuu. Sbb bdo ninakihitaj si kwamba nimekata tamaa kwny ajira. N msaada tu naomba kwenu watu baki. Ili kuweka kauzto kdg sbb mtu kkupa for free n kaz nikaleta ishu za chet. Mbal na hvyo nikufahamiana nakujua ukwel khs mm nakunisaidia
 
Cheti kina thamani zaidi ya hio millioni moja lakini kwa mwenye cheti sio mwengine pesa hio million 1 ina thamani kwa watu wote Duniani, elimu ndogo tu Hapo ni makaratasi tu kwa mtu mwengine.
Sbb bdo ninakihitaj si kwamba nimekata tamaa kwny ajira. N msaada tu naomba kwenu watu baki. Ili kuweka kauzto kdg sbb mtu kkupa for free n kaz nikaleta ishu za chet. Mbal na hvyo nikufahamiana nakujua ukwel khs mm nakunisaidia
 
Nitachagua cheti mkuu. Sbb bdo ninakihitaj si kwamba nimekata tamaa kwny ajira. N msaada tu naomba kwenu watu baki. Ili kuweka kauzto kdg sbb mtu kkupa for free n kaz nikaleta ishu za chet. Mbal na hvyo nikufahamiana nakujua ukwel khs mm nakunisaidia
Sawa endelea kusubiri msaada kupitia cheti

Tunasubiri mrejesho
All the best
 
Mtu mwenye akili hawezi kutoa ata buku kwa dhamana ya cheti. Maana ya dhamana ni mbadala wa ulichopewa sasa usipofuata cheti au kitambulisho chako nakipeleka wapi kwangu cheti ni karatasi au uchafu tu. Kwako wewe cheti ndio kina thamani ata million 20 lakini sio kwa mwenye pesa.
 
Back
Top Bottom