Naamini mmeamshwa vyema wakuu.
Niende kwenye mada, nina shida sana na Tsh. Milioni moja, naihitaji kwa ajili ya mtaji, (kuna jiko la kupikia chakula sehemu ya bar nataka kulichukua niweke vijana wapike) nikisema kukopa sina cha kuweka dhamana, ukisema uombe kwa ndugu hamna kila mtu anasema hana.
Nikiwaza maisha ndo hivo yanaenda kasi bila kuwekeza wekeza hufanikiwi.
Sent using
Jamii Forums mobile app
Nimepita hapo ulipo, na kwa sababu ya passion niliyokuwa nayo nikaipata, watu ni wagumu sana hasa wanaposikia kwamba ni kwa ajili ya biashara, maana who knows kama itafanikiwa!
Mwombe Mungu, huku unaendelea kuwaza na somehow atatokeza na utafanikiwa kuupata huo Mtaji, ushauri wangu: Usilazimishe, na kuwaza oh jiko likienda ndo basi tena, au oh nikipata ndo maisha yamenyoka, ukilikosa pia mshukuru Mungu.
Kuna vitu nimewahi kulazimisha nikapata vikanipelekea kwenye uharibifu, kuna vitu nimewahi kukosa na nikapata vitu bora zaidi Baadae! Mungu akupe hekima na akupe vitu sahihi kwenye maisha yako!
Huu ni ushuhuda wa kweli, Nina shemeji yangu mmoja, wife wa rafiki yangu sana, Mme wake ali paralyse, sasa tulikuwa twaishi mikoa mbalimbali, so nilikuwa nawasiliana na shemeji yangu mara nyingi!
Kuna mpango wa cheti cha shemeji yangu alikuwa anasaiwa 1m hivi kupata ili aanze kazi, kweli baada ya mawasiliano nikamwambia nitakupa, ila ukianza pata mshahara urudishe: 20,000 kila mwezi.
Nikamtumia 1m - sikuongea na mme wake maana alikuwa kaparalyse, na hawezi ongea vizuri..... baada ya kumpa mawasiliano yakafa, ni kawa na wasiwasi na mshikaji wangu kapatwa na nini?
Nikapanda Bus kwenda muona, dah..... baada ya kumpa mwanamke hela, kamtelekeza jamaa, hakumwaga wala kumwambia mtu, then jamaa akafarariki........
Toka siku hiyo, kila wakati mtu akinambia hela, nakumbuka kaburi la mshkaji wangu na kwamba Siku pata hata fursa ya kuongea naye au kumwaga au kwenda kwenye mazishi.....
Sisemi wewe ni mtu mbaya, Hapana, nasema unaweza usipate msaada maana watu wamepitia mambo mengi, wewe mwamini Mungu, mwombe Mungu na Mungu ndiye atafanya usaidike kama wewe ni wa kusaidika