Nawezaje kushikilia msimamo wangu bila kuwakwaza wazazi?!

Nawezaje kushikilia msimamo wangu bila kuwakwaza wazazi?!

HumbleBoy98

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2020
Posts
387
Reaction score
396
Habari zenu Wana Jamiiforums.
Mimi ni kijana ambaye umri wangu upo kwenye mid 20's.

Nipo chuo kimoja hapa nchini ambapo nasomea kozi ya uuguzi.

Nia na madhumuni ya kuleta Uzi huu ni kuomba ushauri kuhusu ni jinsi Gani ninaweza kushikilia msimamo wangu kuhusu Nini nataka kwenye maisha yangu bila kuwafanya wazazi wahisi kama nimewadharau.
Iko hivi...

Baba yangu ndiye anayenisomesha mpaka sasa, hivi karibuni nilipokuwa likizo ya kumaliza mwaka wa pili kuingia mwaka wa tatu wa masomo hapa chuoni Mzee wangu alinishauri kwamba nikimaliza kozi Hii ya nursing (diploma) nirudi Tena chuo kusomea Tena kozi ya pharmacy miaka mingine mitatu (diploma). Hoja yake ni kwamba nikifanya hivyo baadaye naweza kujiajiri Kwa kufungua pharmacy yangu Mimi mwenyewe na kwamba pharmacy ni biashara inayolipa vizuri sana.

Lakini Mimi binafsi Kwa upande wangu siko tayari kufanya hivyo kwasababu malengo niliyojiwekea Mimi ni kwamba baada ya kumaliza hii diploma ya nursing nitafute ajira inishikize Kwa miaka kadhaa huku nikiwa nafanya shughuli za ujasiriamali pembeni Kisha biashara zikiwa nzuri na nikiona Nina kipato Cha kueleweka niachane kabisa na ajira ya uuguzi nijikite Moja Kwa Moja katika biashara kwasababu moyoni mwangu nawiwa kuwa mjasiriamali mkubwa tu, Maana hata hii kozi ya uuguzi ninayosomea sasahivi sikuitaka kabisa, nilipomaliza kidato Cha nne nilitaka nikasome business administration au kozi za masuala ya entrepreneurship Ili baadaye niweze kujiajiri katika biashara na ujasiriamali kwani ndoto zangu ni kumiliki kampuni yangu binafsi. Lakini Mzee wangu alipinga vikali wazo hili akisisitiza kuwa kozi za biashara hazina tija na wapo wengi wanaozunguka mitaani na vyeti vyao bila ajira miaka nenda Rudi na Wana degree kabisa.

Nilijaribu sana kumwelewesha kwamba lengo langu si kutafuta ajira Bali ni kujiajiri mwenyewe kutokana na elimu nitakayopata lakini hakukubaliana kabisa na Mimi.

Baadaye akanitafutia vyuo vya afya na kufanikiwa kupata nafasi katika kozi Hii ya uuguzi chuo Fulani hapa nchini na Mimi Kwa kuepuka kumkwaza nikakubali kuja kusoma japo haikuwa passion yangu kabisa!

Sasa kinachofanya nije kuomba ushauri ni hiki...

Mzee wangu ni mtu ambaye anataka akiongea kitu basi ufanye kama alivyokwambia yeye, ukitaka kufanya tofauti anakuona kama mbishi, unampuuza au unamdharau!

Of course Baba yangu ni mtu mmoja mzuri sana kwasababu ana upendo wa ajabu Kwa wanae yupo tayari kufanya chochote na ku sacrifice Kila kitu Ili kutupatia kile ambacho yeye anaamini kuwa ni Bora katika maisha ni mtu mwenye upendo wa ajabu sana na familia yake na watoto wake na Kwa Hilo nimemfanya kuwa role model wangu. Shida yake ndio hiyo Moja hataki uende tofauti na anavyotaka yeye.

Mimi Kwa upande wangu siamini kama kusoma saaana ndio kufanikiwa na ninataka nikimaliza hii diploma nianze kupambana na maisha sasa lakini yeye anasisitiza kuwa diploma ni level ndogo sana Kwa maisha ya sasa.

Of course inaweza kuwa kweli lakini Mimi naamini katika ndoto zangu na malengo Yangu na sitaki Tena kuendelea kupoteza muda kukaa darasani maana umri unazidi kwenda Mimi sio wa kuendelea kumtegemea mzazi Tena lakini nikimwambia hataki kabisa kuelewa.

Sasa wanajamvi shida yangu ninaomba mnisaidie nitumie mbinu Gani kumwelewesha na kumshawishi Mzee wangu akubali Mimi nifuate kile nilichojipangia katika maisha yangu lakini bila kumkwaza na kumfanya ahisi kama nampuuza au kumdharau?

Nawapenda sana wazazi Wangu sitaki kuwakwaza lakini pia sitaki kunyimwa opportunity ya kupambania malengo niliyojiwekea katika maisha na natamani pia wazazi wanipe Uhuru wa kujiamulia ninachotaka katika maisha yangu pia!

Nimepanga nikirudi home nikazungumze nae kuhusu hili lakini nashindwa kujua nitumie mbinu Gani kumuelewesha Maana najua nikishikilia uamuzi wangu tunaweza kuishia kupishana kauli kitu ambacho sitaki kitokee kwani pamoja na hayo sitaki kumkwaza.

Sasa naombeni ushauri wadau ni vipi naweza kushikilia msimamo wangu bila kuwakwaza wazazi?

Asanteni nawasilisha.
 
Nini unahitaji kwenye maisha yako??kumfurahisha mzazi au kutimiza malengo yako???kwenda kosomea course ambayo hukutaka ulifanya kwaajili yake,ukimaliza nursing fanya Jambo kwaajili yako,wazazi wanatupenda Sana pia nao kama watu wengine Wana mtazamo tofauti kuhusu maisha ni Nini...atakua na maoni tofauti kuhusu mwanamke unaetaka kumuoa,ili kumfurahisha utafanya kila kitu???
 
Kwanza pole sana kwa kuwa na wazazi wenye uelewa mdogo kuhusu uhuru wa mtoto kufata ndoto zake so long ni njia sahihi.. Pili baba yako alikosea toka Mwanzo kukutoa toka kwenye Njia ya masomo ya biashara na akakuforce usomee mambo ya science akiamini ndo kwenye Ajiraa pole sana lakini Ulifanya kosa kubwa sana maana kuajiriwa siku hizi haijalishi umesomea nini hakuna hajira isipokuwa hadi leo NIMESHUHUDIA washkaji zangu waliosoma masomo ya bisahara wakimaliza na Kuajiriwaaa faster hasa kama walikuwa wanaperfom vizuri darasani mfano mzuri ni Mdogo wangu kamaliza masomo ya biashara hama Miezi sita nyumbani Kashapata kazi tema serikalini... Tuliosoma masomo ya science hadi leo tupo private tunaunha unga so haya mambo sio ya Kukariri kabisa mdogo wetu alieonekana anapotea njia leo yupo serikalini mapema tu na huko ana nafasi ya kupanda cheo na kulipwa vizuei zaidi.


Tatu kosa ulilofanya mwanzo kufata ndoto za mzazi juu yako badala ya Ndoto zako Usilirudie tena sasa Huwezi soma diploma nursing leo umemaliza urudi ukasome Diploma ya pharmacy kisa tu eti famasi unaweza jiajiri Alokwambia kujiajiri famasi inahitaji Diploma nani??? Mtaji huna hata usome mpaka masters huwezi jiajiri kamwe... Labda kama baba yako atakupa mtaji wa kufungua famasi ukimaliza diploma na bado itakuwa haijakusaidia maana itabdi Umlipe mfamasia ili kuendesha famasi yako so Diploma haina msaada direct kwenye kupunguza Cost za kuendesha famasi.

Nne USIRUDI KUSOMA FAMASI. achana na mambo ya kuteseka kutimiza ndoto ya mazazi wako ushasoma nursing inatosha sasa Fata ndoto zako achana na Upuuzi wa kusikiliza ujinga anaokwambia mzee wako wakati hali halisi haipo Hivyo kabisaaa ukikaa vibaya Siku atakwambia usisome famasi soma Diploma ya Udaktari na wew utababaika.. Ur old enough kusimamia misimamo yako umri unaenda acha kuishi ndoto za mzazi wako akikasirika akasririke tu.

Mwisho pole sana ila KUWA NA MSIMAMO.
 
Habari zenu Wana Jamiiforums.
Mimi ni kijana ambaye umri wangu upo kwenye mid 20's.
Nipo chuo kimoja hapa nchini ambapo nasomea kozi ya uuguzi.
Nia na madhumuni ya kuleta Uzi huu ni kuomba ushauri kuhusu ni jinsi Gani ninaweza kushikilia msimamo wangu kuhusu Nini nataka kwenye maisha yangu bila kuwafanya wazazi wahisi kama nimewadharau.
Iko hivi...
Baba yangu ndiye anayenisomesha mpaka sasa, hivi karibuni nilipokuwa likizo ya kumaliza mwaka wa pili kuingia mwaka wa tatu wa masomo hapa chuoni Mzee wangu alinishauri kwamba nikimaliza kozi Hii ya nursing (diploma) nirudi Tena chuo kusomea Tena kozi ya pharmacy miaka mingine mitatu (diploma). Hoja yake ni kwamba nikifanya hivyo baadaye naweza kujiajiri Kwa kufungua pharmacy yangu Mimi mwenyewe na kwamba pharmacy ni biashara inayolipa vizuri sana.
Lakini Mimi binafsi Kwa upande wangu siko tayari kufanya hivyo kwasababu malengo niliyojiwekea Mimi ni kwamba baada ya kumaliza hii diploma ya nursing nitafute ajira inishikize Kwa miaka kadhaa huku nikiwa nafanya shughuli za ujasiriamali pembeni Kisha biashara zikiwa nzuri na nikiona Nina kipato Cha kueleweka niachane kabisa na ajira ya uuguzi nijikite Moja Kwa Moja katika biashara kwasababu moyoni mwangu nawiwa kuwa mjasiriamali mkubwa tu, Maana hata hii kozi ya uuguzi ninayosomea sasahivi sikuitaka kabisa, nilipomalixa kidato Cha nne nilitaka nikasome business administration au kozi za masuala ya entrepreneurship Ili baadaye niweze kujiajiri katika biashara na ujasiriamali kwani ndoto zangu ni kumiliki kampuni yangu binafsi. Lakini Mzee wangu alipinga vikali wazo hili akisisitiza kuwa kozi za biashara hazina tija na wapo wengi wanaozunguka mitaani na vyeti vyao bila ajira miaka nenda Rudi na Wana degree kabisa.
Nilijaribu sana kumwelewesha kwamba lengo langu si kutafuta ajira Bali ni kujiajiri mwenyewe kutokana na elimu nitakayopata lakini hakukubaliana kabisa na Mimi.
Baadaye akanitafutia vyuo vya afya na kufanikiwa kupata nafasi katika kozi Hii ya uuguzi chuo Fulani hapa nchini na Mimi Kwa kuepuka kumkwaza nikakubali kuja kusoma japo haikuwa passion yangu kabisa!
Sasa kinachofanya nije kuomba ushauri ni hiki...
Mzee wangu ni mtu ambaye anataka akiongea kitu basi ufanye kama alivyokwambia yeye, ukitaka kufanya tofauti anakuona kama mbishi, unampuuza au unamdharau!
Of course Baba yangu ni mtu mmoja mzuri sana kwasababu ana upendo wa ajabu Kwa wanae yupo tayari kufanya chochote na ku sacrifice Kila kitu Ili kutupatia kile ambacho yeye anaamini kuwa ni Bora katika maisha ni mtu mwenye upendo wa ajabu sana na familia yake na watoto wake na Kwa Hilo nimemfanya kuwa role model wangu. Shida yake ndio hiyo Moja hataki uende tofauti na anavyotaka yeye.
Mimi Kwa upande wangu siamini kama kusoma saaana ndio kufanikiwa na ninataka nikimaliza hii diploma nianze kupambana na maisha sasa lakini yeye anasisitiza kuwa diploma ni level ndogo sana Kwa maisha ya sasa. Of course inaweza kuwa kweli lakini Mimi naamini katika ndoto zangu na malengo Yangu na sitaki Tena kuendelea kupoteza muda kukaa darasani maana umri unazidi kwenda Mimi sio wa kuendelea kumtegemea mzazi Tena lakini nikimwambia hataki kabisa kuelewa.
Sasa wanajamvi shida yangu ninaomba mnisaidie nitumie mbinu Gani kumwelewesha na kumshawishi Mzee wangu akubali Mimi nifuate kile nilichojipangia katika maisha yangu lakini bila kumkwaza na kumfanya ahisi kama nampuuza au kumdharau?
Nawapenda sana wazazi Wangu sitaki kuwakwaza lakini pia sitaki kunyimwa opportunity ya kupambania malengo niliyojiwekea katika maisha na natamani pia wazazi wanipe Uhuru wa kujiamulia ninachotaka katika maisha yangu pia!
Nimepanga nikirudi home nikazungumze nae kuhusu hili lakini nashindwa kujua nitumie mbinu Gani kumuelewesha Maana najua nikishikilia uamuzi wangu tunaweza kuishia kupishana kauli kitu ambacho sitaki kitokee kwani pamoja na hayo sitaki kumkwaza.
Sasa naombeni ushauri wadau ni vipi naweza kushikilia msimamo wangu bila kuwakwaza wazazi?
Asanteni nawasilisha.
Mawazo yako umeyapata kwa wahamasishaji? Ukidhani biashara rahisi eeeh. Msikilize dingi maliza ukibahatisha ajira ajiriwa kusanya mtaji then fanya biashara ukiwa ajirani then ukiona unajiweza quit the job. Otherwise usidhani mtaani parahisi
 
Japo sijui kwa nini unaona kama ukiwaambia wazi wako juu ya malengo yako mtapishana kauli? Kwa sababu huwenda mzee wako anakuwekea mipango kwa sababu haoni unamipango gani.

Hivyo kwa kuwa bado hujamaliza kusoma hebu jaribu kumueleza mipango yako halafu uone muitiko wake, hilo mosi.

Pili kwa kuwa baada ya kumaliza kutakuwa na muda fulani wewe anza kuyaendea hayo unayoyaamini kwa vitendo, na kama utakuwa umeonyesha uelekeo itakuwa ni rahisi hata kuwashawishi wazazi, kuliko maneno tupu.
 
Moja ya vitu wazaz wanafeli ni kuforce usomee nn sijui wakat hawajui nn ni passion ya mtoto bro chochote utakachofanya ili ufanikiwe lazma uipende kutoka moyon
 
Back
Top Bottom