NBS acheni dhuluma, walipeni Makarani hela zao

NBS acheni dhuluma, walipeni Makarani hela zao

kwaiyo apo ni elfu 40 mara siku 19 sio haba labda wanaandaa taratibu za malipo labda wataweka ktk akaunt za benki si unajua tena mambo ya tozo maana pesa ya serikal nayo kuipata sio poa.
Semina siku 5
 
Kuna tatizo sehemu ,waliokuwa wanaandika namba za nyumba wamekamilishiwa malipo yao? Majuzi tu Mwanza walikuwa wanaadamana.
 
Kwema Wakuu,

Semina Kwa Makarani wa Sensa imeanza Jana. Makarani wameshaanza mafunzo, na mdogo wangu ni mmoja wao akiwa anafanyia Mafunzo yake chuo cha Ustawi wa Jamii.

Sasa toka jana wanapigwa kalenda juu ya fedha zao za Mafunzo, Chakula na za Kujikimu. Hawajalipwa za Jana na za Leo pia.

Sasa cha pili wanaambiwa kua hata chakula hawatapewa hela ya chakula ambayo ni 10,000/- Kwa siku, bali wanalishwa chakula kisha wanakatwa hiyo hela.

Yaani kuna mtu hapo NBS amejipa tenda ya kuwapikia kisha yeye ndo achukue hizo 10,000/- kilazima. Chakula chenyewe anachowapikia hata Cha Mama Ntilie Cha Buku kina afadhali.

Hivi ni lazima kila kitu tuingize mambo ya dili? Kama hela zipo si muwape wajigharamie nauli za kuja huko kwenye semina? Hata chakula wapeni hela zao kisha pikeni hapo kwenye semina anaetaka kununua kwenu aje kununua kwa hiari yake Kwa bei ya Soko, sio kulazimishana kwa bei mnazozitaka nyinyi.

Hili ni zoezi muhimu sana, lakini mnaanza kuliharibu mapema tu sababu ya ulafi na uroho wenu wa hela za watu. Watu wanakuja kwenye semina huku wamenung'unika, mnadhan lengo la semina litafikiwa kweli hapo?
Mkuu, nilishiriki zoezi la sensa mwaka 2012 kama karani, mwaka huo nikiwa ndiyo nimemaliza Chuo Kikuu, njaa kali mtaani.

Hapo kuna upigaji. Hata kipindi chetu budget ya chakula ilikuwepo. Pesa ambayo kama utaratibu ungefuatwa tulipaswa tupewe mkononi ili kila mtu ajitegemee maswala ya msosi, kilichotokea ni kwamba walilazimisha kumpa tender mtu wa catering! Sababu yao eti kila mtu akienda kula anapopajua kuna ambao watachelewa kurudi kuendelea na semina kwasababu wataenda kula mbali na muda wa lunch ulikuwa mchache (tulikuwa tunapewa an hour; ambayo kiuhalisia haukuwa muda mchache kwa mtu anayejua kujiratibu vizuri).

Ukweli ni kwamba kuna 10% yao kutoka kwa mtu anayepewa tender ya msosi. Na uzoefu unaonyesha kwamba chakula huwa hakilingani na thamani ya kiasi cha fedha kinachotolewa kwa sahani.

Halafu malipo yoyote huwa hayafanyiki kabla ya zoezi husika, hapo watafanya semina kwa siku kadhaa ndiyo walipwe kiasi, baadaye wataendelea na semina halafu watalipwa mkupuo mwingine wa mwisho.

Fedha inayolipwa kabla ni ile ya on-cite, kwa maana ya kwamba kabla ya kwenda kuhesabu watu ndiyo kila mtu atalipwa posho yake yote pamoja na kukabidhiwa vitendea kazi.

All in all mpe dogo pole (kama siyo wewe mwenyewe [emoji3]), mwambie awe/uwe mvumilivu.

Ikumbukwe kuwa Hayati Mwl Nyerere aliwahi kusema, "utumishi wa umma (likiwemo zoezi la sensa) ni kazi ya kujitolea, siyo kazi ya kulipwa mamilioni".

Asante.

Sent from my TECNO RC6 using JamiiForums mobile app
 
Hivi naomba mniambie, huu mchongo wa sensa unakaa siku ngapi yaani ile kazi ni ya siku ngapi na malipo ni kiasi gani?
 

Attachments

  • IMG-20220801-WA0002.jpg
    IMG-20220801-WA0002.jpg
    57.9 KB · Views: 9
Hata kama mtu anakandamizwa ulitaka akae kimya kisa Hana ajira?
Walimu wana inferiority complex ndio maana mnawapelekesha mnavyotaka
Mtabakia kulalamika hvyo hvyo mitandaoni. Sasa kama ni haki Yao siwaungane pamoja kudai huko walipo itaonyesha wako serious kuliko kuja kujaza maneno mengi huku. Ndio maana nkasema vijana wa hovyo, kuungana kudai haki hawawezi kazi ni umbea na manung'uniko tu. Nikuulize tu swali hivi wanajua hata wanalipwa shilingi ngapi? Wengi hawajui badala waulize kabla wajue ili mtu aamue kwa kiwango hiki nakubali au nakataa, wao washakubali kabla badae wakilipwa elfu ishirini malalamiko, unainguaje kazini bila kujua malipo?
 
Ila za Serikali hazigawi kama njugu za kuchoma kwa kifuu
 
Umeongea Fact Sana
Hii nchi ngumu

Chakula wanaweka mwiko mmoja na Andazi 1 na chai....huu ni unyanyasaji

Wanawa-wa- underrate makarani lakin they forget hawa ndo kitovu Cha sensa when you treat them wrong. In early stage what do you expect?
Huo mwiko mmoja mchana na andazi moja asubuhi ndio dogo kasema hivyo hivyo. Hapo amekatwa 10,000/- kwa huo msosi. Yaani kwenye kila project kubwa watu wanawaza upigaji tu.
 
Mkuu, nilishiriki zoezi la sensa mwaka 2012 kama karani, mwaka huo nikiwa ndiyo nimemaliza Chuo Kikuu, njaa kali mtaani.

Hapo kuna upigaji. Hata kipindi chetu budget ya chakula ilikuwepo. Pesa ambayo kama utaratibu ungefuatwa tulipaswa tupewe mkononi ili kila mtu ajitegemee maswala ya msosi, kilichotokea ni kwamba walilazimisha kumpa tender mtu wa catering! Sababu yao eti kila mtu akienda kula anapopajua kuna ambao watachelewa kurudi kuendelea na semina kwasababu wataenda kula mbali na muda wa lunch ulikuwa mchache (tulikuwa tunapewa an hour; ambayo kiuhalisia haukuwa muda mchache kwa mtu anayejua kujiratibu vizuri).

Ukweli ni kwamba kuna 10% yao kutoka kwa mtu anayepewa tender ya msosi. Na uzoefu unaonyesha kwamba chakula huwa hakilingani na thamani ya kiasi cha fedha kinachotolewa kwa sahani.

Halafu malipo yoyote huwa hayafanyiki kabla ya zoezi husika, hapo watafanya semina kwa siku kadhaa ndiyo walipwe kiasi, baadaye wataendelea na semina halafu watalipwa mkupuo mwingine wa mwisho.

Fedha inayolipwa kabla ni ile ya on-cite, kwa maana ya kwamba kabla ya kwenda kuhesabu watu ndiyo kila mtu atalipwa posho yake yote pamoja na kukabidhiwa vitendea kazi.

All in all mpe dogo pole (kama siyo wewe mwenyewe [emoji3]), mwambie awe/uwe mvumilivu.

Ikumbukwe kuwa Hayati Mwl Nyerere aliwahi kusema, "utumishi wa umma (likiwemo zoezi la sensa) ni kazi ya kujitolea, siyo kazi ya kulipwa mamilioni".

Asante.

Sent from my TECNO RC6 using JamiiForums mobile app
Ahsante kwa ufafanuzi.
Hizi semina zinafanyikia vyuoni, vipi kama wangeruhusu wapishi huru (wafanyabiashara wa vyakula) karibu na hapo ili muda wa chai au chakula wakapate msosi hapo ?
 
Wadau naomba kujua mshiko wote ambao makarani wa sensa watalipwa.

Msaada jamani.
 
Sasa siku ya pili hawajalipwa. Pili hiyo 40,000 ni baada ya kua 10,000/~ imechukuliwa hiyo unayosema ya chakula.
Una kichwa kigumu! Wanapewa 40,000 kwa siku kwa vile wamepewa half per diem. Kumbuka wametoka katika maeneo hayo. Chakula ni ziada na wala hawakatwi popopote
 
Kwa taarifa yako pesa ni 50 na chakula ujitegemee
Hakuna hiyo kitu! Unapotosha tu! Pesa ya sensa ni ya serikali na inafuata miongozo ya serikali. Full per diem ni 80,000 na half per diem ni 40,000 tu
 
Zoezi limeshikiliwa na Madiwani..... Litafanikiwa vizur tu.......... [emoji1787]
 
Back
Top Bottom